Saturday, June 20, 2015

CHAMA CHA MSALABA MWEKUNDU TANZANIA(REDCROSS)KIMETOA MAFUNZO KWA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA MKOA WA MBEYA.

Mwenyekiti wa Chama cha Msalaba mwekundu (Redcross) Mkoa wa Mbeya, Ulimboka Mwakilili, akifungua mafunzo ya Redcross kwa Viongozi wa vyama vya siasa Mkoa wa Mbeya.

Meneja wa Idara ya Habari na Uhamasishaji wa Redcross Makao makuu, Stellah Marealle akizungumza na washiriki wa Semina ya Redcross kwa viongozi wa vyama vya siasa Mkoa wa Mbeya

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mikoa na Matawi Redcross makao makuu, Julius Kejo, akitoa mada kwa viongozi wa vyama vya siasa Mkoa wa Mbeya katika mafunzo yaliyotolewa na Chama cha Msalaba mwekundu

Mratibu wa Chama cha Msalaba mwekundu Zanzibar, Ubwa Suleiman akiwasilisha mada katika mafunzo ya Redcross kwa viongozi wa vyama vya siasa Mkoa wa Mbeya

Afisa Mahusiano wa Kamati ya kimataifa ya Redcross (ICRC) Nairobi Kenya, Viginia Njiru akiwasilisha mada kuhusu historia ya Redcross duniani pamoja na matumizi ya nembo zake wakati wa semina ya viongozi wa vyama vya siasa Mkoa wa Mbeya


Baadhi ya viongozi wa Vyama vya Siasa Mkoa wa Mbeya wakifuatilia mafunzo kuhusiana na Chama cha Msalaba mwekundu

Mwenyekiti wa Chama cha SAU, Charles Mwampagama akishukuru kwa niaba ya washiriki wengine





Washiriki wa mafunzo wakifuatilia mada zinazowasilishwa.
  VIONGOZI wa Vyama vya Siasa mkoani Mbeya wamepatiwa mafunzo na Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania katika mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Mbeya Paradise Soweto jijini Mbeya.
 
Akifungua mafunzo  kwa viongozi hao, Mwenyekiti wa Redcross Mkoa wa Mbeya, Ulimboka Mwakilili, alisema lengo la mafunzo hayo ni kutoa elimu juu ya historia ya Msalaba mwekundu pamoja na shughuli zake ili ziweze kufahamika kwa viongozi wa vyama vya siasa.
 
Mwakilili alisema madhumuni makubwa ya Chama cha Msalaba mwekundu duniani ni kusaidia wenye dhiki na mateso na kazi yake kubwa ni kuokoa binadamu wanaopatwa na maafa yanayotokana na majanga mbali mbali yakilenga kutekeleza kanuni 7 za msingi za Redcross.
Alivitaja vyama vya siasa vilivyohudhuria mafunzo hayo kuwa ni pamoja na Chama cha Mapinduzi(CCM), Chama cha Wananchi(CUF),SAU,Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA),UPDP,TADEA,DP na APPT- Maendeleo.
 
Kwa upande wake Afisa mahusiano wa Kamati ya Msalaba mwekundu duniani(ICRC) kutoka Nairobi nchini Kenya, Viginia Njiru ambaye alitoa historia ya Msalaba mwekundu uanzishaji wake pamoja na matumizi ya nembo za Redcross.
 
Aidha alitoa wito kwa watu mbali mbali kutumia nembo za Redcross kinyume cha sheria kwa madai kuwa baadhi yao wamekuwa wakitumia kwenye maduka ya madawa, magari ya kubebea wagonjwa na kwenye mabucha ya nyama jambo alilodai ni kinyume cha utaratibu na kuongeza kuwa wakibainika hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
  Mwisho.

No comments: