Tuesday, March 26, 2013

Katibu mtendaji tume ya uchumi Afrika atembelea wizara ya Nishati na Madini



Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Sospeter Muhongo amekutana na katibu mtendaji wa Tume ya Uchumi Afrika (ADF), Dr. Carlos Lopes ofisini kwake jumanne asubuhi.

 Akizungumzia ujio wake Dr Carlos alisema chombo hicho chenye makao makuu yake Adis Ababa kinafanya kazi kwa ushirikiano na Umoja wa Africa, Benki ya Maendeleo ya Africa (AfDB) na washirika wengine muhimu katika kuleta maendeleo kupitia programu maalumu za kimaendeleo. 

 Carlos alisema tume ya uchumi ina wadau ambao hufanya midahalo ya kujadili na kuanzisha mikakati madhubuti kwa ajili ya maendeleo ya Africa.
Alisema, lengo la ADF ni kuwasilisha matokeo ya utafiti na maoni juu ya masuala muhimu ya maendeleo ili kuweka malengo, vipaumbele na mipango pamoja na kufafanua mazingira yatakayo wezesha mataifa ya Afrika kutekeleza programu husika.

Aliendelea  kusema mabadiliko makubwa yanatarajiwa kufanyika katika sekta za madini na nishati na kwamba wanamaono ya kuanzisha kituo cha maendeleo cha madini (Mining development centre), kuhamasisha utunzaji wa mali asili pamoja na kuboresha masuala ya kilimo.

Mpango huu huwasilishwa kwa wadau mbalimbali Afrika wakiwemo wakuu wa nchi na serikali, watunga sera, wadau wa maendeleo, taasisi za kimataifa na taasisi zisizo za kiserikali ili kujadili namna ya kuleta mapinduzi hayo yatakayoinua uchumi wa bara la Africa.

Mheshimiwa Waziri alimshukuru Dr. Calos kwa kuona umuhimu wa kufika na kuzungumza nae, Mheshimiwa  Muhongo alisema amefurahishwa na mpango wa UNECA (United Nation, Economic Commision for Africa) wa kufanya mabadiliko ya kiuchumi na kukazia kwamba yuko tayari kushirikiana katika kuleta mabadiliko hayo. Aidha, Mheshimiwa Muhongo alisisitiza kuwa ni lazima kubadilisha mtazamo wa baadhi ya waafrika wa kujiona hawawezi kila wakati.

Muhongo alisema anaamini kwamba Tanzania inaweza kuongoza katika uzalishaji wa madini miaka ijayo na japo kuwa inakabiliwa na tatizo la uhaba wa wataalamu na mafundi katika sekta za nishati na madini. Muhongo alisema wataalamu wengi waliopo wamefikia umri wa kustaafu na hivyo kuacha pengo kubwa kwa tasnia za nishati na Madini. 

Muhongo alisisitiza umuhimu wa kujenga uwezo wa kitaaluma katika Nyanja za utafutaji na uendelezaji wa mafuta na gesi aliomba ADF kusaidia katika kufanikisha suala hilo.

Mpaka sasa Wizara imejitahidi kutafuta na kupata wafadhili ili kuwawezesha  watanzania kujiendeleza katika masuala ya petroli na gesi katika nchi za Brazili na China  na mpaka sasa kuna jumla ya wanafunzi 40. Lakini pia vyuo mbalimbali nchini ikiwemo Taasisi ya Technolojia Dar es Salaam na chuo kikuu cha Dodoma watawezeshwa kutoa  mafunzo katika tasnia ya  mafuta na gesi.

Waziri aliongeza kwamba tunahitaji kuongeza uwezo pia katika masuala ya nishati katika maeneo ya uzalishaji wa umeme, usafirishaji pamoja na usambazaji kwani nishati ni huduma muhimu ya msingi sana katika kupata maendeleo.
Nuru I. Mwasampeta
Information Officer II
Ministry of Energy and Minerals
.............................................................................................................................................................

 

WANAFUNZI 10,000 WALIOKATA RUFAA YA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE-2012 WAMEFELI TENA



Wakati tume ya kuchunguza matokeo mabaya ya kidato cha nne mwaka 2012 ikiendelea na kazi, imebainika kuwa wanafunzi waliokata rufaa kutaka mitihani yao isahihishwe upya wamefeli zaidi baada ya
kusahihishiwa.Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambazo zimethibitishwa na baadhi ya maofisa, wanafunzi waliokata rufaa wamefeli zaidi na hata walioongezewa alama matokeo hayakubadilisha madaraja waliyopata awali.Habari zinaeleza kuwa, wanafunzi waliokata rufaa NECTA kutaka mitihani yao isahihishwe upya ni takribani 10,000 na kwamba baraza bado limetoa muda zaidi kwa wengine wanaotaka kukata rufaa.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya NECTA viliieleza NIPASHE kuwa mitihani kwa wanafunzi waliokata rufaa ilianza kusahihishwa Machi 12 na kuhitimishwa Machi 15, mwaka huu na kwamba wengi wamefeli zaidi.“Baada ya wanafunzi kadhaa kukata rufaa, NECTA iliamua kuwaita walimu waandamizi katika masomo yote na kuanza kufanya kazi ya kusahihisha mitihani hiyo upya kwa umakini, kilichowashangaza walimu hao ni kuona kiwango cha kufeli kimeongezeka,” alisema ofisa mmoja wa NECTA ambaye aliomba jina lake lisiandikwe gazetini kwa maelezo kuwa siyo msemaji wa baraza hilo.

Wakizungumza na NIPASHE, baadhi ya walimu walisema walioshiriki kusahihisha mitihani hiyo walisema kuwa maoni yaliyokuwa yanatolewa na baadhi ya watu kwamba matokeo mabaya ya mtihani huo yalitokana na uchakachuaji, hayakuwa ya kweli.Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Joyce Ndalichako, akizungumza na NIPASHE jana alithibitisha kuwa mitihani ya wanafunzi waliokata rufaa ilianza kusahihishwa Machi 12 mwaka huu.

Dk Ndalichako alisema hata hivyo, hana taarifa kama matokeo ya wanafunzi hao yanaonyesha kuwa wanafunzi wengi wamefeli zaidi kwa kuwa alikuwa safarini kikazi.“Unavyozungumza na mimi nipo Arusha na wageni, sifahamu kama baada ya kusahihishwa upya mtihani wa wanafunzi waliokata rufaa matokeo yamekuwaje, nitafahamu baada ya kurejea Dar es Salaam Jumatano wiki hii,” alisema Dk Ndalichako ambaye hata hivyo, hakutaja idadi ya wanafunzi waliokata rufani.Dk Ndalichako alisema suala la kufeli zaidi wanafunzi waliokata rufaa linawezekana kutokea kwa sababu kila mwaka imekuwa ikijitokeza hali kama hiyo, hivyo ni jambo la kawaida
NIPASHE
..................................................................................................................................

ABOMOLEWA NYUMBA NA KUCHOMEWA VYOMBO VYA NDANI KWA TUHUMA ZA  USHIRIKINA ILEMI MBEYA

Wananchi wenye hasira kali wakibomoa nyumba ya mama Atupele Kalile akidhaniwa kuwa mchawi maeneo ya ilemi Mbeya
Kazi ya kubomoa nyumba ya mama huyo inaendelea
Wengine wameshaingia ndani na kuanza kutoa vyombo nje tayari kwa kuvichoma
Mtoto wa mama Atupele akijaribu kuokoa vitu vya mama yake visichomwe moto na wanakijiji
Vyombo vinazidi kutolewa ndani ilivichomwe moto
Tayari wameshaanza kuchoma moto vyombo vya mama Atupele
Mwingine anaendelea kubomoa nyumba ya mama Atupele
Wamefyeka shamba lake lote la mahindi
Wengine wanapongezana kwa kazi waliofanya
Kushoto mama Atupele Kalile anaedhaniwa kuwa ni mshirikina akiwa na mtoto wake

MWANAMKE mmoja aliyejulikana kwa jina la Atupele Kalile (60) mkazi wa Mtaa wa Masewe Kata ya Ilemi Jijini Mbeya amenusurika kifo baada ya wananchi wa Mtaa huo kutaka kumpiga kisha kubomoa nyumba yake wakimtuhumu kwa ushirikina.
  
Wananchi hao kumtuhumu Mwanamke huyo kuhusika na upotevu wa motto mwenye umriwa miaka mitatu(3) (Judith Chengula) aliyepotea katika mazingira ya kutatanisha Februai 22, Mwaka huu.
  
Kwa mujibu wa wakazi hao walisema Mtoto huyo alipotea majira ya saa 11 jioni baada ya kupoteana na dada yake  Anitha Mgaya wakiwa wametokea kanisani ambapo hadi sasa mototo huyo hakuweza kupatikana licha ya juhudi kubwa za wakazi hao kumtafuta bila Jitihada.
  
Walisema katika vikao kadhaa vilivyoitishwa mtaani hapo kwa ajili ya kutafuta mbinu za kupatikana kwa mtotolakini Mwanamke huyo hakuonesha ushirikiano jambo ambalo lilizua hofu miongoni mwa wakazi hao hali iliyopelekea kuhisiwa kuhusika na tukio hilo.
  
Walisema katika kikao kilichofanyika Machi 23 Mwaka huu majira ya Asubuhi mtaani hapo wananchi hao waliendelea kusisitiza kuwa Mwanamke huyo achukuliwe hatua kwa kuwa ndiye anayehusika na upotevu wa motto ambapo iliamriwa kwenda nyumbani kwake kufanya upekuzi.
  
Walisema baada ya kufika nyumbani kwake na kufanya upekuzi walikuta vitu vinavyohisiwa kuwa vinahusika na ushirikina ambavyo ni vitovu vya watoto wachanga watatu ambapo Mwanamke huyo baada ya kuulizwa alishindwa kutolea ufafanuzi hali iliyosababisha wananchi kupandwa na hasira na kuanza kumpiga.
Kutokana na tukio hilo Kaimu Mwenyekiti wa Mtaa huo Nedy Mwamlima alimnusuru Mwanamke huyo katika kipigo kutoka kwa wananchi kwa kumpeleka katika kituo kikuu cha Polisi kwa usalama zaidi.
  
Baada ya mtuhumiwa huyo kunusuriwa na kukimbizwa katika kituo cha Polisi wananchi hao hawakupoza jazba zao ambapo waliamua kuteketeza nyumba ya mtuhumiwa ikiwa ni pamoja na kufyeka mazao yaliyokuwa yamepandwa jirani na nyumba yake.
Hata hivyo hasira za wananchi hao hazikuishia hapo bali walimsakama Mwanamke mwingine aliyejulikana kwa jina la Agnes Sika ambaye ni mke wa Mchungaji wa kanisa la Pentecost Groly  kwa madai kuwa ni rafiki wa mtuhumiwa na amekuwa akimfichia siri.
  
Jeshi la Polisi liliwahi kufika eneo laTukio na kumnusuru Agnes asipatwe na madhara ikiwa ni pamoja na kutochomewa nyumba yake ambayo tayari wananchi hao walionekana kuikimbilia kwa ajili ya kutaka kuibomoa.
  
Aidha Jeshi la polisi linaendelea kumshikilia mtuhumiwa kwa ajili ya mahojiano zaidi pamoja na upelezi ambapo Baba mzazi wa Mtoto anayesadikiwa kupotea katika Mazingira ya kutatanisha akisema anamwachia Mungu  baada ya juhudi za kumtafuta kushindikana.
picha na E. Kamanga
................................................................................................................................

BAISKELI; USAFIRI UNAOTEGEMEWA NA WAJAWAZITO KYELA

 
kyela

Wanawake wa kijiji cha Masoko wakiwa wamekusanyika ili kuongea na mwandishi wa habari hii
Na Stella Mwaikusa
Wajawazito wa vijiji vya Masoko na Busoka vinavyopatikana kata ya Busale wilaya ya Kyela, wamekuwa wakitumia usafiri wa baiskeli wakati wa kwenda kupima maendeleo ya ujauzito katika zahanati ya Lema, ambayo iko umbali wa km sita kutoka vijiji  hivyo.
Zawadi Oscar (22) mkazi wa kijiji cha Masoko  anasema alipokuwa na ujauzito alikuwa akitumia usafiri wa baiskeli kwenda kliniki ,kutokana na zahanati ya Lema kuwa mbali na kijiji hicho.
“Nilikuwa na ujauzito wa miezi nane, ,lakini  niliendesha baiskeli kwenda kliniki, maana afadhali kwenda huko kwa baiskel kuliko kutembea kwa mguu, unachoka sana” anaeleza Zawadi.
Chistina Musa  mkazi wa kijiji cha Masoko anasema usafiri wa baiskeli kwa wajawazito katika kijiji hicho ni kitu kilichozoeleka, kwani hata yeye hutumia usafiri huo anapoenda kliniki katika zahanati ya Lema.
Anasema haoni tatizo kuendesha baiskeli, japo alikiri kwamba baada ya kutoka zahanati hujisikia kuchoka, lakini hana namna kwani katika kijiji anachoishi hakuna zahanati.
Mganga mkuu wa zahanati ya Lema, Mariam Ninde anasema ni kweli wajawazito kutoka vijiji vya Masoko na Busoka hutumia usafiri wa baiskeli na kuutaja usafiri huo kutokuwa na madhara kiafya kwa wajawazito. 

“Mjamzito anapoendesha baiskeli ni moja kati ya mazoezi kwa hiyo hakuna ubaya,” anaeleza Ninde.
...............................................................................................................................
 WABUNGE ZITTO, AZAN WAMALIZA MAFUNZO YAO YA JKT KAMBI YA MGAMBO 835KJ

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe pamoja na Wabunge wenzake kadhaa vijana leo Machi 26,2013 wamemaliza rasmi mafunzo yao ya awali ya JKT katika kambi ya Mgambo 835KJ kilichopo Mkoani Tanga.
Pichani juu ni Zitto na Azan akijiandaa kwenda katika gwaride la mwisho na picha chini akiwa shambani pamoja na Mbunge mwenzake  Iddi Azan, Abdallah haji, Raya Ibrahim na Antony Mbassa kambi ya Mgambo 835KJ.
Aidha Zitto Kabwe amesema anafuraha iliyo pitiliza kumaliza mafunzo hayo na ameweka historia ya kubwa katika maisha yake. 
.............................................................................................................................

ELIZABETH T. MOSHI AMBAYE NI AFISA UTUMISHI WA WILAYA YA RUNGWE AFANYIWA SHEREHE YA KICHENPART NA WAMAMA WA TUKUYU MJINI ANATARAJIA KUFUNGA NDOA MWANZONI MWA MWEZI WA NNE JIJINI ARUSHA

ELIZABETH MOSHI AKIWASHUKURU WAKINA MAMA WA TUKUYU KWA KUMUAGA KWA SHEREHE ILIYOFANA NA KUFUATA MAADIRI
ELIZABETH AKIWA NA MPAMBE WAKE WAKIINGIA UKUMBINI
MWENYEKITI WA KAMATI AKIMSHUKURU BIBI HARUSI MTALAJIWA KWA KUJITUNZA NA KUFIKIA UTU UZIMA WA KWENDA KUOLEWA


KATI YA ZAWADI NYINGI ALIZOPEWA ELIZABETH MOSHI

MWL ELIZABETH SEKILE AMBAYE NDIYE MC WA SHEREHE AKIMFURAHISHA JAMBO ELIZABETH HA HA HA HA HA HA MWANAMKE KUTUNZA NDOA ( MIE NILIISIKIA KWENYE MKANDA WA VIDEO MAANA HUMO NDANI SIRUHUSIWI KUINGIA)

ALIYESHIKA CAMERA KULIA NDIO MKE WA BAROZI WENU KINGO YEYE ALIKUWA NDIYE KATIBU WA SHEREHE YA ELIZABETI AMABAYE NI AFISA UTUMISHI ANAYETARAJIA KUFUNGA NDOA MWANZONI MWA MWEZI WA NNE JIJINI ARUSHA.

No comments: