Thursday, July 11, 2013

ALIYE TUMBUKIZA KICHANGA CHOONI AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MITANO JELA.


 Rukia Haruna (31) pichani aliye kutwa na hatia ya kutupa mtoto chooni.
 Rukia Haruna (31)  akitolewa nje  na Askari wa Jeshi la Polisi akitolewa nje ya  Mahakama kwenda Gerezani kutumikia kifungo cha miaka 5 Jela


****************************
HIVI NDIVYO ILIVYO KUWA JUNI 14 .2013 ENEO LA MANGA A JIJINI MBEYA


*********************
Mwanamke mmoja mkazi wa Manga A Jijini Mbeya amehukumiwa kifungo cha miaka 5 jela kwa kosa la kutupa mtoto wake chooni.
 
Tukio hilo lilitokea Juni 14, Mwaka huu katika eneo hilo baada ya watoto waliokuwa wakicheza kugundua kuwepo kwa Mtoto katika choo cha shimo.
 
Mtuhumiwa baada ya kukamatwa amekiri kutenda kosa hilo na kwamba alifanya hivyo baada ya mzazi mwenzie kumkataa.
 
Ameongeza kuwa amelazimika kutupa katika choo cha jirani kwa sababu ni cha shimo tofauti na chao ambacho asingeweza kutupa mtoto huyo.
 
Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Archiles Mulisa mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya, Zabibu Mpangula, amemtaja Mtuhumiwa kuwa ni Rukia Haruna (31) mkazi wa Manga A Jijini Mbeya na kwamba kosa lake ni kinyume cha kifungu  218 kifungu kidogo cha 35 sura ya 16 ya mwaka 2002.
  ......................................................................................

HOT NEWS: DEREVA WA DALADALA ASUSIWA MAITI BAADA YA KUZAA NA MWANAFUNZI

.  Atoweka nyumbani kwa siku mbili
 Mwenyekiti wa Mtaa wa Ihanga Kata ya Ilomba Emanuel Mwasibata akiwa amesimamia kikao cha usuruhishi
 Dereva wa daladala Aswile Mwalukoba aliyeshika fimbo baada ya kurejea nyumbani na kuhudhuria kikao cha usuruishi  ambapo alikili kuzaa  na mwanafunzi huyo na kukubali kuzika .
 Daladala iliyobeba mwili wa Marehemu kutoka Uyole.
 Wakazi wa Uyole wakiwa wameshikwa na butwaa baada yakumkosa mwenyeji wao
 Mwili wa mtoto ukiwa umefunkwa na kitenge na kutelekezwa kwenye kiti
 Kulia ni Carolina Kyando akiwa na dada yake baada ya kuleta mwili wa mtoto nyumbani kwa Mwalukoba eneo la Mama John jijini Mbeya
Majirani pande zote mbili wakingojea kujua hatma ya mazungumzo yanayo endelea baada ya Mwalukoba kurejea

Vitendo vya ukatili dhidi ya  watoto na wanawake  jijini mbeya vimeendelea chukua sura mpya  baada ya dereva wa daladala jijini humo kumzalisha mwanafunzi wa Masomo ya jioni kituo cha Juhudi kilichopo  Ilomba.
.
 Tukio hilo limetokea hivi karibuni  eneo la mama John Mtaa wa Ihanga Kata ya Ilomba ambapo dereva wa daladala aliyefahamika kwa jina la Aswile Mwalukoba (45 ) kutelekezewa wa miezi saba ambaye alikwisha fariki baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Akizungumzia tukio hilo Mwenyekiti Mtaa huo Ndugu Emanuel Mwasibata amesema kuwa mgogoro huo umetokana  na dereva huyo kugoma kuuzika mwili huo kwakile alicho dai kuwa hivi sasa haishi na binti huyo kwa muda mrefu sasa.
Kwa upande wake binti huyo aliyefahamika kwa jina la Calorina Kyando amedai kuwa kitendo cha yeye kuuchukua mwili wa mtoto huyo hadi kwa baba yake unatokana   kutelekezwa na bwana huyo kisha kupigwa marakwa mara na kusababishiwa ulemavu wa sikio la kushoto baada ya kung’atwa na mwanaume huyo.
Mwanamke huyo amefafanua kuwa mara baada ya mtoto huyo kufariki wakati akipatiwa matibabu katika Hospital ya Igawilo jijini humo aliamua kumpigia simu mzazi mwenzie kwa lengo la kumpa taarifa za msiba huo.
Amesema mara baada ya kutoa taarifa hiyo mwanaume huyo alikubali na kumueleza mwanamke huyo kuwa yuko tayari kwa ajili ya mazikoya mtoto huyo ambapo anafanya taratibu za kuwasiliana na ndugu zake walioko Tukuyu Wilayani Rungwe.
Amesema katika siku iliyofuata mwanaume huyo hakupatikana kwa simu ya kiganjani na wala hakuwepo nyumbani kwake anapo ishi eneo la Mama John hali iliyo plelekea baadhi ya majirani na mwanamke huyo kutoka Uyole kusaidiana na kuutoa mwili huo Hospitalini hapo kwa lengo la kufanya taratibu nyingine .
Aidha majirani hao waliamua kuchukua mwili huo hadi nyumbani kwa Mwalukoba ambapo waliuweka kwenye kiti ndani ya nyumba yake huku wakiendelea kumsubiri mwalukoba arudi aliko  ambapo baadaye alirudi nyumbani hapo akisindikiazwa na Mdogo wake aliyefahamika kwa jina Gabriel Mwalukoba hadi nyumbani hapo.
Kitendo hicho cha kurejea kwa mwanaume huyo kilifanya mwenyekiti wa mtaa huo Ndugu Emanuel Mwasibata kuhoji juu ya  kutoweka kwa nyumbani kwakwe kwa muda wa siku mbili huku kukiwa hakuna mawasiliano yoyote.
 Baada ya kikao cha muda mrefu kati ya pande zote mbili mwanaume huyo alikubali kuupokea mwili huo na hivyo kuanza kufanya taratibu za mazishi ambapo mazishi hayo yalifanyika katika makaburi ya Iyela mida saa 12 jioni na kuhudhuriwa na familia zote mbili pamoja na majirani wengine kutoka Uyole na Mama John.
NA Ezekiel Kamanga MBEYA YETU 

No comments: