Tuesday, July 25, 2017

WANANCHI WA KATA YA BAGAMOYO WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA WASHIRIKI UJENZI WA BARABARA




Diwani wa kata ya Bagamoyo Bwana Zakayo Yohana Njate,ameelezea namna shughuli za maendeleo zinavyo endelea katika kata yake, huku akiwa pongeza wananchi pamoja na wadau mbalimbali kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo katika kata hiyo.

Baadhi ya wananchi wa kata hiyo wamezungumzia namna wanavyo shiriki katika shughuli za kimaendeleo zinazo endelea katika kata hiyo ya Bagamoyo,hususani katika ukarabati wa miundo mbinu unao endelea katika eneo hilo.

Hata hivyo  Diwani wa kata ya Bagamoyo Zakayo Njate,amezungumzia namna shughuli za bomoa bomoa  zilivyo waathiri wananchi wa kata hiyo,kutokana na nyumba zao nyingi kubomolewa kupisha upanuzi wa bara bara.

Aidha diwani huyo amesema kuwa kunamiradi mbali mbali ambayo inafanyika kwa nguvu za  wananchi,hususani katika ukarabati wa vyoo katika shule nne,ambapo shule mbili tayari ukarabati umekamilika.


Sanjari na hayo amesema kuwa anawaomba wananchi kuendelea na moyo huo huo katika shughuli za kimaendeleo,ambapo ameiomba halmashauri iweze kuongeza nguvu kwa wananchi hao wa kata ya Bagamoyo katika shughuli za maendeleo. 

No comments: