Wednesday, December 5, 2012

DNA

DNA Yabaini Watoto Wengi Wa Kusingiziwa


Na Florence Majani, MWANANCHI
ASILIMIA 44 ya wapenzi wanaokwenda Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kupima vinasaba (DNA), kwa ajili ya kujua uhalali wa watoto kwa baba, wamethibitishiwa kuwa watoto hao si wa kwao.
Takwimu za mwaka 2012 kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, zimeainisha kuwa kati ya watu 90 waliokwenda kupima DNA, 40 ambao ni sawa na asilimia 44, wameonekana kubambikiziwa watoto.
Takwimu hizo za kuanzia Januari hadi Oktoba mwaka huu, zilionyesha kuwa katika kesi 50 za waliokwenda kupima, matokeo yalionyesha kuwa ni wazazi halisi wa watoto wao.
Hata hivyo, idadi hiyo inayoonyesha kuwa kinababa siyo wazazi halisi wa watoto, imeshuka ikilinganishwa na takwimu za mwaka 2008/2009 ambazo zinaonyesha kuwa asilimia 60 ya watu waliochukua vipimo hivyo wamebainika kuwa si wazazi halisi wa watoto hao.
 
Wakati huohuo
 Ujue utamaduni wa kabila la wasafwa wa jijini Mbeya


Mkazi wa Mwasanga jijini Mbeya Sosteli Mponzi (kulia) akimuonyesha Victoria Zitta Mnyanyi (kushoto) ambaye ni Mshauri wa wanafunzi wa chuo kikuu cha Mzumbe tawi la Mbeya moja ya nyumba ya kale iliyokuwa inatumiwa na kabila la wasafwa ambalo ni kabila maarufu mkoani humo. Mponzi ameamua kujitolea kujenga kituo cha utamaduni wa kabila hilo ambacho kitatunza kumbukumbu za utamaduni na mila zote ili kizazi kijacho kiweze kufahamu mambo yaliyofanywa na mababu zao.
Msafwa wa Mwasanga jijini Mbeya Ibrahim Saimon akipuliza pembe ya Mnyama aina ya Tandala “Ndundwe” iliyokuwa inapingwa wakati wa sherehe za kumaliza msiba “matanga” za kabila la wasafwa. Sosteli Mponzi ameamua kujitolea kujenga kituo cha kutunza utamaduni na mila za kabila hilo ili kizazi kijacho kiweze kufahamu mambo yaliyofanywa na mababu zao.
Baadhi ya wasafwa wa Mwasanga jijini Mbeya wakimuangalia Mary John akisaga unga wa ulezi kwa kutumia jiwe aina ya “Lwala” wakati walipotembelea ili kujionea ujenzi wa kituo cha utamaduni wa kabila lao kinachojengwa kwa kujitolea na Sosteli Mponzi. Baadhi ya wasafwa waishio maeneo ya vijijini bado wanasaga unga wa ulezi kwa kutumia jiwe hilo kwa ajili ya kutengenezea pombe.
Mkazi wa Mwasanga jijini Mbeya Sosteli Mponzi (kushoto) akimuonyesha Victoria Zitta Mnyanyi ambaye ni mshauri wa wanafunzi wa chuo kikuu cha Mzumbe tawi la Mbeya mti wa asili aina ya msulusulu ambao wazee wa kabila la wasafwa walikuwa wakiutumia kwa ajili ya kutibu mifugo. Mponzi ameamua kujitolea kujenga kituo cha utamaduni wa kabila hilo ili kumbukumbu zisiweze kupotea kwani hivi sasa kutokana na utandawazi makabila mengi yamekuwa yakipoteza utamaduni wao.
Baadhi ya wasafwa wa Mwasanga jijini Mbeya wakicheza ngoma aina ya Mbeta ya kabila hilo ambayo inachezwa wakati wa kumaliza msiba “Mwengulo” kama walivyokutwa na mpiga picha wetu hivi karibuni alipotembelea kituo cha kutunza utamaduni na mila za kabila la wasafwa. Ujenzi wa kituo hicho unajengwa kwa kujitolea na Sosteli Mponzi ili kizazi kijacho kiweze kufahamu mambo yaliyofanywa na mababu zao.
Mkazi wa Mwasanga jijini Mbeya Juma Changa akionyesha jinsi wazee wa zamani walivyokuwa wakichonga mpini wa jembe kwa kutuma teso “menzo” wakati mpiga picha wetu alipotembelea kituo cha kutunza utamaduni na mila za kabila la wasafwa huku Said Mbata (kulia), Victoria Zitta Mnyanyi (katikatia) na Sosteli Mponzi (kushoto) wakimuangalia. Ujenzi wa kituo hicho unajengwa kwa kujitolea na Mponzi ili kizazi kijacho kiweze kufahamu mambo yaliyofanywa na mababu zao.
Baadhi ya wasafwa wa Mwasanga jijini Mbeya wakimwonyesha mpiga picha wetu jinsi wazee wa zamani wa kabila hilo walivyokuwa wanakunywa pombe aina ya Kimpumu wakati alipotembelea kujionea ujenzi wa kituo cha kutunza utamaduni na mila za kabila hilo.Kutokana na kuenea kwa magonjwa mbalimbali ya kuambukiza hivi sasa kila mtu anakunywa pombe hiyo kwa kutumia chombo chake.
na

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA (TCRA) YATOA ZAIDI YA SHILINGI MILION 15 KWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA KWA AJILI YA KUBORESHA MFUMO MPYA WA UTOAJI HUDUMA ZA MATIBABU KWA NJIA YA MAWASILIANO (TELE MEDICINE)

Meneja wa TCRA Kanda ya Nyanda za Juu kusini Deograsias Moyo kwa niaba ya mkurugenzi wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania akimkabidhi hundi ya zaidi ya sh milioni 15 mkurugenzi wa hospitali ya rufaa Mbeya eliuter Samnkey 

ZAIDI  ya shilingi million 15 zimetolewa na mamlaka ya mawasiliano Tanzanzania (TCRA)  nyanda za juu kusini   ajiri ya  kuboresha mfumo  mpya wa utoaji  huduma za matibabu kwa njia ya mawasiliano (TELE MEDICINE) ili kupunguza vifo na  gharama za usafiri kwa wagonjwa.


 Mhandisi  na kaimu meneja wa mamlaka ya mawasiliano ya simu (TTCL) George Mtikila akipokea hundi hiyo  kwa mkurugenzi wa hospitali ya rufaa dr Eliuter Samnkey kwa ajili ya kuleta vifaa hivyo na kufunga katika hospitali hiyo ya rufaa Mbeya

ZAIDI  ya shilingi million 15 zimetolewa na mamlaka ya mawasiliano Tanzanzania (TCRA)  nyanda za juu kusini   ajiri ya  kuboresha mfumo  mpya wa utoaji  huduma za matibabu kwa njia ya mawasiliano (TELE MEDICINE) ili kupunguza vifo na  gharama za usafiri kwa wagonjwa.

Mkurugenzi  Mkuu wa Hosptal ya Rufaa jijini Mbeya Eleuter Samky alishukuru mamlaka hiyo na kueleza kuwa mfumo huo utaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa   kupunguza  vifo na jamii kupatiwa huduma bora licha kuwepo na changamoto ya upungufu wa madaktari bingwa.
“Mfumo huu utatusaidia sana na kuweza kuokoa maisha ya watanzania kwani kutakuwepo na mawasiliano mazuri na kuelimishana njia mbalimbali za kuweza kutoa matibabu kwa wagonjwa wetu hususan magonjwa ya watoto  na mgonjwa sugu yaliyoshindikana kutibika“Alisema.

Mhandisi  na kaimu meneja wa shirika la simu (TTCL) George Mtikila alisema kuwa  mkataba huo  wameingia na mamlaka ya mawasiliano (TCRA) utaanza kutumika kwa wakati na kwamba  lengo kuu ni kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa  katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora zaidi.

Jengo la TTCL Mbeya
Mitambo ya kisasa ya mkonge wa taifa
Hudi iliyokabidhiwa leo
Moja ya wataalam wa mkonge wa taifa Humphrey Ngowi akiwaeleza waandishi wa habari jinsi mtambo huo unavyofanya kazi
 na 

WANANCHI SONGWE MBEYA WAANDAMANA KUTAKA MATUTA





 SISI NI WANAFUNZI, WAZAZI NA WENZETU WAMEPOTEZA MAISHA HAPA KWA KUGONGWA INGAWA KUNA PUNDA MILIA LAKINI MADEREVA HAWAJALI KAULI ILE YA KIBURI SI MAUNGWANA

 JAMANI SISI NI VIONGOZI WA WILAYA HII, TUNAOMBA MTUSIKILIZE

 NAITWA SIMON MKINA KAIMU MENEJA WA TANROAD MBEYA, KWA LEO HAIWEZEKANI LAKINI TUTAJENGA MATUTA



BAADHI ya wananchi wa kijiji cha Songwe wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani Mbeya wameandamana tangu asubuhi kwa ajili ya kuishinikiza Serikali kuweka matuta eneo hilo baada ya kutokea ajali za mara kwa mara eneo hilo.
Wamesema kuwa hatua hiyo wameifikia baada ya kushuhudia ajali mbaya jana ambapo aligongwa mtoto Ezekiel Mwaula wa shule ya Msingi Saruji.
Uongozi wa wilaya ya Mbeya pamoja na Tanroad mkoa wa Mbeya wakiongozwa na Injinia Simon Mkina wamefika kuwaomba wananchi kutuliza hasira, hatimaye wananchi wamekubali kwa kuchagua viongozi watano ii kufuatilia 
utekelezaji.
kwa hisani ya jem mwaisango

No comments: