Saturday, June 8, 2013

MAHAFALI YA KUFUNGA MAFUNZO YA UONGOZI DARAJA LA KWANZA KOZI NAMBA 20 KWA ASKARI MAGEREZA YAFANYIKA KATIKA CHUO CHA MAFUNZO CHA MAGEREZA WILAYANI RUNGWE MKOANI MBEYA.

 Kamishna wa Fedha na utawala wa Magereza Gaston Sanga akipokea Salamu za heshima kutoka kwa wahitimu wa mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi namba 20 katika sherehe za kufunga mafunzo hayo yaliyo fanyika katika chuo cha Magereza Kiwira Tukuyu Rungwe Mkoani Mbeya
 Kamishna wa Fedha na utawala wa Magereza Gaston Sanga akikagua wahitimu wa mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi namba 20 katika sherehe za kufunga mafunzo hayo yaliyo fanyika katika chuo cha Magereza Kiwira Tukuyu Rungwe Mkoani Mbeya
 Kamishna wa Fedha na utawala wa Magereza Gaston Sanga akimtunuku cheo cha Ukoplo Askari B4448 Patric Babara kwa niaba ya wahitimu wa mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi namba 20 katika sherehe za kufunga mafunzo hayo yaliyo fanyika katika chuo cha Magereza Kiwira Tukuyu Rungwe Mkoani Mbeya
 Kamishna wa Fedha na utawala wa Magereza Gaston Sanga akimtunuku cheti muhitimu B7348 Patrick Chalemta  aliye fanya vizuri masomo ya Darasani katika  mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi namba 20
  Kamishna wa Fedha na utawala wa Magereza Gaston Sanga akimtunuku cheti muhitimu aliye fanya vizuri somo la kulenga shabaha 3163 Tatu Amri  katika  mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi namba 20 
  Kamishna wa Fedha na utawala wa Magereza Gaston Sanga akimpa zawadi  muhitimu 3914 Leonida Hillu ya mwnafunzi mwenye Nidhamu usafi na ukakamavu katika  mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi namba 20
 Baadhi ya Maofisa wakitoa heshima katika mahafali ya mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi namba 20 katika sherehe za kufunga mafunzo hayo yaliyo fanyika katika chuo cha Magereza Kiwira Tukuyu Rungwe Mkoani Mbeya
 Kamishna wa Fedha na utawala wa Magereza Gaston Sanga (kushoto) akiwa na Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira Staniford Ntirudura wakipokea Salamu za heshima kutoka kwa wahitimu wa mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi namba 20 katika sherehe za kufunga mafunzo hayo yaliyo fanyika katika chuo cha Magereza Kiwira Tukuyu Rungwe Mkoani Mbeya
 Wahitimu wakiwa kwenye Gwaride  wakipita kwa mwendo wa Haraka mbele ya Mgeni Rasmi.
 "Hima..... Hima.... Hima!.... " Ni salamu ya utii ikiongozwa na Parade Kamanda SP Lucas Ndoteela
 Baadhi ya Maofisa wakifuatilia kwa Makini shughuli za Mahafali
 Baadhi ya Wahitimu wakionesha umahili wa kupambana na maadui
 Watoto wanaolelewa na kituo cha malezi ya watoto wadogo katika chuo cha Magereza wakitumbuiza katika Sherehe za Mahafali
 Mkuu wa Chuo cha Magereza Kiwira, Kamishina msaidizi wa Magereza  Staniford Ntirudura akizungumza jambo katika mahafali hayo.
 Wahitimu wa mafunzo ya uongozi daraja la kwanza kozi namba 20 katika sherehe za kufunga mafunzo hayo yaliyo fanyika katika chuo cha Magereza Kiwira Tukuyu Rungwe Mkoani Mbeya, wakifuatilia matukio yanayo endelea katika Sherehe zao.
 Wahitimu B5414 Peter Ndalahwa na 3469 Matha Mwanjala wakisoma Risara katika mahafali yao
 Muhitimu B3494 Willy Timoth akisoma Shairi wakati wa mahafali
 Kamishna wa Fedha na utawala wa Magereza Gaston Sanga akizungumza na wahitimu

********************
JUMLA ya Askari 984 wa Jeshi la Magereza, wanaume 845 na wanawake 139  wametunukiwa  Vyeo vya Ukoplo baada ya kuhitimu mafunzo ya Uongozi daraja la Kwanza kozi namba 20 katika Chuo cha Magereza Kiwira Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya.
Vyeo hivyo vilitolewa na Kamishina wa Fedha na Utawala Gaston Sanga kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Magereza katika Sherehe za ufungaji wa mafunzo hayo zilizofanyika katika Viwanja vya Chuo hicho leo Juni 7, Mwaka huu.
Akizungumza katika mahafali hayo, Kamishina wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga amesema Askari wa Jeshi la Magereza Nchini wanatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili, taratibu na kanuni za kazi kwa kufuata uwajibikaji, unyenyekevu, ukakamavu, ujasili, upendo, ushirikiano, uvumilivu, uaminifu na nidhamu.
Kamishina Sanga amesema Maaskari wanapaswa kuzingatia elimu waliyopewa wakati wa mafunzo ili wakawe mfano kipindi cha utendaji kazi wao ikiwa ni pamoja na kuhamasisha na kuwaongoza wenzao ambao hawakupatiwa elimu kama yao.
Aidha amewaasa kutowatesa Wafungwa walioko magerezani bali kuwahudumia kwa kuzingatia kuwa wanamhudumia binadamu kama walivyo wao  na siyo kuchukua nafasi ya kuwanyanyasa bila kuogopa haki na Stahili za binadamu japokuwa ni wafungwa.

Picha na Mbeya yetu Blog
......................................................................................................................... 

MBEYA CITY MOTO WAKE HAUZIMWI, WASUKA KIKOS MATATA CHA MAKINDA KUZISUMBUA TIMU ZA LIGI KUU MSIMU UJAO!!

488123_216997305113321_161758080_n 
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe Dar es salaam
Ikiwa katika harakati za kujenga timu ya muda mrefu, klabu mpya ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu ujao, Mbeya City ya jijini Mbeya anaendelea na mpango wake wa kuandaa kikosi cha pili cha klabu hiyo kwa lengo la kuwa na timu ya ushindani kitaifa na kimataifa.
Kocha msaidizi wa klabu hiyo inayonolewa na kocha Juma Mwambusi, Mwalimu Maka Mwalwisyi ameimabia FULLSHANGWE kuwa kwa sasa wanaendelea na mazozezi ya kikosi cha pili ambacho kimeteuliwa na benchi la ufundi la klabu hiyo, wakati viongozi wa timu  wakiweka mambo safi ili timu A iingeia kambini kujiandaa na michuano ya ligi kuu msimu ujao.
“Tunataka kuijenga falsafa ya Mbeya City, kufanikisha hilo tunahitaji kuwa na timu bora ya vijana ambao tutakuwa tunawapandisha timu A.  Kwasasa tupo na vijana wengi sana, tunajaribu kuchambua wanaotufaa ili kupata timu ya chini ya umri wa miaka 20”. Alisema Mwalwisyi.
Kocha huyo alisema kuwa wachezaji wao wanaonesha juhudi kubwa ya kujifunza, jambo ambalo linatia matumaini kwa benchi la ufundi.
“Vijana wana vipaji vya hali ya juu. Wanacheza kwa kujituma sana, mbali na hayo wana nidhamu ya mazoezi, wanazingatia sana maelekezo ya waalimu wao”. Alisema Mwalwisyi.
Mwalwisyi alisisitiza kuwa malengo yao ni kuifanya Mbeya City kuwa klabu ya ushindani mkubwa na sio washiriki wa ligi kuu bara.
Aidha alisema katika kuhakikisha hilo, benchi la ufundi linataka kuwekeza katika soka la vijana ambao ndio chagua sahihi kwa soka la sasa.
“Soka la kisasa kwa kweli linahitaji sana vijana ambao wanaenda sambamba na kasi ya mpira wa dunia, kwa kulijua hilo, Mbeya City lazima iwe kitalu cha kuzalisha wachezaji wa Tanzania”. Alisema Mwalwisyi.
Pia kocha huyo aliwataka mashabiki wa Mbeya kuwaunga mkono wao na ndugu zao Tanzania Prisons, wawakilishi wa jiji la Mbeya michuano ya ligi ya Premia ya Tanzania bara.
....................................................................................................................................................
 

Mbatia ataka walioruhusu vitabu ‘feki’ vitumike sasa wasulubiwe

Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia  

Dodoma. Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia ameitaka Serikali isiishie kuivunja Kamati ya Ithibati ya Vifaa vya Elimu, (EMAC), na badala yake iende mbali zaidi kwa kuwachukulia hatua za kisheria wajumbe wote wa kamati hiyo.
Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa NCCR-Mageuzi alisema jana mjini Dodoma kuwa kamati hiyo inahusika moja kwa moja kuua elimu nchini kutokana na kufumbia macho ufisadi ulioruhusu kusambazwa kwa vitabu visivyo na ubora.
“Hawa ni wahujumu uchumi wa nchi yetu; wanahusika kuididimiza elimu yetu... Inaonyesha wazi kuwa watunzi wa vitabu vile hawakutumia mitalaa. Kutokuongozwa kwa mitalaa kumesababisha vitabu vile kukosa ubora. Haiwezekani mwandishi, mhariri na mhakiki, awe mtu mmoja.” alisema.
Mbatia alisema Emac imetoa ithibati kwa vitabu vyenye maudhui yasiyo sahihi au dhaifu na ambayo hayamo kwenye mihutasari huku baadhi yao vikiwa vimeiwakilisha vibaya Bendera ya Taifa pamoja na Nembo ya Taifa kwenye baadhi ya vitabu hivyo.
Alisema miongoni mwa vitabu vilivyopitishwa na Emac havina majina ya waandishi na kwamba badala ya jina la mwandishi limewekwa jina la kampuni ya uchapishaji.
“Hakuna hata kitabu kimoja chenye wasifu wa mwandishi na karibu vitabu vyote havina wahariri wakati ni lazima kila kitabu kiwe na angalau mhariri mmoja” alisema Mbatia.
Alisema kasoro nyingine iliyopo katika vitabu hivyo ni makosa mengi ya lugha iliyotumika kuandikia ambayo ni Kiswahili, hali inayoonyesha kuwa vitabu hivyo havikupitishwa na Baraza la Kiswahili la Taifa (Bakita).
“Aibu nyingine ipo katika maelezo ambapo eti wameandika mitalaa ya shule za awali unamwezesha mwanafunzi kukua kiuchumi, kisiasa na kijamii…na kwa wale wa shule ya msingi, wanasema mtalaa unamsaidia mwanafunzi kupata uelewa wa lugha ya Kifaransa ili aweze kupata ajira…Kweli mwanafunzi wa shule ya awali anatakiwa akue kiuchumi, kisiasa na kijamii….na hii lugha ya Kifaransa inatoka wapi katika mtalaa wa Tanzania” alihoji Mbatia.
Mbatia aliitaka Serikali vilevile iviondoe sokoni vitabu vyovyote vya kiada na ziada vyenye maudhui potofu kama inavyofanya kwa bidhaa nyingine zisizo na ubora.
“Adhabu zitolewe kwa watayarishaji na wamiliki wa vitabu duni vitakavyoingizwa shuleni kinyume na taratibu ili kuzuia matendo ya rushwa…chombo cha kupokea taarifa kutoka kwa wadau wa elimu kuhusu vitabu duni kiundwe” alisema.
Alisema endapo Serikali itapuuza na kuviacha vitabu hivyo visivyo na ubora kuendelea kutumika, ubora wa elimu utazidi kuporomoka kwa sababu wanafunzi watalazimika kutumia vitabu visivyo na ubora.
........................................................................................................................................................

No comments: