Wednesday, April 17, 2013

HARIMASHAULI YA RUNGWE YAPONGEZWA NA SERIKALI KWA USIMAMIZI MZURI WA PESA ZA MIRADI INAYOTEKELEZWA KATIKA JAMII HUKU CHANGAMOTO IKIWA NI KUMALIZA KWA WAKATI NA KUISHIRIKISHA JAMII MIRADI INAYOTEKELEZWA ILI WANANNCHI WENYEWE WAWE NA WAJIBU WA KUISIMAMIA MIRADI YAO


OFISI NA UKUMBI WA JOHN MWANKENJA ULIPO NA NDIPO KIKAO CHA MADIWANI KINAFANYIKA. NA HALMASHAURI YA RUNGWE YAKUSANYA 38% YA MAKUSANYO YA MAPATO YA NDANI KWANI KWA ROBO MWAKA TANGU MWEZI WA KWANZA 2013 MAKISIO ILIKUWA 2,060,800.00 HIVYO KUFANIKIWA KUKUSNYA TSH 787,700,396.27 SAWA NA 38%

JENGO JIPYA LA HALMASHAURI YA RUNGWE AMBALO LIMEANZA KUTUMIKA BAADA YA UJENZI ULIJENGWA KWA AWAMU KWA PESA YA MAPATO YA  NDANI
MADIWANI WA HALMASHAURI YA RUNGWE LEO WAKIWA KATIKA KIKAO CHA KAWAIDA

MADIWANI WAKIWA KWENYE KIKAO

KUSHOTO MR SHIRIMA DT WA WILAYA YA RUNGWE
WATENDAJI WA HALMASHAURI YA RUNGWE

MHE. A.M MWAKASANGULA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA RUNGWE

KUSHOTO MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA RUNGWE NA MKUU WA WILAYA YA RUNGWE WAKIMSIKILIZA MWENYEKITI WA HALMASHAURI AKIELEZA JINSI SERIKALI IMEIPONGEZA HALMASHAURI YA RUNGWE KWA USIMAMIZI MZURI WA PESA ZA UMA 

MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA AKIONGEA NA MADIWANI NA WATENDAJI PAMOJA NA WANANCHI WA WILAYA YA RUNGWE KUHUSU MAMBO MUHIMU YALIYOFANYIKA WILAYANI NA HALI YA USALAMA KATIKA WILAYA HUKU AKITOA TAARIFA YA UJIO WA ZIARA YA RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MKOANI MBEYA HUKU TAREHE 30 MWEZI HUU. RAIS JAKAYA MLISHO KIKWETE AKIWA NA ZIARA YA SIKU NZIMA WILAYANI RUNGWE NA ATAKAGUA SHUGHURI ZA MAENDELEO, PIA KUZINDUA MIRADI MIKUBWA MITATU 1. JENGO LA MRADI WA SACCOS KIWIRA 2. MRADI MKUBWA WA UCHIMBAJI WA GESI KATUMBA 3 MRADI WA UMWAGILIAJI WA SIKIMU YA BUSOKELO.

KATIKA KIKAO HIKI KIKATAMBULISHWA KIKUNDI KILICHOSAJILIWA KISHERIA AMBAO NI UMOJA WA WAKULIMA WA NDIZI NA KAHAWA WILAYANI RUNGWE HII NI JITIHADA ZA KUONGEZA UZARISHAJI WA ZAO LA KAHAWA NA NDIZI NA KUPAMBANA NA WALANGUZI HASA WANAO CHUMBIA NDIZI ZIKIWA SHAMBANI AMBAPO WAKULIMA WANAPATA HASARA SANA KWA KUUZA NDIZI  TSH 3000/= HUKU MUUZAJI AKIPATA FAIDA ZAIDI

MHE, MWALUSAMBA  AKICHANGIA MAADA YA UJENZI WA BARABARA ZINAZOSIMAMIWA NA HALMASHAURI ILI KUONGEZA UBORA NA KUJENGWA KWA WAKATI
MHE. MWASAKILALI DIWANI KATA YA KAWETELE AKIWASHUKURU WATENDAJI WA HALMASHAURI YA RUNGWE KWA KUFANIKISHA SUALA LA ELIMU NA HADI HALMASHAURI YA RUNGWE KUWA MSHINDI WA PILI KATI YA SHULE ZA MKOA WA MBEYA KWA MATOKEO YA DARASA LA SABA

EGN WA UJENZI RUNGWE AKIELEZA JINSI UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UJENZI UNAVOENDELEA WILAYANI RUNGWE

ENG, WA MAJI RUNGWE AKIONGEA NA MADIWANI JINSI MIRADI YA MAJI INAVYOENDELEA NA PIA MRADI ULIOSIMAMA, MRADI WA MAJI WA MASOKO AMBAPO HADI SASA MRADI UTAANZA UTEKELEZAJI WAKE KWA KUWA MKANDALASI MWINGINE AMEPATIKANA ILI KUUMALIZIA MRADI HUO NA VIJIJI KUMI NASITA KUANZA KUFAIDIKA NA MAJI

KATIKATI NI MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA RUNGWE MHE, MWAKASANGULA HAPO AMENUNA KIUKWELI AKIWA ANAONGEA NA WATENDAJI KUTEKELEZA KWA HARAKA MIRADI YA WANANCHI INAYOTEKELEZWA KATIKA JAMII KULIKO TABIA ILIYOANZA KUZOELEKA MIRADI YA MWAKA 2011 HADI SASA KUSUASUA KUITEKELEZA HIVYO KUFANYA BARAZA LA MADIWANI KUFIKIA AZIMIO LA IFIKAPO MWEZI WA SITA MIRADI YOTE ILIYOSIMAMA KUANZA KUTEKELEZWA ILI WANANCHI WAFAIDIKE NA MIRADI HIYO KULIKO KITU CHA AIBU KUONA PESA ZA WALIPA KODI ZIKO BENKI BILA YA KUFANYIWA KAZI

KATIKA KIKAO HIKI ALITAMBULISWA KWA MALA YA KWANZA DAS WA WILAYA YA RUNGWE NDUGU ALINANUSWE MWALUFUNA ANAYE HAMIA RUNGWE AKITOKEA WILAYA YA MAKETE HUKU MOSSES MWIDETE AKIHAMA WILAYANI RUNGWE NA KUPANGIWA MAJUKUMU MENGINE

WATENDAJI WA HALMASHAURI YA RUNGWE

...............................................................................................................................

BI KIDUDE AMEFARIKI DUNIA


1 5de2d
Msanii mkongwe na maalufu wa muziki wa  taarabu Fatma bint Baraka (Bikidude) amefariki Dunia leo mchana huku visiwani Zanzibar,habari zaidi zitawajia hivi punde. 

Bi Kidude 7a829
Mwanamuziki gwiji nchini Fatuma Binti Baraka "Bi Kidude" hatunaye tena. Taarifa toka kwa familia yake zinasema Bi Kidude aliekuwa akipatiwa matibabu katika hospitali ya Hindu Mandal amefariki leo. Bi Kidude atakumbukwa kama mwanamuziki mkongwe zaidi nchini ambaye alianza muziki akiwa na umri wa miaka 10 tu na aliwahi kupokea tuzo mbalimbali kutokana na mchango wake katika muziki wa mahadhi ya mwambao. Hakika sanaa nchini imepoteza moja ya nguzo kubwa.
Pumzika kwa amani Fatuma Binti Baraka.

 ................................................................................................................................

WATU watatu wamefariki dunia na wengine wawili wa familia moja kujeruhiwa baada Gari aina ya Scania kuvamia Nyumba yao wakiwa ndani jana Usiku. Ilongo wilayani Mbarali mkoani Mbeya

Gari aina ya scania yenye nambali za usajiri T578 ALS likiwa na tela nambli T125 AGM lililobomoa nyumba na kusababisha vifo vya watu 3 wa familia moja

Tunaomba radhi kwa kuonyesha picha hizi hii ni miili ya watu walifariki kwa gugongwa na roli hilo







Wananchi wa kijiji cha Ilongo wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya wakiwa msibani
WATU watatu wamefariki dunia na wengine wawili wa familia moja kujeruhiwa baada Gari aina ya Scania kuvamia Nyumba yao wakiwa ndani jana  Usiku. Ilongo wilayani Mbarali mkoani Mbeya
  
Tukio hilo lilitokea jana majira ya saa Tatu na Robo usiku katika Kijiji cha Ilongo Wilaya ya Mbarali Mkoani hapa.
Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, Barakael Masaki amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa ajali hiyo ilihusisha  magari kugongana na kugonga nyumba na kusababisha vifo na majeruhi.
Alisema chanzo cha ajali kilitokana na Gari lenye namba za usajili T578 ALS likiwa na tela lenye namba za usajili T125 AGM aina ya Scania likiendeshwa na dereva ambaye hakuweza kutambulika liligonga  kwa nyuma  gari lenye namba T959 ASC aina ya Scania.
  
Alisema gari hilo lilikuwa likiendeshwa na dereva Juhudi Saimon(34)Mnyiha mkazi wa Dar Es Salaam kisha gari hilo  kugonga nyumba mali ya Matia  Mwagala mkazi wa Kijiji cha Ilongo.
  
Aliwataja matrehemu kuwa ni Asia Yahaya (52)mkulima na Msangu, Abubakari Yahaya(8) Msangu na mwanafunzi darasa la pili  aliyekuwa anasoma katika Shule ya msingi Ilongo na Fatuma Yahaya (6) Msangu mwanafunzi wa darasa la kwanza  Shule ya Msingi Ilongo wote wakazi wa kijiji hicho.
Aidha aliwataja majeruhi wa ajali hiyo kuwa ni pamoja na Abuu  Fadhil (22)Mzigua mkazi wa Dar Es Salaam ambaye ni tingo wa gari lililogonga Nyumba pamoja na Steven  Chiwa (26) mbembe raia na mkazi wa Nchi jirani ya Zambia ambaye ni msindikizaji wa gari hilo ambao wamelazwa katika Hospitali ya Misheni ya Chimala.
  
Hata hivyo wa dereva wa gari lililosababisha ajali alikimbia na gari mara baada ya tukio ambapo Kaimu Kamanda  anatoa rai kwa yeyote mwenye taarifa juu ya mahali alipo dereva wa gari lililosababisha ajali hiyo azitoe katika mamlaka husika ili akamatwe na sheria ichukue mkondo wake, vinginevyo ajisalimishe mara moja.
  
Wakati huo huo  Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya linamshikilia  Asajile Mwamtina (46) mkazi wa kijiji cha Syukula Wilaya ya Rungwe mkoani hapa akituhumiwa kufanya mapenzi na binti yake wa miaka 13.
  
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa lilitokea juzi  majira ya saa Kumi na Mbili jioni baada ya kumvizia binti huyo (jina limehifadhiwa) ambaye aliacha shule akiwa darasa la tano mwaka 2011 kwa matatizo ya ugonjwa wa kifafa akiwa anapika.
  
Alisema mtuhumiwa alipata mwanya wa kufanya unyama huo kutokana na mkewe  ambaye  mama mzazi   wa mhanga huyo Tumikigwe Samalinga akiwa kijiji cha Kiwira kuuguza mgonjwa na kuongeza kuwa taratibu za kumfikisha mahakamani zinafanyika.
  
Aidha katika tukio lingine eneo la Makunguru Jijini Mbeya Vyumba 12 vya biasharaa viliteketea kwa moto jana majira ya saa Tano asubuhi vilivyokuwa vimetoka kujengwa  mali ya Dominick Mbinga Mkazi wa Dar Es Salaam.

Hata hivyo hakuna madhara ya kibinadamu yaliyojitokeza baada ya moto huo kudhibitiwa kwa ushirikiano baina ya kikosi cha zima moto na uokoaji na wananchi.
Thamani halisi ya uhalibifu bado kujulikana pamoja na chanzo ingawa kwa mujibu wa majirani walisema inawezekana ikawa ni hitilafu ya umeme kutokana na muda huo wapangaji wa nyumba hiyo kutokuwepo wakati moto ukitokea ambao ulijulikana baada ya majirani kuona.
.....................................................................................................................

DKT. MUKANGARA ATAJA WAJUMBE WA KAMATI YA USHINDI WA TAIFA STARS WATAJWA

FENELA
Kama mnavyofahamu, hivi sasa Timu ya Taifa ya mpira wa Miguu kwa Wanaume (Taifa Stars) ipo kwenye michuano ya kufuzu kushiriki Fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika nchini Brazil mwaka 2014.
Katika Afrika, Tanzania (Taifa Stars) imepangwa kundi C kati ya makundi 10. Kundi C linajumuisha timu za Ivory Coast, Morocco, Gambia na Tanzania.
 Kwa sasa katika kundi C, Taifa Stars inashika nafasi ya pili ikiwa na alama sita (6), nyuma ya Ivory Coast yenye alama saba (7), Morocco ina alama mbili (2) na Gambia ina alama moja(1).
 Kwa mara nyingine Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo inapenda kuwapongeza Taifa Stars, kwa kazi nzuri ambayo wameishaifanya ikiwemo ushindi wa Bao Tatu kwa Moja dhidi ya Morocco. Watanzania wote na Wadau wa Soka nchini wamefurahishwa sana na mafanikio yaliyofikiwa na Taifa Stars na yenye kutupa matumaini  katika kuitayarisha Taifa Stars kufuzu kucheza Fainali za Kombe la Dunia  kwa mwaka 2014 nchini Brazil.
 Kwa hali ilivyo hivi sasa, Taifa Stars ipo katika nafasi nzuri ya kufuzu. Ili Tanzania tuweze kufuzu, Taifa Stars inatakiwa ishinde mechi zote tatu (3) na kuongoza kundi C na baadae iingie katika Timu kumi (10) bora na kisha zipatikane Timu tano (5) kutoka Afrika ambazo zitakuwa zimefuzu kwenda Brazil katika Fainali za Kombe la Dunia kwa mwaka 2014.  Tunaamini hili linawezekana.
 Sasa kwa kuzingatia uzito wa jukumu lililo mbele yetu na kwa Taifa Stars kwa ujumla; Serikali imeunda Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars.
 Jukumu la msingi la Kamati tunayoiunda ni kuhakikisha Taifa Stars inawezeshwa na kuandaliwa ipasavyo ikiwa ni pamoja na kuunda kikundi cha kuishangilia timu ya Taifa ndani na nje ya nchi. Wajumbe wa Kamati ya Taifa Stars Stars itakayoongozwa na Mhe. Mohamed Dewji ni hawa wafuatao:-

1.   Mhe Mohamed Dewji           -       Mbunge
2.   Bi. Teddy Mapunda             -       Montage
3.   Dkt. Ramadhani Dau           -       Mkurugenzi Mtendaji NSSF
4.   Bw. Dioniz Malinzi               -       Mwenyekiti BMT
5.   Bw. Abji Shabir                  -       New Africa Hotel
6.   Bw. George Kavishe            -       TBL
7.   Mhe. Mohamed Raza           -       Zanzibar
8.   Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
9.   Bw. Joseph Kusaga             -       Clouds
10.   Mhe. Kapt. John Komba    -       Mbunge
11.   Mhe. Zitto Kabwe             -       Mbunge
 Kamati hii iliyoteuliwa leo, naomba ianze kazi mara moja.  Hadidu za rejea zitakazowaongoza kutekeleza majukumu yao chini ya Kamati hii watazipata kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. Kamati itashirikisha wadau mbalimbali kadri itakavyoona inafaa.
 Serikali inaahidi kutoa ushirikiano utakaohitajika katika kuhakikisha Kamati hii inafanya kazi vizuri ili kuiwezesha Taifa Stars kushinda Mechi zote zilizombele yetu.
 Aidha nichukue fursa hii kutoa wito kwa Watanzania wote, kuiunga mkono Taifa Stars na Kamati ya Ushindi ya Taifa Stars kwa hali na mali katika kuhakikisha timu yetu inafuzu kucheza Fainali za Kombe la Dunia.
 Kwa niaba ya Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri Mkuu naomba niwasilishe salaam zao za kuwapongeza Vijana wetu wa Taifa Stars, pamoja na benchi la ufundi likiongozwa na Kocha Mkuu Kim Poulsen. Kwa pamoja wanaomba Taifa Stars iendelee kujipanga kwa mechi zijazo.  Nawahakikishia kuwa Serikali, Watanzania na wadau wa Soka nchini wapo nyuma yao.
 Mungu Ibariki Taifa Stars. Mungu Ibariki Tanzania.
Dkt. Fenella Mukangara (Mb)
WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
 16 Aprili, 2013
 ...................................................................................................................................

No comments: