Sunday, May 19, 2013

MASAA 6 YA MAPAMANO KATI YA MACHINGA NA POLISI IRINGA YAMWEKA PABAYA MBUNGE MSIGWA SASA KUFIKISHWA MAHAKAMANI KESHO ......


Mbunge mchungaji  Peter Msigwa
Polisi  waliotoka  kumkamata  mbunge Msigwa  leo

2 f9988

3 fd59e

5 d26e3
POLISI YATUMIA NGUVU KUTAWANYA WANANCHI MTAA WA MASHINE TATU, WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO MAARUFU KWA JINA LA MACHINGA WAKIWA NA MBUNGE WAO,


  Francis Godwin, Iringa
MASAA  zaidi ya 6 ya mapambano kupiga  mabomu ya machozi na kurushiana  mawe kati ya wafanyabiashara  ndogo  ndogo (machinga ) na  askari  wa  kikosi cha  kutuliza  ghasia (FFU) mkoani Iringa  yaishia pabaya  kwa  jeshi la  polisi kumkamata  mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa  (chadema) na  watu  wengine zaidi ya 60
Polisi  watumia  mabom ya machozi  kutawanya machinga  wapiga mabomu hadi stendi kuu ya mabasi  abiria  walazimika  kutimua  mbinu na kuacha mizigo  yao katika magari   huku machinga  hao wakitumia mawe  na kuchoma mataili  moto barabarani  kuvunja vioo vya gari  la Zimamoto na kuharibu mali mbali mbali kama  njia ya  kupambana na  polisi
Tukio hilo la Mapambano  kati ya machinga na polisi lilitokea leo  kuanzia  muda wa saa 3  asubuhi  na kuendelea  hadi saa 8 mchana katika  eneo la Mashine  tatu  mjini  Iringa na maeneo mbali mbali ya mji  wa Iringa .

Askari  huo  walilazimika  kukesha wakilinda eneo hilo  kufuatia  kauli ya  mbunge  Msigwa aliyoendelea  kuitoa katika  mikutano yake ya hadhara  mjini hapa  kuwhamasisha  machinga  hao ambao  Halmashauri ya Manispa ya  Iringa  iliwahamisha  eneo hilo la mashine tatu  na kuwapeleka  eneo la Mlandege kabla ya  mbunge Msigwa kuwahamasisha  kurejea  tena  eneo hilo.
Kabla ya  mbunge Msigwa  kufika  eneo hilo majira ya  saa 3 asubuhi machinga  hao ambao  walikuwa  wamejikusanya makundi madogo madogo   bila  kupanga  biadhaa zao  walisikika  wakidai  kumsubiri  mbunge Msigwa kama alivyopata  kuwaahidi  kuwa atafika  eneo hilo kuungana nao kwa  kuwa machinga  mpya  .
Hata  hivyo baada  ya mbunge  huyo kufika akiwa na gari lake  la kibunge  ambalo lilikuwa lilikokota tela  la  kuhifadhia mizigo  alisimama  eneo hilo na  kuendeleza msimamo  wake  wa kuwataka machinga  kupambana na baada ya  muda alitoweka  eneo hilo kabla ya  polisi  kuanza  kuwatawanya  machinga hao kwa mabomu ya machozi .
Wakizungumzia  hali hiyo  ambayo ni ya  kwanza kutokea katika  mji  wa Iringa wakazi  wa mji  wa Iringa  walisema  kuwa mbunge  na  viongozi  wengine  wa  serikali  wanapaswa  kulaumiwa kwa  kushindwa  kutumia njia nzuri ya  kukutana  kwa ajili ya kumaliza  mvutano huo  ambao unaendeshwa  kisiasa  zaidi.
Festo Sanga  alisema  kuwa  hali  ilipofikia  ni mbaya zaidi na  hivyo  busara  zinahitajika kwa ajili ya  kutatua  tatizo  hilo  ikiwa ni pamoja na kutazama  eneo zuri kwa ajili ya machinga  bila  kuendelea  kuonyeshana  ubabe .
Sanga  alisema  kuwa machafuko  yaliyojitokeza leo   ni machafuko ambayo wakazi  wa mji  wa Iringa  walikuwa  wakishuhudia katika  vyombo  vya habari  katika  mikoa  mingine  ukiacha  lile la Septemba 2 mwaka  jana lililotokea  kijiji  cha Nyololo kati ya  wafuasi  wa Chadema na polisi na kupelekea kifo cha aliyekuwa mwenyekiti  wa klabu  ya  waandishi  wa habari mkoa  wa Iringa marehemu Daud Mwangosi.
“Kweli katika hili  mbunge wetu hapaswi kuendelea  kulazimisha machinga  kuvunja  sheria  ila anayo nafasi ya  kukutana na viongozi  wenzake  ili  kutafuta  suluhu  ya jambo  hilo vinginevyo wanaoteseka  na machinga na  wale  waliokamatwa kwa  vurugu hizo  ujue  wengi  waliopigwa mabomu ya machozi si machinga  wengine  walikuwa  wasafiri na badhi yao  walikuwa  wakielekea makanisani ”
KUhusu  kukamatwa kwa mbunge  huyo na kuhojiwa na  polisi  juu ya vurugu  hizo Sanga  alisema kwa upande  wake analipongeza  jeshi la  polisi kwa  kutumia busara  zaidi  ya  kumkamata  mbunge   kama mhusika mkuu  na  kuliomba  jeshi la  polisi kuwaachia  wananchi  waliokamatwa  kwa  vurugu  hizo.
Huku  Sarah Kalinga  alidai  kuwa  chanazo cha machafuko hayo ni mvutano kati ya  CCM na Chadema na  kuwa  ilipaswa  vyama vyote  viwili  kukutana na  kuwasaidia  machinga  badala ya  kuwanyanyasa  kwa  kutumia nguvu  kuwabana .
Hata   hivyo  alisema wao kama walalahoi wanampongeza  mbunge wao kwa kuonyesha kuwapigania japo haungi mkono njia  inayotumiwa na mbunge ya  kuwahamasisha   kuvunja  sheria na kuwa  matatizo na majeraha  wanapata  wao  wananchi  na sio mbunge.
Awali  mbunge mchungaji Msigwa  kabla ya  kukamatawa na  jeshi la  polisi alitoweka katika mazingira  tata katika  eneo hilo la mashine  tatu na  kuibukia eneo la chuo  kikuu cha Tumaini Iringa ambako kulikuwa na harambee  ya  kuchangia Kanisa na mgeni  rasmi akiwa  waziri mkuu mstafu Frederick Sumaye na mara  baada ya  shughuli  hiyo  kumalizika ndipo alipokamatwa na polisi na kufikishwa  kituo cha  polisi.
Kabla ya  kukamatwa  kwake mbunge Msigwa alizungumza na mwandishi  wa habari hizi na kuwa  yupo tayari kukamatwa  wakati  wowote na  kuwa kamwe  ataendelea  na msimamo  wake  wa  kuwataka Machinga  kufanya  biashara  eneo hilo.
Mbali ya  kukamatwa  kwa  mbunge  Msigwa  kwa  kuhusishwa na vurugu  hizo pia  jeshi la  polisi  mkoani Iringa  linawashikilia  watu  wengine  zaidi ya 60 akiwemo  aliyekuwa kampeni meneja  wa Chadema  jimbo la Iringa mjini na mgombea  udiwani  kata ya  kwa Kilosa  Abuu Changawa Majeck.
Huku  idadi ya majeruhi  waliojeruhiwa kwa  kupigwa mawe na machinga na  badhi ya machinga  waliokamatwa kwa  vurugu  hizo pia wakijeruhiwa  vibaya  wakati  wakipambana na  polisi hao.
Taarifa  kutoka  jeshi  la polisi zilizothibitishwa na kamanda  wa polisi mkoa  wa Iringa Michael Kamuhanda  zinadai  kuwa  watu  zaidi ya 60 ndio  wamekamatwa  hadi  sasa na  jitihada za  kuwasaka wengine  waliohusika katika  vurugu  hizo ambazo zimesababisha uharibifu mkubwa wa mali  za  wananchi unaendelea.
Huku akidai  mali  mbali mbali  zimeharibiwa likiwemo gari  hilo la zimamoto mjini Iringa pamoja na uharibifu  mwingine  mdogo  mdogo  wa mali za  wananchi .
Jeshi  hilo la polisi  limesema kamwe halipo tayari  kumwachia mbunge Msigwa kwa leo hadi hapo atakapofikishwa mahakamani Kesho 
.................................................................................................................

Rais Kikwete afungua na kuongoza semina ya Wabunge wa CCM Dodoma

Mwenyekiti Wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifungua semina maalum ya wabunge wa CCM ilkiyofanyika katika ukumbi wa White House mjini Dodoma leo.Wengine katika picha kutoka kushoto ni Spika wa bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM Jenista Mhagama, Waziri mkuu Mizengo Pinda,Makamu wa CCM Bara Ndugu Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana(picha na Freddy Maro)8E9U6446 
Baadhi ya wabunge wa CCM waliohudhuria semina maalum iliyofanyika katika ukumbi wa White House mjini Dodoma leo.
..............................................................................................................................

UMOJA wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM) na Umoja wa Wanawake (UWT) wa Chama hicho Mkoa wa Mbeya wametoa matamko makali kupinga kauli zilizotolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Dk. Wilbroad Slaa pamoja na Mkewe juu ya Raisi Kikwete.

Mwenyekiti wa Uwt  Mkoa wa Mbeya Prisila Mbwaga alisema kama Wanawake wa Chama cha Mapinduzi hawako tayari kuona matusi yanayotolewa na Mke wa Dk Slaa Josephine Shumbusho juu ya Mama Salma Kikwete kwamba anachangia kuibomoa Nchi.
 Mwenyekiti wa Uvccm Mkoa wa Mbeya Amani Kajuna alisema Umoja wa Vijana hauko tayari kufumbia macho matusi anayotukanwa Raisi Kikwete  na Dk Slaa anapokuwa akihutubia wanachama wake jukwaani.

UMOJA wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi(UVCCM) na Umoja wa Wanawake (UWT) wa Chama hicho Mkoa wa Mbeya wametoa matamko makali kupinga kauli zilizotolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Dk. Wilbroad Slaa pamoja na Mkewe juu ya Raisi Kikwete.
Matamko hayo yalitolewa  na Wenyeviti hao katika Mkutano na Vyombo vya habari uliofanyika katika Ofisi za UVCCM Mkoa wa Mbeya, ambapo walisema kamwe hawawezi kufumbia macho maneno ya uzushi na uchonganishi kati ya Serikali na wananchi.
  
Akisoma tamko Mwenyekiti wa Uvccm Mkoa wa Mbeya Amani Kajuna alisema Umoja wa Vijana hauko tayari kufumbia macho matusi anayotukanwa Raisi Kikwete  na Dk Slaa anapokuwa akihutubia wanachama wake jukwaani.
Alisema katika Mkutano alioufanya Mei 12, Mwaka huu Wilayani Mbozi Mkoa wa Mbeya Dk. Slaa akihutubia wananchi kuwa Raisi Kikwete ni Freemason,  Mdini, Mawaziri hawamsaidii pia ni Mafisadi na kuongeza kuwa ana ushahidi wa  Cd ambazo Raisi Kikwete akihamasisha udini na kuhusu uchinjaji.
Alisema maneno ya Dk. Slaa ni uzushi ambao unalengo la kufitinisha Watanzania na Serikali ya Chama cha Mapinduzi hususani anapofanya mikutano ya Hadhara katika Mkoa wa Mbeya ambapo aliongeza kuwa Ufisadi anaousema yeye kwa Mawaziri wa Ccm ili hali yeye mwenyewe anaongoza kwa ubadhilifu wa fedha za Wananchi.
Alitolea mfano wa ubadhilifu uliofanywa na Chadema mkoani Mbeya kuwa ni pamoja na Kitendo chaMwenyekiti wao Freemani Mbowe kuchangisha fedha Milioni Tatu kwa wananchi kwa kile alichodai zingetumika kununulia maji na matibabu wakati wa maandamano lakini hazikufanya kazi hiyo na hazijulikani zilipo.
Kajuna alisema mbali na fedha hizo kutokujulikana matumizi yake  pia Dk. Slaa alichangisha fedha zingine Shilingi Laki saba kwa ajili ya posho ya Wabunge waliofukuzwa bungeni jambo ambalo lilileta sintofahamu kwa wakazi wa Jiji la Mbeya.
Alisema ufisadi mkubwa uliopo ndani ya Chadema ambao kila Mwezi wanapata ruzuku ya takribani Milion mia Tatu lakini hawajawahi kujenga hata chumba kimoja cha Zahanati wala kutoa msaada kwa wananchi wasiojiweza lakini wao wanazidi kuwachangisha wananchi.
“ Jamani watanzania fungukeni muone huyu kiongozi wa namna gani Mlafi, Mchoyo na mchochezi  asiyependa kuona amani ya Nchi ikistawi” alisema Kajuna.
Aliongeza kuwa pamoja na Chadema kupata fedha zote hizo bado zinaishia mikononi mwa watu wachache hususani Dar Es Salaam ambapo Mikoani hawazipati na ndiyo sababu Ofisi za Chadema Mkoa wa Mbeya zilifungwa kutokana na kutolipia pango la Nyumba deni la Shilingi Laki tatu.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Uwt Prisila Mbwaga alisema kama Wanawake wa Chama cha Mapinduzi hawako tayari kuona matusi yanayotolewa na Mke wa Dk Slaa Josephine Shumbusho juu ya Mama Salma Kikwete kwamba anachangia kuibomoa Nchi.
Alisema Shumbusho alinukuliwa akitoa matusi makubwa dhidi ya Mama Salma katika mkutano wa hadhara uliofanyika Wilayani Mbozi akisema ameshindwa kumshauri raisi kuhusu uongozi na namna ya kuongoza nchi.
Aliongeza kuwa katika matusi yake alimtuhumu Mke wa Raisi kuwa ni Mwanamke Mpumbavu anayeibomoa nchi nyumba yake kwa mikono yake Mwenyewe kama Biblia inavyosema na kwamba yeye atakuwa tayari kumshauri Dk. Slaa atakapokuwa Raisi mwaka 2015.
Kutokana na tuhuma hizo Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Mbeya wamemtaka Mke wa Dk. Slaa kuacha tabia ya kumsema vibaya Mama Salma na akiendelea hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Picha na Mbeya yetu

No comments: