Tuesday, February 17, 2015

BEI ZASHUKA KATIKA SOKO LA TANDALE WILAYANI RUNGWE KWA KWAKUKOSA WATEJA WA MAZAO YA CHAKULA

WAKLIMA NA WANUNUZI WA MAZAO YA CHAKULA  WAKIWA KATIKA SOKO LA TANDALE WILAYANI RUNGWE

MKULIMA AKIFIKA KUUZA MKUNGU WA NDIZI AMBAO KWA SASA MKUNGU KAMA HUO UNAUZWA SHILINGI ELFU MBILI


NDIZI ZIKIWA ZIMEKOSA WANUNUZI KATIKA SOKO LA TANDALE TUKUYU NA HII INATOKANA KUWA  HUU NI MSIMU WA ZAO LA NDIZI HIVYO BEI YA NDIZI HUYUSHA SANA NA WAKULIMA KUUZA KWA BEI YA CHINI BILA YA KUPATA FAIDA

MMOJA WA WANUNUZI WA ZAO LA MAPARACHICHI KATIKA SOKO LA TANDALE

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA RUNGWE MHESIMIWA MWAKASANGULA  AKIONGEA NA KINGOTANZANIA AMESEMA KUWA HALMASHAURI YA RUNGWE IMEANZISHA UHUSIANO WA KIBIASHARA NA MANISPAA ZA KINONDONI NA ILALA JIJIN DSM KUANZISHA BIASHARA YA PAMOJA HASA KWA ZAO LA NDIZI, HIVYO WAKULIMA WATEGEMEE SOKO ZURI LA ZAO LA NDIZI KUANZIA MPANGO HUU UTAKAPOANZA HUKU TARATIBU ZOTE ZIKIWA ZIMEKAMILIKA



Soko kuu la  wakulimaTandale mjini Tukuyu Wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya limekosa wateja wa mazao ya chakula na kusababisha kushuka kwa bei ya mazao hayo hasa mazao ya ndizi mbalimbali maparachichi  na mazao ya mbogamboga ambayo ndio hutegemea  kwa wingi na wateja wanao toka mikoa ya jirani 

Wakizungumza sokoni hapo wakulima na wanunuzi wa mazao ya chakula wamesema kwamba gulio la kipindi hiki wateja wamekuwa wachache ukilinganisha na vipindi vingine na bei ya mazao hutegemeana na wateja waliofika siku hiyo ya gulio hivyo kipindi hiki wakulima hulazimika kuuza kwa bei ya hasara kufuatana na bei anayoitaka mnunuaji kwa  kuogopa kubakiwa na mzigo mkubwa ambapo kwa sasa mkungu  mzuri wa ndizi katika soko la Tandale unafikia shilingi elfu tatu.

“Kipindi hiki bei imeshuka kabisa na kumumiza mkulima wa mazao ya chakula hasa zao la ndizi  na maparachichi ndiyo yamekuwa na bei ya chini sana kwani mkungu mkubwa  moja wa ndizi aina ya mzuzu unauzwa kwa shilingi elfu nne kwa elfu tatu na ndizi aina ya malindi na aina zingine zinauzwa kwa shilingi elfu moja mia tano kwa elfu moja kwa mkungu uliokomaa vizuri na mkubwa na kwa upande wa maparachichi ujazo wa gunia moja limeuzwa kwa shilingi elfu ishirini na tano, wakati kipindi kukiwa na wateja wengi  ndizi huuzwa kwa bie ya shilingi elfu nane kwa elfu saba kwa aina ya mzuzu na elfu nne kwa elfu tatu mia tano kwa  aina nyingine za ndizi na gunia la maparachichi huuzwa kwa shilingi elfu thelathini hadi  elfu Alobaini.

Bei ya jumla  kwa mazao ya chakula katika soko la tandale mjini Tukuyu  gunia la mahindi limeuzwa kwa bie ya shilingi elfu therathini, viazi mviringo ujazo wa gunia vimeuzwa kwa shilingi elfu sitini na gunia la maparachichi limeuzwa kwa shilingi elfu ishirini na tano huku ndizi mkungu moja mkubwa umeuzwa kwa shilingi elfu nne kwa elfu tatu kwa aina ya mzuzu na elfu moja kwa aina ya malindi.
TUMAIN OBEL
KINGO TANZANIA

No comments: