RUNGWE,
Sheria ndogo ya halmashauri juu ya uhifadhi mazingira ya mwaka 2012 kifungu na 16
kinaeleza kuwa ni marufuku kulima ,kukata miti,kuchunga,na kufanyana shughuli
yoyote umbali wa mita 60 katika vyanzo
vya maji.
katika kutekeleza sheria hiyo Watu ishilini na moja [21] wakazi wa
kata ya ibigi kijiji cha katumba
wamepelekwa mahakamani kwa kosa la kufanya shughuli za kibinaadam katika vyanzo
vya maji kwenye mto ijingija na mto katumba .
Halmashauli ya wilaya ya rungwe imewafumgulia kesi watu hao katika
mahakama ya mwanzo katumba one ambapo kesi hiyo ilikuwa imesikilizwa tarehe 24
/7/2017 kutokana na tarifa za watuhumiwa
kuto wafikia kwa muda muwafaka hivyo kesi imeahirishwa mpaka tarehe 31/7/2017.
Afisa mazingira wilaya ya Rungwe amewaasa watu kuto kufanya shughuli
katika vyanzo vya maji wala kumiliki eneo lililopo katika chanzo cha maji kwani
ni kinyume cha sheria na husababisha maji kukauka hivyo kupelekea ukame.
No comments:
Post a Comment