Tuesday, March 12, 2013

WAMILIKI NA MADEREVA WA MAGARI KUANZIA TANI MOJA MPAKA TANO WASHANGILIA KUFUTWA KWA SHERIA NDOGO YA HALMASHAURI YA JIJI LA MBEYA YA KUWATAKA WALIPE USHURU WA SH 58,000 KWA MWAKA


Meya wa Jiji la Mbeya Ndugu  Attanus Kapunga akiwaomba watulie ili awasikilize shida yao wamiliki na madereva wa magari ya biashara kuanzia tani moja
Makamu mwenyekiti wa chama cha wamiliki na madereva waendesha maroli jijini mbeya Gorden Mwamakula akieleze wanavyonyanyaswa na wakala aliyeteuliwa na jiji la mbeya kukusanya usajiri wa magari yao huku akiwatoza kiwango kikubwa na kuwalipisha faini zisizoeleweka

Paulo Mwasilelwa Dereva wa Pick up ambaye pia ni katibu
 wa Chama cha waendesha maroli Jiji la Mbeya amesema
 wanapingana na ushuru huo ambao unatozwa unawaumiza kwa sababu hulazimika kulipia gharama za usajili wa gari linaponunuliwa, bima ya gari,Tra, maegesho na zimamoto ambavyo lazima vilipiwe.
Wamiliki na madereva wao wakiwa makini kumsikiliza meya wa jiji la mbeya
Emmanuel Mbuza  mmilikiwa Mbuzax Auction Mart & Court Brockers akiingia ukumbini hapo huku madereva na wamiliki wa maroli wakimtolea macho
Moja ya wanasheria wa jiji la Mbeya Kaijage akielezea sheria inayotumika kukusanya ushuru huo wa maroli yanayofanya biashara katika jiji la Mbeya
Jamani kwakweli kiwango cha shilingi 58,000/ kwa mwaka ni kikubwa sana kwani kila siku tunalipa shi 1000 kwa maegesho ya magari yetu pili huyu wakala mliyempa kazi hii hatuelewi ni kigezo gani kilitumika kumpatia kazi hiyo kwani ni mnyanyasaji sana moja ya madereva akitoa malalamiko yake kwa meya
Mheshimiwa meya siku ytulipokuja ofisini kwako kukueleza juu ya huyu wakala wenu ukasema humtambui sasa leo nashangaa unasema unamtambua sasa tukueleweje hapo mweshimiwa meya unatuchanganya
Kwa ujumla huyu wakala hatumwelewi tunamlipa hiyo kodi risiti anatupatia za malipo ya Taxi 
Emmanuel Mbuza akinyoosha mkono ili apatenae kuzungumza kidogo hapo ndipo palikuwa pangumu kelele zilitawala ukumbi mzima kutaka akae la sivyo hali ya hewa humo ukumbini itachafuka

Naibu meya Fungo akijaribu kuwatuliza wamiliki hao wasiendelee na kelele jamani tumewaelewa Mbuza tunaomba ukae ili kikao kiendelee 
Ndugu zangu tumegundua kweli kwenye sheria hiyo kunamapungufu mengi ya kukusanyaji wa ushuru huo hivyo basi zoezi hili nalisimamisha mpaka tukakae na wenzangu ili tuiangalie upya sheria hiyo pia wakala huyu hata takiwa tena kukusanya ushuru huo kuanzia leo hapo ukumbi ulilipuka kwa vifijo na fulaha baada ya mweshimiwa meya kutamka tamko hilo
Jamaa wakiondoka kwa furaha kufuatia ushindi wa matatizo waliotoa kwa meya wa jiji la Mbeya

Emmanuel Mbuza amesema kutokana na kuvunjwa na kufutwa kwa sheria hiyo kutampunguzia yeye kufanya kazi katika mazingira magumu yanayosababisha kuwa na ugomvi na wananchi wanaotakiwa kulipia ushuru huo.


HALMASHAURI ya Jiji la Mbeya limelazimika kuifuta Sheria ndogo ya Halmashauri hiyo namba 376 (4)na (1) ya Mwaka 2011 iliyokuwa inataka kusajili magali ya kukodi, teksi,Bajaji na Pikipiki kwa kulipia ushuru Shilingi 58,000/=kwa Mwaka.
Sheria hiyo imefutwa  baada ya kutokea ugomvi mkubwa baina ya wamiliki na madereva wa magari kuanzia tani moja hadi tano nne na wakala aliyepewa zabuni ya kukusanya ushuru huo.
Ushuru unaolalamikiwa na wamiliki hao wa magari ni ule unaokusanywa na Halmashauri hiyo kupitia kwa wakala aliyejulikana kwa jina la Mbuzax Auction Mart & Court Brockers inayomilikiwa na Emmanuel Mbuza.
Wananchi hao walitoa malalamiko hayo kwenye mkutano wapamoja kati ya wamiliki wa magari, madereva na viongozi wa Halmashauri ya Jiji chini ya Meya uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri uliopo Sokomatola Jijini hapa.
Wakizungumza kwenye mkutano huo Madereva hao wamesema utaratibu wa ushuru huo unawaumiza sana kutokana na kuwa na gharama kubwa kama ushuru wa usajili kwa mwaka Shilingi 58,000/= pamoja na ushuru wa kuegesha magari kila siku shilingi 1000/=.
Paulo Mwasilelwa Dereva wa Pick up ambaye pia ni katibu wa Chama cha waendesha maroli Jiji la Mbeya amesema wanapingana na ushuru huo ambao unatozwa unawaumiza kwa sababu hulazimika kulipia gharama za usajili wa gari linaponunuliwa, bima ya gari,Tra, maegesho na zimamoto ambavyo lazima vilipiwe.
Amesema Kodi ya Maegesho ni zaidi ya Shilingi 360000 kwa mwaka hivyo ukiongeza na ushuru wa usajili gari haliingizi fedha yoyote badala yake linadumaza uchumi wa mwananchi wa kawaida ambapo aliongeza kuwa biashara ya magari hiyo haina uhakika kutokana nakutokuwa na wateja wanaoeleweka badala yake wanasuburi kukodishwa.
Wameongeza kuwa utaratibu unaofanywa na wakala huyo ni mbovu ambao walidai kuwa wakala huyo hutumia nguvu nyingi hali inayosababisha kuhatarisha maisha yao kutokana na watumishi wa wakala huyo kutumia mapanga kuwatishia maderev pamoja na kuwajeruhi.
Akijibu tuhuma hizo Meya wa Jiji la Mbeya Ndugu  Attanus Kapunga aliyekuwa amefuatana na Kamati ya Fedha ya baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo alisema kutokana na sheria iliyokuwa imepitishwa na madiwani hao kutotolewa elimu kwa wananchi wanaotakiwa kulipa kodi inamakosa.
Kapunga amesema kama sheria haileti amani baina ya wananchi inatakiwa iangaliwe upya hivyo wakala anatakiwa kusimama mara moja ili Sheria hiyo iangaliwe upya kwa maslahi ya maendeleo ya Jiji hilo.
Amesema kitendo cha wakala huyo kukusanya ushuru kinyume na maeneo aliyoaambiwa ni kosa kubwa ikiwa ni pamoja na kutumia ubavu kudai kodi ambayo Halmashauri haijamtuma ni kinyume na taratibu alizopangiwa.
Ameongeza kuwa kutokana na mapungufu yaliyojitokeza kwenye sheria hiyo lazima wakala asimame asubiri vikao vikae upya na kuitazama upya ili isiwagombanishe na wananchi hali itakayosababisha uvunjifu wa amani.
kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Mbuzax Emmanuel Mbuza ambaye awali hakupewa nafasi ya kujitetea kutokana na madereva kumzomea pindi aliponyoosha mkono akitaka kujitetea hadi mkutano unafungwa aliwaambia waandishi wa habari kuwa anaishukuru Halmashauri hiyo kwa kugundua mapungufu ya sheria zao.
Mbuza amesema kutokana na kuvunjwa na kufutwa kwa sheria hiyo kutampunguzia yeye kufanya kazi katika mazingira magumu yanayosababisha kuwa na ugomvi na wananchi wanaotakiwa kulipia ushuru huo.
Amesema kilichofanyika ni Hlmashauri ya Jiji kugundua kuwa sheria iliyokuwa ikitumika ilikuwa na mapungufu ambayo wakala asingeweza kuyajibu badala yake walipa kodi walikuwa wakitoa lawama ambazo zilikuwa nje ya uwezo wake.
 

BALOZI KHAMIS KAGASHEKI AWATAKA WAANDISHI WA HABARI 

WANAWAKE KUHAMASISHA AMANI KWA KALAMU ZAO

Na Mwanishi Wetu
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki amewataka waandishi wa Habari wa Kike kutumia kalamu zao katika kuandika mambo yanayohamasisha amani na utulivu nchini.
Pia aliwataka kutumia kalamu zao katika kuandika na kuibua vitendo vya unyanyasaji na vya kikatili wanavyofanyiwa wanawake nchini.
Hayo aliyasema hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika Hotel ya Lamada , wakati wa uzinduzi wa kikundi cha Habari Group kinachojumuisha waandishi mbalimbali wa habari hapa nchini.
Alisema ni vyema wakatumia fursa zao katika kufichua viashiria mbalimbali vya fujo kwa kuwa endapo itatokea uvunjifu wa amani wanaoathirika zaidi ni wanawake na watoto.
Kikundi cha habari kinajihusisha na ununuaji wa hisa, kukopeshana na kufanya miradi mbalimbali ya kikundi na mmoja mmoja hivyo aliwataka wanakikundi kujibidiisha zaidi na kuongeza wanachama wake.
“Uwezeshaji wa wanawake kiuchumi ni moja ya maadhimio 12 ya ulingo wa Belgin hivyo mnachofanya hapa ni katika kujikwamua wenyewe kiuchumi na kama mnavyofahamu wanawake wanamajukumu mengi katika familia na pia kutingwa na mambo mengi katika tasnia yenu lakini mmethubutu kufanya hivyo hivyo endeleeni,”alisema Kagasheki
Pia alitoa wito kwa wanawake kuhakikisha kuwa majukumu waliyonayo yasiwe kikwazo kwao kushiriki katika kukuza uchumi.
Alisema kinachotakiwa ni kuondoa fikra kuwa haiwezekani na kuhakikisha wanapiga vita mambo yanayomgandamiza mwanamke kwa kuondoa fikra kwamba haiwezekani kujikwamua kiuchumi.
Naye mlezi wa kikundi hiko ambaye pia ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angella Kairuki alisema atakuwa bega kwa bega na wanakikundi hiko katika kuhakikisha kuwa kinasonga mbele.
“Nimefurahishwa sana na wazo la wanahabari hawa na nina ahidi nitakuwa nao bega kwa bega katika kuhakikisha kuwa kikundi kinakua zaidi na kuwatafutia fursa mbalimbali za kukiendeleza pia,”alisema Kairuki.
 
 
UPOTEVU WA DAWA ZA KULEVYA


Sehemu ya mbele ya gari ikiwa imefunguliwa kwa uchunguzi zaidi
Picha chini :Askari polisi akilinda sehemu ya madawa ya kulevya yaliyotolewa kwenye gari hiyo



Baadhi ya maofisa hao ni kamanda wa kikosi cha upelelezi mkoani Mbeya (RCO) Elis Mwita, naibu RCO Jacob Kiangi na mkuu wa kikosi cha FFU Charles Kinyongo. 
 
Hii ni baada ya kupeleka sukari na chumvi kwa mkemia mkuu badala ya madawa ya kulevya KILO 1.9. Maafisa hao ni wa jeshi la polisi Mbeya;

WAZIRIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, amesema Jeshi la polisi limewasimamisha kazi, na kuwafungulia mashtaka ya kijeshi askari wake katika maeneo mbalimbali nchini kwa kwenda kinyume na kanuni za kijeshi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Dk Nchimbi, alisema katika kikao cha Maofisa na Makamishna wa polisi kilichoketi Dodoma havi karibuni waliazimia kuanza kuchukua hatua za kinidhamu kwa askari wote watakaokwenda kinyume na kanuni na maadili ya jeshi hilo. 
Nchimbi aliwataja waliosimamishwa na kufunguliwa makosa ya kijeshi ni pamoja na Elis Mwita, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi ambaye alikuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Mbeya, Jacob Kiango, Mrakibu msaidizi wa Polisi, aliyekuwa msaidizi wa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mbeya, na Charles Kinyongo mrakibu msaidizi wa Polisi ambaye alikuwa mkuu wa kikosi cha kutuza ghasia Mkoa wa Mbeya.

Dk Nchimbi alisema askari hao wote wanatuhumiwa kushiriki mchakato wa kutunza na kusafirisha mihadarati aina ya cocaine, yenye uzito wa kilo 1.9, yaliyokamatwa katika kituo cha Tunduma, kuthibitishwa na Maofisa wa Malaka ya Mapato (TRA), kuwa kweli ilikuwa ni mihadarati.


Alisema lakini walipoyaleta kwa Mkemia Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam, na kufanyiwa chunguzi ikabainika kuwa haikuwa mihadarati bali ilikuwa ni Chumvi na sukari.
Dk Nchimbi alisema baada ya taarifa hiyo Kamati ya Mkoa wa Mbeya ikaomba ifanyiwe uchunguzi na kubaini kuwa kilichopelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali sicho kilichokamatwa, bali kulikuwa na udanganyifu, jambo lililosababisha wizara iunde tume iliyobaini kuwa wana tuhuma ya kujibu.

“Askari wadogo wakishirikiana na maofisa wa TRA waliokamata mihadarati hiyo wanajua chumvi na sukari, hivyo vigogo hao walishiriki katika njama ya kubadilisha”alisema DK Nchimbi.
Akizungumzaia mgogoro wa Ardhi kati ya mwekezaji na wanakijiji, Dk Nchimbi alimtaja Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Peter Mtagi, kuwa amesimamishwa kazi na kufunguliwa mashtaka ya kijeshi.

Alisema Mtagi ambaye pia alikuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Kagera anatuhumiwa kuwabambikizia kesi wananchi kuwa majambazi, waliiba kwa kutumia silaha ili wasipatiwe dhamana baada ya kupokea rushwa.
“Mimi sipendi watu wafanye vurugu lakini napenda haki itendeke sasa katika hili askari hawa hawakufuata taratibu na walikuwa wanajua kuwa wananchi wale walifanyavile baada ya kufanya mkutano wa hadhara na kubaini kuwa mwekezaji yule hakuwa na haki ya kumiliki ardhi kiasi hekari 4000”alisema.
Dk Nchimbi alisema wakati wananchi hao wakiwaswaga ng’ombe kuwapeleka kwa Mkuu wa wilaya, lakini wakiwa njiani walikamatwa na polisi, na wengine walikimbilia Dodoma kuonana na waziri mwenyewe.
Alisema lakini wakiwa huko, alipigiwa simu na askari polisi kutoka Kagera na kuelezwa kuwa watu hao ni majambazi sugu, hata hivyo, Nchimbi aliomba akutane nao, baini kuwa wananchi hao hawajawahi kuwa majambazi hivyo walisingiziwa tuhuma hizo kwa makusudi.

Naye Mkuu wa Kituo cha Polisi wa wilaya ya Serengeti, Paul Mng’ong’o (SSP), amefukuzwa kazi baada ya kuingia katika Hifadhi ya Mbuga ya Wanyama Serengeti na kupanga njama ya kuchimba madini aina ya dhahabu kinyume cha sheria, ambapo hivi sasa amefunguliwa kesi.
Kwa upande mwingine Dk Nchimbi alisema suala Kamishna Msaidizi Mwandamizi Renatus Chalamila, ambaye alikuwa anasimamia ajira za jeshi la polisi, anatuhumiwa kwa pamoja na maofisa wa polisi kujihusisha na vitendo kupokea rushwa na kuwaingiza vijana wengi katika Chuo cha polisi kilichopo Moshi, kinyume cha utaratibu.

“Katika tukio hili vijana 95 ambao waliingizwa katika chuo hicho cha askari bila ya kufuata utaratibu tumechukulia hatua za kuwafukuza chuoni hapo”alisema Dk Nchimbi
.
Nchimbi alisema kutokana na cheo chaka hicho mwenye madaraka ya kumfukuza kazi ni Rais hvyo taarifa hizo zomefikishwa kwenye mamlaka hiyo ambapo wakati wakisubiri maamuzi mengine wanawajibika kumpa likizo ya mwzi mmoja.

Katika hatua nyingine Dk Nchimbi alisema hawezi kuzungumziwa matukio ya kutekwa na kuteswa kwa Mwenyekiti wa Chama cha Dk Stephen Ulimboka na tuhuma zinazowakabili polisi kukwapua fuko lililokwa na sh milion 150 wakati wakitaka kuzima tukio la ujambazi eneo la Kariakoo mwaka jana, Nchimbi alisema, “hayo ni masuala ambayo bado yako ngazi ya chini mnaweza kumuuliza Kova, sio lazima yajibiwe na Waziri endapo atashindwa kufanya hivyo basi nitawajibika kujibu”.
 

No comments: