Tuesday, January 29, 2013

chadema waanza rasmi kutekeleza sera ya majimbo


 

  Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akifungua mkutano huo

 Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akimkabidhi kadi ya uanchama wa chama hicho aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Bara wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Clemence Tara baada ya kujiunga na chama hicho.

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepitisha mpango mkakati wake wa kuelekea kushika dola mwaka 2015 kwa kumega madaraka ya makao makuu katika kanda kumi. Maazimio hayo yalipitishwa na Kamati Kuu (CC) juzi kwa agenda moja kubwa ambayo ni kupitisha mpango mkakati wa mwaka 2013 ili kushinda chaguzi zote kuanzia serikali za vitongoji, vijiji na mitaa mwaka 2014 na Uchaguzi Mkuu 2015.


Akizungumza na wajumbe wa kikao cha dharura cha Baraza Kuu jana, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema kuwa mpango mkakati huo umelenga kufanya mabadiliko ya uongozi kuanzia ngazi ya taifa kwenda katika majimbo na kukipanga upya chama hicho kwa mustakabali wa taifa. “Mtakumbuka kwamba wakati tunakianzisha chama chetu, tulizungumzia sera ya majimbo na kuainisha kazi zake…sasa tumeanza kupanga kazi zenyewe kwa kugawa majukumu katika kanda kumi. “Tunataka tuishi vile tunavyosema kwa kuwa katika miaka mingi ya kuwa chini ya uongozi wa serikali ya CCM, wananchi wamekuwa wakiamriwa mambo yao na kundi dogo la watu wanaojikusanya sehemu moja ya nchi, hilo kwetu si mfano bora wa uongozi,” alisema.

Mbowe aliongeza kuwa katika miaka 20 ya kuhimili misukosuko ya kisiasa chama hicho kimejifunza mengi na sasa kiko tayari kushika dola ndio maana wameanza kugawa majukumu kwa wananchi kupitia uongozi wa kikanda. Alisema kuwa wamejiandaa kwa mashambulizi ya aina zote na sasa jukumu kubwa la kila kanda litakuwa ni kuhakikisha kila mwananchi anaiunga mkono CHADEMA katika eneo atakalokuwa.
Mwenyekiti huyo alitaja kanda hizo na mikoa husika kuwa ni
  1. Kanda ya Ziwa Magaharibi (Mwanza, Geita, Kagera),
  2. Ziwa Mashariki (Mara, Simiyu, Shinyanga),
  3. Ziwa Magharibi (Kigoma, Tabora, Katavi)
  4. Kati (Singida, Dodoma, Morogoro).
  5. Nyanda za Juu Kusini (Mbeya, Ruvuma, Iringa),
  6. Kusini (Lindi na Mtwara),
  7. Mashariki (Pwani, Dar es Salaam na Tanga),
  8. Kaskazini (Kilimanjaro, Manyara, Arusha),
  9. Pemba na Kanda ya Unguja.

Mbowe alisema katika kuhakikisha vikosi hivyo vinafanya kazi zake vizuri, kila kanda itajengewa ofisi, kununuliwa magari, pikipiki na vifaa vyote vya ofisini na za mikutano. “Lengo la mkakati huo pia ni kuhakikisha CHADEMA inasimama katika chaguzi zote bila kupingwa…tunataka CCM ndiyo ipingwe katika chaguzi na hili tutalifanikisha,” aliongeza.

Katika suala zima la Muungano, Mbowe alisema uwepo wa serikali tatu hauepukiki kwa kuwa tayari Tanzania Visiwani wameshakuwa na serikali yao hivyo ni jukumu la Watanzania Bara kupata serikali ya Tanganyika na kisha kuwepo na serikali ndogo ya Muungano. Alisema serikali tatu inawezekana ikiwa viongozi wataacha unafiki wa kusema muungano utavunjika huku tayari wakitoa uhuru wa Zanzibar kuwa na Rais, bendera na wimbo wao ya taifa. Tunawaunga mkono wenzetu Wazanzibar katika kupigania uhuru kamili na kwa sasa sisi ndio tunaoonekana wa ajabu kushindwa kuuliza serikali ya Tanganyika,” alisema.

Mbowe pia aligusia tume huru ya uchaguzi akisema serikali ihakikishe Watanzania wanapata tume hiyo kwa kuwa tayari hata viongozi wa chombo hicho wameshatoa maoni na kutaka wapewe uhuru wa kufanya kazi.
Alisema serikali kama inafikiri kuwa CHADEMA itaingia katika uchaguzi wa 2015 ikiwa chini ya tume iliyopo sasa watakuwa wanajidanganya na badala yake watalazimisha upatikanaji wa tume hiyo.

 

SHITAMBALA KUONGOZA MAANDAMANO WANANCHI 5000 KUMVAA KANDORO KUPINGA KUHAMISHWA

MJUMBE wa Halmashauri kuu CCM Taifa  Bw.Sambwee Sitambala



,asema  yatakuwa ya amani bila  Vurugu
,asema  sera ya  CCM ni kutetea  wananchi
MJUMBE wa Halmashauri kuu CCM Taifa  Bw.Sambwee Sitambala  anatarajiwa kuongoza  maandamano  ya amani  ya wananchi  zaidi ya  5000 wa  mtaa  wa Gombe  kusini  kwenda  kwa mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwa ajili ya kupinga amri ya kutaka  kuwahamisha  kwenye  nyumba zao na eneo hilo kupewa  watu wengine.

Akizungumza   na waandishi wa habari baada ya kwisha  kwa mkutano wa wananchi hao diwani wa Kata ya  Itezi  jijini Mbeya  Bw.Frank Mayemba ambaye  pia ni mjumbe wa Mkutano  mkuu Taifa  CCM alisema kuwa  katika  maandamano hayo  watashirikiana  na  Bw.Shitambala  kuongoza   hadi kufika kwa mkuu wa Mkoa.

Alisema kuwa wananchi hao ambao zaidi ya asilimia  90 ni wanachama wa CCM walifikia  hatua hiyo baada ya kuona  hawasikilizwi  katika kilio chao ambacho wamekuwa wakitoa kwa Jiji la Mbeya kuwataka kutowagusa kwa kuwa walipewa maeneo hao kihalali baada ya kubadilishwa  matumizi yake  ya awali ambayo yalikuwa viwanda.

Bw.Mayemba alisema kuwa  kutokana na hali hiyo wamedhamiria  kudai haki yao kwa mkuu wa Mkoa ambaye  ndiye msimamizi wa Halmashauri zote Mkoa wa Mbeya  ambapo kutokana na hekima  yake  walisema kuwa wana imani kuwa atawasaidia kuwasikiliza  ombi lao na kusitisha  zoezi hilo ambalo ni  athari kubwa kwa wananchi hao.

Alisema kuwa  wananchi hao baada ya kupewa viwanja hivyo  wamekaa katika eneo hilo kwa zaidi ya miaka  20 na hivyo kisheria kuwa  wamiliki haklali wa  maeneo haio wasio takiwa kubughudhiwa  na hivyo kushangaa wakati wote wanapoambiwa kuwa watahamishwa na  maeneo yao kupewa  watu wengine.

"sisi tunasema    kama viongozi wa chama   hakika hatutakubali  suala  hili kwa kuwa ni wamiliki  halali wa eneo hili  na hivyo kama wanataka kugawa  basi tuweke mkataba ambao  watatugawia  sisi na wala si wengine  kama wanavyotaka kufanya  sasa  hawa  wataalam."alisema.

Naye  Bw.Shitambala ambaye pia  ni Kaptain wa jeshi mstaafu na mwanasheria  maarufu alisema kuwa  ataongoza  maandamano hayo ya amani hadi kwa mkuu wa Mkoa   na hakuna vurugu itakayotokea  kwa kuwa  CCM ni chama kinachohamasisha  amani na utulivu na  hivyo wao wataonesha  mfano.

Kada huyo wa CCM ambaye awali alikuwa mwenyekiti wa CHADEMA kabla   ya kumamia  chama hicho alisema kuwa wataomba vibali polisi kwa ajili ya kulinda maandamano  hayo na kamwe hawatachoma  barabara kama wanavyofanya  wengine  ambnapo watapata nafasi ya kumweleza  mkuu wa Mkoa   hoja  zao zinazopinga  kuondolewa katika  eneo hilo .

Alisema   yeye kama  mkazi aliyejenga  eneo hilo ni dhambi kubwa kuona  wananchi wenzake na yeye akiwemo wakinyanyaswa   na hivyo kupelekea  hasira kali kwa chama  hali ambayo alisema kuwa katika  mkutano mkuu wa chama  na  vikao mbali mbali wamekubaliana kupinga  hali hiyo  na kuwapa haki yao wanachama .
Kwahisani ya Charles Mwakipesile Mbeya
 
 
 

lugarawa kujengewa chuo cha veta

DEOO7 05345

Mh Deo akimuonyesha eneo la ujenzi wa Chuo Mkurugenzi mkuu veta Ndg. Zebadieli Mushi lenye ukubwa wa hekali sabini.

DEOOE1 fd06f
 Mh Deo akimkabidhi zawadi ya kuku Mkurugenzi mkuu wa Vyuo vya veta Tanzania
DEOOE2 033be
Mkurugenzi wa Vyuovya veta nchini akiongea na wananchi wakijiji cha Ludewa juu ya ujenzi wa chuo cha veta katika kijiji chao kwaniaba ya wana Ludewa.
DEOOE 02ccc
Mh Deo  Filikunjombe akiongea na wananchi wa kijiji cha shaulimoyo  walipo ijiwa na mkurugenzi wa vyuo vya veta Tanzania kuwathibitishia ujenzi wa chuo cha veta wilayani Ludewa.Ndg.Zebadieli Moshi


SHAHIDI AIOMBA MAHAKAMA KUMWONDOA NCHINI MWEKEZAJI KAPUNGA

Na Venance Matinya
KESI inayowakabili Wawekezaji wa shamba la Kapunga Wilaya ya Mbarali Mkoani hapa imechukua sura mpya baada ya mashahidi kujitokeza na kuiomba mahakama iwaamuru wawekezaji hao kuondoka.
Akitoa ushahidi wake mbele ya hakimu Michael Mtaite wa mahakama ya Hakimu mkazi Mkoa wa Mbeya, Shahidi Daison Tonyela(50) Mkazi wa Kijiji cha Kapunga akiongozwa na Mwendesha mashtaka wa Serikali Archiles  Mulisa alidai mahakamani hapo kuwa tangu Mwkezaji apewe eneo hilo hana uhusiano mzuri na wanakijiji.
Alisema tangu mwekezaji huyo apewe eneo hilo amekuwa akiwanyanyasa wakazi wa Kapunga kwa kuwafungia njia na kubomoa matofali na madaraja kitu kinachoonesha Mwekezaji kutotoa ushirikiano na wanakijiji.
Alidai Mahakamani hapo kuwa kutokana na Mwekezaji huyo kumwaga dawa inayodaiwa kuwa sumu katika mashamba hayo  tayari wameingia hasara kubwa kutokana na kukosa mazao hali iliyopelekea kushindwa kuishi kutokana na njaa.
Aliongeza kuwa yye binafsi amepata hasara iliyopelekea kushindwa kuwapeleka shule watoto wake kutokana na kukosa fedha ambazo angezipata baada kuuza mpunga ambao angekuwa amevuna kabla ya kuharibiwa na mwekezaji huyo.
Shahidi huyo anayedai kuharibiwa kwa shamba lake lenye ukubwa wa ekari 4 ambalo angeweza kuvuna zaidi ya gunia 20 kwa kila Ekari  huku gunia moja angeuza kwa Shilingi Laki mbili.
Aidha aliiomba mahakama hiyo kumwamuru mwekezaji huyo kuwalipa fidia wananchi kutokana na hasara waliyoipata ikiwa ni pamoja na kufukuzwa katika eneo hilo na kuwaachia wananchi.
Hata hivyo kesi hiyo iliahirishwa hadi  Machi 5, Mwaka huu ambapo mashahidi wengine wataendelea kutoa ushahidi wao hali iliyokubaliwa na upande wa utetezi chini ya wakili Vicent Mtavangu.
Awali Wawekezaji hao  watatu  raia wa Afrika kusini walifikishwa mahakamani  kwa kosa  la kumwaga sumu kwenye mashamba ya mpunga ya  wakulima 153 wilayani Mbarali Mkoani Mbeya.
 Mashtaka ya awali yalisomwa mbele ya hakimu Mfawidhi wa mahakama ya Wilaya ya Mbeya mjini Girbeti Ndeuluo, na mwendesha mashtaka mwanasheria wa serikali, Achiles Murisa ambaye alidai kosa hilo  lilitokea January 12/2012.
Achiles aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni WalderVeemad, Segeer Backer na Andress Dafee ambapo wote ni wafanyakazi wa kampuni ya Kapunga rice.
Alisema, watuhumiwa wamefanya kosa hilo wakati wakipiga dawa katika mashamba yao kwa kutumia chombo cha usafiri wa anga (ndege).
Alisema, dawa hiyo inasemekana  ilipitiliza hadi kwenye mashamba jirani na kufanya uharibifu kwenye mazao yaliyokuwa shambani.



CHUNYA MBEYA

Wajawazito Mbeya wasukumana kwa wakunga wa jadi kujifungua

 MJAMZITO AKIWA KWA MKUNGA AKISUBIRI KUJIFUNGUA WILAYANI CHUNYA MKOANI MBEYA.

  by Gordon Kalulunga 
 
KATIKA vijiji vya Totowe na Mbuyuni hakuna serikali. Ni utawala binafsi. Huku ni katika wilaya ya Chunya mkoani Mbeya. 

Kwani Sera ya Afya ya mwaka 2007 inasema wajawazito kote nchini watapata huduma bure kabla na wakati wa kujifungua. Lakini hayo hayaonekani katika vijiji hivyo. 

Pamoja na kuwepo zahanati katika kata ya Totowe, wanawake kwa mamia wanasukumana wakitafuta kupewa huduma ya uzazi kwa wakunga wa jadi ambao serikali haijawatambua. 

Hilda Said Kawinga (80), mkazi wa kijiji cha Malangali mpoa kata ya Totowe ni mkunga kwa miaka 30. Anaishi katika banda la vyumba viwili ambavyo anaita sebule na chumba cha kulala. 

Kwa umri wake Hilda hatetemi mikono. Kwa rekodi za sasa, ameweza kusaidia wajawazito 70 kujifungua katika kipindi cha miezi 10 (Januari hadi Oktoba mwaka 2012). 

Kijiji cha Totowe kipo umbali upatao kilometa zaidi ya 100 kutoka Chunya mjini. Hapa ndipo wajawazito wanaita kwa jina la kirafiki, “nyumbani salama,” kutokana na kujifungua salama na kuondoka kwa kicheko na watoto wao mikononi. 

Hapa ni nyumbani kwa Hilda. Pale kuna mafiga Ndilo jiko. Kuna kuni. Hapa kuna vyombo vya kupikia. 

Alipokaa mwandishi kuna mkeka na ndiyo sehemu inayotumika wakati wa kusaidia wajawazito kujifungua. Wajawazito wakija, basi hakuna mgeni. 

Bibi Hilda hana mkasi. Hana vyombo vya kisasa kama vya zahanati, kituo cha afya au hospitali kwa huduma za uzazi. Hana kitanda. Hana godoro wala mipira ambako wajawazito hujilaza wakati wa kujifungua. 

Lakini hapa ndipo wanawake wanamiminika kwa huduma ya uzazi na wanaondoka na watoto wao salama. 

Akiongea kwa sauti nyembamba anasema, “Ninamworodhesha kila anayejifungulia hapa katika daftari langu. 

Nafanya hivi ili kuisaidia serikali kupata takwimu endapo watazihitaji; ingawa tangu nimeanza shughuli hakuna kiongozi wa serikali aliyewahi kuja kuangalia wala kuuliza kuwa ninafanyaje kazi.” 

Hilda anajigamba kwamba alipata ujuzi kutoka kwa mama na kuongeza, “…kwa watoto wangu sikuwahi kujifungulia hospitali; ilikuwa kazi ya mama. Hapo ndipo nilijifunzia kazi tena bila vifaa vya kisasa. Sharti kuu ni kuwa msafi tu.” 

Hivi sasa anasema anapokea wajawazito 10 kwa mwezi na kila mmoja anaondoka kwa kicheko. Tangu aanze kazi hii, hakuna mtoto wala mama aliyepoteza maisha akiwa mbele yake. 

Bibi Hilda ni kama mkunga mwingine Agripina Frederick Sikanyika wa kijiji cha Mbuyuni wilaya ya Chunya. Tofauti ni kwamba Agripina ametenga nyumba rasmi kwa wajawazito kulala na kujifungulia. 

Agripina, mwenye umri wa miaka 37 anafahamika sana kwa jina la “Mama Namwinji.” Anasema imemlazimu kuwaachia nyumba wajawazito wanaokwenda kwake kwa ajili ya kusubiri kujifungua kutokana na idadi yao kuongezeka kukicha. 

agripina Kulia ni Mkunga Agripina Sikanyika akimkabidhi mtoto mmoja wa wajawazito waliotoka kujifungua nyumbani kwake  
Katika kipindi cha miezi 10, Januari hadi 9 Oktoba 2012, Mama Namwinji amehudumia wajawazito 212. Alianza huduma kwa wajawazito mwaka 2000. 
Kwa Mama Namwinji, idadi ya waliojifungulia mikononi katika kipindi hicho ni rekodi. Mwaka 2011 ni wajawazito 98 waliojifungulia kwake.
kwa-mkunga
PICHA: Mwonekano wa Nyumba inayotumika kujifungulia wajawazito kwa Mkunga Agripina Mama Namwinji.
 
Kitu kimoja kimemkwaza Mama Namwinji.

Watoto wawili kati ya 212 waliozaliwa mwaka jana walikuwa na ulemavu. Ilikuwa Septemba 15, 2012 wakati mwanamke mmoja alipojifungua mtoto mwenye sikio moja, mguu mmoja, mdomo na pua vikiwa vimeungana. Mtoto huyo alifariki muda mfupi baada ya kuzaliwa.
Ambulance-punda
Mkokoteni unaokokotwa na Punda hutumika pia kubebea baadhi ya wajawazito kwenda katika kituo cha afya cha Mbuyuni na kwa Mkunga wa jadi Mama Namwinji
 
Siku iliyofuata, Septemba 16, 2012 alizaliwa mtoto aliyekuwa na kichwa kikubwa chenye umbile la kichwa cha ng'ombe lakini mwenye kiwiliwili cha binadamu. 

Mkunga amesema hawezi kutoa majina ya waliojifungua “watoto wa ajabu” kwa alichoeleza kuwa ni siri ya wazazi wao na aliyekuwepo.

namwinji
Mama Namwinji akionesha mkeka aina ya Msengele anaotandika wanapojifungulia wajawazito wanapofika kwake
Changamoto anazokabiliana nazo Agripina hazina tofauti na zile za Bibi Hilda na wakunga wengi wa jadi nchini. Hana kitanda, hivyo huwalaza wajawazito kwenye mkeka wa matete (maarufu kama Msengele). 

“Hii ni hatari kwa sababu wanaweza kupata magonjwa hasa kipindi cha masika,” anasema Agripina.


Kama Hilda, Agripina naye anaorodhesha wajawazito katika daftari maalum, ingawa yeye anachukua hatua zaidi kwa kuangalia kadi za kliniki na kuzijaza mara wanapojifungua. 

Anasema pamoja na kuwepo kwa kituo cha afya jirani cha Mbuyuni (Chang’ombe), lakini wajawazito wengi wanakimbilia kwake kwa madai kwamba wakienda hospitalini wanaweza kufanyiwa upasuaji. 

“Wapo ambao walikwenda hospitalini wakafanyiwa upasuaji, lakini walipofika hapa katika uzazi wao mwingine wameendelea kujifungua bila upasuaji,” anasema. 

Kama ilivyo kwa Bibi Hilda, Agripina naye anasema huwa hatozi kiwango chochote cha fedha kabla na baada ya mjazito kujifungua, ingawa wote wanakiri kwamba akinamama au ndugu zao “…huleta chochote walichojaliwa kama asante.” 

“Wanawake wengi Tanzania wanakufa kipindi cha ujauzito au baada ya kujifungua ndani ya siku 40. Hii ni hatari sana,” anasema Dk. Magoma akiwa anafundisha waandishi wa habari Tanzania wanaobobea katika habari za afya ya uzazi akiwemo mwandishi wa makala haya na kuongeza kuwa, kwa upande mwingine, watoto wanakufa ndani ya kipindi cha miezi sita baada ya kuzaliwa huku akibainisha kwamba asilimia 57 ya wanawake wote wanaojifungua hawahudhurii kliniki. 

Mtafiti wa Masuala ya Afya nchini, Dk. Kahabi Ganka Isangula, anasema zaidi ya wanawake 300,000 wanafariki kila mwaka wakati wa kujifungua au wakati wa kipindi cha ujauzito kutokana na sababu mbalimbali huku 800 kati yao wakifa kwa “matatizo yanayoweza kuzuilika.” 

Kati ya vifo hivyo, asilimia 99 hutokea katika nchi zinazoendelea hasa vijijini kwa watu maskini ambapo wajawazito wengi hutokwa na damu nyingi wakati wa kujifungua. 

Anashauri wanawake wajifungulie katika vituo vya afya akieleza kuwa moja ya changamoto kwa huduma za wajawazito, “ni kutoa kondo la nyuma ambalo linahitaji utaalamu.” 

Hata hivyo, Dk. Isangula hapingi matumizi ya wakunga wa jadi katika kuhudumia wajawazito. Anasema, “…hakuna ubaya wowote kwa wanawake kujifungulia kwa wakunga wa jadi, tatizo linakuja katika upatikanaji wa vifaa vinavyomwezesha mkunga wa jadi kumhudumia mama mjamzito katika hali ya usalama.” 

Naye Mratibu wa Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto kutoka hospitali ya mkoa wa Mbeya, Prisca Butuyuyu, anasema wanatambua kuwepo kwa wakunga wa jadi na kwamba watoto wote wanaozaliwa huko wanawahesabu kuwa wanazaliwa nyumbani kwa sababu hakuna mwongozo wa wizara unaowatambua wakunga wa jadi. 

Sera ya Afya ya mwaka 2007 inaagiza kwamba wajawazito wapewe huduma bure katika sehemu zote za huduma ya afya. Je, hawa wanaojifungulia kwa Hilda na Agripina wanapata huduma gani au huduma inayotajwa haiwahusu? 

Je, kama wajawazito hawapati huduma, wakunga wanasaidiwa vipi au wanawezeshwa vipi na serikali ili wafanye kazi yao kwa ustadi na weledi ambao tayari umedhihirishwa kwa kuhudumia mamia kwa mamia ya wajawazito waliojifungua salama?

Majibu kwa maswali haya yako mikononi mwa serikali. 
Mungu ibariki Tanzania

MBEYA

Serikali yasikia kilio cha watoto
Na, Gordon Kalulunga, Mbeya
SERIKALI imesikia kilio cha wanafunzi wa shule za Msingi hasa darasa la kwanza na la pili katika shule za serikali kwa kuwapunguzia masomo.
Wanafunzi hao wamerejeshewa mfumo unaowasaidia kujua kusoma na kuandika ujulikanao kwa jina la KKK yaani kusoma kuandika na kuhesabu.
Uchunguzi uliofanywa na Mtandao wa www.kalulunga.blogspot.com ambao uliwahi kulipoti kuhusu mlundikano wa masomo kwa wanafunzi hao hali iliyokuwa inachangia wengi wao kuhitimu darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika.
Masomo yaliyokuwa yakifundishwa kwa wanafunzi wa madarasa hao kutokana na mfumo wa kila waziri anayekuwepo madarakani kubadili mitaala bila kushauliana na walimu ni pamoja na somo la Kiingereza, Kiswahili, Hisababti, Stadi za kazi, Tehama, Haiba na michezo na Sayansi.
Baadhi ya walimu waliohojiwa wamethibitisha kurejeshwa kwa mfumo huo wa KKK katika shule za Msingi tangu shule zilipofungua Januari 14, mwaka huu.
Hata hivyo uchunguzi umebaini kuwa bado kuna mfumo mbaya wa elimu hapa nchini ambapo wanafunzi wanafundishwa kwa Lugha ya Kiswahili lakini wakati wa kuajiliwa wanasailiwa kwa Lugha ya Kiingereza.


KUNDI LA WANANCHI WAFANYA VURUGU NA UHARIBIFU MTAA WA ISENGO KATA YA IZIWA. MBEYA

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA ATHUMANI DIWANI ENEO LA TUKIO

WANAKIJIJI ISENGO IZIWA WAKIWASIKILIZA WANAUSALAMA HUKU WAKIWA NA SIRAHA ZAO ZA JADI

CHANZO CHA MAJI IZIWA

MAMA WA KISAFWA AKIWA AMEFICHA PANGA


SIRAHA ZA JADI ZILIZOKAMATWA NA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA

MNAMO TAREHE 28.01.2013 MAJIRA YA SAA 11:00HRS MAAFISA WA HIFADHI YA MALIASILI NA UTALII  WAKIONGOZWA NA MENEJA WA HIFADHI HIYO KASMIR S/O NGOWI NA AFISA MISITU WA JIJI  LYOWA S/O WAYANGA KWA KUSHIRIKIANA NA  ASKARI POLISI WALIOKUWA KATIKA WALIFIKA KATIKA MTAA WA ISENGO KATA YA IZIWA KWA AJILI YA KUENDELEA NA OPERESHENI YAO YA KUWAONDOA WATU WALIOVAMIA NA KULIMA  NDANI YA HIFADHI YA SAFU YA MLIMA MBEYA [MBEYA RANGE FOREST RESERVE] ENEO AMBALO NI CHANZO CHA MAJI NA VIUMBE HAI ZOEZI LILILOANZA TANGU TAREHE 28.12.2012.
 HATA HIVYO KABLA ZOEZI HILO KUANZA KUNDI KUBWA LA WANANCHI WA ENEO HILO WAPATAO 400 WAKIWA NA SILAHA ZA JADI WALIFIKA ENEO HILO WAKIWA WAMEJIANDAA  KUFANYA VURUGU WAKISHINIKIZA KUTOFANYIKA KWA ZOEZI HILO. KATIKA VURUGU NDOGO ILIYOTOKEA  YOHANA S/O MDEWA,MIAKA 54,MSAFWA,MWANACHAMA WA ASASI YA KIRAIA YA KUTUNZA MAZINGIRA  MKAZI WA KIJIJI CHA IHOMBE , ALIJERUHIWA KWA KUKATWA PANGA KICHWANI , WAKIDAI NDIYE MSALITI ALIYEWALETA WATU HAO ,HIVYO POLISI WALIMUOKOA NA KUMHIFADHI KATIKA OFISI YA MTENDAJI KATA.
 PIA KATIKA VURUGU HIZO KULITOKEA UHARIBIFU KATIKA GARI STJ 1830 MALI YA WAKALA WA HIFADHI YA MISITU NYANDA ZA JUU KUSINI  KWA KUPASUKA WIND SCREEN YA MBELE NA SIGHT MIRROR YA KUSHOTO  NA MAGARI MENGINE YA IDARA HIYO STJ 1821 NA STJ 1832 KURUSHIWA  MAWE PIA  KUBOMOA MADARAJA MAWILI  YALIYOPO KIJIJINI HAPO. KUFUATIA HALI HIYO  KIKOSI CHA KUTULIZA GHASIA MKOA WA MBEYA  WALIFIKA ENEO HILO HATA HIVYO WANANCHI WALITAWANYIKA KWA KUKIMBIA. POLISI  KWA KUSHIRIKIANA NA VIONGOZI WA ENEO HILO WALITOA WITO KWA           WANANCHI KUTOJICHUKULIA SHERIA MKONONI AMBAPO WALIKIRI NA KUDAI HAWAKUELEZWA JUU YA ZOEZI HILO NA WAMEAHIDI KUJENGA  WAO WENYEWE MADARAJA WALIYOKUWA WAMEBOMOA.
UONGOZI WA SERIKALI YA WILAYA YA MBEYA CHINI YA MKUU WA WILAYA DR NORMAN SIGALA NA MSTAHIKI MEYA WA JIJI ATHANAS KAPUNGA NA VIONGOZI MBALIMBALI WAKIWEMO  MHE DIWANI NA MTENDAJI  KATA YA IZIWA KATIKA KIKAO KILICHOFANYIKA BAADAE WAMEKUBALIANA KUWA WATU WOTE WALIOVAMIA ENEO HILO WAHAKIKISHE WAMEHAMA KABLA YA MWEZI AGOST – 2013.  KWA SASA HALI IMEREJEA KUWA SHWARI KIJIJINI HAPO.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANAENDELEA KUTOA WITO KWA JAMII KUACHA MARA MOJA TABIA YA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI NA BADALA YAKE WAHESHIMU NA KUTII SHERIA PASIPO KUSHURUTISHWA. PIA ANAZIDI  KUSISITIZA KUWA MAZUNGUMZO NDIO  NJIA MUHIMU NA SAHIHI YA KUWASILISHA MALALAMIKO/KERO BADALA YA FUJO NA VURUGU ZISIZOKUWA NA TIJA KWANI ZINAWEZA KULETA MADHARA  NA KURUDISHA NYUMA MAENDELEO YAO. KAMANDA AMEAHIDI KUWA WALIOVUNJA SHERIA KWA KUMJERUHI YOHANA S/O MDEWA NA KUFANYA UHARIBIFU WA MADARAJA WATAFUATILIWA ILI SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
Signed By,
[DIWANI ATHUMANI – ACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

 

 

 

ABDURAHMAN KINANA AONGOZA SEKRETARIETI YA YA CCM KUKAGUA MRADI WA UJENZI DARAJA LA MTO MALAGARASI MKOANI KIGOMA

8Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi ndugu Abdurahman Kinana akimsikiliza Meneja mradi wa ujenzi wa Daraja la mto Malagarasi Bw. Jung- Sik Yu kutoka nchini Korea wakati akikagua ujenzi wa Daraja  hilo Mkoani Kigoma jana katika ziara ya Wajumbe  Sekretarieti ya CCM wanaotembelea mkoa huo na kukagua miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuongea nao kusikiliza kero za wananchi.
Daraja la Malagalasi ambalo linagharimu kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 78 za Tanzania lina urefu wa mita 275 na linatarajiwa kukamilika Oktoba 16 mwaka huu ambapo linatarajiwa kuzinduliwa na Rais Jakaya Kikwete, Kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa Halmashauri Kuu Itikadi na uenezi wa CCM.
6Meneja Mradi wa Ujenzi wa daraja la Malagarasi Bw. Jung Sik- Yu akimuonyesha Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana jinsi eneo hilo lilivyosumbua wakati wa utekelezaji wa mradi huo kutokana na kuwa na majimaji wakati mwingi.
20Wananchi wa Uvinza wakiwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana katika mji huo na kuhutubiwa na Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana.
IMG_2173Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana akihutubia wananchiwa Tarafa ya Nguruka mkoani Kigoma.
19Wananchi wa Tarafa ya nguruka wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana hayupo pichani wakati wa mkutano huo
17 
 Msanii Dokii akiimba katika mkutano huo uliofanyika tarafa ya Nguruka.

16 
Katibu wa Halmashauri Kuu Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha- Rose Migiro akicheza na mmoja wa wazee wa tarafa ya Nguruka wakati Sekretarieti hiyo ilipopokelewa kijijini hapo.

13Katibu wa Halmashauri Kuu Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro akiongozana na Asha Baraka Mjumbe wa NEC CCM wilaya ya Uvinza mara baada ya kuwasili katika tarafa ya Nguruka jana.
14Wananchi wakipokea Wajumbe Sekretarieti ya CCM kwa furaha wakati ilipowasili kijijini hapo.

15Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akipiga ngoma sambamba na wasanii wa  kikundi cha ngoma cha Nguruka.

10
Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana akikagua kipande cha Barabara kinachounganisha madaraja hayo wakati alipokagua ujenzi wa Daraja la Mto Malagarasi mkoani Kigoma jana, aliyeongozana naye ni Meneja Mradi Bw. Jung-Sik Yu.

12
 Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana akizungumza jambo na Bw. Kadudu Issa Tawfiq mkazi wa eneo hilo ambaye alielezea faida za ujenzi wa daraja hilo katika maisha ya watu wa Kigoma.
3Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana akiongoza wajumbe wa Sekretarieti  ya CCM wakati walipokagua ujenzi wa Daraja la mto Malagarasi jana.


5 
Hiki ni moja ya vipande vya daraja la mto Malagarasi chenye urefu wa mita 200

No comments: