Tuesday, January 22, 2013

Mkapa ajitosa sakata la gesi



                                                                               
Na: Fredy Azzah
RAIS Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ameelezea kufedheheshwa kwake na mgogoro wa gesi, huku akiwataka wananchi na wadau wa maendeleo wa Mkoa wa Mtwara kusitisha harakati za maandamano na mihadhara. Mkapa alitaka wakazi hao
kuacha kulumbana na Serikali kuhusu suala hilo, badala yake wajiandae kukaa meza moja nayo kutafuta mwafaka kwa njia ya amani.
Katika tamko lake alilolitoa Dar es Salaam jana, Mkapa alisema: “Fujo, vitisho, kupimana nguvu na malumbano siyo masharti ya maendeleo.
“Nikiwa kama mwana - Mtwara na raia mwema, mpenda nchi, nimefedheheshwa sana na matukio haya ya siku za karibuni Mtwara. Kwa sababu hiyo natoa wito kwa wadau wote wa maendeleo ya Mtwara, kusitisha harakati hizi na maandamano na mihadhara.
“Badala yake wajipange kukaa pamoja katika meza moja,  kupitia historia, kutathmini mipango, kuchambua kwa kina mikakati ya utekelezaji wake, hatimaye kufikia mwafaka wa ujia wa maendeleo. Liwezekanalo leo lisingoje kesho.”
Mkapa alisema mwenendo wa mazungumzo, maandamano na mikutano ya hadhara inayoendelea mkoani Mtwara, inaelekea kuashiria kuvunjika kwa amani hali aliyosema kuwa inajenga kutokuelewana kati ya viongozi wa vyama vya siasa na Serikali, wananchi na vyama vya siasa na wananchi na viongozi wa Serikali.
“Mtafaruku huu haufai kuachwa na kutishia usalama, mipango ya maendeleo siyo siri, mikakati na mbinu za utekelezaji wake siyo siri,” alisema Mkapa na kuongeza:
“Maelezo yake mazuri yanaweza kutolewa yakadhihirisha namna na kasi ambayo rasilimali zinawanufaisha wananchi wa eneo zilimo na taifa zima.”
Mkapa alisema hali hiyo ni tishio kwa wawekezaji wa ndani na nje, kwani mara zote hawapendi vurugu, fujo na vitisho.

Kauli hiyo ya Mkapa imekuja siku kadhaa tangu kuwapo kwa maandamano na vurugu zinazofanywa na baadhi ya wananchi wa Mkoa wa Mtwara wanaopinga gesi kusafirishwa kwenda Dar es Salaam.
Tayari viongozi kadhaa akiwamo Rais Jakaya Kikwete wametoa tamko juu ya suala hilo wakionya kuwa halikubaliki kwa kuwa rasilimali hiyo si kwa ajili ya wana Mtwara pekee.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo aliyalaani maandamano hayo akisema walioyaandaa wamelenga kuigawa nchi vipandevipande, Chadema kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kumbana waziri huyo ili aondoe udhaifu uliopo katika sekta ya nishati.
Desemba mwaka huu, maelfu ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara waliandamana wakipinga uamuzi wa Serikali kusafirisha gesi kwa njia ya bomba kutoka hapa kwenda Dar es Salaam.
Maandamano hayo yaliyoratibiwa na vyama vya Chadema, NCCR-Mageuzi, Sau, Tanzania Labour Party (TLP), APPT- Maendeleo, ADC, UDP na DP yakishirikisha wananchi wa wilaya za mkoa huo, zikiwamo Tandahimba na Newala  yalianzia katika Kijiji cha Mtawanya hadi Mtwara Mjini kupitia barabara ya kwenda Msimbati eneo ambako gesi asilia inapatikana.
MWANANCHI

Rais Obama awasifu Lincoln, Luther King


Rais Barack Obama akiapishwa na Jaji Mkuu wa Marekani, John Roberts kushika wadhifa huo kwa kipindi cha pili Ikulu ya White House jana. Kulia ni watoto wake, Malia na Sasha. Picha na AFP 

RAIS Barack Obama wa Marekani ameapishwa rasmi kushika muhula wa pili wa urais, katika sherehe maalumu iliyofanyika kwenye Ikulu ya nchi hiyo jana.
Obama ambaye ni Rais wa 44 wa Marekani, aliingia madarakani katika uchaguzi wa kihistoria mwaka 2008 uliomfanya kuwa Rais wa kwanza mwenye asili ya Afrika katika taifa hilo kubwa duniani.
Sherehe za kuapishwa kwake Ikulu jana zilikuwa za faragha na zilihudhuriwa na watu wachache maalumu, leo ataapishwa katika sherehe za jumla zitakazowajumuisha watu wote kwenye Uwanja wa National Mall.
Katika kiapo chake, Obama atatumia Biblia mbili, moja iliyokuwa ikitumiwa na Martin Luther King na nyingine ilikuwa ikitumiwa na aliyekuwa Rais wa 16 wa Marekani, Abraham Lincoln.
Lincoln aliongoza taifa hilo kuanzia Machi 1861 hadi alipouawa Aprili 1865.
Akiwa Ikulu jana, alitumia Biblia iliyowahi kutumiwa na Lincoln, katika sherehe za leo  atatumia Biblia ya Martin Luther King.
Lincoln, ndiye aliyeliongoza taifa hilo kipindi kigumu cha kusimamia umoja na kufuta biashara ya utumwa.
Martin Luther King ambaye alikuwa mchungaji na mwanaharakati wa haki za watu wenye asili ya Afrika nchini Marekani, aliuawa Aprili 4, 1968, muda mfupi baada ya kutoa hotuba yenye nguvu ya I have a Dream (Nimeota ndoto).
Hotuba hiyo ikuwa ikieleza ndoto yake kwamba muda siyo mrefu watu wenye asili ya Afrika watapata nguvu na kupata haki yao kama raia wa Marekani.
Viongozi hao wawili wana historia ya pekee, Lincoln ndiye aliyetumia muda wake mwingi akiwa Ikulu ya Marekani kuhakikisha watu wenye asili ya Afrika ambao walikuwa watumwa wananasuliwa utumwani.
Luther alikuwa mwanaharakati aliyechochea mabadiliko kwa kushinikiza Serikali kuwapa haki zao za msingi.
Obama aliapishwa rasmi jana ikiwa ni siku ya kwanza kati ya siku mbili zilizopangwa, leo ataapishwa mara ya pili katika viwanja maalumu vya Nationa Mall mjini Washington, ambako maelfu ya watu watapata fursa ya kushuhudia.
Hotuba ya kuapishwa kwake  itakayotolewa leo inatarajiwa kuweka historia mpya, pia kuhitimisha matukio ya siku mbili hizi za kuapishwa, ataweka wazi mtazamo wake wa kipindi cha miaka minne ijayo.
Mkusanyiko utakaoshuhudia kuapishwa kwake na kusikiliza hotuba yake moja kwa moja katika uwanja huo unakadiriwa kupungua kutoka ule wa watu 1.8 milioni mwaka 2009 na kufikia kati ya 600,000 na 800,000, huku mamilioni wakishuhudia kupitia televisheni.


JAMBO LEO


IMG-20130122-00429 d91ae

 

UKUTA WA KITUO CHA MABASI UBUNGO WAANGUKA NA KUHARIBU MAGARI

1           Gari linalosadikiwa kuwa ni la polisi likiwa limeharibiwa vibaya na ukuta wa kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo Bus Terminal baada ya nguzo zake kudondokea magari mbalimbali yaliyokuwa yameegeshwa katika eneo hilo, jumala ya magari 24 yameharibiwa vibaya katika tukio hilo Bajaji 4 na watu watatu wamejeruhiwa na mkukimbizwa Hospitali.

2
3
4 5 6 7 8 10

 

Mtoto afariki dunia kwa ajali ya Moto...

Mwili wa mtoto huyo ukichukuliwa na polisi kwenda kuhifahiwa na kuchunguza chanzo cha moto huo
Nyumba hii ndimo alimoungulia mtoto huyo
Baadhi ya majirani wakiwa katika tukio hilo 


 Mtoto Halaika Bushiri (7) mwanafunzi wa shule ya msingi Mwanyanje iliyopo kata ya Igawilo jijini hapa amefariki dunia baada ya kuketea kwa moto akiwa nyumbani kwao jana majira ya saa 7:45 ya mchana, Januari 21 mwaka huu.
  
Shuhuda wa tukio hilo Recho Jeseph (36) amesema mtoto huyo aliza kupiga kelele za kuomba msaada mara baada ya kutokea kwa moto wakati mama wa mtoto Nuru Mlele akiendelea shughuli zake licha ya majira kujitokeza na kuuzima moto huo.
  Katika hali ya kushangaza mama huyo hakuonesha kustushwa na kitu chochote na wakati tukio hilo aliendelea kufua nguo, hadi pale majirani walipofanikiwa kuudhibiti moto huo ambao uliteketeza samani za nyumba yake ikiwemo seti moja ya kochi
Aidha kutokana na juhudi za majirani kushirikiana ndani ya dakika kumi walifanikiwa kuudhibiti moto huo na kuuzima lakini mtoto huyo alikuwa tayari ameshafariki.
Hata hivyo licha ya polisi kupewa taarifa majira ya saa tisa kamiliwalifika majira ya saa kumbi na mbili na robo jioni, eneo la tukio lenye umbali wa mita mia sita kutoka kituoni, hali iliyowasononesha sana wananchi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Diwani Athumani amekiri kupokea taarifa za tukio hilo na kuongeza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Rufaa na uchunguzi zaidi wa tukio hilo bado unaendelea.

Na Ezekiel Kamanga,Mbeya
 

MWENYEKITI WA MBEYA PRESS CLUB ALIYE KUJIUZURU KWA NGUVU YA WANACHAMA AKABIDHI OFISI KWA MWENYEKITI WA MUDA

KULIA CHRISTOPHER NYANYEMBE ALIYEKUWA MWENYEKITI WA MBEYA PRESS CLUB AKIMKABIDHI NYARAKA MUHIMU ZA OFISI MWENYEKITI WA MUDA BRAND NELSON MAKABIDHIANO HAYO YAMEFANYIKA KATIKA OFISI ZA MBEYA PRESS CLUB
KWA UJUMLA SASA NIMEWAKABIDHI OFISI NAOMBENI FANYENI KAZI KWA KUSHIRIKIANA MSIPENDE KUPOKEA MAJUNGU KUWENI MAKINI SANA KATIKA  KAZI YA KUWATUMIKIA WANACHAMA MAANA KILA MWANACHAMA ANAMAWAZO YAKE TOFAUTI HAYO NI MANENO ALIYOKUWA AKISEMA MWENYEKITI ALIYEJIUZURU CHRISTOPHER NYANYEMBE
MWENYEKITI WA MUDA WA MBEYA PRESS CLUB BRADY NELSON AKIWA MAKINI KUMSIKILIZA  NYANYEMBE
BRANDY NELSON MWENYEKITI WA MUDA AKIMSHUKURU NYANYEMBE KWA KUMKABIDHI OFISI NA PIA AMEMTAKA AONYESHE USHIRIKIANO PINDI ANAPOHITAJIKA 
BAADHI YA WAJUMBE WALIYOSHUHUDIA MAKABIDHIANO HAYO
HII NI OFISI MPYA YA MBEYA PRESS CLUB AMBAYO IPO MAENEO YA SOWETO MBEYA PIA MWENYEKITI ALIYEJIUZULU ALIIKABIDHI KWA MWENYEKITI WA MUDA
HAPA WANATOKA BAADA YA MAKABIDHIANO

PICHA NA Jem 

No comments: