Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernald Membe
akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa JNICC jijini Dar es
salaam, Wakati alipotoa tamko la serikali ya Tanzania kuhusu machafuko
yaliyotokea wiki iliyopita nchini Afrika Kusini kwa wenyeji wa nchi hiyo
kufanya mashabulizi dhidi ya wageni kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika
wanaoishi nchini humo.
Amesema
Tanzania inaunga mkono Tamko lililotolewa na Mwenyekiti wa SADC na AU
Rais wa Zimbabwe Mzee Robert Mugabe kuhusu machafuko hayo na hatua
ambazo serikali ya Afrika kusini imechukua ili kuzuia yasiendelee.
(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
Wapiga
picha kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakichukua picha na taarifa
muhimu wakati Waziri huyo akizungumuza na waandishi wa habari kwenye
ukumbi wa JNICC jijini Dar es salaam asubuhi hii.
Baadhi
ya waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini wakati Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikini wa Kimataifa akizungumza na waandishi wa habari
jijini Dar es salaam.
Balozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa Mh ModestJ Mero pamoja na viongozi
wengine kutoka wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
wakifuatilia mkutano huo.
No comments:
Post a Comment