Saturday, January 26, 2013

TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM MWAKA 2005 HADI 2012 KWA WANANCHI WA WILAYA YA RUNGWE MKOANI MBEYA




MOSES MWIDETE AKIONGEA KWA KUWAKARIBISHA WANANCHI NA VIONGOZI MBALIMBALI KUMSIKILIZA MKUU WA WILAYA AKIELEZA MAFANIKIO NA CHANGAMOTO  ZA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM

MKUTANO ULIFANYIKA KATIKA UKUMBI WA MWANKENJA KATIKA JENGO LA HALMASHAURI YA RUNGWE

BAADHI YA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA MBEYA WAKIWA TAYARI KWA KAZI YA KUSIKILIZA NINI YALIYOFANYIKA WILAYANI RUNGWE IKIWA NI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM KWA WANANCHI
ALLY MWAKALINDILE MWENYEKITI WA CCM WILAYA YA RUNGWE YENYE HALIMASHAURI MBILI  BUSOKELO NA RUNGWE AKIONGEA NA WANANCHI , WATENDAJI WA BUSOKELO NA RUNGWE NA WAANDISHI WA HABARI WA MKOA WA MBEYA KABLA HAJAMKARIBISHA MKUU WA WILAYA YA RUNGWE KUELEZA MAFANINIKIO YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM

WATENDAJI WA HALMASHAURI YA BUSOKELO NA RUNGWE WAKISIKILIZA KWA MAKINI
 
MAKADA WA CCM NA MADIWANI WILAYANI RUNGWE WAKIMSIKILIZA KWA MAKINI MKUU WA WILAYA


MKUU WA WILAYA AKIONGEA KWA MSISITIZO

MKUU WA WILAYA CHRISTIN MEELA NA MEZA KUU WAKITOKA UKUMBINI BAADA YA KUMALIZA KUONGEA NA WAANDISHI WA HABARI. FUATANA NAMI ILI KUJUA MAMBO YALIYOFANYIKA WILANI RUNGWE KWA KIFUPI NI UJENZI WA SIKIMU ZA UMWAGILIAJI NNE ZILIZO ANZA UZALISHAJI WA MPUNGA, UTEKELEZAJI WA MIRADI 11 YA MAJI, UJENZI WA JENGO JIPYA LA HALMASHAURI, UJENZI WA OFISI YA BONDE LA MAJI, UJENZI WA BARABARA KWA KIWANGO CHA CHANGALAWE , UANZISHWAJI WA OFISI YA MAMLAKA YA MJI MDOGO TUKUYU, KUANZISHWA KWA HALMASHAURI YA BUSOKELO NA MENGINE MENGI KATIKA SEKTA YA AFYA, KILIMO, MIUNDOMBINU , MAJI, NA MAZINGIRA PIA MICHEZO.  MAKALA INAKUJA YA MAENDELEO NA CHANGAMOTO ZAKE



 JUKWAA LA VIJANA TUKUYU LAENDESHA MDAALO LEO . KICHWA CHA MDAALO KIKIWA WAJIBU WA SEKTA MBALIMBALI KATIKA KUWAENDELEZA VIJANA NCHINI USUSANI WILAYANI RUNGWE
HALI YA HEWA YA LEO TUKUYU

VIJANA TUKUYU WILAYANI RUNGWE WAUNGANA NA KUUNDA JUKWAA LA VIJANA 

FILEMON MWANSASU KATIBU WA AMANI THE FOUNDATION OF LIFE (AFL) MKOA WA MBEYA

WAWEZESHAJI WA MAADA KWA VIJANA KULIA NI KASSIM MHINA KAMANDA WA TAKUKURU  RUNGWENA KUSHOTO NI YOHANA SANGA YEYE NI MKUU WA CHUO CHA GIBONSI MWAIKAMBO TUKUYU
SUZAN MHOJA AFISA MICHEZO WILAYA YA RUNGWE AKIONGEA NA VIJANA JIISI YA KUJITAMBUA NA KUJALI UTAMADUNI WAO WA KITANZANIA ZAIDI NA KUFUFUA MICHEZO KATIKA WILAYA YA RUNGWE






WAKINA DADA WA TUKUYU WANA MWITIKIO WA JUKWAA LAO ILI KUPATA ELIMU YA KUHUSU NCHI YAO YA TANZANIA

VIJANA WAKISIKILIZA MAADA KWA MAKINI



GWAMAKA MWAKATOBE MWENYEKITI WA JUKWAA LA VIJANA WILAYANI RUNGWE AKIFUNGA MDAALO WA LEO  KWA KUWASIHI VIJANA KUWA WAADIRIFU SANA KATIKA JAMII KWAKUWA VIJANA NI KIOO CHA JAMII



 MVUA ILIYONYESHA KIDOGO NA KUAMBATANA NA UPEPO MKALI WILAYANI RUNGWE KATIKA MJI WA TUKUYU UMEEZUA BATI LA MAJENGO YA SHULE YA BULYAGA SECONDARY
 

Add caption

MADARASA MAWILI IKIWEPO NA MAABARA  NA OFISI YA MKUU WA SHULE NDIZO ZILIZOPATA SHIDA YA KUEZURIWA NA UPEPOMKALI ULIOAMBATANDA NA MVUA YA WASTANI
SEHEMU YA NYUMA YA JENGO LILILOEZURIWA

MKUU WA WILAYA AKIJIONEA UHARIBIFU ULIOJITOKEZA NA MVUA HIYO


MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPINI MEELA AKIONGEA NA AFISA ELIMU SEKONDARI WILAYA YA RUNGWE

KINGO AKIWA KAZINI


 MECHI ZA LIGI DARAJA LA NNE WILAYA YA RUNGWE ZAANZA KWA KISHIDO HUKU TANDALE WAKIAMBULIA KICHAPO CHA GOLI 3 KWA MOJA KUTOKA TIMU YA USHIRIKA




WACHA NIANGALIE MPIRA MIMI MAANA HAPA SASA KUNA KAZI MBILI MPIRA NA VILOBA

KAZI IPO

MR NGENYILE AKIJITAHIDI NAYE KUKAMUA HUKU HATA HANA HABARI NA KUANGALIA MPIRA

Pombe toka Malawi zawagalagaza Vijana. Mbeya


* Paketi moja sawa na bia 8, huuzwa Shilingi 100. 
*Zazagaa Mbeya nzima, zadaiwa kupunguza mbegu za kiume

MIAKA takribani 11 tangu pombe kali aina ya Power No.1 super kadansana kutoka nchini Malawi kuua watu mkoani Mbeya, pombezingine zenye kilevi cha kati ya asilimia 40 na 42 zinaingizwa nchini Tanzania na kuathiri afya za watumiaji.



Kati ya pombe hizo ni aina ya Mowa Mafumu (pombe ya machifu) yenye kilevi asilimia 42 na Rider (chaguo la washindi) yenye kilevi asilimia 40.
Pombe hizo ambazo zipo kwenye makaratasi ya plastiki, zimezagaa kila kona ya wilaya ya Kyela, Rungwe, Mbeya mjini, Mbeya Vijijini, Mbarali, Mbozi na Momba huku zikiuzwa bei ya kati ya Sh.100-300 bei gharama ambazo vijana wengi wanaimudu na wanapokunywa wengi huzidiwa na kuanza kutokwa na jasho.
Hali hiyo imejidhihilisha baada ya Mwandishi wa habari hizi kutembelea wilaya ya Kyela iliyopo mkoani Mbeya na kukuta vijana wengi wakinywa pombe hizo ambazo wamekiri kuwa zinaathari kwa Afya zao.
Wakiongea kwa ombi la kutoandikwa majina yao, vijana wa eneo la Kasumulu, Kyela Mjini na Ipinda walisema kuwa wengi wanaotumia pombe hizo hugeuka vituko na wale wanaotumia vyombo vya moto hasa pikipiki huishia kugonga watu na baadhi yao kupoteza maisha.
’’Pombe hizi ni nzuri kwa bei lakini zina madhara makubwa kwasababu wengi tumewaona wakitumia pombe hizi huanza kutokwa jasho jingi katika miili yao jambo ambalo linaonesha kuwa pombe hizi zinakausha maji mwilini lakini vijana wanashindwa kuiacha kutokana na bei ni ndogo na hazikatazwi na Serikali’’ alisema mmoja wa vijana waliohojiwa.
Sanjari na hilo walibainisha moja ya athari iliyowahi kutokea kuwa ni kifo cha kijana mwenzao  John  Mwakapisye kilichotokea Julai 20,2010 baada ya kijana huyo kunywa pombe hizo kisha kuendesha pikipiki na baadaye kupinduka na kujisababishia kifo.
Waliongeza kuwa uwepo wa pombe hizo ambazo zinatengenezwa na kiwanda cha Bwenda Group Limited kilichopo mjini Lilongwe nchini Malawi kumetokana na kuadimika kwa pombe iliyojulikana kwa jina la Kadansana kutoka huko huko nchini Malawi.
Wakielezea kwa kina uwepo wa uholela wa pombe hizo ambazo wamekiri kuwa huingizwa nchini kwa njia za magendo, walisema kuwa pombe aina ya Kandasana nayo pia ilikuwa na madhara kwa watumiaji ambapo wengi wao hasa wanaume walikuwa wakiishiwa nguvu za kiume baada ya kunywa pombe hiyo.
’’Unashangaa hizi Mowa wa Mafumu na Rider! Mwanzo kulikuwa na pombe ilikuwa inaitwa Kadansana ambayo ilikuwa na athari kubwa zaidi kwasababu wanywaji hasa wanaume walikuwa wakiishiwa nguvu za kiume’’ alieleza mmoja wa vijana mjini Kyela.
Uwepo wa pombe hizo hapa nchini ni mwendelezo wa udhibiti mdogo wa dawa na vyakula hapa nchini hususani mkoa wa Mbeya ambapo hivi karibuni tuliweka wazi matumizi mabaya ya vidonge vya Crolofenical kutumika katika pombe za kienyeji huku Mamlaka ya udhibiti wa dawa na chakalu TFDA wakisema kuwa hawajui lolote.
Kwa upande wake mkaguzi wa TFDA nyanda za juu kusini Rodney O. Atananga, alisema  utaratibu wa kukamata bidhaa zilizopigwa marufuku nchini na ambazo hazifai kwa matumizi ya binadamu huhusisha pia Jeshi la polisi na idara ya afya.
Alisema wamekuwa wakifanya ukaguzi wa mara kwa mara ili kubaini ubora wa bidhaa zilizoko sokoni ili kubaini usalama wake na kama zinafaa kwa matumizi ya binadamu.
Atananga alisema watu wanaokamatwa na bidhaa hizo wanafikisha mahakamani kwa sababu ni kinyume na sheria ya chakula na dawa ya mwaka 2003 ambayo inakataza kuuza na  kusambaza bidhaa ambazo hazijasajiliwa na kupigwa marufuku.
Alisema baadhi ya bidhaa zilizopigwa marufuku ni vipodozi vyenye viambato vyenye sumu pamoja na vinavyoingia nchini bila kibali au kusajiliwa.
Aliongeza kuwa bidhaa zenye viambapo vyenye sumu zinakatazwa kwa sababu zinamadhara kwa mwili wa binadamu ambapo alisema madara yake hutokea baada ya muda mfupi na mengine huchukua muda mrefu kujitokeza.
Alisema baadhi ya madhara hayo ni kansa ya ngozi na damu ambayo hujitokeza baada ya muda mrefu lakini madhara ya muda mfupi ni uharibifu wa ngozi na wajawazito kuharibu uzio wa ubongo wa mtoto akiwa tumboni pamoja na kuumwa kichwa.
Kwa sasa pombe kali zilizozagaa mkoani Mbeya ni pamoja na Zed pineapple spirit, double punch,Assorted sarit, Power na Rider can. 

FAMILY DAY YA POLISI YAFANA MBEYA

MKUU WA MKOA MBEYA ABAS KANDORO AKIKAGUA  GWARIDE LA KIKOSI CHA KUTULIZA FUJO KATIKA KIWANJA CHA FFU MBEYA HIVI KARIBUNI
MKUU WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMANDA DIWANI AKIMKARIBISHA MKUU WA MKOA MBEYA KATIKA SHEREHE HIZO ZA WANAFAMILIA WA POLISI JIJINI HAPA
MKUU WA MKOA MBEYA AKIONGE NA WANAFAMILIA WA POLISI
BAADHI YA WAGENI WAALIKWA WAKIMSIKILIZA MGENI RASMI
BAADHI YA ASKARI 21 WALITUNUKIWA VYETI VYA UTUMISHI MZURI KATIKA JESHI HILO LA POLISI
BAADHI WA WANAFAMILIA WA POLISI WAKICHEZA TAARABU UWANJANI HAPO
BAADHI YA WADAU WALITUNUKIWA VYETI VYA USHIRIKIANO MWEMA NA JESHI LA POLISI HAPA KIONGOZI WA DINI AKIPOKEA HATI HIYO
MAKAMPUNI YA ULINZI YA WATU BINAFI PIA WALIPOKEA HATI HIYO YA USHIRIKIANO NA JESHI LA POLISI
MOJA YA WAFANYABIASHARA WA JIJI LA MBEYA JULIUS KAIJAGE AKIPOKEA HATI HIYO

PIA MKUU WA MKOA MBEYA ALIKABIDHI PIKIPIKI KWA JESHI HILO LA POLISI

PICHA NA Jem

Vurugu tupu Tanzania ni kwa faida ya nani?

Vijana wakazi wa Dumila na vitongo vyake wakiangusha gari aina ya Land Cruizer T 241 AMS mali ya mfugaji katika barabara kuu ya Dodoma-Morogoro wakati wa vurugu zilizodumu kwa masaa sita kwa kuweka vizuwizi kwa lengo la kumshinikiza mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bebdera kusikiliza kero za wakulima.         Picha na Juma Mtanda 
MAENEO ya mikoa ya Morogoro, Mtwara na Dar es Salaam, jana yaligeuka uwanja wa fujo na vurugu zilizosababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali, huku polisi wakitumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi.
Vurugu hizo zimehusisha wakulima na wafugaji wa jamii ya Kimasai kwa upande mmoja wa Morogoro, Mtwara Mikindani wananchi waliizingira nyumba ya Diwani wa Kata ya Mikindani kwa madai ya kuwahifadhi watu wanaodaiwa kuwa washirikina ndani ya nyumba yake, huku Dar es Salaam eneo la Kariakoo, polisi na Wamachinga wakipambamba na Mgambo wa Jiji.
Mkoani Mororgoro mtu mmoja aliyefahamiwa kwa jina la Mohamed Msigara (60) amefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya kutokea vurugu kati ya wakulima na wafugaji Kijiji cha Dumila, wila yani Kilosa, baada ya wafugaji wa Jamii ya Kimasai kuingiza mifugo yao kwenye mashamba ya wakulima yaliyo katika Kitongoji cha Mfulu, Kilosa.
Pamoja na mauaji hayo, wasafiri waliokuwa wakitumia Barabara ya Morogoro – Dodoma, nao walionja machungu ya vurugu hizo, baada ya kukwama kwa saa 5 kutokana na wananchi wa kijiji hicho, kufunga barabara kwa mawe, magogo ya miti na kuchoma magurudumu ya gari.
Wananchi hao walichukua hatua hiyo huku wakisisitiza kutaka kuonana na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera, ili kumaliza mvutano huo.
Katika vurugu hizo wanakijiji hao walivunja vioo vya madirisha ya baadhi ya nyumba tano za kulala wageni, kuharibu gari dogo aina ya Landcruser pamoja na kupora mali mbalimbali zi nazodaiwa kumilikiwa na wafanyabiashara wa jamii ya Kimasai.
Kabla ya kufanya uharibifu huo saa 2:30 asubuhi, wananchi hao walifanya maandamano sambamba na kusimama katikati ya barabara, hali iliyosababisha polisi kufika eneo hilo kwa ajili ya kuwadhibiti.
Askari wa Kutuliza Ghasia (FFU), walifika eneo la tukio 5:20 asubuhi na kufanikiwa kuwatawanya wananchi hao kwa kutumia mabomu ya machozi, hatimaye kufungua barabara hiyo.
Pamoja na barabara hiyo ya Morogoro – Dodoma, wananchi hao pia walifunga barabara ya Dumila- Kilosa, hivyo kuyafanya magari yaliyokuwa yakitumia barabara hiyo kukwama kwa zaidi ya saa sita na kusababisha usumbufu kwa wasafiri waliokuwa wakitumia barabara hiyo.
Wakati vurugu hizo zikiendelea, wafugaji wa jamii ya Kimasai wakiwamo wanawake na watoto walionekana kukimbilia kwenye kituo kidogo cha Polisi Dumila kwa lengo la kujihami na kupata msaada wa polisi kutokana na hofu ya kushambuliwa na wananchi.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi aliyekuwepo kwenye eneo la tukio, mkulima aliyefahamika kwa jina Mauya Hamadi alisema kuwa wananchi wamelazimika kufanya vurugu hizo baada ya wafugaji wa jamii ya Kimasai kuingiza mifugo kwenye mashamba ambayo tayari yameshapandwa mazao na kufanya uharibifu.
Alisema kuwa tayari suala hilo walishalifikisha kwa uongozi wa kijiji, kata, wilaya hadi mkoa, lakini hakuna jitihada zozote zinazofanywa na viongozi, hivyo kulazimika kumtaka Mkuu wa Mkoa Joel Bendera, kwenda kuzungumzia suala hilo, ambapo hata hivyo mkuu huyo wa mkoa hakuwahi kufika eneo hilo hadi walipoamua kufanya maandamano hayo.

KATIBU MKUU WA CCM ABDURAHMAN KINANA AKAGUA UWANJA WA NDEGE WA KIGOMA

1 
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi akisalimiana na viongozi mbalimbali wakati alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Kigoma ili kukagua ujenzi wa uwanja huo unaofanywa na kampuni ya ujenzi ya Howard Humphrey
4 
Katibu wa Halmashauri Kuu Siasa na Uhusiano wa Kiamataifa Dk. Asha Rose Migiro , Mkuu wa mkoa wa Kigoma Kanali Issa Machibya na Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana wakielekea kwenye magari tayari kwa kukagua ujenzi wa uanjwa wa ndege wa Kigoma
5 
Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana pamoja na wajumbe wa Sekretarieti ya CCM wakikagua uwanja wa ndege wa Kigoma leo.
6Mafundi wa kampuni ya Howard Humphrey wakiendelea na ujenzi wa uwanja wa ndege wa Kigoma.
9 
Meneja wa uwanja wa ndege wa Kigoma Injinia Clipia Tesha akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana wakati alipotembelea kukagua uwanja huo akiongozana na wajumbe wa Sekretarieti ya CCM, Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Kigoma Kanali Issa Machibya na kutoka kushoto ni Dk. Asha Rose Migiro Katibu wa Halmashauri kuu Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM, Nape Nnauye Katibu wa Halmashauri Kuu Itikadi na Uenezi CCM na Martin Shigela Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM UVCCM.11 
Cleopa Mpembeni Meneja mradi wa Ujenzi wa Uwanja huo kutoka kampuni ya Howard Humphrey akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa CCM na wajumbe wa Sekretarieti ya CCM wakati ujumbe huo ulipotembelea kukagua ujenzi wa uwanja huo leo
12 
Meneja wa uwanja wa ndege wa Kigoma Injinia Clipia Tesha akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya Katibu Mkuu wa CCM Abdurahman Kinana kukagua ujenzi wa uwanja huo leo.
by John Bukuku

No comments: