Monday, February 23, 2015

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ampa pole Chief wa Wahehe , Adam Abdu Sapi Mkwakwa

1
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Chief wa Wahehe , Adam Abdu Sapi Mkwakwa   wakati alipokwenda nyumbani kwa Chief huyo, Kalenga Iringa  Februari 20, 2015 baba yake Chief huyo, Marehemu Abdu Adam Sapi Mkwawa uliotokea hivi karibuni.
(Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu)
2
  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akishiriki katika dua mbele ya kaburi la marehemu Abdu Adam Sapi Mkwawa   wakati alipokwenda nyumbani kwa Chief huyo, Kalenga Iringa   kuhani.
6
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizunbgumza na viongozi wa wilaya ya Kilolo baada ya kusomewa taarifa ya wilaya hiyo Februari 21, 2015. Kushoto ni Mkuu wa koa wa Iringa, Amina Masenza.
7
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  na mkewe Tunu  wakisalimiana na walimu  wa sekondari ya Ilula kabla ya kukagua ujenzi wa maabara katika shule hiyo akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa.
8
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua moja ya madara ambayo yamegeuzwa kuwa maabara katika Shule ya Sekondari ya Ilula akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa Februari 21, 2015. Kitendo hicho hakikumfurahisha na aliagiza kisirudiwe tena sehemu nyingine ngo mapya yajengwe kwa ajili ya maabara
9
Mke wa Waziri Mkiuu, Mama Tunu Pinda akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Ilulawilayani Kilolo ambako Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alikagua ujernzi  wa maabara na kuhutubia wananchi. 
10
Mkuu, Mizengo Pinda akikagua banio katika mradi wa umwagiliaji maji wa kijiji cha  Nyanzwawilayani Kilolo akiwa katika ziara ya mkoa wa Iringa Februari 21, 2015.
12
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu wakikagua shmba la vitunguu la Bw. Furaha Ngalali  (kulia)  wakati walipotembelea mradi wa umwagiliaji wa kijiji cha Nyanzwa wilayani  Kilolo Februari 21, 2015.
13
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na   Meneja Mipango wa Kamouni ya Mawasiliano ya simu ya VIETTEL TANZANIA LIMITED tawi la Iringa, Salvatory Elikidus katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri Mkiuu, Mizengo Pinda katika kijiji Nyanzwa wilayani Kilolo Februari 21, 20154.  Kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Tawi la Iringa,  Tran  Nhat Duy na wapili kushoto ni  Mkuu wa Idara ya Fedha, Vo Ngoc Thang.

No comments: