Monday, March 4, 2013

JUMUIYA YA WANAWAKE CCT WILAYANI RUNGWE WATEMBELEA WAGONJWA WA UKOMA MAKETE KIJIJI CHA KISONDELA WILAYANI RUNGWE KWA KUFANYA IBADA YA MAOMBEZI NA KUTOA MISAADA MBALIMBALI IKIWA NI FARAJA KWA WAGOJWA

NILIPOFIKA KATIKA KITUO CHA WAGONJWA WA UKOMA KILICHOFUNGULIWA MWAKA 1895 NA KUJENGWA NA JUMUIYA YA MADOLA KWA USHIRIKIANO WA WAKOLONI NA KITUO KUFUNGWA MWAKA 1950 NA UGONJWA WA UKOMA UKATANGAZWA KUISHA TANGANYIKA  LEO NIMEKUTANA NA TANGAZO HILI
MUONEKANO WA MAKETE WILAYANI RUNGWE KIJIJI WANAPOISHI WAGONJWA WA UKOMA. UGONJWA WA UKOMA KWA KIRUGHA CHA KINYAKYUSA UNATAMBULIKA KUWA NI MAKETE HIVYO ENEO HILI LIMETAMBULIKA KUWA MAKETE KWAKUWA WAGONJWA WA UKOMA WANAISHI HAPA NA MAENEO HAYA ILIKUWA NI MAPORI YA KUTISHA MAANA WAGONJWA ZAMANI WALIKUWA WANATENGWA NA JAMII KWA HOFU YA KUAMBUKIZA WENGINE

MUONEKANO WA MAJENGO YALIYOKUWA KITUO CHA WAGONJWA WA UKOMA MAKETE WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA

MOJA YA MAKANISA YALIYOPO KITUONI HAPO YAKIWA YAMEFUNGWA



WANANCHI WA KIJIJI CHA KISONDELA WAKIWA WANAPITA KITUONI HAPO HUKU WAKIELEZEA KUWA KITUO KIMETELEKEZWA NA SERIKALI NA HAKUNA MATUMIZI MMBADALA YALIYOLENGA KUTUMIA KITUO HICHO HIVYO VITU VINGI VIMEIBWA NA KUBAKI MAJENGO JAPO KWA SASA NI IMARA LAKINIYANAHITAJI USIMAMIZI

KATIKA KITUO HICHO JENGO MOJA NDILO LINATUMIKA KAMA OFISI YA MKUU WA SHULE YA SEKONDARI YA KISONDELA

KWAKWELI KWAKUWA ILIKUWA MALA YANGU YA KWANZA SIJAELEWA KINACHOENDELEA KATIKA KITUO HIKI NAJIULIZA KWANINI PASIENDELEZWE? TUNAHITAJI VYUO VYA VETA, HIGH SCHOOL, HOSPT,  KWANINI HAPA TANGU KITUO KIFUNGWE MWAKA 1950 NA WAGONJWA WENGI WAMEFIA HAPO NA WENGINE KUPEWA MAKAZI AMBAO HADI SASA WATOTO WAO WAPO KATIKA KIJIJI HICHO SASA KWANINI PASIENDELEZWE ILI WANANCHI WAKAFAIDIKA NA KITUO HIKI KULIKO SASA KILIVYO?

NIKAAMUA KUJURUDIA KANISANI AMBAKO AKINA MAMA WA JUMUIYA YA KIKRISTO WILAYANI RUNGWE WAMETEMBELEA WAATHIRIKA WA UGONJWA WA UKOMA WANAOISHI KIJIJI CHA KISONDELA WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA
IBADA IMEFANYIKA KANISA LA MORAVIANI  MAKETE WILAYANI RUNGWE

NIA NA MADHUMUNI ILIKUWA NI IBADA YA MAOMBEZI NA KUMSHUKURU MUNGU

IBADA IKIENDELEA KWA AMANI NA FURAHA MAANA HAYAYOTE HAYATAFANYIKA KAMA TANZANIA IKIINGIA MACHAFUKONI KAMA AMANI ILIYOPO ITACHAFULIWA KILA MTU YAMPASA KUILINDA AMANI ILIYOPO

KATIBU WA UMOJA WA WANAWAKE WA CCT WILAYANI RUNGWE ROSTA MWAMBENJA AKIONGEA NA WAUMINI NA WAGONJWA WA UKOMA JINSI MUNGU ANAVYO WAPENDA KWA KUPITIA WATU MBALIMBALI KUJITOLEA VITU KAMA NGUO, PESA, NA VYAKULA VITAKAVYOGAWIWA  KWA UPENDO WA KUWAJARI WAGONJWA WASIO JIWEZA KWA KUWA MAANDIKO YAMESEMA IBADA YA KWELI NI KUWAJARI WASIOJIWEZA

WAKIWA NJE YA KANISA TAYARI KWA KUPEWA MISAADA

MZEE ALBETO MWALUANDA AKIONGEA KWA UCHUNGU JINSI WASIVYOPATA HUDUMA ZA MSINGI HUKU TATIZO LA UKOMA LIKIONGEZEKA KIJIJINI HAPO NA SERIKALI KUWATELEKEZA HATA KUWATEMBELEA IMEKUWA SHIDA. PIA AMESEMA KUWA SERIKALI ISIMAMIE AMANI YA TANZANIA MAANA KAMA NCHI IKIINGIA MACHAFUKONI JE WAO KAMA WAKOMA WATAKIMBILIA WAPI?

MZEE WA KANISA LA MORAVIANI MAKETE AKISHUKURU WAGENI WA CCT KWA KUTEMBELEA WAKOMA JAPO ALIKUWA NA WITO KWA SERIKALI KUFUFUA HUDUMA TENA MAANA WAGONJWA WANAZIDI KUONGEZEKA KIJIJINI HAPO

BAADHI YA WAGONJWA WA UKOMA

MUDA WA MAOMBEZI KWA WAGONJWA NA KUOMBEA AMANI YA NCHI YA TANZANIA

KIONGOZI WA WAGONJWA WA UKOMA AKIPOKEA ZAWADI KWA NIABA YA WENZAKE

ZAWADI ZIKATOLEWA NA WANAWAKE WA CCT WILAYANI RUNGWE KWA WAATHIRIKA WA UKOMA MAKETE KIJIJI CHA KISONDELA
HUWEZI AMINI KUWA BIBI HUYU HAWEZI KUTEMBEA VYEMA LAKINI HAPO ANASHUKURU KWA CCT KWA KUWAKUMBUKA NA KUWAPA MSAADA WA NGUO, CHAKULA, NA FEDHA IKIWA NI ALAMA YA UPENDO KWAO
BIBI KWA MSAADA WA MJUKUU WAKE WAKIFUNGA ZAWADI ZAO ILI WARUDI MAKWAO

MAMA AKIFUNGA ZAWADI ZAKE
BALOZI WENU NIKIONGEA NA MZEE SWILLA MMOJA WA WAATHIRIKA WA UKOMA AMBAPO NILIPATA MENGI SANA KWAKE NA KWANINI SERIKALI NA JAMII IMEWATENGA KWA KIASI KIKUBWA KWA KUTOWAKUMBUKA KWA KUPEWA HUDUMA ZA MSINGI KAMA DAWA, MAVAZI NA MALAZI, LAKINI SWILLA ANASEMA WAGONJWA WA UKOMA BADO WAPO NA WANATESEKA SANA HIVYO AMEIOMBA JAMII NA SERIKALI KUWATEMBELEA ILI KUJUA MAHITAJI YAO YA MSINGI. PIA AMESEMA UGONJWA WA UKOMA UMEKUWA TISHIO MAENEO HAYO KWAKUWA SERIKALI HAIJAWEKA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA UGONJWA HUO HIVYO WATU WENGI WATAENDELEA KUATHIRIKA                                                                                                                                                                                                                                                                           ( KINGOTANZANIA INATOA WAZO KWA WADAU WA HUMU NDANI KUWASAIDIA WENZETU WANAOUMWA UKOMA ILI TUWE NA WAZO LA PAMOJA NI JINSI GANI TUTAKAVYOWAFIKIWA WENZETU WENYE UHITAJI HUU WA MATIBABU, MALAZI, MAVAZI NA ZAIDI CHAKULA)                                                                                                 ASANTE NDIMI BALOZI WENU KINGO 


ASKOFU DR ESRAEL PETER MWAKYOLILE AONGOZA MAZISHI YA MCHUNGAJI YOHANA MWASAMPETA KKKT USHARIKA WA MASEBE WILAYANI RUNGWE MKOA WA MBEYA
ASKOFU DR ESRAEL MWAKYOLILE KKKT DAYOSISI YA KONDE


USHARIKA WA MASEBE MAZIKO YALIPOFANYIKA

MFIWA MCH MWASAMPETA MDOGO WA MAREHEM AKIWA NA WACHUNGAJI WENZAKE KABLA YA IBADA KUANZA

WACHUNGAJI WA KKKT DAYOSISI YA  KONDE WAKIWA WAMEBEBA JENEZA KUELEKEA MAKABURINI

JENEZA LIKISHUSHWA KABURINI


YOHANA MWASAMPETA , ULIKUJA KWA UDONGO, NA UTARUDI KWA UDONGO, SIKU YA MWISHO UTAFUFULIWA,. NIMANENO YA MWISHO BABA ASKOFU MWAKYOLILE AKIHITIMISHA MAZIKO YA MCHUNGAJI YOHANA MWASAMPETA

MKE WA MAREHEM NA WAFIWA WENGINE


MCH MWASAMPETA MDOGO WA MAREHEM MWENYE SUTI NYEUPE AKIWA ANARUDISHIWA UDONGO KATIKA KABURI LA KAKA YAKE

ZAIDI YA ABIRIA 50 WA BASI LA SUMRY LITOKALO SUMBAWANGA KUJA MBEYA WANUSURIKA KUFA KWENYE AJALI ILIOTOKEA MPAKANI MWA SONGWE NA MBOZI MBEYA






ZAIDI YA ABIRIA 50 WA BSI LA SUMRY LITOKALO SUMBAWANGA KUJA MBEYA LIMEPATA AJALI MAENEO YA SONGWE MPAKANI MWA WILAYA YA MBOZI CHANZO CHA AJALI HIYO NI KUWA ROLI LA MIZIGO LA KAMPUNI YA KANJILAJI LILIKUWA LINAIPITA GARI NYINGINE HIVYO KUHAMIA UPANDE WA BASI LA SUMRY NA NDIPO DEREVA WA SUMRY AKAONA KUA WATAGONGANA USO KWA USO AKAAMUA KULIINGIZA SHAMBANI ILI KUJIOKOA KATIKA AJALI HIYO













 MOJA YA MAJERUHI BENO GILBET MKAZI WA ZANZIBAR ALIKUWA ANATOKEA SUMBAWAGA KWENDA ZANZIBAR SASA AMELAZWA KATIKA HOSPITALI YA TEULE YA IFISI

MAJERUHI MUSA KAPINUKE



MAJERUHI CHALES KAUZENI  15

MUUGUZI ELMAT KAKAKU AMESEMA WAMEPOKEA MAJERUHI 47 KATI YA HAO WAWILI WAMEPELEWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA BAADA YA HALI ZAO KUWA MBAYA ZAIDI




HABARI KAMILI YA AJALI HII TUTAWAFAHAMISHA BADO TUNAFUATILIA

PICHA NA Jem WA MBEYA YETU

PINDA: TUSAIDIENI KUTAFUTA KIINI CHA KUSHUKA KWA ELIMU

pinda121 *Azindua tume ya watu 15, aipa wiki sita kukamilisha kazi
  WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amezindua Tume maalum aliyoiunda ili ifanye uchunguzi wa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne yaliyotangazwa Februari 18, mwaka huu na kuwataka wajumbe wa Tume hiyo watafute kiini cha mserereko wa kushuka kwa ufaulu kuanzia mwaka 2010 hadi 2012.
 
Ametoa kauli hiyo leo asubuhi (Jumamosi, Machi 2, 2013) wakati akizungumza na wajumbe wa Tume hiyo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Magogoni, jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa.
 
“Nimetafuta takwimu za tangu mwaka 2005, Serikali ya Awamu ya Nne ilipoingia madarakani na kubaini kuwa tangu wakati huo hadi mwaka 2009 tulikuwa tukifanya vizuri, lakini kuanzia mwaka 2010 hadi 2012 matokeo yamekuwa yakishuka sana,” aliwaambia wajumbe wa Tume hiyo na waandishi wa habari waliohudhuria uzinduzi huo.
 
Alisema hali hiyo haikuwa kwenye shule za sekondari za umma (kata) peke yake bali hata kwa shule za Serikali, za watu binafsi na kwenye seminari ambazo kwa miaka mingi zimekuwa na sifa ya kufanya vizuri kuliko shule za kawaida.
 
Akitoa mfano, Waziri Mkuu alisema: “Mwaka 2005 kiwango cha ufaulu kilikuwa asilimia 89.3; mwaka 2006 asilimia 89.12; mwaka 2007 asilimia 90.6; mwaka 2008 asilimia 83.6 na mwaka 2009 asimilia 72.5, hapa napo tulikuwa bado tuko vizuri japo si sana ikilinganishwa na miaka mine iliyotangulia.”
 
“Lakini mwaka 2010, kiwango cha ufaulu kilishuka na kufikia asilimia 50.4, mwaka 2011 kilipanda kidogo na kufikia asilimia 53.6 na kilishuka zaidi mwaka jana ambapo kilifikia asilimia 34.5. Hapa ni lazima mtu utapata maswali ya msingi na kujiuliza nini kimetokea katika miaka ya hivi karibuni,” alisema.
 
 

Wafugaji wa Kimasai wamtembelea Rais Kikwete kijijini Msoga

8E9U4419Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete  akiwaonesha ng’ombe wafugaji wa Kabila la Wamasai waliomtembelea katika shamba lake la mifugo kijijini Kwake Msoga,Kata ya Chalinze,wilayani Bagamoyo jana(Jumapili)(picha na Freddy Maro).
……………………………………………………………..
Na Freddy Maro Msoga,Bagamoyo.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ametoa wito kwa wafugaji nchini kupima na kupanga ardhi kwaajili ya ufugaji wa bora wenye tija na kuepusha migogoro kati ya wakulima na wafugaji inayotokana na ufugaji wa kuhamahama kutafuta malisho.
Rais Kikwete alitoa rai hiyo wakati alipokuwa akizungumza na wafugaji wakabila la wamasai kutoka mkoa wa Pwani na Morogoro waliomtembelea nyumbani kwake kijijini Msoga kata ya Chalinze, wilayani Bagamoyo jana(Jumapili).
“Ni lazima mtambue kwamba ufugaji wa kuhamahama hauna tija kwakuwa watu wengi sasa wametambua thamani ya ardhi wanaipima na kuimiliki na hivyo maeneo ya kuchunga mifugo yanapungua.Huu ni wakati muafaka wa kupima ardhi na kuimiliki kwaajili ya ufugaji wa kisasa,” alisema Rais Kikwete.
Sambamba na kutenga maeneo maalumu kwaajili ya ufugaji Rais Kikwete amewahimiza wafugaji hao kuotesha  majani kwaajili ya malisho ya mifugo ili kuepuka upungufu wa lishe ya wanyama wakati wa kiangazi na kuhakikisha mifugo hiyo inabakia na afya njema kwa faida ya wafugaji.
Wakizungumza awali,wafugaji hao waliiongozwa na kiongozi wao Mkuu Laiboni Tikwa Moreto walimshukuru Rais Kikwete kwa kuwajengea Shule ya Sekondari kwaajili ya Watoto wa wafugaji ambayo sasa hivi ina jumla ya wanafunzi 146.
“ Tunakushukuru sana kwa kutujengea shule ya Sekondari Moreto na watoto wetu sasa wamepata fursa ya kusoma na tuna kuomba utusaidie ili tuweze kuongeza madarasa,mabweni na maji ya kutosha ili wanafunzi waliopo waweze kusoma kwa ufanisi,”walisema katika risala yao kwa Rais Kikwete.
Akijibu Rais Kikwete aliwapongeza kwa kuitunza shule hiyo na kusema kuwa maisha ya kuhamahama  kwa wafugaji yanawakosesha watoto wao fursa ya kupata elimu na kuahidi kuendelea kuisadia shule hiyo ili watoto wengi zaidi waweze kunufaika na elimu ya sekondari.
Baadaye wafugaji hao walipata fursa ya kutembelea shamba la mifugo la Rais Kikwete kijijini Msoga na kujionea ufugaji wa kisasa unaozingatia kanuni bora za kitaalamu ambapo ngo’mbe mmoja anaweza kufikia uzito wa kilo miasaba.

No comments: