Thursday, February 14, 2013

ASKARI WA FFU ANAYETUHUMIWA KUFANYA MAUWAJI YA MWANGOSI MAHAKAMANI LEO

akipelekwa chumba cha kusikilizia kesi yake
 
Mtuhumiwa wa mauaji hayo Pacificus Cleophace Simon akiwasili mahakamani



akielekea mahabusu ya mahakama ya mkoa wa Iringa
akielekea katika chumba hicho

Katika pozi zake tofauti huku akisindikizwa na askari huyu

bado hataki sura yake itambuliwe kirahisi

Akitolewa mahakamani

akirudi mahabusu
mwili  wa marehemu Mwangosi  ukikanywagwa na askari waliokuwa  wakimsaidia mwenzao aliyejeruhiwa kwa bomu  lililomuua Mwangosi
ASKARI  kikosi cha kituliza ghasia (FFU )mwenye namba G2573 Pasificus Cleophace Simoni (23) anayetuhumiwa  kumuua  aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha Chanel Ten mkoani Iringa marehemu Daudi Mwangosi kupandishwa tena kizimbani leo katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Iringa.
Mtuhumiwa  huyo  leo anatarajia  kufikishwa tena mahakamani huku tayari mahakama hiyo chini ya hakimu Dyness Lyimo ikiwa imetoa onyo kwa askari  waliomfikisha mahakamani hapo mara ya mwisho  kutokana na kitendo cha kuidharau mahakamani  hiyo kwa kumtoa mtuhumiwa huyo ndani ya chumba cha mahakama kabla ya shughuli za mahakama kuhitimishwa .
Askari hao na mtuhumiwa  walionyesha kuidharau mahakamani  hiyo kwa kumtoa mtuhumiwa huku  mahakama ikiwa inaendelea na kupelekea hakimu kumwagiza wakili wa serikali kuwafuata askari hao na mtuhumiwa ili kurudi ndani ya chumba hicho na kuwahoji askari hao kwa kitendo walichokifanya kabla ya kuomba msamaha .

Kesi hiyo namba   namba 1 ya mwaka 2012 ya mauwaji hadi  sasa mtuhumiwa huyo amefikishwa mahakamani hapo zaidi ya mara nne na kesi hiyo ikiendelea  kutajwa .

Mtuhumiwa  huyo anatuhumiwa  kumuua kwa  kwa   bomu aliyekuwa  mwandishi  wa habari wa Chanel Tena  mkoa  wa Iringa  marehemu Mwangosi  septemba 2 Septemba mwaka jana  katika kijiji cha Nyololo Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa  wakati  wa vurugu kati ya  polisi na wafuasi wa  Chadema .kinyume na kifungu cha sheria namba 148 kifungu kidogo 5A.i cha makosa ya jinai. Kwa mujibu wa kesi za jinai, sheria kifungu 196 kanuni ya adhabu Cap. 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002, 
- Iringa

ccm na gesi ya mtwara

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza na waaandishi wa habari juu ya Tamko la Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM,katika ukumbi wa Sekretarieti, mjini Dodoma.Picha zote na Adam Mzee-idara ya itikadi na Uenezi-CCM

1.       Halmashauri Kuu ya Taifa imepokea maelezo ya Serikali kuhusu maandamano na vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara tarehe 27 Desemba, 2012 tarehe 25 Januari, 2013 na tarehe 26 Januari, 2013. Maandamano na vurugu hizo zilizodaiwa kuwa na lengo la kupinga mradi wa bomba la Gesi kujengwa na kupeleka Gesi Dar es Salaam.

2.       Baada ya kupokea maelezo haya ya Serikali, Halmashauri Kuu ya Taifa imebaini kuwa: -

(a)           Kwa sehemu kubwa Wananchi wa Mkoa wa Mtwara hawakuwa wamepewa elimu ya kutosha juu ya uendelezaji wa Gesi na jinsi watakavyonufaika.

(b)           Baadhi ya Wanasiasa na baadhi ya Viongozi wa Makundi mbalimbali waliamua kutomia suala la Gesi kupandikiza lugha za chuki, uchochezi na upotoshaji wa maendeleo ya Mradi wa Gesi kwa lengo la kujitafutia umaarufu.

(c)            Suala la Gesi limetumika kama kisingizio tu cha kufanya vitendo vya rurugu na uvunjifu wa amani.



3.       Kutokana na ukweli huu, Halmashauri Kuu ya Taifa inaelekeza ifuatavyo:-

(i)             Imesikitishwa na vurugu zilizotokea na kusababisha watu kadhaa kupoteza maisha na uharibifu mkubwa wa mali  na majengo  ya CCM, Serikali, Wabunge na watu binafsi. Halmashauri Kuu ya Taifa inawapa pole wafiwa na waliopoteza mali zao.

(ii)      Inaiagiza Serikali kufanya uchunguzi wa kina kuhusu waliofanya vurugu na uharibifu mbalimbali na kuwachukulia hatua kwa mujibu wa Sheria. Pia, kuwa makini na kuhakikisha matukio kama haya hayajitokezi tena.

(iii)        Inaiagiza Serikali kuendelea kutoa elimu ya kutosha kwa Wananchi wa maeneo husika  kuhusishwa na kuelimishwa juu ya miradi mbalimbali kwenye maeneo yao.

(iv)        Halmashauri Kuu ya Taifa inawataka Wananchi wa Mkoa wa Mtwara kuendelea kuishi kwa amani na utulivu kama ilivyo desturi yao, maana vurugu pamoja na kuharibu mali na kugharimu maisha  vinaweza kuwakimbiza wawekezaji waliojitokeza na ambao  shughuli zao zitawafaidisha  wananchi wa Mkoa huu na Watanzania kwa ujumla .

HALMASHAURI KUU YA TAIFA
Dodoma 10 – 11 Februari,2013

Dhahabu Ikiisha Tutawapeleka Wapi Wafanyakazi Wetu?

images 00a5a
Mikataba ya kuchimba dhahabu hapa nchini ilianza kusainiwa na serikali ya awamu ya tatu ya Mzee Benjamen William Mkapa; mikataba hii imesainiwa katika taratibu na mazingira ya kifisadi kwa vile kwanza muda wa mikataba ni miaka 99 na murahaba wa asilimia tatu (3%), mikataba ya aina hii haipo popote pale duniani zaidi ya hapa kwetu Tanzania! Sasa mimi najiuliza kwamba hivi Mkapa alikuwa anafikiria nini kusaini mikataba ya asilimia tatu tena kwa kipindi cha miaka 99 wakati alikuwa anajua kwamba yeye amechaguliwa kwa kipindi cha...

miaka 10 tu! Je, alijiona kwamba amepata wawekezaji wajinga sana kiasi kwamba wamekubali
kutoa asilimia tatu hivyo aliona akiwaachia hawawezi kupatikana tena!? Na ndiyo maana akaona
madhali wamekubali kusaini mikataba basi asiwape nafasi bali awagandamize kwa kuwapa
mikataba ya miaka 99! Mimi ninavyooona hata hiyo asilimia tatu hatuipati kulingana na hali
halisi ya ufisadi uliopo hapa nchini, kama kuna kitu tunachopata kutoka katika mikataba hii
ya kifisadi ya dhahabu haiwezi kuzidi nusu asilimia kwa mwaka (0.5%)! Ni kwanini Mkapa
asingelisaini mikataba hata ya zero point one percent (0.1%) lakini iwe mkataba wa miaka 10 tu!
Tukiachana na mambo ya asilimia (murahaba) ambayo nitayachambua baadae katika makala
hii, ningependa nijaribu kuzungumzia hujuma zinazofanywa katika migodi yetu; migodi yetu
ya dhahabu inafanyiwa hujuma ambazo huwezi kuamini kama nchi hii kweli ina wenyewe, na
hata kama wapo wenyewe lakini hawapo hai bali watakuwa wameshakufa! Nasema hivyo kwa
vile kulingana na taratibu za uchumbaji wa madini duniani, hasa tukijifunza kutoka kwa nchi
kiongozi wa uchumbaji wa madini duniani ya Afrika ya Kusini; mgodi wa madini ya aina yoyote
ile ni lazima uwe umeajiri wafanyikazi ambao hutekeleza majukumu mbali mbali katika mgodi
huo kulingana elimu au ujuzi waliokuwa nao, hawa wote ni wafanyikazi ambao wanautegemea
mgodi huo kwa ajili ya kupata mishahara na kutunza familia zao; baadhi ya wafanyikazi ni
vijana ambao hawana familia na wengine ni watu wazima ambao wana familia zinazowategemea
ikiwa ni pamoja na kusomesha watoto, matibabu, kuwalisha na kuwavalisha, hivyo jinsi
shughuli za mgodi zinavyodumu kwa muda mrefu ndiyo ambavyo wafanyikazi wanavyoishi
maisha mazuri ikiwa ni pamoja na kuzimudu familia zao. Kwa serikali yoyote ile makini lazima
ihakikishe kwamba inalinda ajira za wananchi wake kwa kuhakikisha kwamba umri wa mgodi
unadumu kwa muda mrefu kadri inavyowezekana ili kuendelea kutoa ajira kwa wafanyikazi


MAHAKAMA KUU INAYOENDELEA NA KIKAO CHAKE MBOZI YAMHUKUMU KUNYONGWA HADI KUFA MSHTAKIWA



Mahakama kuu kanda ya Mbeya imemhukumu  PETER MWAFRIKA mkazi wa  Ndolezi wilayani Mbozi kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kuua kwa kukusudia.
Akisoma hukumu hiyo iliyochukua saa 1.30 Jaji mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya mbeya  NOEL CHOCHA amesema licha ya mikono ya mahakama kufungwa kutoa adhabu ndogo kwa kosa la maauaji ya kukusudia, pia adhabu hiyo ni hatua ya kukomesha watu wenye tabia kama za mtuhumiwa kujichukulia hatua mikononi mwao.
Akirejea mazingira ya kesi hiyo jaji Chocha amesema mnamo Februaly 11,2010 mshatakiwa na wenzake watatu walifanya kosa la mauaji ya kukudia chini ya kifungu 196 chasheria ya mwenendo wa makosa ya jinai  kwa kumuua KOSAM MWAFRIKA ambaye ni kaka wa marehemu  katika kijiji cha Shaji kwa kumkata koromeo na kulitenganisha vipande viwili.
Jaji Chocha katika maelezo yake alisema mshtakiwa akiwa na wenzake ambao walitoweka baada ya mauaji hayo walimvamia Kosam akiwa na mkewe shambani kwake eneo la Zanzule, Ndolezi na kisha kumkamata marehemu kwa maelezo kuwa walikuwa wametumwa kumkamata ili wampeleke polisi kwa kosa la wizi wa Ng'ombe.
Hata hivyo katika mabishano shambani hapo, marehemu na wenzake walitamka wazi kuwa walikuwa wametumwa kumuua marehemu hivyo kuongeza nguvu za ushahidi wa kumtia hatiani.
sababu za mauaji hayo ni ugomvi wa muda mrefu uliokuwepo kati ya marehemu na mama yake mzazi wa mshtakiwa ambao walikuwa wakigombea ardhi,(wote ni ndugu) na kwamba siku moja kabla ya tukio hilo kulikuwa na kesi katika mahakama ya mwanzo Mlowo iliyokuwa imefunguliwa na Mama mzazi wa mshatakiwa.
Inaelezwa pia kuwa wakiwa njiani kumpeleka polisi, baada ya kubaini kuwa kuna watu wanawafuatilia ghafla mtuhumiwa mwingine (ambaye hakuwepo mahakamani) alimkata marehemu panga la shingo na kumfanya marehemu akose nguvu na kuanguka, hata hivyo kwa kuonyesha kutoridhika na hali hiyo mtuhumiwa aliongezea kwa kumkata marehemu na panga kwenye koromeo na kulitenganisha kabisa.
Jaji kabla ya kutoa hukumu alirejea mazingira ya tukio hilo na kujiridhisha na miongozo, viini vya shauri la mauaji na hoja zilizotolewa na washauri wa mahakama ambapo ilithitika kuwa kulikuwa na dhamira ya mauaji na  tendo la mauaji lilifanyika 
Katika ushahidi wa shauri hilo jumla ya mashahidi watatu waliletwa mahakamani akiwemo kaka wa mshtakiwa ambao wawili kati yao walithibitisha pasipo shaka kwamba mshtakiwa  Peter kuhusika na tukio la kumuua kwakukusudia Kosam .
Katika utetezi wake wakili wa mshtakiwa ZAKIA SULEIMAN aliiomba mahakama impe adhabu nafuu mshtakiwa kutokana na umri wake mdogo hivyo mchango wake kuhitajika katika ujenzi wa taifa, pamoja na kuwa na wategemezi wakiwemo wake wawili na watoto wane.
Serikali iliwakilishwa na Wakili  Rogers Francis
katika hatua nyingine jaji Chocha aliamua kufanya kazi ya kutoa elimu mahakamani humo, akirejea matukio yaliyojitokeza hivi karibuni wilayani Momba na Mbozi aliyoyaita ni yanafanywa na watu wasiopenda ama hawana habari na Utawala wa sheria yakiwemo kuwazika watu wakiwa hai, ambapo amesisitiza hali hii inaonyesha kuwepo kwa watu waliovuka kiwango cha ukatiri katika jamii.
amesema hali ya kushamiri mauaji wilaya za Mbozi  na Momba kuhaonyesha namna jamii na watu wenye tabia kama za mshitakiwa wasivyopaswa kuvumilika mbele ya sheria na kwamba adhabu hiyo itasaidia kuwaelimisha wengine wenye mitazamo kama ya mshtakiwa Peter Mwafrika.
Habari kwa hisani ya Danny Tweve Mbozi


Fistula inatibika

FISTULA PRESS AD-01 100b1

Finland yataka nchi ilinde matumizi ya maliasili


images
BALOZI wa Finland nchini, Sinikka Antila, amewetaka viongozi wa Tanzania kusimamia vizuri matumizi ya maliasili kutokana na maliasili  hizo, kuwa ndiyo ufunguo wa ukuaji wa maendeleo ya nchi.
Antila alitoa kauli hiyo, jijini Dar es Salaam jana, wakati wa mkutano uliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi, kwa ajili ya uzinduzi wa Jukwaa la Uchumi wa Kijani, uliowakutanisha  viongozi wa taasisi mbalimbali kujadili ushirikishwaji wa jamii katika kusimamia ukuaji wa uchumi.


LOWASSA AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUREJESHA AMANI KATI YA WAISLAMU NA WAKRISTO


WAZIRI Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, amewataka viongozi wa dini nchini kusaidia kurejesha hali ya amani kati ya Waislamu na Wakristo ambayo inaonekana inaanza kupotea.

Akizungumza nyumbani kwake Monduli, wakati akipokea ujumbe kutoka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kusini Mashariki mwa Ziwa Victoria, Lowassa alisema vurugu na mauaji yaliyotokea huko Buseresere mkoni Geita yanasikitisha sana na kuongeza kuwa ni dalili mbaya ya kutoweka kwa amani ya Tanzania.

``Rais ameelezea masikitiko yake, kwa kweli inasikitisha sana, mimi nawaomba viongozi wa dini na madhehebu yote wasimamie kuzuia mambo haya, nawaomba Watanzania wenzangu tusali kwa imani zetu kuomba amani yetu isipotee,” alisema.

Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, aliongeza kuwa Watanzania wameoleana, wamekuwa wakiishi pamoja kwa miaka yote bila kubaguana kwa misingi ya dini, rangi wala kabila, na kuhoji haya mambo yanatoka wapi.

Alisema kuwa Tanzania imekuwa ni mfano wa kuigwa kote dunia kutokana na amani iliyopo, ambayo ni matunda ya uongozi wa waasisi wa taifa hili hayati Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Aman Karume.

Katika fujo hizo za Buseresere, mchungaji mmoja wa kanisa aliuawa baada ya kuzuka kwa mapigano kati ya Waislamu na Wakristo, chanzo kikiwa ni Wakristo kuamua kuchinja ng’ombe na kuuza kwenye bucha yao, hatua iliyopingwa na Waislamu.

Ujumbe huo uliofika nyumbani kwa Lowassa uliongozwa na msaidizi wa askofu mteule wa KKKT dayosisi hiyo, ulimshukuru kutokana na kusimamia na kuendesha harambee ya ujenzi wa kanisa kuu la Shinyanga Januari mwaka jana ambapo zaidi ya sh milioni 200 zikiwa ni fedha taslimu pamoja na ahadi zilipatikana.

KATA, TARAFA, JIMBO BORA KWA USALAMA 2012 ZAPEWA TUZO

IGP-SAID-MWEMA
Na. Christina Mponji-Jeshi la Polisi, Dodoma.
………………………………………………………
Wito umetolewa kwa Majimbo, Tarafa na Kata zote nchini kuimarisha dhana ya Polisi jamii na ulinzi shirikishi katika maeneo yao, ili kukabiliana na vitendo vya uhalifu kuanzia ngazi ya familia ambako ndiko hasa chimbiko la uhalifu.
Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IJP Said Mwema, wakati akitoa tunuku ya hati ya utendaji bora kwa Kata/Shehia, Tarafa, na Jimbo  zilizofanya vizuri katika mapambano dhidi ya uhalifu nchini kwa mwaka 2012.

Tuzo hizo zimetolewa  katika Mkutano Mkuu wa Maofisa wakuu Waandamizi wa Jeshi la Polisi unaoendelea mjini Dodoma katika ukumbi wa Pius Msekwa, ikiwa ni sehemu ya  utekelezaji wa mpango wa maboresho ndani ya jeshi hilo.
Kata zilizofanya vizuri ni pamoja na kata ya Bukwe Mkoa wa kipolisi  Tarime Rorya, Kizwite ya mkoani Rukwa, Isansa ya mkoani Mbeya, pamoja na shehia ya Ng’omeni kutoka mkoa wa Kaskazini Pemba.
Tarafa zilizofanya  vizuri ni tarafa ya Girango ya mkoa wa kipolisi Tarime Rorya, Lwiche ya mkoani Rukwa, Igamba ya mkoani Mbeya pamoja na Jimbo la Mji Mkongwe la Mkoa wa Mjini Magharibi visiwani Zanzibar ambapo tuzo hizo zimepokelewa na makamanda wa mikoa hiyo  kwa niaba ya kata/shehia na tarafa/majimbo yao.
IJP Mwema amesema, endapo kata na tarafa zote nchini zitaimarisha dhana ya ulinzi shirikishi na polisi jamii, ni wazi kuwa matukio ya uhalifu yatapungua kwa kiasi kikubwa na hatimaye kuwa historia.
Akiongea katika hafla hiyo Mkuu wa Huduma za Polisi Jamii, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Lazaro Mambosasa alisema kuwa kata na tarafa zilizofanya vizuri, zilikuwa na kiwango kikubwa cha  matukio ya kihalifu lakini kupitia dhana ya ulinzi shirikishi na polisi jamii wamefanikiwa kudhibiti vitendo hivyo huku akitolea mfano kata ya Bukwe ambako kulikuwa na migogoro ya kikabila, na hivi sasa migogoro hiyo imekoma kabisa.  
Akiongea kwa niaba ya wenzake, kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya  kamishna Msaidizi Diwani Athumani, amesema jamii sasa imeanza kuelewa umuhimu wa kushirikiana na jeshi la polisi katika mapambano dhidi ya uhalifu na kwamba wamekuwa mstari wa mbele katika kuhamasishana juu ya uanzishwaji wa vikundi vya ulinzi shirikishi.
Jeshi la polisi limekuwa likifanya jitihada mbalimbali za kuimarisha hali ya ulinzi na usalama kuanzia ngazi ya kata/shehia, ambapo hivi karibuni wametoa pikipiki kwa wakaguzi tarafa ili kuwarahisishia utendaji katika tarafa zao.

UKIFIKA MBEYA TU? KARIBUNI WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA MJIONEE MAAJABU YA MUNGU

ZIWA KISIBA (MASOKO) WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA
ZIWA NGOSI WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA. KATI YA MAAJABU KUMI NA TISA YANAYOPATIKANA WILAYANI RUNGWE MAYA MAZIWA NI SEHEMU YA MAAJABU YALIYOAINISHWA KAMA SEHEMU KUU YA UTALII. MAZIWA HAYA YAPO JUU YA MILIMA NA HAYANA SEHEMU YA KUINGILIA MAJI WALA MAJI KUTOKA HATA KUPUNGUA KWA KINA CHA MAJI WALA KUONGEZEKA
 
MUONEKANO WA MLIMA RUNGWE

No comments: