Wednesday, December 19, 2012

Precision Air Kuanzisha Safari za Mbeya Hivi Karibuni-Stay Tuned

Kampuni ya Precision Air hivi karibuni Kuanzisha Safari za Kwenda Mkoa wa Mbeya kutoka Dar es salaam ambayo itakuwa mara nne kwa wiki...Wakazi wa Mbeya Stay tuned 

KUPITIA UKURASA WA FACEBOOK WA MH.SUGU
NATANGAZA VITA NA MADAKTARI: MARA ZOTE NIMEKUWA MSTARI WA MBELE KWA KUTETEA HAKI NA MASLAHI YA MADAKTARI WETU BUNGENI,LAKINI KWA NIABA YA WANANCHI WA MBEYA LEO NATANGAZA VITA NA MADAKTARI WA HOSPITALI YA RUFAA-MBEYA KITENGO CHA MIFUPA,WAMENICHOSHA KWA RUSHWA AMBAYO IMEKITHIRI KAMA AMBAVYO SIJAWAHI KUONA MAHALI POPOTE.WANANCHI MASKINI WANALAZIMISHWA KULIPA TSHS 300,000/= MPAKA TSHS 500,000/= KWA AJILI YA KUWEKEWA JUST A ‘P.O.P’, AU VINGINEVYO MGONJWA ANAAMBIWA ANA TATIZO KUBWA LINALOHITAJI OPERESHENI NA KWAMBA AENDE PERAMIHO AU MUHIMBILI-DAR…KUNA TAARIFA KUWA KUNA WANANCHI WENGI WAMEKUFA NA WENGINE KUKATWA MIKONO NA MIGUUU KWA KUWA TU HAWAKUWA NA FEDHA ZA KUWAPA MADAKTARI HAO WA RUFAA-MBEYA…SASA KWA KUWA NIMEJARIBU SANA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI AKIWEMO RC MH. KANDORO BILA MAFANIKIO KWA MADAI KUWA HAKUNA USHAHIDI,SASA WAKIENDELEA KUKAA KIMYA NA WATU WETU WANAENDELEA KUTESEKA NA KUFA BASI TUTALAZIMIKA KUTUMIA NGUVU YA UMMA KUJITETEA KAMA KAWAIDA YETU….

 Msanii Sajuki Aanguka Jukwaani- Arusha

  

Msanii wa filamu nchini,Juma Kilowoko akiwa ameshikwa na wasanii wenzake mara baada ya kuanguka jukwaani juzi ndani ya uwanja wa Sheikh Amri katika tamasha la wasanii wa muziki wa kizazi kipya na wale wa filamu.
 
Msanii huyo akitafakari kwa kina mara baada ya kuanguka chini ya jukwaa huku wenzake wakimpa pole.
 
Msanii wa filamu nchini,Juma Kilowoko akiwa ameshikiliwa na wenzake wakimshusha chini ya jukwaa mara baada ya kuanguka alipopewa nafai ya kuwasalimia mashabiki wake




Na: Mahmoud Ahmad,Arusha

  HALI ya msanii  wa filamu nchini,Juma Said Kilowoko maarufu kama Sajuki imeelezwa si ya kuridhisha  mara baada ya msanii huyo juzi kuanguka jukwaani mara baada ya kuishiwa na nguvu wakati alipopewa kipaza sauti kuwasalimia mashabiki waliofurika kumtizama.


Tukio hilo lilitokea juzi jumapili katika tamasha la wasanii wa filamu na wale wa muziki wa kizazi kipya lililofanyika  ndani ya uwanja wa michezo wa Sheikh Amri Abeid  wakati msanii huyo alipopandishwa jukwaani kuwasalimia mashabiki wake.


Mara baada ya msanii huyo kupandishwa jukwaani alipewa kipaza sauti ili aweze kuwasalimia mashabiki wake lakini katika hali ya kawaida alifanikiwa kutamka neno moja tu”ahhh” na kisha kudondoka chini ya jukwaa lakini kabla ya kutua chini alidakwa na wasanii waliokuwa pembeni yake.


Hatahivyo,wasanii hao walimkalisha chini ya jukwaa hilo ili aweze kupumzika na kisha baada ya muda mfupi walimshusha chini ya jukwaaa hilo ili aweze kupata muda wa kupumzika zaidi.


Akihojiwa na gazeti hili muda mfupi mara baada ya kushuka jukwaani Sajuki kwa sauti ya upole alisema kwamba hali yake kiafya si nzuri kwa kuwa hana nguvu na anahitaji matibabu zaidi.


”Kaka hali yangu si nzuri kabisa naumwa sana sijisikii vizuri”alisema Sajuki huku akionekana mnyonge zaidi

 Hatahivyo,baadhi ya mashabiki waliokuwa wamefurika uwanjani hapo walionyeshwa kustushwa na hali ya msanii huyo huku wengine wakiwatupia lawama nzito baadhi ya wasanii wa filamu nchini walioambatana na msanii huyo kwa madai kwamba wanamtumia ili wapate pesa ilhali mwenzao ni mgonjwa.


Wakihojiwa kwa nyakati tofauti mashabiki hao kwa jazba walisema kwamba msanii huyo alipaswa kupewa muda mwingi wa kupumzika kuliko kuambatana na wenzake mikoani kwani hali hiyo inamchosha zaidi.

  “Hawa watu wa Bongo movie ni watu wa ajabu sana huyu mtu anaumwa sana sisi tunashangaa wanaambatana na mtu mgonjwa mikoani wampe muda apumzike na si kumtumia kwa kupata pesa”alisikika shabiki mmoja akiongea kwa jazba
na
 Mwanamke Dereva Wa Basi La Shabiby


NUSRA Maguluko (28) ni msichana jasiri na anayependa kujaribu na kupata mafanikio ya majaribio yake bila woga wala kujali ni aina gani ya kazi anayotakiwa kufanya yeye kama mwanamke na ipi asiyostahili kufanya yeye kama mwanamke.

Ni ujasiri wake hasa ndiyo ulimuwezesha kumfikisha hatua aliyonayo kwa sasa, ambaye ni miongoni mwa wanawake wachache na hasa kwa Tanzania waliopata kuifikia na kujiamini hadi kuwa na ujasiri wa kubeba roho za watu zisizopungua 40 kila safari moja ya kwenda Dodoma ama kotoka Dodoma kuja Dar.
Nusra ni mzaliwa wa Mkoa wa Manyara katika wilaya ya Kiketo, na ni mtoto wa nne kuzaliwa kati ya 12 wa familia ya baba yake mzazi mzee, Maguluko na Elimu yake ni Kidato cha pili tu.
Alimaliza elimu ya Msingi mwaka 1997, katika Shule ya Msingi Matui iliyoko Wilayani Kiteto, baada ya kuhitimu elimu ya msingi alijiunga na elimu ya Sekondari ambayo kwa bahati mbaya hakuweza kumaliza na kuishia Kidato cha pili baada ya kusumbuliwa na maumivu ya kichwa mara kwa mara.
Nusra, alishauriwa na madaktari kupumzika kwa muda wa miaka mitatu bila kusoma ama kuwa akiangalia karatasi nyeupe mara kwa mara, jambo ambalo lilimfanya kuamua kumsumbua Baba yake mkubwa, Hamis Mang'endi aliyekuwa ni fundi wa magari ili amfundishe ufundi na udereva wa gari.
Baada ya kumsumbua sana baba yake mkubwa, kwa kuwa akiripoti katika gereji yake kila asubuhi na kushinda hapo huku akimfuatilia kila analofanya katika magari, Mzee Hamis, baada ya kuona kuwa Nusra alikuwa na moyo wa kweli wa kujifunza ufundi, aliamua kuanza kumfundisha ufundi hatua kwa hatua.
  Baada ya kumudu kidogo kishika Spana, Mzee Hamis, mwaka 1998, alianza kumfundisha udereva, tena kwa kumfundishia katika gari aina ya Comb Volkswagen, ambapo baada ya miezi sita tu Nusra tayari alishamudu kuendesha gari na kutulia barabani.
Nusra alipomudu kufanya vurugu za barabarani, alikabidhiwa na baba yake mzazi, Canter ya Tani 3 na robo ili aweze kufanyia kazi ya kubebea mizigo, huku akikodishwa ambapo alifanya kazi hiyo kwa muda wa miaka miwili.

Hatimaye mwaka 2001, Nusra, aliamua kuachana na kazi ya kuendesha Canter ya kubeba mizigo na kuamua kuanza kazi ya kulima kwa Treka, ambapo alikuwa akikodishwa na wakulima na alimudua kulima hadi Heka 10 kwa siku kwa ujira wa Sh. 10, 000 kwa kila heka moja.






Mwaka 2003, Nusra alianza kuendesha Min Bus, huku akiwa na Leseni ya Clac C baada ya wakati huo kudanganya umri ili aweze kupata uhalali ya kufanya kazi anayoipenda ya udereva.
Alifanya kazi hiyo ya kutoa huduma usafiri kwa abiria kutoka Wilaya ya Kiteto kwenda Vijijini hadi mwaka 2006, alipokabidhiwa Basi aina ya Fuso lenye uwezo wa kubeba abiria 40, nakutoa huduma hiyo ya usafirishaji wa abiria kutoka Wilaya ya Kiteto hadi Dodoma, kazi aliyoifanya hadi mwaka 2011.
Baada ya kuchoshwa na njia za Vijijini na kile alichodai kuaua kutafuta maslahi zaidi, Nusra, aliamua kuvaa, Mbunge wa Gairo, he Shabiby, na kumuomba kazi jambo ambalo lilimshangaza na kumuhoji kama anaweza kweli kuendesha gari kubwa tena la abiria.
''Baada ya kuniuliza swali hilo, mimi nilimjibu Mheshimiwa samahani wewe nisaidie unipe kazi, halafu ndiyo utaniona nikiwa kazini kama naweza ama siwezi, kwani najiamini na ndiyo maana nimekuja kwako''. alisimulia Nusra
Baada ya maongezi marefu ya maswali na majibu juu ya ujasiri wa Binti huyo, aliyeonekana mdogo akiwa na maelezo ya mambo makubwa, Mhe. Shabiby, aliamua kumwajiri, Nusra ambapo hadi sasa anapiga mzigo katika kampuni hiyo ya Shabiby, akiburuza Basi linalofanya safari zake Dar-Dom.
Hivi Sasa Binti huyo, anandoto za kufungua Chuo cha Mafunzo ya Udereva kwa wanawake, akiwa na lengo la kuwafikisha mbali wanawake wenzake ili waweze kuwa na ujasiri wa kuendesha magari makubwa na si gari ndogo pekee.
Kwa hatua hiyo sasa Nusra, ameanza kusaka wafadhili, ili aweze kutimiza ndoto zake hizo, ambapo amewamba wadau mbalimbali pamoja na Serikali kujitokeza kumsapoti, ili kufanikisha kufungua chuo hicho chenye lengo la kuwainua Kinamama.

No comments: