Wednesday, August 14, 2013

UZEMBE WA TANESCO WASABABISHA KIFO CHA BINTI WA MIAKA 26 MBALIZI MBEYA.

 HAPA NDIPO MAREHEMU ALIPOGUSA NA KUKUTWA NA MAUTI

NYAYA ZA UMEME AMBAZO ZIMENING'INIA MITA MOJA KUTOKA USAWA WA ARDHI ZIMESABABISHA KIFO CHA NEEMA B. KIPENYA (26) ALIPOTELEZA NA KUKAMATA NYAYA HIZO KISHA KUFARIKI PAPO HAPO.
 KATI YA NGUZO HADI NGUZO NI UMBALI WA ZAIDI YA MITA 75 MAHALI AMBAPO PALIPASWA KUWA NA NGUZO TATU LAKINI IKAWEKWA NGUZO MOJA , HALI MTEJA WA ENEO HILO ALIKUWA AMELIPIA NGOZO TATU ZAIDI YA MIAKA MIWILI ILIYOPITA .
 HAPA NDIPO ALIPO TELEZA MAREHEMU NEEMA NA KUANGUKIA NGUZO HIZO
 ASKARI AKIPATA MAELEZO KUTOKA KWA MASHUHUDA 
 MWENYEKITI WA KIJIJI CHA MSHIKAMANO BWANA KISMAN MWANGOMALE AMBAYE NDIYE MTEJA WA KWANZA KULIPIA TANESCO NGUZO TATU  NA KUFUNGWA NGUZO MOJA , NA AMETOA TAARIFA MARA KADHAA TANESCO NA HATA KUANDIKA BARUA KWA NIABA YA KIJIJI LAKINI HAKUNA UTEKELEZAJI ULIOFANYIKA HADI MADHARA YAMETOKEA NDIPO TANESCO WAMEFIKA.

MMOJA KATI YA WATUMISHI WA TANESCO AMBAYE ALIFIKA ENEO LA TUKIO NA KUKATA UMEME USILETE MADHARA ENEO HILO , HATA HIVYO ALINUSURIKA KUPIGWA NA WANANCHI WENYE HASIRA KALI AMBAO WALIKERWA NA TUKIO HILO.

 MWENYEKITI WA KIJIJI CHA MSHIKAMANO WA KWANZA KUSHOTO NA WATUMISHI WA TANESCO WAKIANGALIA NGUZO ZILIZO ELEMEWA NA UZITO WA NYAYA HIZO NA KUSABABISHA NGUZO KUSHINDWA KUHIMILI UZITO WA NYAYA HIZO. 
 WAOMBOLEZAJI WAKILIA KWA UCHUNGU KWANI MUDA MFUPI ULIOPITA WALIKUWA NA MAREHEMU NYUMBANI HAPO.
 MOJA KATI YA NDUGU AMBAYE ALIZIRAI KATIKA ENEO LA TUKIO
MWILI WA MAREHEMU UKIWA KATIKA CHUMBA CHA MAITI HOSPITALI YA IFISI ILIYOKO WILAYA YA MBEYA UKISUBIRI UCHUNGUZI ZAIDI WA KITABIBU.

PICHA NA EZEKIEL KAMANGA

 

..............................................................

TRAFIKI FEKI ADAKWA


New Picture 2 10540


Askari Bandia wa Kikosi cha Usalama Barabarani aliyekamatwa leo mchana maeneo ya Kinyelezi Mnara,Tabata jijini Dar es Salaam akiwa ndani ya sare zake mara baara ya kukamatwa. Askari huyu feki amefikishwa kwenye Kituo cha Polisi Stakishari ili taratibu za kisheria ziweze kuchukuliwa juu yake.

Afande huyo akiwa chini ya ulinzi wa Polisi mara baada ya kukamatwa mchana wa leo akila vichwa maeneo ya Kinyelezi Mnara,Tabata jijini Dar es Salaam.Askari huyu feki amefikishwa kwenye Kituo cha Polisi Stakishari ili taratibu za kisheria ziweze kuchukuliwa juu yake.

  ................................................................

MZEE WA MIAKA 50 MBARONI KWA KUBAKA WATOTO WAWILI UMRI MIAKA 4 NA 5 KWA KUWAPAKA MAFUTA YA KULA SEHEMU NYETI KATIKA DUKA LAKE.

MBAKAJI ERASTO MWAKYOMO (50) ANAYETUHUMIWA KWA UBAKAJI AKIWA KATIKA OFISI YA MWENYEKITI WA MTAA WA MAPELELE KABLA YA KUCHUKULIWA NA MWENYEKITI WA DAWATI LA WATOTO NA UKATILI WA KIJINSIA MARY GUMBO.
WATOTO WALIOKUWA WAKIBAKWA WAKITOA MAELEZO JINSI WALIVYOKUWA WAKITENDEWA
 MWENYEKITI WA MTAA WA MAPELELE CHRISTOPHER MWAKIBETE AKIANDIKA BARUA KWA WAZAZI NA MTUHUMIWA KUPELEKWA POLISI 
 BAADHI YA WAZAZI NA NDUGU WA WATOTO WAKIWA NYUMBANI KWA MWENYEKITI WA MTAA.

***************

Ezekiel Kamanga

ERASTO MWAKYOMA mwenye umri wa miaka hamsini mkazi wa mtaa wa Mapelele Kata ya ILEMI jijini Mbeya anahojiwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuwadhalilisha watoto wawili wa kike wote wakazi wa Mapelele.

Wazazi wa watoto hao baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa watoto hao ambao mmoja ana umri wa miaka minne na mwingine mitano walitoa taarifa kwa Balozi wa mtaa Bwana CASIAN MWEZIMPYA ambapo baada ya kutafakari kwa kina aliamua kulipeleka suala hilo kwa Mwenyekiti wa Mtaa.

Mwenyekiti wa mtaa Bwana CHRISTOPHER MWAKIBETE Aliamua kuwaita wazazi na mtuhumiwa kuwahoji yaliyotukia ambapo nao watoto walipewa nafasi ya kueleza ambao walieza kuwa ERASTO Alikuwa akiwashika sehemu za siri na kuwapaka mafuta kabla ya kufanya nao mapenzi.

Baada ya kusikiliza kwa makini MWAKIBETE aliamuru kuwa suala hilo ni la kisheria na kitaalamu hivyo hawezi kuchukua hatua zozote bali suala hilo analazimika kulipeleka Polisi ambapo Mwenyekiti wa Dawati la watoto na jinsia MARY GUMBO Alimchukua mtuhumiwa hadi kituo cha Polisi kati.

Baada ya mahojiano ya awali GUMBO aliwachuchukua watoto hadi Hospitali ya Rufaa kwa uchunguzi na mtuhumiwa kubaki kituo cha kati kwa mahojiano zaidi,hata hivyo uchunguzi umebaini kuwa baadhi ya watoto mtaani hapo wamekuwa wakitendewa vitendo vya ukatili lakini vimekuwa vikifumbiwa macho na baadhi ya wazazi wakihisi ni aibu kwa watoto wao.

No comments: