Friday, February 22, 2013

TAMKO LA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA WA MBEYA KUHUSU UCHOCHEZI WA KIDINI

MWENYEKITI
KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA-MBEYA
NORMAN SIGALLA 
BAADHI YA VIONGOZI WA
KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA-MBEYA
MWANDISHI WA HABARI FELIX MWAKYEMBE AKIULIZA SWALI KWA KAMATI HIYO
EMMANUEL LENGWA  MWANDISHI  AKIULIZA SWALI KWA KAMATI HIYO YA ULINZI YA MKOA WA MBEYA
MOJA YA WANAKAMATI YA ULINZI MKOA WA MBEYA KAMADA DIWANI AKIJIBU BAADHI YA MASWALI YALIOULIZWA NA WAANDISHI WA HABARI 


TAMKO LA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA WA MBEYA KUHUSU UCHOCHEZI  WA KIDINI
Kwanza kabisa tungependa kutoa pongezi kwa Viongozi na Waumini wa Dini na Madhehebu mbalimbali hapo Mkoa Mbeya kuendeleza utamaduni wetu wa kuishi na kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kijamii. Bila kuweka hisia za udini. Tunawashukuru kwa kuendelea kuvumiliana. Pamoja na kuendelea katika hali hii, kumejitokeza viashiria mbalimbali vyenye kuonyesha dalili za kumomonyoka kwa maadili, katika Mkoa wetu.
    2.   Kumejitokeza baadhi ya viongozi wa dini ambao wamekuwa   
Wakuzitumia nyumba zetu takatifu za Ibada kuhubiri mambo  ambayohayahusiani kabisa na mambo yanayohusu Mwenyezi Mungu na mafundisho yake, kwa kuhubiri mambo ya siasa za chuki kwa dhamira ya kupandikiza chukidhidi ya Serikali au dini na madhehebumengine. Baadhi yao wamediriki kuyasema hayo hadharani kwenye miadhara yao au mikusanyiko ya waumini wao.
   Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya inaona hali hii haina  
   afya njema kwa mustakabali wa amani na utulivu wa Mkoa wetu na    
   Nchi kwa ujumla.
3.               Pamoja na mahubiri hayo pia kumekuwepo nyaraka mbalimbali za kimaandishi za sauti katika kanda, CD zenye kuhubiri chuki, uchochezi dhidi ya dini au dhehebu lingine. Kumekuwepo na video katika kanda, CD au DVD zenye kuhubiri chuki, uchochezi, dharau na kebehi dhidi ya dini nyingine au Serikali na baadhi ya kanda hizo zimediriki kuhamasisha waumini wake vurugu na hata kuua jambo ambalo Kamti ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya inaamini hakuna dini ya aina yoyote dunianiinayohimiza waumini wote kutumia kwa jambo lolote lile.
4.               Baada ya kutafakari, Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa  Mbeya imeamua yafuatayo:- inapiga marufuku:
(i)               Kuuza, kusambaza au kuonyesha, Kanda za sauti CD za sauti, Kanda   
za Video, CD, DVD, nyaraka na maandiko yoyte yenye uchochezi wa aina yoyote ile au kukashifu dini yeyote katika Mkoa wa Mbeya.
(ii)             Chombo chochote cha Habari kilichopo Mkoani Mbeya kiepuke   
           kuandika makala, kunakili au kurusha hewani hotuba, mahubiri au   
           kuonyesha video zenye kuchochea, kudharau, kuhubiri au kukashifu 
           dini yoyote ile 
5.       Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa inawaasa viongozi wa dini
 Mbalimbali kutohubiri siasa kwenye majumba ya Ibada kwani kwa   
 kufanya hivyo watakuwa wanakiuka sheria za nchi. Mtawagawa       
 waumini wenu kwa sababu waumini wanaelewa hayo si maagizo ya 
 Mungu, na hayamo kwenye vitabu vitakatifu.
6.       Waandishi wa Habari epukeni kushabikia matamko ya Viongozi wa   
          Dini au Siasa yenye kulenga kuleta mgawanyiko katika taifa hili kwa  
          Misingi ya kidini au kisiasa kwa kisingizio cha Uhuru wa Habari,  
          kumbukeni Amani Umoja na Mshikamano wa Mkoa na Taifa
          utategemea mchango wenu katika kushabikia au kukemea kauli hizo
          bila kujali zimetolewa na kiongozi gain.
Mwisho, Serikali itamchukulia hatua za kisheria mtu yeyote atakayekwenda kinyume na haya, bila kujali itikadi yake, dini yake au wadhifa wake. Wananchi wanaaswa kuzikabidhi nyaraka, kanda CD na DVD kwa ofisi za Serikali ngazi ya Vijiji, kata Wilaya na Mkoa au kituo chochote cha Polisi. Endapo watakabidhi kwa hiyari hawatachukuliwa hatua.
Imetolewa na:
MWENYEKITI
KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA-MBEYA
 

VIONGOZI na Watumishi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya wametakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano na vyama vya siasa vya upinzani ili kuwaletea maendeleo wananchi.


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dk. Norman Sigalla ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya wakati akifungua warsha juu ya Demokrasia na Stadi za uongozi inayotolewa kwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi pamoja na Madiwani wa Mkoa wa Mbeya.
Mwaandaaji wa Mafunzo hayo Dk. Marry Mwanjelwa Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Mbeya

Mfadhili wa Mafunzo hayo Dk. Stefan Chrobot ambaye ni Mkurugenzi Mkazi wa shirika la Fes- Tanzania kutoka Ujerumani 

Katibu wa CCM wilaya ya Mbeya mjini, Raymond Mwangwala,






VIONGOZI na Watumishi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya wametakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano na vyama vya siasa vya upinzani ili kuwaletea maendeleo wananchi.
Hayo yamesemwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dk. Norman Sigalla ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya wakati akifungua warsha juu ya Demokrasia na Stadi za uongozi inayotolewa kwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi pamoja na Madiwani wa Mkoa wa Mbeya.
  
Dk. Sigalla alisema Chama cha Mapinduzi ni mlango wa kuingilia ili kupata uongozi ili kuwahudumia wananchi lakini siyo sababu ya kuwachukia viongozi wa vyama vya upinzani.
  
" Si sahihi kugombana na na kiongozi wa chama kingine bali shirikianeni ili muwaletee maendeleo wananchi ambapo mtakapokuwa na ushirikiano na upendo ndipo watakapo watamani na kuhamia kwenye chama chenu" alisema Mkuu huyo.
  
Aliongeza kuwa Warsha zinazotolewa kwa viongozi zinasaidia kuwakumbusha wajibu wao kwa chama na kwa wananchi ili wasijisahau katika utendaji kazi wa kila siku ikiwa ni pamoja na kutekeleza Ilani za Chama.
Alisema kazi ya kiongozi wa Chama ni kujibu hoja za wananchi na siyo kiongozi kujifanyia mambo ambayo wananchi hawayahitaji na ambayo yanasababisha kuwachukia viongozi.
  
Kaimu Mkuu wa Mkoa huyo alisema ili Chama kiendelee kubaki madarakani ni wajibu wa Viongozi waliopewa dhamana na wananchi kuyatendea kazi madai yao ambayo yataepusha migogoro isiyokuwa na sababu.
  
Kwa upande wake Mwaandaaji wa Mafunzo hayo Dk. Marry Mwanjelwa Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Mbeya alisema mafunzo hayo yanafanyika ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya mkutano mkuu wa wajumbe wa CCM Taifa walioagizwa kuwajengea uwezoviongozi wa Chama.
  
Alisema lengo la kutoa mafunzo hayo ni kuwakumbusha viongozi waliokuwepo madarakani kuhusu uwajibikaji pamoja na kuwajengea uwezo viongozi wapya walioingia madarakani hivi karibuni.
  
Naye mfadhili wa Mafunzo hayo Dk. Stefan Chrobot ambaye ni Mkurugenzi Mkazi wa shirika la Fes- Tanzania kutoka Ujerumani alisema wameamua kufadhili mafunzo hayo kutokana na shirika hilo kuwa na ushirikiano na Chama cha Mapinduzi.
  
Alisema kazi ya Shirika hilo ni kukuza demokrasia na utawala katika jamii, kuinua haki za binadamu za kupata huduma muhimu za kijamii na namna ya kuepukana na rushwa.
Na Mbeya yetu 

Baada ya matokeo yasiyoridhisha msimamizi wa mtandao huu Ally Kingo nimepotelewa na mjomba wangu Atupakisye mwalwega baada ya matokeo sijui aliko huku Vigogowa hapa nchini wakitema cheche    


 MWANANCHI
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Lowassa alisema matokeo hayo ni aibu kwa taifa na kuilaumu Serikali kwa kuzitelekeza shule za sekondari za kata.Alisema taifa kwa sasa linazalisha wabeba kuni na maji na siyo wasomi ambao wanaweza kushindana kwenye soko la ajira.

WAKATI Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akiinyooshea kidole Serikali kwa kuzitelekeza shule za sekondari za kata, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa amesema hatajiuzulu ng’o kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne. Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha), nalo limetishia kuitisha maandamano ya nchi nzima kwa kushirikisha wanafunzi wote waliopata sifuri ikiwa waziri huyo hatajiuzulu. Taifa limeshikwa na mshtuko kutokana na matokeo hayo ambayo yanaonyesha kuwa asilimia 60 ya wanafunzi waliofanya mtihani huo mwaka jana, walipata sifuri.

Dk Kawambwa
Akizungumza jana katika uzinduzi wa Mpango Maalumu wa Mafunzo ya Kompyuta katika Shule ya Msingi ya Majengo wilayani Bagamoyo, Dk Kawambwa alisema hawezi kuachia ngazi kwa shinikizo la
wanasiasa.

Alisema yeye si wa kulaumiwa kutokana na wanafunzi hao kufanya vibaya kwenye mtihani wa kidato cha nne na kwamba wanaosema waziri anapaswa kujiuzulu hawana hoja za msingi zaidi ya kutaka kujipatia umaarufu kwa kudandia hoja zinazokuwapo kwa wakati husika.
“Unajua katika mfumo wa vyama vingi, kila linapotokea jambo baya basi wanaona dawa ni kiongozi mhusika kung’oka. Unapozungumza waziri kujiuzulu hiyo ni lugha ya kisiasa lakini hata akijiuzulu inakuwa bado tatizo halijaweza kupatiwa ufumbuzi,” alisema.

Dk Kawambwa alisema hata Serikali haijafurahishwa na matokeo hayo mabaya na kushauri njia nzuri ni kutafuta dawa ya kukabiliana na tatizo la wanafunzi kufeli huku akiahidi kuwa wizara yake inaangalia tatizo hilo kwa karibu zaidi ili kujua chanzo chake.

Alisema amesikitika kuona hata shule ambazo zilikuwa zinategemewa kufanya vizuri zikiwamo za seminari, watu binafsi na kongwe za Serikali, nazo zimefanya vibaya.
Aliunga mkono maoni ya kutaka mfumo mzima wa elimu nchini uangaliwe upya kwa kushirikisha wadau mbalimbali wa elimu.
Lowassa
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Lowassa alisema matokeo hayo ni aibu kwa taifa na kuilaumu Serikali kwa kuzitelekeza shule za sekondari za kata.
Alisema taifa kwa sasa linazalisha wabeba kuni na maji na siyo wasomi ambao wanaweza kushindana kwenye soko la ajira.

Alisema sekondari za kata ambazo zilianzishwa chini ya usimamizi wake akiwa Waziri Mkuu, zilikuwa ukombozi kwa Watanzania wengi wa kipato cha kawaida na ndiyo sababu waliitikia wito kwa kuchangia ujenzi, hatua ambayo alisema ilimpa faraja kubwa.

“Serikali tuliahidi kuzikamilisha shule hizo kwa kuzijengea maabara na kuhakikisha zina walimu. Ni wajibu wake kutimiza. Mimi ndiyo maana hata kwenye Katiba Mpya nilipendekeza uwezekano wa elimu ya sekondari kuwa bure, elimu ni kama mapigo ya moyo ya taifa ukiona hayaendi vyema lazima ujiulize,” alisema.

Lowassa, ambaye alijiuzulu uwaziri mkuu mwaka 2008, alisema tangu aondoke madarakani, shule hizo nazo zimetelekezwa.

Alimwomba Rais Jakaya Kikwete kuchukua hatua za makusudi, ikiwa ni pamoja na kuunda tume ili ichunguze kwa makini kiini cha matokeo hayo mabaya.

“Matokeo hayo ni aibu kwa taifa, walimu, wazazi na wanafunzi wenyewe. Namwomba kwa dhati Rais afanye kitu cha ziada, natambua mchango wa juhudi zake katika sekta nyingine ikiwamo ujenzi wa barabara nchini lakini elimu ndiyo iwe ya kwanza,” alisema.

Alitaka ufike wakati nchi iamue kuwekeza katika elimu tofauti na ilivyo sasa kwa Tanzania kuwa nchi inayotenga fedha kidogo zaidi katika sekta hiyo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
 

TAASISI ya Utawala Bora Tanzania (CEGODETA) yaiomba serikali kukifuta kikundi cha Uamsho

TAASISI ya Utawala Bora Tanzania (CEGODETA), imeiomba serikali kukipiga marufuku kikundi cha Uamsho na Jumuiya ya Kimataifa itangaze kuwa Uamsho ni kikundi hatari cha kigaidi kama ilivyofanya kwa vikundi vya Al-Qaeida, Alshabab na Bokoharam.
 
Kauli hiyo ilitolewa kupitia vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana, na Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo, Thomas Ngawaiya, kuhusu vitendo vya ukabila na udini vinavyojitokeza kwa watu wachache ambao baadhi yao sio wazawa wa Zanzibar, kusababisha kuuawa kwa  watu wasio na hatia kama vile Mapadre kwa makusudi wakidhani kwa kufanya hivyo  wanachi wataogopa na kuwaachia watawale kwa misingi ya udini.
 
Kwa mujibu wa  Katiba ya Tanzania, inakataza uanzishwaji wa taasisi ye yote au chama chochote cha siasa kuandikishwa nchini kama malengo yake ni ya kidini au kuvunja Muungano, kutokana tetesi kwamba mauaji yanayotokea Zanzibar yanahusishwa na kikundi hicho, ni vema kikafutwa.
 
“Kwa kuzingatia hilo CEGODETA, tunaunga tamko lililotolewa na Rais Jakaya Kikwete kwamba uchunguzi wa kina ufanyike ambao utashirikisha mashirika ya nje na wote wanaohusika na mauajji hayo pamoja na wanaofadhili watu wao wachukuliwe hatua za kisheria ili kukata mzizi wa fitina” alisema.
 

Kongamano la nane la Wanahabari na Wadau wa NHIF lafunguliwa leo Mkoani Mtwara

 Mgeni Rasmi katika Kongamano la Nane la Wanahabari na Wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,Dkt. Seif Rashid (kulia) akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara,Mh. Joseph Simbakalia (katikati) pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara,Mh. Wilman Kapenjama Ndile (kushoto) wakiwasili kwenye Ukumbi wa Benjamin Mkapa uliopo ndani ya Chuo cha Ualimu Mkoani Mtwara leo,tayari kwa ufunguzi wa Kongamano hilo ambalo ni la siku mbili.
Mwenyekiti wa Kongamano la Nane la Wanahabari na Wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),John Bwire akitoa utambuliwa wa Wanahabari waliohudhulia kongamano hilo toka sehemu mbali mbali hapa nchini,linaloendelea kufanyika hivi sasa kwenye Ukumbi wa Benjamin Mkapa uliopo ndani ya Chuo cha Ualimu Mkoani Mtwara.
Mgeni Rasmi katika Kongamano la Nane la Wanahabari na Wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,Dkt. Seif Rashid akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa Kongamano hilo linalofanyika hivi sasa kwenye Ukumbi wa Benjamin Mkapa uliopo ndani ya Chuo cha Ualimu Mkoani Mtwara.Kauli mbiu ya Kongamano hilo kwa mwaka huu ni “Matumizi Sahihi ya Fedha za Uchangiaji Katika Halmashauri ili kuboresha huduma katika vituo vya matibabu”.
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara,Mh. Joseph Simbakalia akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni Rasmi kuhutubia na kufungua Kongamano hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ambaye ni Mwenyekiti wa Wakuu wa Mikoa yote Nchini,Mh. Abbas Kandoro akitoa salamu kwa Wanahabari na Wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wanaoshiriki Kongamano hilo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Emmanuel Humba akitoa taarifa fupi ya Mfuko wa Bima ya Afya kutokana tafiti mbali mbali zilizofanywa na baadhi ya Wanahabari katika Halmashauri 26 hapa nchini.
Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri wa vyombo vya Habari hapa nchini,Nevile Meena akizungumza machache wakati wa Kongamano hilo la nane la Wanahabari na Wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya,linaloendelea hivi sasa kwenye Ukumbi wa Benjamin Mkapa uliopo ndani ya Chuo cha Ualimu Mkoani Mtwara.
Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Raphael Mwamotto akitoa muongozo na utambulisho kwa baadhi ya viongozi kutoka sehemu mbali mbali wanaohudhulia Kongamano hilo.


 Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Eugin Mikongoti akiwasilisha mada yake kwenye Kongamano la Wanahabari na Wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Wadau wakifatilia Mada zinazotolewa kwenye Kongamano hilo.
Baadhi ya Wanahabari kutoka Vyombo mbali mbali vya Habari wakifatilia kwa makini Kongamano hilo la nane la Wanahabari na Wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),linalofanyika hivi sasa kwenye Ukumbi wa Benjamin Mkapa uliopo ndani ya Chuo cha Ualimu Mkoani Mtwara
 
 

No comments: