Saturday, June 20, 2015

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AITIKISA KATORO MKOANI GEITA


????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha ishara mbalimbali kwa msisitizo wakati akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye  mji mdogo wa Katoro jimbo la Busanda mkoani Geita wakati Katibu mkuu huyo akiendelea na  ziara yake mkoani humo, Kinana anafanya ziara mkoani Geita yenye lengo la kukagua na kuhimiza utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010-2015 inayotekelezwa na serikali huku akihimiza uhai wa Chama cha Mapinduzi CCM, Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM.

Katika mkutano huo Kinana amewaambia wananchi hasa wachimbaji wadogowadogo wa Nyarugusu kwamba hataki kuwa mmoja wa wanaotoa ahadi bila kutekelezeka na hataki kuahidi uongo, Mimi ninalichukua hili ili nikalifanyie kazi na  nitarrudi hapa Katoro kuwapa jibu kama nimefanikiwa au sijafanikiwa.

Lakini nilichoambiwa ni kwamba Rais ameshabariki ili wachimbaji wadogo wapewe eneo fulani hapo Nyarugusu  ili waendelee kuchimba na kujipatia riziki yao, Lakini  jambo la kushangaza ni kwamba amri ya Rais haijatekelezwa yaani watendaji wamemwangusha Rais kwa madai kwamba Shirika la madini la serikali la STAMICO na kampuni ya madini ya TANZAM bado hawajaafikiana kisheria ili  kuachia eneo hilo la Nyarugusu ili wachimbaji wadogo kukabidhiwa kwa ajili ya kuendeleza uchimbaji ili kujipatia riziki yao.

“Serikali hii ni ya CCM na inatakiwa kuwasaidia watanzania masikini. Lakini inashangaza kuona watendaji wa serikali wanachelewa sana kuchukua hatua na kushughulikia matatizo ya wananchi jambo ambalo linazua malalamiko kwa wananchi, Niachieni hili ninalichukua na sitaki kuahidi lolote ila nitarudi na majibu baada ya mwezi mmoja na nina imani litakwisha na kupata suluhisho la kudumu”.
(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-BUSANDA-GEITA)
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Umati wa wananchi ukiwa umefurika katika mkutano huo ambao umefanyika kwenye mji mdogo wa Katoro mkoani Geita.
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Nape Nnauye akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mji mdogo wa Katoro mkoani Geita.
????????????????????????????????????
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM akisisitiza jambo wakati alipokuwa akiwahutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Katoro.
????????????????????????????????????
Mbunge wa jimbo la Busanda Mh. Rolensia Bukwimba akiwahutubia wapiga kura wake wakati mkutano huo ukiendelea.
????????????????????????????????????
Mh.Vick Kamata Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Geita  akiwasalimia wananchi katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Baadhi ya wananchi waliofurika ili kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
????????????????????????????????????
Katibu wa CCM mkoa wa Geita  Ndugu Gustav Muba akimkaribisha Ndugu Nape Nnauye hayupo pichani  ili apande jukwaani na kuzungumza na wananchi wa Katoro.
????????????????????????????????????
Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale na kaimu Mkuu wa mkoa wa Geita Ndugu Ibrahim Nyankanga Marwa akiwasalimia wananchi katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Wananchi wakimsubiri Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ili awahutubie.
????????????????????????????????????
Baadhi ya wachimbaji madini wadogo wadogo wakimsikiliza Ndugu Kinana 
????????????????????????????????????
Mmoja wa wachimbaji wadogo akiwa ambaye jina lake halikfahamika akiwa ameshikilia kifaa chake cha kazi akifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati alipkuwa akizungumza nao.
????????????????????????????????????
Selemani Magesa na Diwani wa Kata ya Nyarugusu akitoa maelezo ya mgogoro huo mbele ya Kinana.
????????????????????????????????????
 ????????????????????????????????????
Baadhi ya wachimbaji wadogo wakiwa katika mkutano huo wakati Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipowatembelea huko Nyarugusu.
????????????????????????????????????
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Geita Mh. Vick Kamata  akiwasalimia wananchi katika kijiji cha Chikobe mkoani Geita.
????????????????????????????????????
Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimia wananchi wakati alipowatembelea katika kijiji cha Chikobe.
????????????????????????????????????
Kutoka kulia ni Manzie Mangochie Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale Ndugu Ibrahim Marwa, Mbunge wa viti maalum mkoa wa Geita Mh. Vick Kamata na Mbunge wa jimbo la Busana Mh. Rolensia Bukwimba wakiwa katika picha ya pamoja. 
????????????????????????????????????
Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wakati alipfanya ziara katika kijiji cha  Inyala na kushiriki katika ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho.
????????????????????????????????????
Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupiga lipu katika ukuta wa zahanati ya kijiji cha Inyala jimbo la Busanda.
????????????????????????????????????
Katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika kazi ya kulima barabara ya kijiji cha Nyankanga pamoja na wananchi.

No comments: