Monday, February 18, 2013

TAMKO RASMI KUTOKA KTK JUKWAA LA WAKRISTO MKOA WA MBEYA

 VIONGOZI WA JUKWAA LA WAKRISTO MKOA WA MBEYA WAKITOA TAMKO KWA VYOMBO VYA HABARI MBEYA
BAADHI YA WAANDISHI WA HABARI WAKIWA MAKINI KUSIKILIZA TAMKO HILO



TANZANIA CHRISTIAN FORUM (TCF) MKOA WA MBEYA
TAMKO RASMI KUTOKA KTK JUKWAA LA WAKRISTO MKOA WA MBEYA
MHESHIMIWA NDG. ABAS KANDORO,
KAMA MKUU WA MKOA NA MWAKILISHI WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE MKOA WA MBEYA, TUNAPENDA KUSOMA MBELE YAKO TAMKO RASMI LA JUKWAA LA WAKRISTO MKOA WA MBEYA (TCF).
NDUGU MKUU WA MKOA,
            “HAKI HUINUA TAIFA BALI DHAMBI NI AIBU YA WATU WOWOTE” (Mit. 14:34).
Katika mkutano wa jukwaa la Wakristo Tanzania mkoa wa mbeya ulionyika tarehe 12/02/2013 Jijini Mbeya, wajumbe tulitafakari kwa undani juu ya hali inayoendelea kujitokeza katika nchi yetu na hasa katika mahusiano baina ya dini mbili kuu UKRISTO NA UISLAMU.
Jukwaa hilo lilijumuisha taasisi zake kuu (yaani mabaraza ya Madhehebu ya Kikristo)
Tanzania Episcopal Council (TEC), Christian Council of Tanzania (CCT) na Pentecostal Council of Tanzania (PCT).Mbali na mambo yake ya kawaida jukwaa hilo lilitafakari utekelezaji wa Serikali juu ya tamko Rasmi la jukwaa la Wakristo kitaifa lililotolewa tarehe 06/12/2012 na kusomwa katika makanisa yote ya Kikristo nchini kwenye sikukuu ya Krismas tarehe 25/12/2012. Katika tafakari letu jukwaa la Wakristo wa Mkoa wa Mbeya tumeona kuwa kunabaadhi ya mienendo inayojitokeza katika nchi yetu ambayo kama isipodhibitiwa na kukomeshwa na Serikali italeta athali kubwa na hata kuondoa amani na uthabiti (Stability) wan chi.
Katika kutafakari kwa jukwaa juu ya athari zinazoweza kujitokeza, kumekuwepo na mambo yanayotendeka waziwazi yenye athri kubwa kwa amani na usitawi wan chi na wanchi wake kwa ujumla. Kwa mfano, uchochezi, kashfa, matusi na uchokozi wa wazi unaofanywa na baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu kupitia vyombo vya habari vya kidini (rediona magazeti), mihadhara, kanda za video, CD na DVD pamoja na kauli zinazotolewa na viongozi wa dini hiyo kwenye baadhi ya nyumba zao za ibada(ushahidi upo kama vile uhamasishaji wa Sheikh Ilunga) pasipo serikali kuchukua hatua stahiki na badala yake kubaki kimya au kupambana na wanaofichua harakati hatarishi kwa utulivuwa nchi.
Miongoni mwa harakati hatarishi zinazosambazwa kwa njia ya CD na DVD za Sheikh Ilunga, kuhusu kuua Wachungaji, Mapadri na Maaskofu zimeanza kuwa matokeo mabaya; kwani Padri kule Zanzibar alipigwa risasi na watu walioitwa na serikali wahuni na sasa kifo
Kimetokea na mchungaji Mathayo Kachila kule Buselesele Mkoani Geita na kikundi kinacho dhaminiwa ni wanaharakati hao wa kiislamu wenye jazba na gadhabu kali inayotokana na mvutano uliopo kati ya wakristo na waislamu kuhusu nani mwenye haki kisheria KUCHINJA WANYAMA. Hatua zinazochukuliwa na Serikali hazilizishi wala kukidhi matakwa ya wananchi wapenda amani. Tuna mifano kadhaa ya matukio kama haya yaliyojitokeza kwa wanchi wenzetu moja ni ile ya wenzetu aliyepigwa risasi kule Rungwe Ndg. John Mwankenja (Mwenyekiti wa CCM Rungwe) aliyepigwa risasi kwa mambo yanayodhaniwa kuwa ni ya kisiasa) Serikali ichukuwe hatua madhubuti kwa kutuma wachunguzi kutoka Dar es salaam kwa swala hilo na wote tuliridhika kwa hatua hizo madhubuti. Hatua kama hizo mbona hazichukuliwi katika masuala haya ya kidini na badala yake Serikali inakaa kimya au ina chukua hatua ambazo kimsingi hazitatui tatizo ili wananchi waridhike na Seeikali yao? Je tuseme Serikali inaangalia haiba (Personality) za watu au aina ya vikundi? Swala la uchinjaji lilipo jitokeza kule Mwanza waziri wan chi ndg. Steven Wasira alienda na kutoa majibu mepesi katika swala zito je, tuseme aliyoyatamka huko yalikuwa ni KAULI YA SERIKALI au kauli yake mwenyewe? Na kama yake mwenyewe mbona Serikali haijakanusha waziwazi? Na kama ni kauli ya serikali hiyo haki ya kuchinja kwa waislamu inatokana na sheria zipi za nchi? Je huo ndio utawala wa sheria tuliyoahidiwa na serikali ya awamu ya nne kuwa itatenda kazi kwa kuzingatia utawala wa sheria.
Kupigwa risasi kwa Pdri na kuuwawa kwa mchungaji kunathibitisha hazma halamu na batili ya “Ua, chinja” mapadri, wachungaji na maaskofu iwe kwa siri au kwa wazi iliyohasisiwa na Sheikh Ilunga ambayo sio tu inahatarisha amani ya nchi lakini pia inavunja haki za kuishi za binadamu zilizoainishwa katika katiba ya serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Aidha harakati hizi ziana muelekeo wa kudhoofisha ukristo Tanzania kama sio kuumaliza kabisa. Pamoja na mambo mengine kinachosikitisha ni namna ambavyo serikali inavyoyashughulikia mambo mazito yanayotikisa amani na utulivu wan chi. Utasikia mala ikisema “Mtu haruhusiwi kujichukulia sheria mkononi” na ndipo kikundi Fulani kitaibuaka na kuvunja mabucha na kuchoma nyama iliyomo humo hapo tena utasikia serikali hiyohiyo ikitowa kauli kwamba “Mvumiliane” je tunakwenda wapi?
Kwa misingi hiyo kwanini tusite kusema kwamba serikali ya chama cha mapinduzi (CCM) inaibeba dini ya kiislamu? Kwakuwa jukumu la serikali ya chama cha mapinduzi ni kuhakikisha kuwa wananchi wote wa Tanzania bila kujali dini zao, makabila yao na hata rangi zao wanaishi katika misingi ya uhuru, haki, udugu na amani kama raisin a watendaji wake walivyotoa kiapo mara baada ya kupewa dhamana ya kuiongoza nchi na wananchi wake kwa ujumla pasipo na ubaguzi wowote.
HITIMISHO: Ili wakristo wote nchini warudishe imani yao kwa serikali ya chama cha mapinduzi mambo ya fuatayo ni lazima yachukuliwe hatua za haraka iwezekanavyo:    
  1. Tunataka Serikali izingatie utawala washeria kulingana na ahadi yake katika kushughulikia maswala ya kijamii na sio vinginevyo. Kwa kuzingatia sheria maswala ya imani na dini yapo wazi kabisa kama zilivyoanishwa kwenye katiba ibara ya 19 (1), (2) (3) (4)  na kufanya vinginevyo ni uvunjifu wa sheria.
  1. Swala la kuua lisichukuliwe kama mazoea ya kawaida na inapotokea popote ni lazima Serikali ichukuwe hatua inayostahiki kwa kuzingatia utawala wa sheria kwakuwa wote wako sawa mbele ya sheria ibara ya 12, 13 (1) –(5).Usawa huo ni lazima uonekane katika swala la mauaji ya Mchungaji Mathayo Kachila na kama hatua zilivyochukuliwa katika mauaji ya aliyekuwa mwenyekiti wa halmashauri na mwenyekiti ya CCM Wilaya ya Rungwe Ndg. John A. Mwankenja. Hiyo ni haki ya msingi kkwa kila mtantania bila kuangali haiba (Personality) yake kama katiba ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania inavyoainisha haki xza kuishi, kulindwa na kushughuklikiwa kisheria katika ibara ya 14 na 15 pamoja na vifungu vyake viwili vidogo.
  2. Tunataka Serikali itueleze ni ushahidi gain zaidi inayoutaka kuliko ule unaopatikana kwenye CD na DVD zilizotolewa na Sheikh Ilunga kama inazingatia utawala utawala wa sheria.
  3. Tunataka Serikali iwajibike kutolea ufafanuzi kauli ya waziri wan chi Ndg. Steven Wasira inayohusu haki ya kuchicha kwa waislamu kama inatokana na sheria gain ya nchi?
  4. Kama Serikali inatekeleza utawala wa sheria, tunataka wakristo tuwe na machinjio na bucha zetu kulingana na imani yetu.
  5. Kama Serikali haitachukuwa hatua za makusudi katika kutekeleza madai yetu sisi kama viongovi wa dini ya kikristo tutachukua hatua ya kuwaambia waumini wetu kwamba Serikali ya chama cha mapinduzi inaibeba dini ya kiislamu na wao watajua la kufanya.
Pamoja na kutaka utekelezaji wa haraka kutoka kwa Serikali bado tunawaomba wakristo tuwe katika hali ya maombi na utulivu kwa wakati huu ambapo tumo katika vita vya kiroho ili Mungu akatuimarishie amani ambayo ni nguzo kuu ya Taifa letu. Tamko hili rasmi la jukwaa la wakristo Mbeya lisomwe katika makanisa yetu yote siku ya juma pili tarehe 24/02/2013
Tunakuambatanishia na nakala ya Tamko Rasmi la TCF Taifa la tarehe 6/12/2012.
NDUGU MKUU WA MKOA NAWASILISHA.
Nakala kwa:
  1. Mwenyekiti wa CCM Mkoa.
  2. Tanzania Christian Furum Taifa
  3. Mwenyekiti wa the Tanganyika Law Society.
  4. Vyombo vya habari TV, Redio na magazeti
  PICHA NA MBEYA YETU

 

HATIMAYE YAMETIMIA,  MAHAKAMA ya Wilaya ya Mbeya imemhukumu kifungo cha maisha Wilvina Mkandara(24) kutokana na kesi iliyokuwa inamkabili ya kumtesa hadi kumsababishia

Wilvina Mkandala (24) akitolewa mahakamani mara tu baada ya kusomewa hukumu ya kifungo cha maisha huku watu walio hudhuria Mahakamani hapo wakipunga mikono ishara ya kwaheri na huku Askali akicheka
Baadhi ya wakazi wa majengo alikokuwa anaishi mtuhumiwa wakimsifu hakimu kwa hukumu aliyotoa kwa mtuhumiwa huyo
kila aliyepita mbele ya kamela yetu alikuwa anatabasam kwa furaha bada ya kutolewa kifungo cha maisha kwa mtuhumiwa
Mtoto Aneth kabla ya kukatwa kwa mkono wake wa kushoto hapo ni siku alipokuwa na wasamalia wema akiwa katika hali mbaya na huku ameshika kinyesi kwa ajili ya kula ikiwa ni adhabu
Mtoto Aneth mara baada ya kukatwa mkono wa kushoto kwa ujumla mtoto huyu anaendelea vizuri na alishatoka hospitalini


MAHAKAMA ya Wilaya ya Mbeya imemhukumu kifungo cha maisha Wilvina Mkandara(24) kutokana na kesi iliyokuwa inamkabili ya kumtesa hadi kumsababishia ulemavu mtoto wa shemeji yake.
Akisoma hukumu hiyo Hakimu mkazi wa mahakama hiyo Gilbert Ndeuruo alisema mshakiwa amehukumiwa kutokana na kifungu cha 235 cha mwenendo wa makosa ya jinai cha mwaka 1985.
Amesema Mahakama inaweza kumtia hatiani mtuhumiwa kutokana na ushahidi wa mazingira au ushahidi wa moja kwa moja ambapo alisema mshtakiwa anahukumiwa kutokana na ushahidi wa mazingira kwa sababu mhangwa wa tukio hilo alishindwa kutoa ushahidi wa moja kwa moja.
Ameongeza kuwa mahakama hiyo imeona mshtakiwa anastahili adhabu kutokana na mtuhumiwa huyo kama mzazi kushindwa kujali afya ya mtoto ili hali alikuwa mama mlezi ikiwa ni pamoja na kumpeleka Hospitali kwa wakati ili apatiwe matibabu.
Ndeuruo amesema pia mahakama hiyo haikuridhishwa na na ushahidi wa mtuhumiwa alioutoa mahakamani kuwa majeraha yaliyokutwa mwilini mwa mhanga wa tukio hilo yalitokana na kuugua kwa tetekuwanga jambo ambalo alisema si la kweli.
Amesema kuwa mshtakiwa ametoa maelezo wakati wa utetezi wake yanayopingana na na maelezoya daktari aliyemtibu mgonjwa alipofikishwa hospitali wakati akitoa ushahidi mahakamani hapo.
Hata hivyo kabla ya kutoa hukumu hiyo Hakimu huyo alisema kutokana na ibara ya 16 ya sheria ya African Charter inayotaka Nchi itunge sheria ya kulinda haki za watoto ambapo Tanzania haina sheria hiyo hivyo kusababisha watu kuwanyanyasa watoto.
Hakimu huyo ametoa wito kwa taasisi zinazohusika kutunga sheria hiyo mara moja ili kulinda haki za watoto ambayo itatamka wazi adhabu kwa wale watakaobainika kuwatesa na kuwanyanyasa watoto.
Kwa upande wake mwendesha mashtaka wa Serikali Archiles Mulisa ameiiambia mahakama hiyo kumpa adhabu kali mtuhumiwa huyo ili liwe fundisho kwa wazazi wengine wenye tabia kama hizo ambao hajakamatwa.
Amesema kitendo kilichofanya na mshtakiwa huyo ni kitendo chakinyama ambacho kinatakiwa kulaaniwa vikali hivyo kupitia adhabu atakayopewa mtuhumiwa inaweza kupunguza unyasasaji kama huyo katika jamii.
Aidha mshtakiwa Wilvina alipotakiwa kujitetea ili apunguziwe adhabu kabla ya kusomewa aliomba mahakama hiyo impunguzie adhabu kwa kile alichodai kuwa ni mjamzito, pia hajui mtoto wake aliyemzaa alipo pamoja na mawasiliano na familia yake.
Akitoa hukumu hiyo hakimu Ndauruo amesema amesikitishwa na kitendo cha mtuhumiwa cha kuomba kupunguziwa adhabu kutokana nakutomwona mtoto wake hali inayoonesha kutomjali mtoto aliyemtendea kosa.
Ameongeza kuwa Mahakama imefuatilia historia ya nyuma ya mtuhumiwa ambayo haioneshi kama anamatukio kama hayo ambayo aliwahi kuyafanya lakini mtuhumiwa anastahili adhabu kali kama upande wa mashtaka ulivyo sahauri na kutokana na mhanga kuwa na ulemavu wa kudumu.
Amesema mahakama inamhukumu kifungo cha maisha kifungo kitakachothibitishwa na mahakama kuu kutokana na mtuhumiwa kuwa na haki ya kukata rufaa kama ameona ameonewa katika kesi hiyo.
Mwanamke huyo alipandishwa kizimbani Novemba 16, Mwaka chini ya Mwendesha mashtaka wa Serikali, Achiles Mulisa aliiambia Mahakama kuwa Mtuhumiwa Wilvina Mkandala (24) alitenda kosa la kusababisha majeraha akiwa na nia ovu ambayo imemsababishia ulemavu mtoto Aneth.

 

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2012 HAYA HAPA

aa
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa (MB) leo ametangaza rasmi matokeo ya Mitihani ya Kidato cha Nne, maarifa-QT.
TAARIFA YA MATOKEO YA MITIHANI YA MAARIFA (QT) NA KIDATO CHA NNE (CSEE)
ILIYOFANYIKA OKTOBA 2012
1.0                 UTANGULIZI
Mitihani ya Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT) kwa mwaka 2012 ilifanyika nchini kote kuanzia tarehe 8-25 Oktoba 2012.  Napenda kuchukua nafasi hii kutangaza rasmi matokeo ya mitihani hiyo kama ifuatavyo :
2.0                 MTIHANI WA MAARIFA (QT)
2.1           Usajili na Mahudhurio
Katika Mtihani wa Maarifa 2012 watahiniwa waliosajiliwa ni 21,310 ambapo wasichana walikuwa ni 13,134 na wavulana ni 8,176. 
Jumla ya watahiniwa 17,137 sawa na asilimia 80.42 ya waliosajiliwa wamefanya Mtihani. 
2.2          Matokeo ya Mtihani wa Maarifa (QT)
Watahiniwa 5,984 kati ya 17,137 waliofanya mtihani wamefaulu Mtihani wa Maarifa (QT).
3.0                 MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2012
Jumla ya vituo 5,058 vilitumika katika kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 ambapo vituo 4,155 vilikuwa vya watahiniwa wa shule na vituo 903 vilikuwa ni vya watahiniwa wa kujitegemea.
ENDELEO KWA KUBOFYA HAPO CHINI

Ali Hassani Mwinyi amewataka viongozi wa kidini nchini kuihami amani na utulivu inaotishiwa kuvurugwa

mwinyi 
RAIS mstaafu wa awamu ya pili, Alhaj Ali Hassani Mwinyi amewataka viongozi wa kidini nchini kuihami amani na utulivu inaotishiwa kuvurugwa na misukosuko ya kidini, kisiasa na kijamii  inayojitokeza katika maeneo mbalimbali yanchi.
Alhaj Mwinyi alisema hayo wakati maadhimisho ya sherehe za siku ya uzawa wa Mtume Mohamma (SWA), yalioandaliwa na Jumuiya ya Khoja Shia Ithnaasheri, kufanyika jijini Dar es Salaam leo.
Alisema nchi hivi sasa inapita kwenye misukosuko inayokana na vitendo hivyo na endapo viongozi wa kidini hawatakuwa makini katika kukemea waumini wao basi huenda nchi ikaingia kwenye matatizo ambayo hayana slahi kwa nchi.
Alhaj Mwinyi alisema mkiwa viongozi wadini mnalo jukumu la kila mmoja wenu kutumia elimu na fursa zilizopo kwa kuwatuliza vijana kutoingia katika vitendo vya uvunjifu wa amani kwa kisingizio cha dini.
“Tanzania inaongoza kwa kudumisha amani, utulivu na ustaarabu kwa miaka mingi kama ingekuwa wachezaji mpira tungesema sisi ni machampioni wa amani katika Bara la Afrika”alisema Alhaj Mwinyi.
Alisema ni wajibu wa Masheikh hao kusimamia na kulinda amani na utulivu uendelee kuwepo ili kila muumini aweze kufanya ibada, kwenda msikitini na kufanya shughuli nyingine za maendeleo kwa maslahi ya nchi.
Aliongeza kuwa hakuna haja ya kufikishana mahala kuwa kila mmoja anakuwa na wasiwasi wa maisha yake kitendo ambacho kinaenda kinyume na mafundisho ya Mtume Mohamad (SWA).
“Tanzania ni nchi kongwe na haikuanza leo pia ni sawa na gunia ambalo limekusanya watu wengi wa dini mbalimbali  na wasio na dini hivyo ni vema watu wakajenga ustaarabu wa kuvumiliana”alisema Alhaj Mwinyi.
Alhaj Mwinyi alisema wajibu wa Waislam ni kuhakikisha wanaishi kwa amani na watu wengine ambao hawajawaingilia na kutaka kuwafuta katika nchi hii.
Vilevile ieleweke wazi kuwa hakuna anaweza kumfuta mwenzake katika kile anachokiamini hivyo ni vema kila mtu akajifunza kumvumilia mwingine.
Alisema kubwa ni kla mmoja kujizuia kumuingilia mwingine kwenye dini yake, kazi hiyo hakuna mwingine wa kuifanya bali ni Masheikh hao.
Aliwaasa Masheikh hao kuacha kushabikia mambo madogo ambako ushabibiki ukiendekezwa iko siku unaweza kuvuruga amani ya nchi hii.



UKIFIKA MBEYA TU? KARIBUNI WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA MJIONEE MAAJABU YA MUNGU

ZIWA KISIBA (MASOKO) WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA
ZIWA NGOSI WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA. KATI YA MAAJABU KUMI NA TISA YANAYOPATIKANA WILAYANI RUNGWE MAYA MAZIWA NI SEHEMU YA MAAJABU YALIYOAINISHWA KAMA SEHEMU KUU YA UTALII. MAZIWA HAYA YAPO JUU YA MILIMA NA HAYANA SEHEMU YA KUINGILIA MAJI WALA MAJI KUTOKA HATA KUPUNGUA KWA KINA CHA MAJI WALA KUONGEZEKA
 
MUONEKANO WA MLIMA RUNGWE
 Photo
DARAJA LA MUNGU

RAIS KIKWETE AZIFARIJI FAMILIA ZA WALIOKUFA KATIKA AJALI YA GARI UBENA ZOMOZI

mso1 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifariji ndugu, jamaa na marafiki wa familia zilizoondokewa na watoto na wazazi kufuatia ajali ya barabarani maeneo ya kijiji cha Kibiki, Ubena Zomozi katika mkoa wa Pwani Februari 11, 2013 iliyoua hapohapo watu wanane wakiwemo wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Chalinze baada ya gari dogo aina ya Toyota Mark II lililokuwa limebeba abiria wanane kugongana uso kwa uso na roli
mso2
mso3
mso4
gari2
gari4Rais Jakaya Mrisho Kikwete Jumamosi hii ya Februari 16, 2015 amekwenda kuhani na kufariji ndugu, jamaa na marafiki wa familia zilizoondokewa na watoto na wazazi kufuatia ajali ya barabarani maeneo ya kijiji cha Kibiki, Ubena Zomozi katika mkoa wa Pwani iliyotokea Februari 11, 2013 na kupoteza  hapohapo maisha ya watu tisa wakiwemo wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Chalinze baada ya gari dogo aina ya Toyota Mark II lililokuwa limebeba abiria wanane kugongana uso kwa uso na roli la mizigo
Familia alizokwenda kuhani na kuzifariji ni pamoja na za marehemu Hassan Erasto Kurunge (57), Maria Sadiki  ((52) na mtoto wa mwaka mmoja Samweli Ismail wa kata ya Ubena.
Wengie ni marehemu Essau Enos Mwamgingo (16) , Stella Isaack Kazimoto (18), Bahati George Mbena (17) na Latifa Maneno (17) 
Akiwa ameongozana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe Mwantumu Mahiza na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Ahmed Kipozi, Rais Kikwete alieleza kusikitishwa kwake kwa ajali hiyo, na kuwataka madereva wawe makini katika kuzingatia sheria za usalama barabarani
Rais Kikwete alisikitishwa zaidi kwa taarifa kwamba gari hilo dogo lilikuwa limebeba abiria wanane, na kuwa  dereva wake ambaye pia alipoteza maisha, hakuwa makini katika kuzingatia sheria za usalama barabarani.

hakuna kulipiza kisasi-kard.pengo


Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo (Pichani) amewataka wakatoliki na watanzania kwa jumla kuwa watulivu katika kipindi hiki ambapo kumetokea kundi la watu wachache kutaka kuvunja amani  hapa nchini kwa kutumia udini.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Kardinali Pengo amesema moyo wa kisasi hautasaidia kitu chochote, kinyume chake utaleta maafa yaliyo makubwa zaidi na kutuingiza katika janga kubwa zaidi.
Ameongeza kuwa siku ya tarehe 20 kutakuwa na ibada katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph itakayoongozwa na Askofu Msaidizi kwa lengo la kumuombea marehemu Padri Evarist Mushi na kuliombea taifa ili watanzania tuendelee kuwa wamoja na tubaki katika amani tuliokwisha kuizoea.
Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amezungumza hayo baada ya kusoma waraka uliotolewa na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu uliozungumzia mambo mengi ikiwemo kuwataja wakatoliki kama ‘makafiri’ na kuwa bado haijawa mwisho wa mapambano.

No comments: