Wednesday, March 27, 2013

JK: afunga rasmi mafunzo ya JKT ya muda mfupi kwa wabunge RUVU JKT

8E9U3121Mwakilishi wa Wabunge waliomaliza mafunzo maalumu ya muda mfupi ya Jeshi la Kujenga Taifa(JKT)katika kambi ya RUVU Ester Bulaya akikabidhi risala kwa niaba ya wenzake kwa Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo mchana. 8E9U3133Wabunge waliomaliza mafunzo ya muda mfupi ya Jeshi la kujenga Taifa wakipita kwa ukakamavu mbele ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mris 8E9U3151Wabunge waliomaliza mafunzo ya muda mfupi ya Jeshi la kujenga Taifa wakipita kwa ukakamavu mbele ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho kikwete wakati wa gwaride maalumu la kumaliza mafunzo hayo huko kambi ya RUVU leo. 8E9U3177Wabunge walihudhuria mafunzo ya muda mfupi Ruvu JKT wakionesha walijifunza kwa vitendo. 8E9U3247Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipiga risasi hewani kuashiria kuzundua mafunzo  ya JKT kwa vijana katika kambi ya RUVU JKT yatakayo itwa Operesheni Miaka Hamsini. 8E9U3275Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Mke wa Rais Mama Salma Kikwete,Waziri wa Ulinzi Mh.Vuai Shamsi Nahodha mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza pamoja na viongozi wa JKT wakiwa katika picha ya pamoja na wabunge waliomaliza mafunzo ya muda mfupi katika kambi ya JKT Ruvu. 8E9U3345Rais Jakaya Kikwete akikagua mradi wa ufugaji kuku katika kambi ya Ruvu JKT leo(picha na Freddy Maro). 8E9U3392 Rais Jakaya Kikwete akikagua mradi wa ufugaji kuku katika kambi ya Ruvu JKT leo(picha na Freddy Maro).

8E9U3088Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi cheti cha kuhitimu mafunzo ya muda mfupi kwa viongozi mbunge wa viti maalum Ester Bulaya leo katika kambi ya RUVU JKT.Rais Kikwete amefunga rasmi mafunzi hayo leo  yaliyofanyika kwa wiki tatu.(Picha na Freddy Maro)

8E9U3018
Wabunge Halima Mdee na Ester Bulaya pamoja na wenzao wakila kiapo wakati wa kuhitimu mafunzo ya muda mfupi yaliyofanyika katika kambi ya jeshi la Kujenga Taifa Ruvu JKT huko kibaha Mkoani Pwani 
.........................................................................................................................................................

NWAKA MWAKISU AKONGA NYOYO ZA VIJANA MBEYA

Nwaka Mwakisu akiongea na vijana wa Uyole hivi karibuni 
Diwani wa Kata ya Itezi Frank Maemba amesema wanachokifanya Vijana hao ni kutekeleza sera za chama cha mapinduzi inayotaka Vijana waunganishwe kwenye makundi ili iwe rahisi kupatiwa misaada ikiwa ni pamoja na kupunguza uhaba wa ajira kwa vijana.
Timu ya Redio  Bomba fm, 
Timu ya  Veterani ya Uyole 
Timu mbali mbali zilikuwepo uwanjani hapo
Vijana mbali mbali walijitokeza kuchangia damu siku hiyo

BAADHI ya Wananchi na wakazi wa Mkoa wa Mbeya wamepongeza jitihada za Vijana wanaojitolea kusaidia makundi ya watu wasiojiweza na wenye uhitaji kutokana na kufanya hivyo bila kujali itikadi za vyama  wala dini zao.
Kijana anayetajwa kukonga mioyo ya wananchi wa Mbeya kutokana na kusaidia makundi mbali mbali ya Vijana, Yatima na wazee ni Mjumbe wa Mkutano mkuu Taifa kupitia Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Mbeya, Nwaka Mwakisu.
Wananchi hao wamesema Nwaka Mwakisu amekuwa kivutio kwa Vijana wengi wa kada mbali mbali kutokana na ushiriki wake katika kazi za maendeleo ndani ya Mkoa wa Mbeya ambapo pia amekuwa akiwaunganisha vijana hao kwenye makundi ili waepukane na shughuli zisizofaa katika jamii.

Wamesema Mwakisu ameonesha moyo wa tofauti miungoni mwa Vijana Mkoani Mbeya ambapo katika kipindi kifupi cha kuanzia Januari hadi Machi Mwaka huu ameshiriki na kuambatana na vijana kutembelea vituo vya watoto yatima vilivyopo Uyole na Simike Jijini Mbeya.
Wakizungumza na Mbeya yetu katika mahojiano maalumu juu na namna Vijana wenye  uwezo wanavyoweza kusaidia makundi mbali mbali katika kuwakomboa kiuchumi  ambapo hawakusita kumtaja Nwaka Mwakisu kuwa ni miongoni mwa vijana wachache wanaojitolea kwa moyo wote.
Iddi Ramadhani ni Mwenyekiti wa Bajaji Jiji la Mbeya ambaye alisema Mwakisu amewatembelea mara kadhaa katika kujua wanahitaji nini ili aweze kwasaidia ambapo ameshwasaidia vijana hao Vifaa vya michezo kama vile Jezi, Soksi na Viatu kwa ajili ya timu ya Waendesha bajaji yenye makao makuu Ilemi Jijini Mbeya.
Mbali na waendesha bajaji vijana wengin walionufaika na Msaada wa Mwakisu ni timu za Mpira kutoka Uyole katika kata ya Itezi Jijini Mbeya ambao walipatiwa vifaa vya michezo ambavyo ni seti tatu za Jezi na mipira kwa ajili ya mashindano ya Umoja yaliyomalizika hivi karibuni.
  
Nwaka Mwakisu alipotafutwa kuzungumzia maswala hayo alisema binadamu tumeumbwa kwa ajili ya kusaidiana hivyo si vibaya kwa yeye kujitolea kwa watu wenye uhitaji ambapo aliongeza kuwa hafayi hivyo kwa ajili ya kujinufaisha yeye binafsi.
Alisema kiu yake ni kuona Vijana wanakuwa na umoja kwani baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakiwatumia vijana kuvuruga amani Mkoani Mbeya ambapo baada ya vurugu viongozi hao hawajitokezi kuwasaidia pindi wanapopata madhara kutokana na athari wanazopata katika vurugu hizo.
Kutokana na kuwaunganisha vijana hao katika baadhi ya michezo ambapo vijana hao hupata nafasi pia ya kuchangia damu kutokana na uhitaji wa damu katika michezo iliyomalizika Uyole Jijini Mbeya katika viwanja vya Shule ya Msingi Gombe iliyowahusisha timu ya kituo cha Redio cha Bomba fm, Veterani ya Uyole na vijana wengine.
Mbali na vijana hao kumpongeza Nwaka Mwakisu kwa kujitolea na kuwaunganisha Vijana hao, Diwani wa Kata ya Itezi Frank Maemba alisema wanachokifanya Vijana hao ni kutekeleza sera za chama cha mapinduzi inayotaka Vijana waunganishwe kwenye makundi ili iwe rahisi kupatiwa misaada ikiwa ni pamoja na kupunguza uhaba wa ajira kwa vijana.
 
Hata hivyo wajibu huo umeonekana kuekelezwa zaidi na viongozi vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoani Mbeya ambao wameonekana kuunga mkono juhudi hizo ambao ni Mjumbe wa Mkutano mkuu taifa(CCM), Charles Mwakipesile ambaye aliwahi kutoa Kompyuta yenye thamani ya Shilingi Laki tano na Nusu(550,000/=) kwa  Vijana wanaoendesha Bajaji Jiji la Mbeya.
...........................................................................................................................
 

IGP MWEMA: HUDUMA BORA KWA WANANCHI SIYO HIARI

IGP-SAID-MWEMA 
Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi.
…………………………………………………………….
Askari Polisi Nchini wametakiwa kuendelea kutoa huduma bora kwa Wananchi ili kuendeleza mahusiano mema na Jamii pamoja na kushirikiana katika kuendeleza mpango wa Polisi  jamii na Ulinzi shirikishi ambao umesaidia kwa kiasi kikubwa kuwafichua wahalifu hapa nchini tangu kuanzishwa kwake.
Hayo yalisemwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema wakati alipokuwa akizindua Programu za Mafunzo kazini kwa askari Polisi Tanzania nzima katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Jijini Dar es Salaam ambapo uzinduzi huo ulihudhuriwa na Maofisa mbalimbali wa  Polisi pamoja na Askari kutoka Makao makuu ya Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam pamoja na Vikosi vilivyopo jijini Dar es Salaam.
IGP Mwema alisema jambo la kutoa huduma bora kwa wananchi siyo la hiari bali ni la lazima hivyo kila askari anapaswa kuboresha huduma anayoitoa kwa  kuzingatia mafunzo aliyonayo ili kuleta ufanisi wa kazi na kuimarisha usalama wa raia na mali zao.
Alisema Wananchi nao wanapaswa kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kutoa taarifa  za uhalifu na wahalifu kwa Jeshi hilo ili ziweze kufanyiwa kazi kwa haraka katika kuzuia, kubaini na kutanzua uhalifu hapa Nchini.
“Usalama unaanza na mimi, wewe na sisi sote hivyo kila mmoja anatakiwa ajiulize anachangia nini katika kuimarisha ulinzi wake binafsi, wa jirani yake na wa taifa kwa ujumla kwa vile suala hili siyo la Jeshi la Polisi peke yake ni wajibu wa kila mmoja” Alisema IGP Mwema.
Aidha aliwataka Maofisa na Askari kuitumia vyema fursa ya Mafunzo kazini kujiendeleza kielimu ili kuboresha ufanisi wao katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku pamoja na kukabiliana na changamoto mbalimbali za kazi na maisha.
Mwema alitoa wito kwa kila Askari na Ofisa kuutumia vyema mpango huo wa mafunzo kazini kujitengea muda vizuri  kwa ajili ya kujisomea  nje na saa za kazi ili kuboresha huduma bora kwa wananchi ambapo alisisitiza suala la  kutoa huduma bora kwa wananchi siyo la hiari ni kuto na maboresho ya Jeshi la Polisi yanayolenga kufanya kazi kwa weledi na usasa katika kuihudumia jamii na wananchi ..
.............................................................................................................................................................................................................

 

No comments: