Wednesday, January 23, 2013

MVUA KUBWA IMENYESHA MJINI TUKUYU WILAYANI RUNGWE KWA MASAA 2 NA KUSABABISHA MIUNDOMBINU YA UMEME KUHATARISHA MAISHA YA WATU KWA KUKATIKA KWA NYAYA ZA UMEME KATIKA MTAA WA TRA TUKUYU MJINI

MVUA IKINYESHA

HIYO HAPO JUU NDIO OFISi YA KINGO PRODUCTION & www,kingotanzania.blogspot.com NDIPO WAYA ZILIPOKATIKA NA KUJIKUTA MAISHA YAKO REHANI KWA MLIPUKO  MKUBWA NA CHECHE ZA MOTO KUTOKEA

KIJANA AKAJITOLEA KUINUA WAYA ILI WATU WAVUKE SALAMA

WATOTO WAKIPITA KWA HOFU

SASA AMANI MAANA MAFUNDI WA TANESCO WAMEFIKA NA KUZIMA UMEME NA KUENDELEA NA MAREKEBISHO



MAFUNDI WAKIENDELEA NA KAZI SASA

Wafanyabiashara na Wanasiasa walioahidi kuisaidia familia ya Mwangosi watakiwa kutekeleza ahadi zao walizoahidi kwa familia mbele ya watanzania .

MKE WA MAREHEM SIKU YA MAZIKO YA MUMEWE AKIMUAGA KWA MALA YA MWISHO

WACHUNGAJI WAKIONGOZA MAZIKO




Mkurugenzi wa umoja wa vilabu vya waandishi wa habari nchini (UTPC) Abubakar Karsan wakati akiongea na waandishi wa habari mkoani Mbeya.

Waandishi wa habari mkoani Mbeya 
 Wadau mbalimbali walioahidi kutoa msaada kwa familia ya Daudi Mwangosi wamekumbushwa kutekeleza ahadi zao ili kuiwezesha familia hiyo kujimudu kimaisha.
Rai hiyo imetolewa na mkurugenzi wa umoja wa vilabu vya waandishi wa habari nchini (UTPC) Abubakar Karsan wakati akiongea na waandishi wa habari mkoani hapa.
 
Amesema licha ya ahadi mbalimbali zilizotolewa na baadhi ya wafanyabiashara na wanasiasa hakuna ahadi hata moja ambayo imetekelezeka hadi sasa.
 
Wakati huohuo amesema tume iliyoundwa kwa ajili ya uchunguzi wa kifo cha Daudi Mwangosi kilichotokea Septemba pili mwaka jana imemaliza kazi yake na kutoa mapendekezo kwa viongozi wa jeshi la polisi waliohusika katika oparesheni hiyo iliyopelekea kuuawa kwa Mwangosi waweze kuwajibika.
 
Hata hivyo amesema umoja wa vilabu vya waandishi wa habari nchini unatarajia kumuanzishia mradi wa ufugaji kuku wa kisasa mjane wa Mwangosi ili aweze kuilea vyema familia yake.

WANAWAKE ILEJE TANZANIA, WAJIFUGULIA CHITIPA NCHINI MALAWI.


HAPA NDIO MPAKANI MWA MWALAWI NA TANZANIA WILAYANI ILEJE
MCHANA NDIO UNAPITA KWA MWENDO WA TOGWA NA KIPANDE CHA MKATE
NIKATAMANI KINACHOUZWA HAPO MMMMM PALIKUWA NA TOGWA PAMOJA NA HUKU TANZANIA NI HALAM MALAWI WANAUZA HADHARANI (GONGO)
SERA ya Afya ya mwaka 2007 haifahamiki wilayani Ileje katika mkoa wa Mbeya. Ni katika sera hii ambamo inatamkwa kwamba wajawazito nchini watapewa huduma za afya bure lakini hali sivyo ilivyo, imebainika.
Kama sera inafahamika, basi haitekelezwi. Baadhi ya wajawazito katika wilaya ya Ileje wanaacha zahanati, vituo vya afya na hospitali wilayani mwao na kuvuka mpaka hadi nchini Malawi kufuata kinachoitwa “huduma bora.”katika hospitali inayojulikana kwa jina la Chitipa.
Kuna nini katika hospitali ya Chitipa nchini Malawi hadi wajawazito wakimbilie huko? Jibu wanalo wanawake na wanaume wa wilayani ileje akiwemo Neema Mbughi mkazi wa kijiji na kata ya Bupigu ambaye anasema kuwa Pale hospitali ya Chitipa wajawazito wanaenda bila madishi, karatasi za nailoni (ambako mjamzito huhala wakati wa kujifungua) wala glovu Kila kitu ni bure, hata chakula ambacho tunapewa bule  kama kimetoka nyumbani.
Wanawake wapatao 27 waliohojiwa na mwandishi wa habari hii, pamoja na kutofautiana katika mambo mengine, wengi waliafikiana kuwa katika hospitali ya Chitipa, wauguzi wanatumia “lugha nzuri” inayompa matumaini mjamzito.
Swali ni kwamba Hivi wanapitaje mpakani penye idara ya uhamiaji? Jibu unalopewa ni kwamba hawapiti mpakani kwenye ofisi za serikali. Wanapita vichochoroni ambako wanaita “njia za panya.”
Wakifika hospitalini Chitipa wanajieleza kuwa wanatoka vijiji vya ndani ya Malawi – wengine wakitaja viongozi katika maeneo hayo kuthibitisha kuwa wanatoka humohumo.
Kuna kichocheo kingine kwa wananchi wa Tanzania kutibiwa na kujifungulia Chitipa? Katika mahojiano nao walieleza, mmoja baada ya mwingine, kuwa ikitokea “bahati mbaya” mama au mtoto akafariki na wakati huo umejitambulisha kuwa anatoka Tanzania, basi maiti inasafirishwa hadi mpakani bila gharama yeyote.
Katika hospitali za mkoani Mbeya mwanamke hutakiwa kwenda na karatasi la kutandika wakati wa kujifugua linalouzwa kwa Sh. 3,000, paketi ya glovu Sh. 2000, beseni Sh. 3,000 na kama mjamzito amelazwa bia kujali kuwa ana ndugu au hana, basi hujitegemea pia kwa gharama za chakula. 
Na, Gordon Kalulunga, Ileje

MAONI YA MH. LOWASSA KWA TUME YA KATIBA MPYA

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa kukusanya Maoni ya Katiba mpya,mara baada ya kutoa maoni yake.

YAFUATAYO NI SEHEMU YA MAONI ALIYOYATOA MH. EDWARD LOWASAA:
Kwanza ningependa kukupongeza wewe mwenyekiti Mh Jaji Warioba pamoja na tume nzima kwa imani kubwa ambayo Rais ameionesha kwenu, ni kwa kuwapa jukumu hilo zito na muhimu kwa nchi yetu.
Wananchi pia wamekuwa na imani kubwa na wamejenga matumaini ya kila kitu kwa tume hii. Kutokana na hilo wamekuwa wakitoa maoni ambayo mengine hayahusiani na katiba, yaani siyo ya kikatiba.Pengine na mimi nitakuwa miongoni mwao, kwa hiyo naomba radhi mapema, iwapo maoni yangu haya mengine , yataonekana si ya kikatiba.
Katiba yetu ya sasa ni nzuri, imetuongoza katika umoja na mshikamano wa kitaifa kwa muda wote huo.Lakini, kutokana na hali ya dunia ya sasa, ni vyema kuwepo na katiba mpya ili kuendana na hali halisi.
Kuna mambo manne ambayo kwa imani na mtizamo wangu ningependa yawemo katika katiba yetu ijayo.
1.ELIMU BURE
Moja ya haki za mtoto ni kupata elimu. Ningependa suala la elimu bure ya sekondari liwemo kwenye katiba yetu. Katiba itamke wazi kuwa elimu ya sekondari ni bure.Nchi yetu bado ina idadi kubwa ya watu wake ambao ni masikini.
Uwezo wao wa kipato ni mdogo.Naamini kabisa hili linawezekana na serikali inaweza kugharimia elimu ya sekondari ikawa bure. Hii itatoa nafasi ya kujenga taifa lijalo lenye idadi kubwa ya vijana watakaokuwa wamepata elimu ya sekondari.Wabunge wenzangu bila shaka wanalijua hili.
Ukweli katika majimbo yetu wazazi wamekuwa wakishindwa kulipia karo ya shule kwa  watoto wao. Wabunge tumekuwa tukibeba mzigo huo japo kidogo. Kwa hiyo, kifungu cha ELIMU BURE KWA SEKONDARI, kiwepo kwenye katiba.
2.ADHABU YA KIFO-DEATH PENALT
Katiba ya sasa haisemi wazi kuhusu adhabu ya kifo.Inazungumzia tu haki ya uhai.Ibara ya 14 ya katiba hii ya jamuhuri ya muungano wa tanzania ya mwaka 1977 inatamka kiujumla tu kuwa KILA MTU ANA HAKI YA KUISHI NA UHAI WAKE KULINDWA.
Lakini , haki hiyo inanyang’anywa na kifungu nambari 196 cha sheria ya kanuni za adhabu sura ya 16(penal code ,cap 16), kinachotamka kuwa adhabu ya kifo(death penalty or capital punishment) kwa kosa la mauaji ya kukusudia.
Adhabu hiyo hiyo pia utolewa kwa kosa la uhaini.Sasa mapendekezo yangu mimi ni kwamba kuwe na ibara katika katiba mpya inayotamka wazi kuwa HAKUTAKUWA NA ADHABU YA KIFO HAPA NCHINI HATA KWA KOSA LA KUKUSUDIA AU UHAINI.
3.MATUMIZI YA FEDHA KATIKA UCHAGUZI
Katika sehemu nyingi hapa nchini mwananchi kama hana fedha hawezi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.Katiba mpya iwe na ibara inayofafanua ni kiasi gani cha fedha ambacho mgombea anaruhusiwa kutumia katika kampeni.Iainishe ni matumizi gani ya lazima ambayo mgombea hawezi kukwepa kutumia fedha katika kampeni zake, mfano kuwakusanya wapiga kura kwenda kupiga kura gharama hizo nani azibebe.
Katiba ifafanue rushwa ni nini kwenye chaguzi hizi.Au tuwe na mfumo wa PROPORTIONAL REPRESENTATION ,vyama viwe ndiyo vinaingia kwenye chaguzi kuwania majimbo na siyo wanachama,huko kila mtu atakuwa anapigania chama chake kupata kura nyingi ili wapate viti vingi zaidi, pengine hii itasaidia kuondoa kikwazo cha mtu kuwa na uwezo wa kifedha ndiyo aweze kuwania uongozi.
4.ARDHI
Kwa mwanadamu, kunyang’anywa haki ya kutumia ardhi ya nchi aliyozaliwa ni sawa na kunyanng’anywa haki ya uraia wake. Katiba hii ya sasa inawapa nguvu wakulima katika suala la ardhi, na kuwasahau wafugaji.
Wafugaji wamekuwa wakimbizi katika nchi yao, wamekuwa wakitangatanga kutafuta malisho ya mifugo yao, ile ardhi waliyokuwa wanaimiliki wakiondoka kutafuta malisho huku nyuma imekuwa ikimilikishwa watu wengine, wakulima au wawekezaji, hili kwakweli si jambo jema .
Tumeshuhudia migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji.Kwa hiyo, mimi ningependa katiba hii mpya impe mfugaji haki katika suala la ardhi kama.Ardhi ya wafugaji ilindwe, ifafanuliwe kikatiba haki yao hiyo. Kuwe na hali ya 50,50 situation kati ya mfugaji na mkulima katika suala zima la umiliki wa ardhi,kikatiba!

Dkt.bilal ataka muungano wa serikali mbili katiba mpya

bilali 327ad
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal amekutana na ujumbe wa Tume ya Kukusanya Maoni ya Katiba Mpya iliyokuwa chini ya Mwenyekiti wake Jaji na Waziri Mkuu Mstaafu Joseph Sinde Warioba pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mkuu Mstaafu Agostino Ramadhan. Mheshimiwa Makamu wa Rais amepata fursa ya kukutana na Tume hiyo Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jaji Warioba kabla ya kumruhusu Mheshimiwa Makamu Wa Rais kutoa maoni yake, alimuelezea namna tume hiyo inavyofanya kazi na namna zoezi zima la kukusanya maoni ya mtu mmoja mmoja lilivyofanyika na kisha akaeleza kuwa, tume hiyo inaendelea na zoezi hilo kwa kukutana na makundi maalum sambamba na mtu mmoja mmoja kufuatia umuhimu wa hoja ambazo tume inakutana nazo na hivyo kuhitaji ufafanuzi.
 Katika muktadha huo, Jaji Warioba sambamba na kumpa fursa ya kuchangia maoni yake mengine anayopenda alimtaka Mheshimiwa Makamu wa Rais kujikita zaidi katika suala la Muungano kufuatia yeye kuwa na uzoefu wa kiuongozi katika serikali zote mbili yaani ya Muungano sambamba na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar.
 Akizungumzia suala la Muungano Makamu wa Rais Dkt. Bilal ameieleza Tume kuwa yeye ni muumini wa Muungano wa serikali mbili na kwamba haoni sababu ya kubadili mfumo uliopo kwa kuwa umeipatia tija nchi yetu na kuipambanua kama nchi yenye muungano wa mfano katika dunia. Pia alifafanua kuwa mfumo wa serikali mbili  umesaidia kujenga na kudumisha udugu, amani na utulivu baina ya wananchi wa Tanzania Bara na Visiwani kwa kipindi cha miaka 49 sasa.
 "Tanzania imechangia kitu kikubwa katika historia, kudumisha Muungano wa mfumo wa serikali mbili kati ya nchi mbili, kubwa na ndogo, jambo ambalo kwa nchi nyingine za Afrika wameshindwa. Kumekuwepo na nchi nyingi ambazo ziliungana na kushindwa kudumu kama tulivyo sisi. Hatuna haja ya kujifunza mfumo mpya wakati tulionao umeweza kudumu," alisema.
 Katika ujumbe wa tume uliofika kuchukua maoni ya Mheshimiwa Makamu wa Rais ni pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu Salim Ahmed Salim, Profesa wa Sheria Palamagamba Kabudi, Ndugu Simai Said, Ndugu Assa Rashid, Ndugu Sasmir Kyuki, Ndugu Salum Athuman, Ndugu Juma Mzalau na Mratibu wa Tume hiyo Ndugu Ramadhan Kailima.

No comments: