Tuesday, July 15, 2014

BILION 293 KUTUMIKA KUBORESHA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA



Tume ya uchaguzi inatarajiwa kutumia zaidi ya bilioni 293 katika kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura ambalo mchakato wake unatarajiwa kuanza hivi karibu huku maandalizi yakiwa yamekamilika .

pia tume ya uchaguzi inatajiwa kuandikisha jumla ya watu wasiopungua milion 24 kwenye zoezi zima la uandikishaji wapiga kura huku tenelojia mpya ya uandikishaji ikibadilika. 
 
Akizungumza na wadnishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wanavyoviwakilisha katika semina ya tume na vyombo vya habari mwenyekiti wa tume Jaji mstaafu Damian Lubuva kuwa tume inatarajia kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura na teyari maandalizi yamekamilika

Jaji lubuva alisema kuwa mfumo huo mpya ambao ulianza kutumika kwenye mataifa mbalimbali na hapa nchini ndio unaingia lakini Zanzibar teyari waliutumia kwa mara ya kwanza kwenye uchaguzi uliopita.
''Mfumo huu wa kuchukuwa au kupima taarifa za mtu za kibaolojia au tabia ya mwanadamu na kuzihifadhi katika kanzi data kwa ajiliya utambuzi utatusaidia sana"alisema jaji mstaafu Lubuva.
Mbali na faida hizo pia mfumo huo utasaidia kuondoa wapiga kura waliojiandikisha zaidi ya mara moja,kutambua wapiga kura siku ya uchaguzi na kuhamasisha wapiga kura waliohama kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Aidha alisema kuwa mfumo huo pia ulikumbana na chqangamoto mbali mbali za kiteknolojia na kimfumo kwenye nchi zilizoanza kuutumia ikiwemo nchi ya kenya ilioingia mwaka 2013 baada ya mfumo wa njia moja ya mawasiliano kukwama wakti wa uhesabuji wa kura na hapa nchini wamejipanga kuhakikisha hayajitokezi hayo.
Jaji mstaafu Akatanabaisha kuwa mbali na changamoto hiyo katika mfumo huo kwenye uandikishaji haukuleta matatizo huku hapa nchini ukitumika kwa ajili ya kuandikisha wapiga kura tu na wala si vingine.
Alisema kuwa mfumo huu utatoa majibu kwenye changamoto ambazo zilijitokeza wakati tume ilipokuwa ikitumia mifumo mbalimbali kabla haijaanza kuutumia mfumo huu wa BVR kwani kwa asilimia kubwa mfumo hu utasaidia.
Jaji Lubuva alisema kuwa uboreshaji huo wa daftari la kudumu utawafanya kadi za wapiga kura kutotumika na badala yake watatoa kadi mpya zenye muonekano kama za benki
 Mahmoud Ahmad Arusha

No comments: