Wednesday, September 3, 2014

TAMKO LA JESHI LA POLISI

01 
JESHI la Polisi nchini limetoa onyo kwa watu wanaotumia mitandao vibaya ikiwemo kutuma ujumbe wa matusi, uchochezi, picha za utupu sanjari na kukashifu viongozi wa Serikali, dini na watu mashuhuri.02Akizungumza Dar es Salaam, Septemba 3,2014  Msemaji wa Polisi, Advera Senso alisema kuwa tayari baadhi ya watu wameshakamatwa na kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo na wengine wanaendelea kuhojiwa.

“Kumejitokeza tabia kwa baadhi ya watu kutumia mitandao ya kijamii na simu za kiganjani kinyume na malengo yaliyokusudiwa kwa kusambaza taarifa za uchochezi, kashfa,kuchafua viongozi wa Serikali.
 “Wengine wamekuwa wanasambaza picha za utupu ambazo hazina maadili, hali ambayo ni kosa la jina, ingawaje mwingine anaweza asijue kuwa kufanya hivyo ni kosa lakini sheria haitamuacha, alisema.

 Senso aliendelea kubainisha kuwa kuvunja kutofahamu sheria kwa kutoifahamu si sehemu ya kuepuka kuchukuliwa hatua za kisheria, atakabainika kutenda kosa hilo bila kujali anaifahamu sheria au la, atachukuliwa adhabu kali.
 Alisema oparesheni ya kuwabaini wanaosambaza ujumbe zinaendelea nchi nzima kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa lengo la kuwakamata waharifu wa aina hiyo.

 Aliongeza kuwa hatua hiyo pia inawatia hatiani wale wote wanaotumia mitandao kufanya utapeli na kujipatia kipato kwa watu mbalimbali nchini sanjari na blogs zinazosambaza picha chafu ambazo ni kinyume na maadili.

“Wapo baadhi ya watu wanatumia mitandao ya simu kutapeli watu na kujipatia kipato, hivyo nao ni sehemu ya waharifu wanaotafutwa na jeshi la polisi na yeyote atayekamatwa hatua kali zitachukuliwa dhidi yake,” alisema.

 Hivyo alisisitiza kuwa Jeshi hilo linatoa onyo kali kwa watu kujiepusha na uharifu huo, na kuwataka wale wanaotumiwa wa aina hiyo kutousambaza kwa wengine bali waufute.
 Pia aliziomba kampuni za simu za mkononi pindi wanapoona ujumbe wa aina hiyo wasiruhusu uende kwa mwingine ili nao wawe sehemu ya kupambana na uovu huo.

Mkongo wa Taifa wasaidia kushuka kwa gharama za mawasiliano nchini.

mHANDISHI ANIFA CHINGUMBEMhandisi Hanifa Chingembe akielezea  na kuonyesha kwa waandishi wa habari jinsi mkongo wa Mawasiliano wa Taifa ulivysambaa nchi nzima.
……………………………………………….
(Picha na Hassan Silayo)
 
Frank Mvungi
Serikali imesema Mkongo wa Taifa umesaidia kushuka kwa gharama za  mawasiliano kwa watumiaji wa mwisho nchini kutoka sh.147 kwa dakika mwaka 2009 hadi shilingi 62 kwa dakika mwaka 2013.
Hayo yamesemwa na Msemaji wa Wizara ya Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mawsiliano Sayansi na Teknolojia Bi Prisca Ulomi wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
Akifafanua Bi Prisca amesema kuwa mkongo wa taifa umesaidia pia kushuka kwa gharama za intaneti kutoka shilingi 36,000 hadi shilingi 9000/Gb kufikia mwaka 2013.
“Mkongo wa Taifa umesesaidia kuharakisha usambazaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo yasiyokuwa na mvuto wa kibiashara”alisisitiza bi Ulomi.
Katika hatua nyingine, Bi Ulomi alisema faida nyingine ya Mkongo ni kuongezeka kwa upatikanaji wa huduma za mawasiliano na uwezo wa kusafirisha masafa.
Akieleza kuhusu gharama Bi Prisca amesema gharama za maunganisho ya mawasiliano ya simu za mkononi kutoka  kampuni moja kwenda nyingine                (interconnection fees) ambapo sasa gharama imepungua kutoka sh. 115 hadi shilingi 34.92 kwa dakika.
Mkongo wa Taifa umesaidia kuongeza ushirikiano wa kikanda  kati ya nchi za Afrika Mashariki na kati ambapo nchi za Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi, Uganda, na Kenya ambapo hali hiyo imeongeza fursa za kibiashara na kukuza uchumi wa nchi.
Kufikia mwaka 2013 makampuni yafuatayo yalikuwa yameunganishwa na mkongo wa Taifa ni TTCL, TIGO, Zantel,  Airtel, Vodacom, Simbanet na infinity.

SHIRIKA LA HUC LATANGAZA UFADHILI WA MASOMO YA UFUNDI VETA, VIJANA CHANGAMKIENI

Na Nathan Mpangala wa HUC
Shirika lisilo la kiserikali la Help for Underserved Communities Inc. (HUC), linatangaza nafasi za ufadhili wa masomo ya ufundi VETA kwa vijana wa Kitanzania. Kozi hizo ni ufundi wa magari, umeme wa magari, udereva magari/pikipiki, ufundi cherehani, hair dressing (urembo), mapambo ya ukumbi na nyinginezo  

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na shirika hilo, inasema, HUC, itafadhili wanafunzi 15 wa kozi mbalimbali za awali VETA kwa mwaka 2014-2015.
Walengwa ni vijana wa kike na kiume waliomaliza shule za msingi ambao wamethibitika kuwa wazazi/walezi wao wameshindwa kuwalipia ada. Imesema sehemu ya taarifa hiyo.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa, mwanafunzi atatakiwa kujaza kwa usahihi fomu ya maombi (imeambatanishwa hapa), akiambatanisha na barua akieleza sababu za kuomba ufadhili huu na barua ya utambulisho toka ofisi ya serikali za mitaa na mwisho wa kupokea barua za maombi ni Jumatano, Oktoba 01, 2014, saa 11 jioni. 

Barua za maombi zitumwe kupitia:
Maombi ya ufadhili wa masomo,
Help for Underserved Communities Inc.
P. O. Box 7022,
Dar es Salaam,
Tanzania.
Au
Help for Underserved Communities Inc.
P.O.Box 6822,
Ellicott City, MD 21042 
Au
Kupitia baruapepe:

SHIRIKA LA NYUMBA TANZANIA (NHC) LAKARABATI SHULE YA HASSANGA UYOLE MBEYA.

 Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Abbas  Kandoro akikata utepe kuzindua ukarabati wa Madarasa manne na Jengo moja la Utawala katika Shule ya Msingi Hasanga uliofanyika leo Uyole Mbeya.
Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Abbas  Kandoro, viongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa Tanzania (NHC), Viongozi wengine wa Serikali na Walimu wa Shule ya Msingi ya Hasanga wakifurahia Baada ya Kuzindua Rasmi ukarabati wa ujenzi huo.
Meza kuu
Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Abbas Kandoro akizungumza na wananchi, wanafunzi na Walimu wa Shule ya Msingi ya Hasanga katika Sherehe ya kukabidhi Majengo ya Shule hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa NHC Nehemia Mchechu akizungumza jambo wakati wa Sherehe hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Dr. Norman Sigallah King akimkaribisha Mkuu wa Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Abbas Kandoro
Mwenyekiti wa Bodi ya Shule Akiwakaribisha Wageni katika Sherehe hizo
Meneja wa Shirika la Nyumba Mkoa wa Mbeya Anthony Komba akisoma Taarifa ya ukarabati wa Shule hiyo
 Mwalimu Neema Sanga (Kushoto) akisoma  Risala ya Shule 
Baadhi ya Wageni waalikwa na Meza Kuu
 Baadhi ya Wanafunzi na Wazazi 
Wanafunzi wakiimba Ngonjera 
Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh Abbas Kandoro Akiendesha Harambee
Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Abbas Kandoro akikagua Baadhi ya Majengo
Muonekano wa Baadhi ya Majengo ya Shule ya Msingi Hasanga yaliyokarabatiwa na Shirika la Nyumba la Taifa 
 Baadhi ya Waandishi wa Habari wakichukua tukio.

SHIRIKA la Nyumba la Taifa(NHC) limefanya ukarabati wa majengo ya shule ya Msingi Hassanga iliyopo Uyole jijini Mbeya ambayo alisoma Mkurugenzi Mkuu Nehemia Mchechu.

Makabidhiano ya mradi huo umefanyika leo katika sherehe zilizofanyika katika viwanja vya shule hiyo na kuhudhuriwa na Mkurugenzi mkuu, viongozi wa Halmashauri ya Jiji, Wilaya na Shirika la Nyumba ambapo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro alikuwa mgeni rasmi.

Aidha ukarabati wa majengo manne na jengo moja la utawala uliofanywa na shirika la Nyumba(NHC) umegharimu zaidi ya shilingi Milioni 31.

Mkurugenzi mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu,katika taarifa yake iliyosomwa na Meneja wa Shirika hilo Mkoa wa Mbeya,Antony Komba, amesema Shirika hilo liliamua kufanya ukarabati wa jengo la utawala na madarasa manne ya shule hiyo kama sehemu ya mchango wake kwa jamii kufuatia maombi yaliyofanywa na Kamati ya shule ya kuombwa ukarabati wa majengo hayo.

Amesema kazi ya ukarabati ilianza Aprili 19 na kukamilika Agosti 20, Mwaka huu ambapo Shirika lilikarabati Jengo la utawala katika ujengaji upya wa kuta za jengo , bimu na uezekaji upya wa paa, upigaji lipu, sakafu na rangi pamoja na kuweka milango na madirisha ya alminium kwa gharama ya shilingi Milioni 22,77,900.

Ameongeza kuwa ukarabati katika madarasa manne ulihusu upigaji upya wa lipu ukutani, utengenezaji wa sakafu , utengenezaji wa shata za madirisha pamoja na upakaji rangi uliogharimu shiringi Milioni 8,803,000 na kufanya jumla ya shilingi Milioni 31, 577,900.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, mbali na kulishukuru shirika hilo kwa msaada wao huo pia ametoa wito kwa Wanafunzi na Walimu pamoja na uongozi wa kamati ya shule kuyatunza majengo hayo ili yaweze kudumu.

Hata hivyo katika hatua Nyingine Mkuu wa Mkoa wa Mbeya alilazimika kuendesha harambee nyingine baada ya Mkurugenzi wa NHC, Mchechu kujibu risala ya walimu walioomba kukarabatiwa majengo mengine ambapo alisema kama wataweza kuchangia chochote Shirika litaweza kumalizia.

Katika harambee hiyo ambayo pia ilichangiwa na Shirika Mkuu wa Mkoa alifanikiwa kukusanya Shilingi Milioni moja na laki tatu ambazo alizikabidhi kwa Mkurugenzi wa Shirika ambaye baada ya kupokea aliahidi kuanza ujenzi kesho wa majengo mengine manne.

Nao Walimu wa Shule ya Msingi Hassanga katika Risala yao kwa Mgeni rasmi,iliyosomwa na Mwalimu Neema Sanga, wamelipongeza shirika la Nyumba kwa kukarabati majengo hayo.

Wamesema ukarabati wa Vyumba vine vya madarasa, ofisi ya Walimu pamoja na Ofisi ya Mwalimu Mkuu ni moja ya kutambua umuhimu wa Elimu na kujenga mazingira rafiki ya kufundisha na kujifunzia.

Na Mbeya yetu Blog.