Tuesday, July 9, 2013

MAKAO MAKUU YA MKOA MPYA WA SONGWE KUBAKI MKWAJUNI


 Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro ambaye pia ndiye Mkuu wa Mkoa Mbeya akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya wakimsikiliza mkuu wa mkoa Mbeya akiongea na waandishi wa habari


Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya hatimaye yatoa ufafanuzi na kupigilia Msumari maamuzi ya Kamati ya Ushauri (RCC) ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa mpya Mkwajuni Wilayani Chunya.
              
Akitoa maamuzi ya Kamati hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya, Abbasi Kandoro ambaye pia ndiye Mkuu wa Mkoa Mbeya akiongea na vyombo vya habari ofisini kwake  amesema Kamati  imeridhika na ushauri uliotolewa na Kamati ya Ushauri iliyofanyika Julai 4, Mwaka huu.
Kandoro amesema lengo la kukutana na kamati ya ulinzi na usalama ni kutokana na kuibuka kwa maneno toka kwa baadhi ya Wananchi ambao wanadai maamuzi yaliyotolewa na Kamati ya kupeleka Makao makuu ya Mkoa Mpya Mkwajuni Wilayani Chunya hayakuzingatia vigezo vya umbali wa baadhi ya maeneo.
Amesema katika kuliletea ufafanuzi jambo hilo Mkuu huyo wa Mkoa alidai kuwa baadhi ya wajumbe wa kamati ya Ushauri wakiwemo Wakurugenzi wa Halmashauri na Wenyeviti wao wameitwa ili kutoa maelezo kwenye kamati ya Ulinzi kama endapo mapendekezo yaliyotolewa na RCC hayakuzingatia matakwa ya wananchi.
Ameongeza kuwa baada ya Kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa kuridhika na maelezo ya wajumbe hao imebariki na kuamua kuwa mapendekezo ya Kamati ya Ushauri yabaki vile vile kwa Mkoa mpya kuwa Songwe inayotokana na Mto Songwe uliopita kila Wilaya zinazounda Mkoa huo ambazo ni Momba, Mbozi, Chunya na Ileje.

KIPANYA LEO


971832 390703241036396 30643933 n 6ac23

KIJANA AJIUA KWA KUJILIPUA KWA PETROLI MJINI DODOMA.



KUJIUA c653a

MWANAFUNZI wa Chuo cha Ufundi (VETA), mkoani Dodoma, Taliki Juma (22), amedaiwa kujiua kwa kujilipua kwa petroli kisa mapenzi.

Taarifa zinasema, kufuatia moto mkali uliotokana na petroli hiyo, mbali na mwanafunzi huyo aliyejitia mhanaga kwa mapenzi, watu wengine wanane waliokuwa karibu na moto huo nao walijeruhiwa vibaya.

Akithibitisha, leo Kamanda wa Polisi wa mkoa, David Misime, amesema tukio hilo lilitokea jana mida ya saa 12.30 jioni katika Kitongoji cha Machaka, Kata ya Nzughuni.
Kamanda alifafanua kwamba mapema mwanafunzi huyo alinunua lita tano za mafuta ya petroli katika kituo cha mafuta cha Nanenane na kisha kujilipua na kisha kwenda kujilipua akiwa katika saluni ya Irene Mapunda ambaye inasadikiwa alikuwa mpenzi wake.
Alisema, mwanzoni watu waliokuwa karibu naye walijaribu kumsihi asijilipue lakini hawakufanikiwa, kwani aliwasha kibiriti ndani ya saluni hiyo na kusababisha moto mkubwa kulipuka ambao uliwaunguza wengine waliokuwa karibu naye pamoja na mali zote zilizokuwa ndani ya Saluni hiyo kuteketea.

"Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi, hata hivyo Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linaendelea na uchunguzi wa kina juu ya tukio hili," ilieleza taarifa ya Kamanda wa Polisi.

Taarifa iliwataja waliojerihiwa kuwa ni Mugina Hessein (32), Benson Mushi (11) Japhet Japhet (18), Meshack John (18), Swaibu Kassim (20),Ester Silau (30), Shaban Pili (20) na Fedrick Gabriel (21) ambao wote wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na tathimini ya hasara iliyosababishwa na moto huo bado haijafahamika.
.................................................................................................................................

No comments: