Monday, May 20, 2013

WILAYA YA RUNGWE WAPATA KIONGOZI MCHAPA KAZI CHRISPIN MEELA ANAYEWEZA KUSIKILIZA CHANGAMOTO ZA WANANCHI NA KUZIFANYIA KAZI

KULIA NI MKUU WA WILAYA YA RUNGWE LEO JIONI TUKIONGEA MENGI ZAIDI NI CHANGAMOTO ZA WANANCHI NA JINSI YA KUKABIRIANA NAZO LAKINI LILILOKUWA KUBWA LEO NI JINSI YA KUWAKUSANYA WAMACHINGA NA KUFANYA BIASHARA PAMOJA ILI KUWAWEZESHA KUPATA FURSA MBALIMBALI HASA ZA MIKOPO

HAPA TULIPOSIMAMA NI UWANJA WA ZAMANI WA MPIRA WA MIGUU WA TUKUYU AMBAO SASA HALMASHAURI YA RUNGWE KUPITIA KIKAO CHAKE CHA MADIWANI IMEBADILISHA MATUMIZI YA UWANJA HUO NA KUWA STAND YA DALADALA NA MAEGESHO YA MAGARI HUKU SEHEM IKIWA NI SEHEMU YA WAFANYA BIASHARA WADOGO WAMACHINGA AMBAPO KUANZIA TAREHE 22.05.2013 MATUMIZI MAPYA YA UWANJA HUU YATAANZA KUTUMIKA

HAPO KUANZIA KULIA NI MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA, ALLY KINGO, MZEE MWAKAPALA KATIBU TARAFA NA ALIYE VAA SHAT JEUSI NI MR MASANJA AMBAYE NI AFISA UTUMISHI WA HALMASHAURI YA BUSOKELO

WILAYA YA RUNGWE WAPATA GARI MPYA KWA AJILI YA OFISI YA DC ILI KUWAHUDUMIA WANANCHI KWA HARAKA NA UFANISI

WANANDOA ENG, UWEZO MWALWEGA NA DR MAGRETH SHIRIMA WAPOKELEWA KWA SHANGWE MBEYA NA KUFANYA IBADA YA SHUKRANI KKKT USHARIKA WA RUANDA MBEYA

MUNGU NA AWABARIKI SANA KATIKA SAFARI YA NDOA YENU MAANA NDOA NI PARADISO NA TAMBALALE

MCH MWASANGUTI  WA USHARIKA WA RUANDA MBEYA AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WANANDOA BAADA YA IBADA YA SHUKRANI YA PEKEE


DADA NA SHEMEJI SALASALA WAKIWA NA MAMA WENYE NYUSO ZA FURAHA
PICHA YA PAMOJA BAADHI YA WANAFAMILIA YA MCH MWALWEGA
HONGERA SANA MR & MRS UWEZO MWALWEGA
KAMATI NDOGO YA MAPOKEZI YA MAHARUSI  ENG, UWEZO NA DR MAGRETH ILIYOANDAA IBADA YA SHUKRANI YA PEKEE  KWA FAMILIA YA MCH MWALWEGA KUMSHUKURU MUNGU KIJANA WAO WA MWISHO KUFUNGA PINGU ZA MAISHA KATIKA KANISA LA KKT MBEZI BEACH DSM

  ..............................................................................................................................

MAKAMANDA wa polisi wa Mikoa ya Kikanda, wamekutana Jijini Mbeya, kujadili hali ya uhalifu ikiwa na kuweka mikakati itakayosaidia kuwabana askari watakaobainika kukiuka sheria na taratibu za kazi.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa mbeya, Ndugu Diwani Athumani ambaye ni mwenyeji wa Mkutano huo , amesema kikao hicho kinatarajia kutoka na mikakati itakayosaidi kupunguza wimbi la uhalifu pamoja na ajali barabarani.
Mwenyekiti wa Mkutano  Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Morogoro, Ndugu Faustine Shilogile amesema katika kikao hicho agenda kuu itakuwa ni kujadili matukio ya uhalifu wa unyang’anyi wa kutumia silaha, matukio ya ajali pamoja na kujadili nidhamu kwa watendaji wa jeshi hilo.
Baadhi ya maafisa wa jeshi hila la Polisi wakiwa makini kusikiliza mwenyekiti wao katika kikao hicho
Baadhi ya makamanda wa polisi wakiwa maetulia kwa umakini kumsikiliza mwenyekiti wa kikao hicho
Picha ya pamoja


MAKAMANDA wa polisi wa Mikoa ya Kikanda, wamekutana leo Jijini Mbeya, kujadili hali ya uhalifu  ikiwa na kuweka mikakati itakayosaidia kuwabana askari watakaobainika kukiuka sheria na taratibu za kazi.
Mkutano  huo unafanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, lengo kuu likiwa ni kujadili hali ya usalama na uhalifu wa maeneo katika  Mikoa ya Morogoro, Iringa, Ruvuma, Njombe na Mbeya  .
Akizungumzia mikakati hiyo, Mwenyekiti wa Mkutano  Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Morogoro, Ndugu Faustine Shilogile alisema katika kikao hicho agenda kuu itakuwa ni kujadili matukio ya uhalifu wa unyang’anyi wa kutumia silaha, matukio ya ajali pamoja na kujadili nidhamu kwa watendaji wa jeshi hilo.
Amesema Wahalifu wamekuwa na tabia ya kuhama hama mara wanapofanya tukio, hawakai sehemu moja hivyo mkutano huu utasaidia kwa wajumbe kubadilishana  na kupeana uzoefu wa kazi,’alisema
Aidha, amefafanua kuwa  jeshi la polisi hivi sasa kupitia baadhi ya askari   limekuwa likikumbwa na matukio ya ukiukwaji wa maadili kwa kukutwa na tuhuma mbalimbali za uhalifu.
Kwa upande wake, Kamanda wa polisi wa mkoa wa mbeya, Ndugu Diwani Athumani ambaye ni mwenyeji wa Mkutano huo , alisema kikao hicho kinatarajia kutoka na mikakati itakayosaidi kupunguza wimbi la uhalifu pamoja na ajali barabarani.
Amesema mara nyingi Wahalifu wamekuwa wakitumia njia nyingi kufanya uhalifu na kukimbilia mikoa ya jirani  hivyo  mkutano huu ambao unahudhuriwa na Makamanda pamoja na wakuu wa upelezi utasaidia kuwabaini ikiwa na kusambaratisha mtandao uliopo
Mkutano huo ni watatu baada ya mkutano wa kwanza kufanyika Mkoani Iringa na  wapili ulifanyika Mkoani Morogoro na kwamba wajumbe wanatarajia kutoka na maadhimio mapya.
Na Mbeya yetu 
................................................................................................................
 
 MUONEKANO WA DARAJA LA KIGAMBONI DSM
DSC08191 
Daraja la muda la kigamboni likiwa limemalizika ambapo hutumiwa na mafundi na magari ya kubebea vifaa mbalimbali vya ujenzi kuvusha upande wa pili kwaajili ya ujenzi wa daraja la kudumu

........................................................................................................................

Wizara yaendelea kusisitiza MSD iliuziwa ARV ‘feki’ Wizara yaendelea kusisitiza MSD iliuziwa ARV ‘feki’

ARVs a27e5
Serikali kupitia Wizara ya ya Afya na Ustawi wa Jamii imeendelea kusisitiza kwamba Kampuni ya TPI Ltd iliiuzia Bohari ya Dawa (MSD) dawa bandia za kupunguza makali ya Ukimwi aina ya TT-VIR 30 toleo Na.0C.01.85,kwa mujibu wa nyaraka zilizopo na kwamba dawa hizo zilibainika kuwa ni bandia.
Msisitizo huo umetolewa katika vyombo vya habari jana na ofisi ya Wizara ya afya na Ustawi wa jamii kupitia kwa msemaji wake Nsachris Mwamwaja ili kuondoa mkanganyiko ambao umeanza kujitokeza kwa wananchi.

Katika taarifa hiyo Serikali imesema kuwa kama ilivyoelezwa katika taarifa mbalimbali za umma zilizokwisha kutolewa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na TFDA kuhusiana na suala hili, bado inasisitizwa dawa hizo zilikuwa bandia.
"Tunapenda kusisitiza kwamba, waziri katika hotuba yake hakukanusha kuwa Kampuni ya TPI Ltd iliiuzia MSD dawa bandia bali alieleza kwamba uchunguzi wa awali katika kiwanda cha kampuni hiyo haukuonyesha dawa hiyo ilizalishwa na TPI Ltd bali vifungashio ni vya TPI Ltd na nyaraka zinaonesha TPI Ltd kuiuzia MSD dawa hizo bandia,"ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Aidha, msemaji huyo wa wizara katika taarifa hiyo alieleza kuwa vyombo vya usalama bado vinaendelea kulichunguza suala hilo ili kubaini chanzo na wahusika wakuu wa dawa hizo bandia .
Hivyo kwa kuzingatia unyeti wa suala hilo,wizara imetoa wito kwa vyombo vya habari kusubiri hatma ya uchunguzi unaofanywa na vyombo vya usalama na kuepuka kutoa taarifa ambazo zinaweza kupotosha umma na jitihada kubwa za Serikali katika kupambana na dawa bandia nchini.
Mnamo Mei 9, 2013, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hussein Mwinyi katika kuhitimisha hoja ya bajeti ya wizara alitolea ufafanuzi suala la dawa bandia ya ARV kufuatia hoja zilizokuwa zimetolewa na Zarina Madabida (Mb) kuhusu kuhusika kwa Kiwanda cha Dawa cha Tanzania Pharmaceutical Industries Ltd (TPI) katika sakata la dawa bandia ya ARV.
..............................................................................................................................................................

Mbunge Msigwa akishuka katika gari ya polisi baada ya kufikishwa mahakamani mchana huu                                        (Picha kwa hisani ya Fununublog)
……………………………………………
Watuhumiwa  70  wa vurugu  za machinga  na polisi mjini Iringa akiwemo mbunge  wa  jimbo  hilo mchungaji Peter  Msigwa   wamefanyiwa  utaratibu  wa  dhamana  kutokana na mahakama  kukubali  kutoa  dhamana  baada ya  kusomewa mashitaka matatu  huku mbunge  akisomewa mashitaka mawili likiwemo  kushawishi  na kufanya mkutano bila  kibali  .

Watuhumiwa  wote  wamekana  mashitaka  dhidi walikuwa wakifanyiwa  utaratibu  wa dhamana  katika  mahakama  hiyo ya  hakimu mkazi  wa wilaya ya  Iringa Mheshimiwa  Godfrey Isaya .

Hata  hivyo wamekana  mashitaka  yote yaliyotolewa ambayo shitaka la kwanza la mbunge ni kushawishi kufanya vurugu  ,huku  wengine  wote  kosa la kwanza kufanya mkutano bila kibali , kuharibu mali kinyume na sheria na  kufanya  vurugu .
Dhamana ya watuhumiwa hao ilikuwa ni wadhamini wao  kusaini hati ya dhamana yenye thamani ya Tsh milioni 1 na  kuwa na mdhamini mmoja mwaminifu.

Mbunge Msigwa akishuka katika gari hilo la polisi tayari kwa kuelekea chumba cha mahakama
Mbunge Msigwa akiwa na gazeti mkononi baada ya kufikishwa mahakamani leo
Watuhumiwa wengine 70 wa vurugu za machinga na polisi wakishuka katika karandinga la polisi

No comments: