Wednesday, July 24, 2013

KUMBEKUCHA TUFANYE KAZI WATANZANIA; hata kuku hupigana!


IMG 0002 64330
..............................................................................................................................................

RAIS KIKWETE AWASILI BUKOBA KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU SITA

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe. Fabia Massawe baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Bukoba leo tayari kuanza ziara ya kikazi ya siku sita mkoani humo
 
Rais Kikwete akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman ambaye pia yuko mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi
 
Rais Kikwete akisalimiana na Mstahiki Meya wa Bukoba Mhe Anatory Amani
 
Vijana wa Skauti wa Bukoba wakimlaki Rais Kikwete uwanjani hapo
Wanahabari toka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa kazini
 
Kijana wa Skauti akipiga saluti kuomba kumvisha skafu Rais Kikwete
 
Rais Kikwete akivishwa skafu
 
 Rais Kikwete akisalimiana na Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli. Kushoto ni Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe
 
 Rais Kikwete akisalimiana na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo
 
Rais Kikwete akisalimiana na viongozi na wananchi waliofika uwanjani kumlaki
 
 Rais Kikwete akisalimiana na Mkuu wa JKT
 
 Rais Kikwete akisalimiana na viongozi wa dini mbalimbali waliokuwepo uwanjani
 
 Rais Kikwete akiangalia ngoma za utamaduni
Ngoma ya Kihaya ikimlaki Rais Kikwete Bukoba
 
 Karibu Bukoba mheshimiwa Rais….
 Sehemu ya viongozi waliohudhuria sherehe ya kuweka jiwe la msingi la ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba
 Viongozi wa dini wakiwa bega kwa bega kwenye sherehe hizo
Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe akimkaribisha Rais Kikwete kuongea na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi la ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba
 
 Rais Kikwete akiongea na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 
 Rais Kikwete akipata maelezo kabla ya kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 
Rais Kikwete akifunua kitambaa kama ishara ya kuweka  jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 
Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe na Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Miundombinu Mhe Peter Serukamba wakishangilia wakati Rais Kikwete akiweka jiwe la msingi
 
 Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wadau baada ya kuweka jiwe la msingi katika ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
 
 Rais Kikwete akisalimiana na Mhashamu Methodius Kilaini, Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba
 
Rais Kikwete akiwasili Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 
 Rais Kikwete akisalimiana na wanachama wa KCU alipowasili Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 
Rais Kikwete akisalimiana na wananchi waliofurika kushuhudia ufunguzi wa  jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 Rais Kikwete akiendelea kusalimia wananchi

Sehemu ya umati wa wananchi kwenye ufunguzi wa jengo hilo
 Jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
 
 
Rais Kikwete akipokea zawadi ya kahawa toka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya KCU (1990)LTD John Binushu 
 
Rais Kikwete akifunua kitambaa kama ishara ya Kufungua rasmi jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
Rais Kikwete akikata utepe Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
Rais Kikwete akihutubia wananchi baada ya Kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
Wananchi wakimsikiliza Rais Kikwete
 
Rais Kikwete akihutubia
Rais Kikwete katika picha ya pamoja na viongozi wa KCU baada ya kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd)
—————————————————————

msajili wa vyama vya siasa aionya CHADEMA

t 7a71b
Na Jennifer Chamila,MAELEZO
Msajili wa vyama vya Siasa nchini amewaasa wanachama na viongozi wa Chama Cha Democrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutumia muda wao kufanya shughuli za siasa ili kuchangia maendeleo ya nchi badala ya kutumia uwezo na muda wao kubuni mambo yanayoleta mtafaruku na kuhatarisha amani ya nchi.
hdg

Pia amepinga tamko la chama hicho la kuanzisha mafunzo ya kujilinda kwa vijana wake nchi nzima.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo jijini Dar es Salaam na kusainiwa kwa niaba ya Msajili wa vyama vya siasa Sisty Nyahoza alisema kuwa hajawahi kuruhusu CHADEMA au chama chochote cha siasa kufanya mafunzo ya ukakamavu au mafunzo ya kutumia nguvu ya aina yoyote kwa wanachama wake au mtu yeyote yule.
Anaongeza kuwa CHADEMA wanaruhusiwa kuanzisha vikundi vya kujilinda lakini hawaruhusiwi kuanzisha mafunzo ya kutumia nguvu kwaajili ya kujilinda kama walivyo tangaza katika mikutano yao ya hadhara kwani ni kinyume na Demokrasia na Katiba ya Jamuhuri ya Muungano.
Nyahozo ametoa ufafanuzi kuhusu vikundi vya ulinzi na usalama vilivyopo katika Katiba ya Vyama vya Siasa kwamba vikundi hivyo haviruhusiwi kufanya mafunzo ya kutumia nguvu ya aina yoyote katika kutekeleza majukumu yao.
Bali wajibu wao ni kutoa taarifa wa vyombo vya Dola pale wanapo sikia au kuona uhalifu ukitokea na wala sio kupambana na wahalifu au watu wanaotaka kuwadhuru kama tamko la CHADEMA la tarehe 9 mwezi huu linavyo sema.

"Hakuna maelezo yoyote katika Katiba ya CHADEMA yanayoruhusu kutumia nguvu kufanikisha shughuli za kulinda mali na Viongozi wa Chama.Ni vyema wananchi wote waelewe kuwa Sheria za Nchi zimeweka masharti maalumu kwa Vyama Vya Siasa kutokana na umuhimu wa vyama hivi katika kudumisha aman utulivu na umoja wa Kitaifa", alisema Nyahoza.

Alisema kuwa kutokana na Ibara ya20(2)C ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1997 inasema kuwa "Bila kujali masharti ya ibara ya (1) na (4),haitakuwa halali kwa chama chochote cha siasa kuandikishwa ambapo kutokana na katiba au sera yake:-kinakubali au kunapigani matumizi ya nguvu au mapambano kama njia za kufikia malengo yake ya kisiasa.

Nyahoza alimaliza kwa kuwataka CHADEMA kuacha kutekeleza mpango walio tangaza wa kuanzisha makambi ya kufanya mafunzo ya kujilinda kwa vijana wao nchi nzima,kwani kufanya hivyo ni kukiuka sheria za nchi na endapo watashindwa kutii agizo hilo hatua za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Mwisho.

No comments: