Wednesday, March 6, 2013

WILAYA YA RUNGWE YAINGIA LAWAMANI KWA KUSHINDWA KUWALIPA STAHIKI WALIMU WAPYA WALIOPANGIWA KWENYE HALMASHAURI HIYO.



Photo: Rungwe leo





Katika hali isiyokuwa ya kawaida halmashauri ya wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya imeingia lawamani baada ya kuwalipa walimu wapya viwango tofauti vya malipo ya kujikimu tofauti na ilivyoagizwa na serikali.
Hatua hiyo imekuja baada ya walimu hao kuripoti katika halmashauri hiyo na kutakiwa kulipwa fedha zao kwa mujibu wa mchanganuo wa serikali.
Walimu wapya wenye shahada walitakiwa kulipwa kiasi cha sh.315,000/=, badala yake wamelipwa sh.240,000/= na walimu wa stashahada walitakiwa kulipwa 240,000 na badala yake wamelipwa 190,000/= .
Hali hiyo imesababisha walimu hao kuhoji kwa nini wao wapewe hivyo ili hali wenzao wa mikoa na halmashauri zingine wakipewa pesa kamili?
Vuta ni kuvute hiyo iliyochukua takribani siku mbili haikuzaa matunda baada ya maofisa wa halmashauri hiyo kudai kuwa pesa hizo zinalipwa kutokana na umbali wa kituo cha kazi cha mwalimu husika.
Hata hivyo majibu hayo hayakuwaridhisha walimu hao na kuendelea kutafuta haki yao na kuamua kwenda kwa Mkurugenzi wa halmashauri yao lakini haki yao haikupatikana kutokana na mkurugenzi huyo kutotaka kuonana na mtu yeyote hivyo kuwaambia katibu muhtasi kuwa hayuko tayari kuonana na mtu yeyote.
Baada ya kuona haki yao haipatikani waliamua kumpigia simu na aliwajibu kuwa wapeleke suala hilo kwa maandishi ili alishugulikie, ndipo siku iliyofuata mkuu wa wilaya hiyo ya Rungwe alikutana na walimu hao na maafisa wa halmashauri na kuanza kufanya nao mazungumzo. 
Lakini katika hali ya kushangaza mkuu huyo wa wilaya alifanya kikao cha faragha kwanza na maafisa wa halmashauri na baadae ndipo akaja kutoa maamuzi na kuwaambia kuwa wao wamepewa fedha kidogo kutoka serikali kuu na ndio maana wameamua kuwapa hizo, lakini majibu hayo yalikuwa yakitofautiana na majibu ya siku zingine yaliyo sema fedha zinatolewa kwa kuangalia umbali wa eneo la kituo cha kazi. 
Baada ya majibu hayo walimu hao walionekana wakiwa na nyuso za huzuni mithili ya mtu aliye achwa nyikani.
“Haiwezekani wenzetu wa wilaya zingine wapewe stahiki zao zote halafu sisi tunapewa nusu, hakika huu ni ufisadi wa machomacho tukienda kufundisha madudu tusilaumiwe maana watu tumefika tangu wiki iliyopita halafu hatuna nyumba tuna lala gesti leo tunalipwa fedha kidogo hakika tutafika tu.” Alisikika mwalimu mmoja akihamaki.
Hii ni mara ya pili halmashauri hiyo kuingia lawamani baada ya mwaka jana 2012 kufanya hivyo hivyo hadi walimu waliamua kuwafungia ofisini maofisa wa halmashauri hiyo na ndipo wakaamua kuwalipa na hii inaonekana wazi kwa halmashauri hiyo kufanya mtindo huu kila mwaka. 
"Tunaiomba serikali na hasa TAMISEMI kuingilia kati suala hili na kuwachukulia hatua watumishi wa serikali wa halmashauri hii ili hali hiyo isijitokeze tena na walimu tupewe haki yetu"
Tayari tena mwee mbeya imezidi maeneo ya mwanjelwa haya
Tayari tena mwee mbeya imezidi maeneo ya mwanjelwa haya

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI ITALAZYA WILAYANI MBEYA VIJIJINI WAMO HATARINI KUKUMBWA NA MAGONJWA YA MLIPUKO KUTOKANA NA UKOSEFU WA VYOO

HIVI NI VYOO VYA WAALIMU WA SHULE HIYO
WANAFUNZI SASA HUJISAIDIA KATIKA VICHAKA HIVI KWAKWELI HATARI SANA KUKUTANA NA NYOKA NA WADUDU WENYE SUMU KALI picha na kamanga wa mbeyayetu

KIBANDA ASAFIRISHWA KWENDA KUTIBIWA AFRIKA YA KUSINI



 Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Absalom Kibanda, akiwa ndani ya Ndege ya Flightlink.

 Absalom Kibanda akiwa na mkewe ndani ya Ndege, Anjella Semaya, tayari kuanza safari ya kuelekea nchini Afrika ya Kusini kwa matibabu.(Picha na Amanitanzania)


 Baadhi ya waandishi na viongozi wa jukwaa la wahariri wakiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbi kwa ajili ya kumjulia hali.

 Absalom Kibanda akiwa amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kabla ya kusafirishwa kwenda Afrika ya kusini.

 Wafanyakazi wa Kampuni ya Ndege ya Flightlink wakimpandisha Absalom Kibanda ndani ya Ndege.

 akiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimili


 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Hussein Bashe akizungfumza na waandishi wa habari kuhusiana na tukio la kutekwa kwa, Absalom Kibanda

 Mwenyekiti wa CHADEMA, Freema Mbowe akimjulia hali Absalom Kipanda katika Hospitali ya Taifa ya Mhumbili Dar es Salaam. Picha na Amanitanzania

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AMJULIA HALI MWENYEKITI WA JUKWAA LA WAHARIRI ABSOLOM KIBANDA MUHIMBILI

2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimjulia hali Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, ambaye pia ni Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari 2006 Ltd, Absolom Kibanda, aliyelazwa katika Wodi ya Moi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, baada ya kujeruhiwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo wakati akiingia nyumbani kwake maeneo ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam. Picha na OMR 4
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, ambaye pia ni Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari 2006 Ltd, Absolom Kibanda, akionekana jinsi alivyojeruhiwa.


     BEATRICE KITAULI                                         ALBAM YA VIDEO YA UMENIINUA                  coming soon
Photo: BEATRICE KITAULI - UMENIINUA coming soon
SEHEMU YA CAVA YA ALBAM YA UMENIINUA

Photo
MAANDALIZI YA ALBAM YA VIDEO YA UMENIINUA

Photo
ALBAM INA NYIMBO 8 NA WIMBO MKUU UKIWA NI  (UMENIUA) IKO TAYARI KUINGIA SOKONI. MUIMBAJI WA NYIMBO ZA INJIRI BETRICE KITALI AMESEMA KUWA WATU WASUBIRI KUBARIKIWA KUTOKANA NA UJUMBE WA MUNGU ALIYE HAI ULIOMO KATIKA NYIMBO HIZI ZAIDI ANAWATAKIA AMANI WATANZANIA KWAKUWA AMANI NA UPENDO NDIO SIRAHA YA MAISHA YA WACHA MUNGU

No comments: