Friday, April 26, 2013

MAADHIMISHO YA MUUNGANO WA TANZANIA MKOA WA MBEYA YAMEFANYIKA WILAYANI RUNGWE YAFANA PAMOJA NA KUNYESHA MVUA NA HARI YA UBARIDI NA UKUNGU ULIOTAWARA MJI WA TUKUYU

MAANDAMANO YA WANANCHI ,WAFANYAKAZI NA WANAFUNZI YALIANZIA KATIKA OFISI ZA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUNGWE NA KUELEKEA KATIKA VIWANJA VYA STANDI KUU YA MABASI TUKUYU MJINI

KWA MUONEKANO HUU HII NDIO RUNGWE YA KIPINDI HIKI CHA MVUA ,BARIDI NA UKUNGU


MAANDAMANO


WIMBO WA TAIFA UKAIMBWA

PAMOJA NA HARI YA HEWA KUWA MBAYA HASA BARIDI KALI ,UKUNGU NA MVUA LAKINI WANANCHI WA TUKUYU WALIVUMILIA




KATIKATI RAS WA MKOA WA MBEYA AKISALIMIANA NA WATANZANIA WALIOJITOKEZA KATIKA SHEREHE ZA MUUNGANO WILAYANI RUNGWE

UMAKINI NA UZALENDO WA WATANZANIA  WAKATI WA KUIMBA WIMBO WA TAIFA LETU LA TANZANIA

UMAKINI NA UZALENDO WA WATANZANIA  WAKATI WA KUIMBA WIMBO WA TAIFA LETU LA TANZANIA

MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA AKITOA TAARIFA YA WILAYA KWA KIFUPI MBELE YA MKUU WA MKOA MBAYE NDIYE MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO HAYA YA MUUNGANO WILAYANI RUNGWE

WANANCHI PAMOJA NA WANAFUNZI WAKIWA MAKINI KUSIKILIZA KWA MAKINI

MKUU WA MKOA WA MBEYA  ABAS KANDOLO AKIONGEA NA WANANCHI WA RUNGWE KATIKA MAADHIMISHO YA MUUNGANO WA TANZANIA YALIYOFANYIKA WILAYA YA RUNGWE KATIKA MJI MDOGO WA TUKUYU MAADHIMISHO HAYA YAKIFANYIKA KIMKOA

PIA MKUU WA MKOA WA MBEYA AMEKEMEA TABIA ILIYOANZA KUJITOKEZA KWA WATANZANIA BAADHI YA KUBAGUANA KWA UDINI HIVYO AMEWATAKA WATANZANIA KILA MTU AMVUMILIE MWENZAKE NA DINI YAKE PIA AMESEMA MUUNGANO SASA NI MIAKA 39 UMEDUMU KWA KUWA WATANZANIA WAMEDUMISHA AMANI LAKINI AMANI IKICHEZEWA KILA KITU KITAVUNJIKA

WAENDESHA PIKIPIKI WAKIPITA MBELE YA MGENI RASM NA KUMSINDIKIZA KUONDOKA UWANJANI HAPO KUELEKEA OFISI YA MKUU WA WILAYA BAADA YA KUMALIZA MAADHIMISHO YA MUUNGANO KATIKA VIWANJA VYA STAND TUKUYU

MKUU WA MKOA AKIONDOKA OFINI KWA MKUU WA WILAYA YA RUNGWE
 .................................................................................................................................................................
 SHEREHE YA MUUNGANO KITAIFA

RAIS DK. JAKAYA KIKWETE AWAONGOZA WATANZANIA MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA MUUNGANO UWANJA WA UHURU LEO


Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya ulinzi na usalama lililoandaliwa maalum kwa ajili maadhimisho ya miaka 49 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika kwenye uwanja wa Uhuru leo jijini Dar es salaam  na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Vyama vya Siasa na Mabalozi pamoja na wageni waalikwa mbalimbali ili kushuhudia maadhimisho hayo. 2 
Rais Dk. Jakaya Kikwete akikagua kikosi cha Jeshi la Magereza wanawake wakati wa maadhimisho hayo 3 
Rais Dk. Jakaya Kikwete akielekea jukwaani mara baada ya kukagua gwaride la vikosi vya ulinzi na usalama katika maadhimisho hayo 4 
Rais Dk. Jakaya Kikwete akiwa jukwaani pamoja na viongozi wengine kutoka kulia ni Rais Mstaafu Benjamin Wiliam Mkapa, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Gharib Bilal, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange na Kutoka kulia ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Rais Wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein. 5 
Rais Wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kulia akiwa na viongozi wengine katika jukwaa kuu kutoka kushoto ni Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, Makamu wa pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Idd, Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda. 6 
Wageni waalikwa mbalimbali wakiwa katika maadhimisho hayo. 7 
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akiingia uwanjani katika gari maalum huku akisindikizwa na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange. 8 
Msafara wa Rais ukiingia uwanjani leo 10 
Kikosi cha Jeshi la  Ulinzi JWTZ kikipita na kutoa heshima  mbele . 11 
 JKT kikitoa heshima kwa Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Kikwete. 13 
Kikosi Maalum Cha Bendera kikitoa heshima zake bele ya Rais Jakaya Kikwete 14 
Kikso cha Askari wa Magereza kikipita na kutoa heshima mbele ya Rais Jakaya Kikwete 16 
Watoto wa halaiki wakionyesha ujumbe mbalimbali kuhusu Muungano wetu mbele ya Rais Jakaya Kikwete na maelfu ya Watanzania waliohudhuria katika maadhimisho hayo 17 


..................................................................................................................................................................
 MAHAFARI YA 36 YA STASHAHADA YA UALIMU CHUO CHA UALIMU TUKUYU YAFANA HUKU KATI WAHITIMU 491 MWANAFUNZI MMOJA TU NDIYE ALIYE SOMEA MASOMO YA SAYANSI YA KEMIA NA FIZIKIA HUKU WANNE WAKIOSOMEA HESABU NA FIZIKIA
MAZINGIRA YA CHUO CHA UALIMU TUKUYU



WALIMU TARAJALI MWAKA 2013



WAKUFUNZI WA CHUO CHA UALIMU TUKUYU KILICHOPO MSASANI TUKUYU MJINI

MKUU WA CHUO CHA UALIMU TUKUYU MATHIAS MVULA AKISOMA TAARIFA FUPI YA CHUO HUKU AKIWATAKA WANANCHUO KUWA MABAROZI WAZURI KATIKA JAMII ILI JAMII ITAMBUE CHUO CHA MSASANI KINA ZALISHA WAHITIMU WALIO WAADIRIFU NA WAPENDA AMANI KATIKA JAMII

MWENYEKITI WA BODI YA USHAURI YA CHUO MR MOSES MWIDETE AKIONGEA MACHACHE KWA WAHITIMU, AMEWATAKA WAHITIMU SASA WANANZA KUJITEGEMEA CHAMSINGI WAJUE KUJIHESHIMU NA WAEPUKANE NA NGONO ZEMBE AMBAZO ZINAPELEKEA KUPATA UGONJWA WA UKIMWI AMBAO HAUNA TIBA WALA KINGA HADI SASA

ISHANTI SHAPWATWA AKISOMA RISALA KWA NIABA YA WAHITIMU KATI YA MAMBO ALIYASEMA NI KUWASHUKURU UONGOZI WA CHUO NA WANANJAMII KUWALEA VYEMA CHUONI HAPO TANGU WAANZE MASOMO AMBAYO MPAKA KUMALIZA HAKUNA MWANANCHUO ALIYE FUNKUZWA CHUO KWA UTOVU WA NIDHAMU JAPO MWANAFUNZI MMOJA GETRUDE KAYOMBO ALIYE FARIKI DUNIA
KUSHOTO MKUU WA CHUO CHA UALIMU MPUGUSO KILICHOPO TUKUYU MJINI

MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA AKIONGEA NA WAHITIMU NA JUMUIA YA CHUO PAMOJA NA WAZAZI WALIOHUDHURIA. MKUU WA WILAYA AMESEMA KUWA MWALIMU NI KIUNGO MUHIMU KATIKA JAMII KWAKUWA MWALIMU ANATEGEMEWA KWA KUWA NA MAWAZO MAZURI NA YENYE SURUHISHO YA MIJADARA YA KIJAMII, HIVYO AMEWATAKA WAHITIMU KWENDA VIJIJINI KUFUNDISHA WANAFUNZI MAANA NDIO TAARUMA YAO ILI KUONGEZA HARI YA UFAURU KWA WANAFUNZI. ZAIDI AMESEMA WAHITIMU KUMBUKENI KUJIENDELEZA KIELIMU KWAKUWA HAPO SIO MWISHO WA ELIMU

MRATIBU TAARUMA WA CHUO CHA TUKUYU FRANK MBUNDA AKISOMA MAJINA YA WAHITIMU NA KUPITA KUCHUKUA VYETI HUKU KUSHOTO MAKAMU WA CHUO STEPHANO KILALE AKIWA MAKINI KUSIKILIZA KINACHOENDELEA

MC WA MAHAFARI YA 36 YA CHUO CHA UALIMU AMBAYE PIA NI MKUFUNZI MWL SANGU

HONGERENI  SANA


KITU KLICHOSHANGAZA NA KUSONONESHA NI KUONA KATI YA WAHOTIMU 491 NI MWANAFUNZI MMOJA TU AMBAYE AMEHITIMU KWA KUSOMEA MASOMO YA YA SAYANSI YA HESABU NA FISIKIA NA HUYU NDIYE MWL MICHAEL SAMBO. HAPA KILA MTU ANAJUKUMU LA KUJIFUNZA KITU WADAU NA SERIKALI SASA NI KUJIPANGA KATIKA HILI MAANA WASOMI WANAOSOMEA SAYANSI HAWAKIDHI HIVYO TANZANIA ITAKOSA WANASAYANSI WA KULISAIDIA TAIFA LETU LA TANZANIA

NA HAO WANNE TU WALIO SIMAMA NI KATI YA WAHITIMU 492 NDIO WALIOHITIMU MASOMO YA SAYANSI YA HESABU NA FIZIKIA

KATI YA WAKUFUNZI WALIOPO CHUONI HAPO MKUFUNZI WALAONZIKU ALITUNUKIWA KUWA MFANYAKAZI BORA NA MCHAPA KAZI MAHIRI

HAPA NI KUPONGEZANA

HII NI MAHAFARI YA 36 TANGU CHUO CHA UALIMU KIANZISHWE MWAKA 1979NA KUPITIA KATIKA HATUA MBALIMBALI NA SASA CHUO KINATOA STASHAHADA YA UALIMU
 ................................................................................................................................................................

WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana waliumbuana na kushutumiana wazi mbele ya Waziri Mkuu,
 Wabunge wa CCM wavuana nguo
 Banner
 WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jana waliumbuana na kushutumiana wazi mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Hatua hiyo ilifikiwa katika kikao chao katika ukumbi wa Msekwa mjini hapa ambako waliumbuana na kushutumiana waziwazi. Kikao hicho kilichoongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kilifanyika baada Spika wa Bunge, Anne Makinda kuahirisha mjadala wa makadirio ya mtumizi ya fedha ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa fedha 2013/14.

Spika aliahirisha mjadala wa makadirio hiyo uliokuwa uhitimishwe jana, baada ya wabunge wengi kuonyesha nia ya kuyakwamisha kutokana na kutoridhishwa na jitihada za Serikali za kukabiliana na kero ya maji nchini.

Chanzo chetu kilichokuwa katika kikao hicho kilisema mjadala ulipoanza, Pinda aliizungumzia kwa kifupi Wizara ya Maji na kuonyesha jinsi Serikali ilivyokubali kwa dhati kurekebisha makadirio ya matumizi ya fedha ya wizara hiyo.

Baada ya hoja hiyo, chanzo hicho kilisema Waziri Mkuu aliwasilisha hoja nyingine iliyowataka wabunge wa CCM kuchangia posho zao za siku moja kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa madiwani unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

“Hoja hiyo ilipopita, Nyoka wa Shaba (Kangi Lugora, Mbunge wa Mwibara), alisimama na kuhoji ni kwa nini chama kimekubali kusaidia uchaguzi wa madiwani wakati huwa hakisaidii kesi za uchaguzi za wabunge.

“Si unajua Nyoka wa Shaba naye ana kesi mahakamani, sasa ndiyo maana akaamua kuhoji iweje yeye hasaidiwi na chama wakati huo huo anaambiwa asaidie uchaguzi wa madiwani.

“Alipomaliza kusema hivyo, akasimama Mbunge wa Sikonge, Said Nkumba. Aliposimama aliwashutumu moja kwa moja Lugora na Filikunjombe (Deo, Mbunge wa Ludewa).

“Akasema wabunge hao badala ya kuisaidia Serikali wanapokuwa bungeni, wao wamekuwa wakiishambulia jambo ambalo halileti picha nzuri kwa wananchi.

“Akasema kitendo cha Filikunjombe kusema bungeni kwamba Serikali ina miwani ya mbao hakikuwa kizuri… akasema ‘hawa wenzetu hatuko nao na kwa kuwa mwezi ujao tutaonana na Mwenyekiti wa Chama (Rais Jakaya Kikwete) nitasema mengi’.

“Alipomaliza kusema hayo akasimama Kibajaji (Livingstone Lusinde, Mbunge wa Mtera). Kibajaji akaungana na Nkumba, akawashambulia Lugora na Filikunjombe kwamba wanaiua Serikali kutokana na maneno yao bungeni.

“Akasema kama Lugora ana kesi mahakamani ni bora akakabiliana nayo mwenyewe kwa sababu inaonekana hayuko pamoja na chama,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:

“Baadaye alisimama Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima ambaye alimshutumu Lugora kwamba kitendo chake cha kuliambia Bunge kuwa kuna baadhi ya mawaziri wanajihusisha na dawa za kulevya, kinawaweka njia panda wananchi kwa kuwa wanahisi wabunge wao ambao ni mawaziri, nao wamo kwenye orodha hiyo ikizingatiwa kuwa hakuwataja majina.

“Pia, akahoji kama wabunge wana kero zao ni kwa nini wasiwafuate mawaziri na kuzungumza nao badala ya kuwasema bungeni.

“Kisha, alisimama Mangungu (Mbunge wa Kilwa Kaskazini) ambaye alionyesha wasiwasi juu ya majaji wanaosikiliza kesi za uchaguzi.

“Yeye akasema kesi nyingi za uchaguzi ambazo CCM inashindwa ni kwa sababu majaji wengi wanaichukia CCM na wanaipenda Chadema.

“Baadaye aliungwa mkono na Dk. Chami (Dk. Cyril Chami, Mbunge wa Moshi Vijijini) ambaye alidiriki kumtaja jaji mmoja kwa jina kwamba ana upendeleo wa wazi wazi kwa Chadema.

“Kisha, alisimama Mbunge wa Karagwe (Gosbert Blandes) na akatoa ushauri kwamba kuna haja chama kusaidia majimbo ya uchaguzi na wakati huo huo, viongozi wakuu wa chama waende kwa wananchi kama wanavyofanya viongozi wa Chadema.”

Mbali na hao, chanzo hicho kilimtaja Waziri wa TAMISEMI, Hawa Ghasia kwamba alimshutumu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi kwamba hakusaidia wakati wa vurugu zilizotokea hivi karibuni mjini Mtwara.

“Ghasia alianza kwa kusema kwamba, siku hizi Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, anafanya ziara za mara kwa mara jimboni kwake Mtwara Vijijini lakini CCM haijali.

“Pia akamlalamikia Waziri Nchimbi kwamba wakati wa vurugu za wananchi mkoani Mtwara alimpigia simu lakini hakupokea na hata alipomtumia ujumbe mfupi wa simu hakumjibu.

“Akahoji pia kwamba iweje wakati wa vurugu zote Mtwara, nyumba zinazochomwa ni za wabunge wa CCM wanawake na nyumba za wabunge wanaume hazichomwi, akahoji kuna kitu gani hapo,” kilisema chanzo hicho.
................................................................................................................................................................

KIPANYA LEO


kp25042013 5ee26


No comments: