Wednesday, January 30, 2013

MCHUNGAJI AACHANA NA MKEWE KWA KUMTUHUMU NI MCHAWI MBEYA

Mchungaji wa kanisa linalojulikana kwa jina la Calnel Centre Mchungaji Elia Ambakisye Jongo alijikuta katika mzozo mkali na aliyedai kuwa ni mke wake baada ya kumtuhumu kuwa ni mchawi.
Sabina Lameck mke wa mchungaji anaedaiwa kuwachwa sababu ya uchawi 
Katikati mama mzazi wa mchungaji Elia Jongo wakiwa katika kikao hicho
Baadhi ya wazee wa kanisa wakiwa makini kusikiliza kisa hicho
“ Ninachotaka ni huyu mwanamke kurudisha nguo zangu kwa sababu alizichukua ili apeleke kwa mganga kwa nia ya kunisaidia mimi nirudiane na mchungaji lakini badala yake naona dawa hizo zimemsaidia mwenyewe hadi anataka kuolewa yeye,” alisema Mwanamke huyo. ambaye alikuwa mke wa mchungaji Elia
Huyu ndiye muumini wa kanisa hilo anayedaiwa kutaka kuolewa na mchungaji Elia pia muumini huyu ni mzee wa kanisa hilo
Mchungaji elia na dada yake wakiwa makini kumsikiliza mchawi wake
“ Huyu mwanamke ni mshirikina maana tangu tutengane alianza kunivurugia huduma ambapo waumini walianza kupungua kanisani nayeye kwenda kwa waganga wa kienyeji kwa lengo la kunivurugia huduma” alisema mchungaji huyo kwa hasira.
Askofu wa kanisha hilo laiyejulikana kwa jina moja la Pasta Lugito 
 Hili ndilo kanisa la Calnel Centre mbeya lipo katibu na kiwanja cha ndege mwanjelwa
 Mchungaji wa kanisa linalojulikana kwa jina la Calnel Centre Mchungaji Elia Ambakisye Jongo alijikuta katika mzozo mkali na aliyedai kuwa ni mke wake baada ya kumtuhumu kuwa ni mchawi.
Tukio hilo la aina yake lilitokea juzi katika kanisa hilo lililopo Airport Jijijini Mbeya baada ya Mchungaji huyo kupokea ujumbe mfupi katika simu yake ya mkononi kutoka kwa Mwanamke anayedai alikutwa mke wake ambaye waliachana miaka mine iliyopita.
Mchungaji huyo akiwa mbele ya wazee wa kanisa, Familia yake, waumini pamoja na wanahabari alisema sababu ya kuwakusanya watu hao kumetokana na mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la Sabina Lameck akitaka kutubu kwa mabaya aliyomtendea mumewe.
Hata hivyo baada ya mwanamke huyo kupewa nafasi ya kuanza kujieleza alianza kumtuhumu muumini wa kanisa hilo kuwa anauhusiano na mchungaji ambaye ni mumewe wa ndoa ambapo pia alidai kuwa mwanamke huyo alichukua nguo za mchngaji na mkewe kwa madai ya kupeleka kwa mganga ili kusudi awasaidie warudiane.
“ Ninachotaka ni huyu mwanamke kurudisha nguo zangu kwa sababu alizichukua ili apeleke kwa mganga kwa nia ya kunisaidia mimi nirudiane na mchungaji lakini badala yake naona dawa hizo zimemsaidia mwenyewe hadi anataka kuolewa yeye,” alisema Mwanamke huyo.
Kwa upande wake mchungaji Jongo alimtuhumu mwanamke huyo kuwa ni mshirikina na kwamba sababu ya kutengana naye ni kutokana na mwanamke huyo kuzaa na mwanaume mwingine nje ya ndoa hali aliyosema alidhalilishwa kama mchungaji.
“ Huyu mwanamke ni mshirikina maana tangu tutengane alianza kunivurugia huduma ambapo waumini walianza kupungua kanisani nayeye kwenda kwa waganga wa kienyeji kwa lengo la kunivurugia huduma” alisema mchungaji huyo na kuongeza.
“ amekuja leo hapa baada ya kusikia mimi nataka kuoa muumini wangu ambapo yeye ameanza kumzushia kuwa ni mshirikiana kitu ambacho si cha kweli lakini kama kuna ukweli wowote utajulikana kwa sababu Mungu yupo,” alisisitiza Mchungaji huyo.
Hata hivyo usuluhishi huo haukufika mwafaka baada ya kuibuka kwa malumbano hali iliyomlazimu msimamizi wa usuluhisho huo Askofu wa kanisha hilo laiyejulikana kwa jina moja la Pasta Lugito kuahilsha mazungumzo hayo huku wakimpiga marufuku mwanamke huyo kukanyaga katika makazi ya mchungaji.
Picha na Mbeya yetu

Hili ni Bunge la hoja au vioja?

3- Spika anne Makinda
Tunaelekea kuzoea bunge la vioja badala ya hoja.mfano,ni kuwa kuna baadhi ya wabunge wanapeleka hoja kuwa bunge lisionyeshwe live.hakya ya nani! .Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Anne Makinda akitoa taarifa kwa wabunge (kawapo pichani) jana mjini Dodoma kuhusu kuundwa kwa kamati itakayokwenda mkoani Mtwara kusikiliza maoni ya wananchi wa mkoa  huo kuhusu tatizo la suala la gesi
1-baadhi ya wabunge wakifuatilia mjadala leo 
Baadhi ya wabunge wakifuatilia masuali na majibu katika kikao cha mkutano wa kumi mjini Dodoma leo,
2-baadhi ya wabunge wakipongeza baada ya kuahirishwa kwa kikao leo 
Baadhi ya wabunge wakisalimiana baada ya kuahirishwa  kwa kikao  leo mjini Dodoma,
5-Mbunge wa Monduli Edward Lowassa (kulia) akimsikilza mbunge wa Bariadi Mashariki John Cheyo (kushoto) a 
Mbunge wa( Monduli )Edward Lowassa ((kulia) akimsikilza Mbunge wa Bariadi Mashariki John Cheyo Kushoto) katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma leo, (Picha na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO).
6-Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Taknolojia January Makamba akijibu hoja Bungeni leo mjini Dom 
Naibu Waziri  Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia , January Makamba akijibu hoja za wabunge zinazohusu wizara yake Bungeni leo- Dodoma, (Picha na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO).
 

Je, Wana Mtwara wamekubaliana na waziri mkuu wa Tanzania ndugu pinda?

DSC00710
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Wafanyabiashara wa Mtwara kuhusu mgogoro wa gesi kwenye ukumbi wa VETA mjini Mtwara, Januari 28, 2013. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Joseph Simbakalia.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


IMG_0245
Baadhi ya Wafanya biashara wa Mtwara wakinyosha mikono kuomba nafasi ya kuchangia katika mazungumzo kati yao na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuhusu mgogoro wa gesi kwenye ukumbi wa VETA mjini Mtwara, Januari 28, 2013.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
IMG_0250Mfanyabiashara wa Mtwara, Fatuma Embe akichangia katika mkutano kati ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na wafanyabiashara wa Mtwara kuhusu gesi kwenye ukubi wa VETA mjini Mtwara, Januari 18, 2013.(PIcha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 “Imani yangu ni kwamba maelezo yametosheleza, mtakua na kiwanda chenu cha kusindika, mtakua na kiwanda cha kusafisha, mtakua na hayo matawi kadhaa kwa ajili ya uzalishaji wa umeme kwa ajili ya usindikaji wa viwanda”- Pinda

Serikali Yataja Manufaa kwa Wana-mtwara Gesi Ikipelekwa Dar

 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene 
Na Mwandishi wa Thehabari.com
 SERIKALI imetaja manufaa na faida ambazo wanatarajia kuzipata wananchi wa Mtwara pamoja na Lindi endapo gesi itasafirishwa kwenda Jijini Dar es Salaam.
 Imesema Mkoa wa Mtwara ndipo utakapo jengwa mtambo mkubwa wa kusafishia gesi hiyo kabla ya kusafirishwa kwenda jijini Dar es Salaam kwa matumizi ya uzalishaji umeme na matumizi ya moja kwa moja viwandani.
 Kauli hiyo imetolewa jana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene alipokuwa akizungumza katika Kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na Kituo cha Radio One jijini Dar es Salaam.
 Naibu waziri huyo ameweka wazi kuwa mkoani Mtwara licha ya Serikali kupanga kujenga viwanda vingine kadhaa, inajenga mtambo wa megawati 250 ambao utakuwa ukizalisha umeme na mwingine kujengwa mkoani Lindi eneo la Somanga Funga utakao kuwa ukizalisha megawati 520.
 Akifafanua zaidi Simbachawene alisema eneo la Mikindani katika Kijiji cha Msijute mkoani Mtwara kinatarajiwa kujengwa kiwanda kikubwa cha saruji Afrika Mashariki na Kati chenye uwezo wa kutoaji ajira kwa watu 6000 jambo ambalo ni manufaa ya Wanamtwara.
 Alisema pia tayari kuna wawekezaji wa viwanda vya mbolea wamejitokeza kujenga viwanda mkoani Mtwara na Serikali itaviacha vinu vya kuchimba na kusindika gesi eneo hilo jambo ambalo bado ni manufaa makubwa kwa wananchi.
 
 

KATIBU MKUU WA UVCCM MARTIN SHIGELA ASHIRIKI SHUGHULI ZA KILIMO NA KUKAGUA MIRADI KIGOMA VIJIJINI

5 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM, UVCCM Bw. Martin Shigela akishiriki katika kupalilia shamba la Karanga katika kijiji cha Nkungwe Tarafa ya Mabembe Wilaya ya Kigoma Vijijini wakati alipotembelea na kujionea shughuli mbalimbali na kukagua miradi inayotekelezwa na wananchi kwa pamoja na Serikali jana.
Sekretarieti ya CCM ikiongozwa na katibu mkuu wa CCM Ndugu Abdurahman Kinana  iko mkoani Kigoma kwa ajili ya  kuangalia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi na sherehe za miaka 36 ya chama hicho zinazotarajiwa kufanyika Februari 3 kwenye uwanja wa Lake Tanganyika mkoani humo, kulia ni Bi Fatma mmiliki wa na kushoto ni Khamis Bitese Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kigoma Vijijini.
3 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Nkungwe wakati alipotembelea katika kijiji hicho jana
4 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akikabidhiwa zawadi ya mihogo na Bi Asha Ibrahim mara baada ya kutembelea shamba lake jana, .Kijiji hicho cha Nkungwe ndicho kinachoongoza kwa kilimo cha muhogo bra katika mkoa wa Kigoma.
8 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akiongozana na Bw.Khamis Bitese Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kigoma Vijijini mbele yake wakati akikagua shughuli za ukulima wa kisasa katika kijiji cha Nkungwe Kigoma Vijijini, Kijiji hicho cha Nkungwe ndicho kinachoongoza kwa kilimo cha muhogo bra katika mkoa wa Kigoma.
9 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akimsaidia Bi. Asha Ibrahim kufukia mbegu ya Viazi, huku viongozi mbalimbali wa CCM  wilaya ya Kigoma Vijijini wakishuhudia tukio hilo.
7 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akimkabidhi zawadi ya shilingi elfu 10,000 mtoto Rehema huku mama yake akimsaidia wakati alipotembelea na kujionea shughuli za kilimo katika kijiji cha Nkungwe jana
11 
Viongozi mbalimbali wakikagua kivuko cha Mto Ruchi katika kijiji cha Nkungwe jana.
12 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akivuka katika kivuko cha Mto Ruchi kwa kutumia Baiskeli huku akiwa ameonozana na viongozi mbalimbali wa CCM wilaya ya Kigoma Vijijini pamoja na watendajiwa kijiji hicho jana inaelezwa kwamba watu wengi walipotea maisha kwa kuliwa na Mamba kabla ya kujengwa kivuko hiki.
13 
Katibu Mkuu wa Umoja wa vijana CCM UVCCM Martin Shigela akimenya muhogo ili kutafuna kidogo mara baada ya kununua kwa mmoja wa wakulima Kijiji cha Nkungwe ndicho kinachoongoza kwa kilimo cha Muhogo mkoani Kigoma
15 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM UVCCM Martin Shigela akiagiza jambo kwa Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Kigoma Bw Peter Msanjila wakati alipotembelea kata ya Mwanduga jana kulia ni Khamis Bitese Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kigoma Vijijini
16 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM UVCCM Martin Shigela akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi ya Kabanda katika kijiji cha Chabwimba jana
18 
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM UVCCM Martin Shigela akisalimiana na wananchi mara baada ya kuwasili katika Kata ya  Mabembe.
19 
Wananchi wa kijiji cha Mabembe wakimsikiliza mwenyekiti wa UVCCM katika Kata ya Mabembe kwenye mkutano wa ndani
20 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM UVCCM Martin Shigela akicheza na msanii chipukizi wa kijiji cha Mabembe ambaye ni mlemavu wakati alipotembelea na katika Kata ya Mabembe
23 
Wananchi wakiwa wamejitokeza kwa wingi katika kata ya Mwanduga Kigoma vijijini jana
24 
Mjumbe wa NEC CCM kupitia Wilaya ya Uvinza Asha Baraka akiwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Mwanduga Kigoma jana kulia ni Khamis Bitese Mwenyekiti wa CCM Kigoma Vijijini na katikati ni Peter Msanjila Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Kigoma.
25 
Martin Shigela Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika jana kwenye kata ya Mwanduga Wilaya ya Kigoma vijijini
26 
Matin Shigela Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa akipata maeleo kutoka kwa Khamis Bitese Mwenyekitiwa CCM Wilaya ya Kigoma Vijijini  wakati alipotembele na kukagua ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi ya Kabanda.
27 
Martin Shigela Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa akipata maeleo kutoka kwa Khamis Bitese Mwenyekitiwa CCM Wilaya ya Kigoma Vijijini  wakati alipotembele na kukagua ujenzi wa numba za walimu  katika shule ya msingi ya Kabanda.
2 
Huu ndiyo mto Ruchi unaotenganisha kijiji cha Nkungwe na mashamba ya wanakijiji hao uliosababisha mauaji ya wananchi kadhaa kutoka na kuliwa na Mamba kabla ya kujengwa kwa  kivuko hicho.


No comments: