Monday, February 25, 2013

BAADA YA SAFARI YA SIKU KADHAA NIMERUDI LEO MCHANA KAZINI SAMAHANI KWA WADAU WA KINGO TANZANIA KWA USUMBUFU WA KUTOPATA HABARI KWA SIKU KADHAA HIZO

USAFIRI LEO ASUBUHI KATIKA BARABARA YA KYELA , TUKUYU HADI  MBEYA KULIKUWA WA SHIDA HADI KUFIKIA WATU KUSAFIRI KWA SHIDA

HAKUNA KAZI HAPA NI KUUCHAPA USINGIZI TU

NIKIWA SAFARI NIKAKUMBANA NA MGOMO WA WASAFIRISHAJI NA SASA IMEKUWA SHIDA SANA KILA KUKICHA MADEREVA NI KUGOMA NA HUU MGOMO NI WA TATU KWA MWAKA HUU
NIMEFIKA SALAMA HOME NA KWAKUWA  KAZI NYINGI HAKUNA KUPUMZIKA NIPO OFISIN NAPIGA KAZI KARIBUNI SANA OFISIN KWA MDAU WENU KINGO

 

MHANGA WA UMEME IRINGA AENDELEA NA MATIBABU KATIKA HOSPITALI YA RUFAA


AJALI YA UMEME 31d91
Ndg. Selemani Mbuma aliepata ajali mbaya ya Umeme hiv ikaribuni bado yuhai akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Rufaa Iringa word namba 9 Pichani mkewe Bi Haule akishirikiana na wauguzi kumuhudumia mume wake Ndugu huyu anahitaji msaada zaidi wamtibabu kulingana na hali alionayo baadaya ajali. PICHA NA SAID NG'AMILO


Maaskofu wa mkoa wa Mbeya wakiwa ofisini kwa mkuu wa mkoa Mbeya wakijadiliana jinsi ya kuimarisha amani katika mkoa wa Mbeya
Maaskofu wa mkoa wa Mbeya wakiwa ofisini kwa mkuu wa mkoa Mbeya wakijadiliana jinsi ya kuimarisha amani katika mkoa wa Mbeya
OFISIN KWA MKUU WA MKOA WA MBEYA MAZUNGUMZO YAKIENDELEA KATI YA SERIKALI NA BARAZA LA MAASKOFU MBEYA
 


Polisi yatangaza dau aliyemuua Padri Mushi


IGP Said Mwema 

Padri Mushi aliuawa kwa kupigwa risasi Jumapili iliyopita wakati akienda kuongoza ibada katika Kanisa la Mtakatifu Teresia lililopo Beit el Ras nje kidogo ya mji wa Zanzibar, ambapo inadaiwa kuwa waliomuua walikuwa wamepanda pikipiki aina ya Vespa na walimfyatulia padri huyo risasi tatu akiwa ndani la gari yake.

WAKATI kukiwa na taarifa kwamba maofisa wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) wametua nchini kwa ajili ya kufanya upelelezi wa mauaji ya Padri Evarist Mushi, Jeshi la Polisi limetangaza dau la Sh10 milioni kwa atakayefichua aliyemuua padri huyo.
Padri Mushi aliuawa kwa kupigwa risasi Jumapili iliyopita wakati akienda kuongoza ibada katika Kanisa la Mtakatifu Teresia lililopo Beit el Ras nje kidogo ya mji wa Zanzibar, ambapo inadaiwa kuwa waliomuua walikuwa wamepanda pikipiki aina ya Vespa na walimfyatulia padri huyo risasi tatu akiwa ndani la gari yake.
Wakati polisi wakitangaza dau hilo, Sheikh Ali Khamis Ali (65) mkazi wa Kitope Kaskazini Unguja, aliuawa jana kwa kukatwa mapanga mjini Zanzibar, baada ya wezi kuvamia shambani kwake.
Habari za kuaminika zilizopatikana juzi zinaeleza kuwa maofisa hao wa FBI, wako nchini na tayari na wamekutana na baadhi ya viongozi wa Serikali kwa ajili ya kuanza kazi hiyo.
Chanzo chetu cha habari kimeeleza kuwa maofisa hao walikutana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi kwa ajili ya kuangalia ni namna gani watafanya shughuli zao katika upelelezi huo.
Pamoja na ushiriki FBI, taarifa zinaeleza kuwa maofisa wa Serikali ya Tanzania wamezungumza na taasisi za upelelezi za nchi tano, ili kuongeza nguvu katika upelelezi huo.
Taasisi nyingine inayotajwa kuwa huenda ikashiriki katika uchunguzi huo ni Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai ya Uingereza (Scotland Yard).
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alilithibitishia gazeti hili kwamba Serikali imeanza kufanya mazungumzo na mashirika mbalimbali ya upelelezi duniani kwa ajili ya kushirikiana nayo kuchunguza mauaji ya Padri Mushi, lakini akasema kuwa ni mapema mno kuyataja.
“Tumefuata maagizo aliyotoa Rais Kikwete kwamba tushirikishe mataifa mbalimbali kuchunguza mauaji yaliyotokea Zanzibar, siwezi kutaja kwa majina, ila tayari tumeanza kuzungumza na nchi mbalimbali,” alisema Silima.
Akizungumza mjini Zanzibar jana, Kamishna wa Polisi visiwani humo, Mussa Ali Mussa alisema kuwa hadi sasa hakuna mtu aliyefikishwa mahakamani kuhusiana na tukio hilo la mauaji.
“Hakuna aliyefikishwa mahakamani, lakini wapo watu ambao wamekamatwa wakihusishwa na tukio hili na tunaendelea kuwahoji, wengine tunawaachia,” alisema na kuongeza:
“Tumeahidi kutoa Sh10 milioni kwa mtu yeyote, atakayetoa taarifa za mauaji ya Padri Mushi, hii itakuwa kama zawadi tu.”

WAZIRI MKUU AUNDA TUME KUCHUNGUZA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE

wpid-Prime-Minister-Mizengo-Pinda
 WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ameunda Tume maalum itakayofanya uchunguzi wa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne ambayo yalitangazwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa Februari 18, mwaka huu. 
Katika matokeo hayo yaliyotangazwa Jumatatu wiki hii, asilimia 60 ya wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha nne Oktoba, 2012 walifeli.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Peniel Lyimo amesema Tume hiyo ambayo inatarajiwa kuanza kazi wakati wowote wiki ijayo inajumuisha wadau kutoka Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi (Tanzania Association of Managers and Owners of Non-Government Schools/Colleges (TAMONGSCO), Taasisi za Dini zinazotoa huduma ya elimu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Asasi zisizo za Kiserikali (NGOs) zinazoshughulikia masuala ya elimu.
Wadau wengine watatoka Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii na Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA).
Amesema Serikali inawaomba wadau wa elimu, wazazi, walezi na wananchi wote kwa ujumla watoe ushirikiano kwa Tume ili iweze kufanya kazi yake kwa ufanisi.

KIMENUKA:TFF YATAKIWA KUFUTA MATUMIZI YA KATIBA YA MWAKA 2012


1
  
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
SERIKALI imeliagiza  Shirikisho la Mchezo wa Mpira wa Miguu nchini (TFF)  kufuta matumizi ya Katiba ya Shirikisho hilo  ya mwaka 2012 badala yake watumie Katiba ya mwaka 2006 kwa kuwa Katiba ya mwaka 2012 imekiuka kanuni  za Sheria ya Baraza la Michezo la Taifa ( BMT) Na.11 (1).
Agizo hilo limetolewa leo na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mhe. Dkt. Fenella Mukangara alipokuwa akiongea na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam kuhusu mgogoro wa uchaguzi wa Viongozi wa TFF.
Dkt. Mukangara  pia ameiagiza TFF kufuata utaratibu wa kurekebisha Katiba za vyama vya michezo, kwa mujibu wa Sheria ya BMT iliyotungwa na Bunge pamoja na kanuni zake ambazo ziko wazi na rahisi kuzifuata.

Alifafanua kuwa TFF walikiuka Sheria Na. 12 ya Baraza la Michezo la Taifa na marekebisho yake Na.6 ya mwaka 1971 pamoja na kanuni za usajili Na. 442 za mwaka 1999.
“Kanuni ya BMT Na. 11(1) inaeleza wazi utaratibu wa marekebisho ya Katiba ambapo walitakiwa wajaze Fomu Na. 6,7,8 na 9 kisha baada ya siku 14 Msajili wa vyama vya michezo anatakiwa kuwajibu, kama anakubali anatumia Fomu Na. 11 na kama anakataa anatumia Fomu Na. 10 lakini TFF walikiuka yote haya.” Ameeleza Dkt. Mukangara

Aidha, Dkt Mukangara ameiagiza TFF kufanya uchaguzi wa Viongozi kwa mujibu wa Katiba ya mwaka 2006 kwa kuzingatia Sheria na Kanuni za BMT  na kama kuna umuhimu wa kurekebisha Katiba  waitishe mkutano Mkuu  kwa kufuata misingi ya Katiba yao ya mwaka 2006 na kanuni za BMT  kwa ajili ya kufanya maboresho hayo.

Akizungumzia taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari kuwa FIFA watakuja nchini kufuatilia mgogoro wa TFF, Waziri amemwagiza  Msajili  wa Vyama vya michezo pamoja na TFF kuwataarifu FIFA kuhusu maelekezo yake ya kutumia Katiba ya mwaka 2006 na wawaeleze hali halisi  iliyojitokeza.

Amesema kuwa hakuna chama chochote cha michezo nchini kilicho juu ya BMT, hivyo vyama vyote na vilabu vyote  vya michezo  viendelee na shughuli zao za kuendeleza michezo kwa kuzingatia Sheria na Kanuni za BMT pamoja na Katiba zao.

Kumekuwepo na mgogoro katika mchakato mzima wa uchaguzi wa Viongozi wa TFF ikiwemo baadhi ya wagombea kulalamika kuenguliwa  na wadau mbalimbali kulalamika kuwa haki haikutendeka na wengine kuonyesha wazi  kutofuatwa kwa utaratibu wa kurekebisha Katiba hali iliyopelekea Wizara yenye dhamana ya michezo kwa kushirikiana na  BMT kuingilia kati hasa katika suala la ukiukwaji wa marekebisho ya Katiba.





No comments: