Monday, July 13, 2015

MAJAMBAZI YATIKISA KATIKATI YA JIJI LA DAR ES SALAAM LEO MCHANA YATIWA MBARONI


 Picha ya 1-2 ni mmoja wa watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi akiwa mikononi mwa polisi baada ya kutiwa mbaroni Mnara wa Saa maeneo ya Stesheni Dar es Salaam leo mchana kwa madai ya kupora kiasi kikubwa cha fedha. Watu hao wanadaiwa kuwa walikuwa wanne.
 Kijana mwingine anayedaiwa kuwa ni jambazi akiwa amekamatwa.
 Watuhumiwa hao wanne wa  ujambazi  wakiwa ndani ya Noah kabla ya kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi. Kulia ni askari Polisi.
 Askari kanzu (katikati), ndiye anadaiwa kuwadhibiti majambazi hayo kabla ya kujificha chini ya uvungu wa taxi zinazoegeshwa jirani na Mnara wa Saa katika makutano ya barabara ya Uhuru, Samora na Nkruma.
 Gari lenye namba T 976 BKK walilokuwa wakitumia majambazi hayo liondolewa eneo la tukio kupelekwa kituo kikuu cha polisi.
 Wananchi wakiwa eneo la tukio.
 Askari Polisi wakilipekua gari walilokuwa wakitumia watu hao wanaodaiwa kuwa ni majambazi.
 Upekuzi ukiendelea.
Maofisa wa polisi wakiteta jambo eneo la tukio baada ya kuwakamata majambazi hayo.

No comments: