Wednesday, October 2, 2013

MWENGE WA UHURU WAZINDUA NA KUWEKA MAWE YA MSINGI MIRADI 22 YENYE GHARAMA YA SHILINGI BILION 1.9 WILAYANI RUNGWE MKOA WA MBEYA

OFISI YA HALMASHAURI YA RUNGWE


BAADHI YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WAKIWA TAYARI KUELEKEA KUUPOKEA MWENGE WA UHURU TAYARI KWA KUUKIMBIZA WILAYANI RUNGWE

MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA KUSHOTO AKIONGEA JAMBO NA MR SANGI AMBAYE NI KAIMU MKURUGENZI WA RUNGWE



VIJANA WA SKAUT WAKIWA TAYARI KUWAPOKEA WAKIMBIZA MWENGE KITAIFA

KUSHOTO ENZI SEME MRATIBU WA MWENGE WILAYA YA RUNGWE AKIMPONGEZA MRATIBU WA MWENGE WA WILAYA YA MBEYA KWA KAZI YA KUUKIMBIZA MWENGE WA UHURU NA KUZINDUA MIRADI WILAYANI MBEYA

MWENGE UKAPOKELEWA MPAKANI MWA MBEYA NA WILAYA YA RUNGWE KATIKA ENEO LA ISYONJE HUKU HALI YA HEWA IKIWA YA UKUNGU MZITO

KULIA MKIMBIZA MWENGE KITAIFA JUMA ALI SIMAI AKISALIMIANA NA MKUU WA WILAYA YA RUNGWE CHRISPIN MEELA KWA NYUSO ZA FURAHA WAKIWA TAYARI KUFANIKISHA KUUKIMBIZA MWENGE WA UHURU AMBAO UTA KIMBIZWA WILAYANI RUNGWE KWA 108 KM

MKUU WA WILAYA YA MBEYA AKIKABIDHI MWENGE WA UHURU KWA UONGOZI WA WILAYA YA RUNGWE

MEELA AKIAPA KIAPO CHA KUUPOKEA MWENGE WA UHURU NA KUAHIDI KUUKABIDHI MWENGE HUO KWA WILAYA YA KYELA BAADA YA KUZINDUA MIRADI 11, KUKABIDHI MIRADI 4 NA KUWEKA MAWE YA MSINGI 7 MIRADI YOTE IKIWA NA GHARAMA YA SHILINGI BILION 1.9



MRADI WA JENGO LA UTAWALA LA SHULE YASEKONDARI YA  KYIMO

MRADI WA KITUO CHA UTAFITI CHA KILIMO KILICHOPO KYIMO WILAYANI RUNGWE

MRADI WA KUSINDIKA MATUNDA ULIOPO KATIKA KATA YA IPONJOLA WILAYANI RUNGWE UKIWA MRADI UNAOJENGWA KWA NGUVU YA SERIKALI NA WANANCHI MRADI UNAOTARAJIA KUONGEZA THAMANI YA MATUNDA YANAYO HALIBIKA SANA WILAYANI RUNGWE



MKURUGENZI WA BUSOKELO AKIKILI KUKABIDHIWA MWENGE WA UHURU  NA TAYARI KUENDELEA NA RATIBA

VIONGOZI WA HALMASHAURI YA BUSOKELO WAKIONGOZWA NA MWAKIPUNGA MWENYEKITI WA H/BUSOKELO WA PILI KUSHOTO

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA YA RUNGWE

KWAKUWA WILAYA YA RUNGWE INA HALMASHAURI MBILI HIVYO SIKU YA PILI MWENGE UNAENDELEA NA RATIBA YA KUZINDUA NA KUWEKA MAWE YA MSINGI KATIKA HALMASHAULI YA BUSOKELO
KINGOTANZANIA
......................................................

Ujumbe kutoka Wizara ya Nishati na Madini ukiongozwa na waziri wake Profesa SOSPETER MUHONGO umefanya ziara ya kikazi nchini MORWAY yenye lengo la kubadilishana uzoefu katika masuala ya uchimbaji gesi na mafuta.

Profesa SospeterMuhongo akisikilizakwamakini madai nayowasilishwa na Meneja wao paresheninaufundi wa Mradi wakusindika gesi asilia( STATOIL) nchini Norway kabla ya kutembezwa mahali ambapo mitambo  hiyo ya kusindika gesi imejegwa.

Profesa Sospeter Muhongo akielekea mahali ilipo mitambo ya kusindika gesi asilia ya kampuni la Statoil Norway ili kujionea uwekezaji mkubwa ulivyofanyika na    kuleta manufaa makubwa kwa wananchi wa Norway ambao idadi yao haizidi watu milioni 5.

WaziriwaNishatinaMadiniSospeterMuhongowapilitokakushotoakifuatiwanabaloziwa Norway nchini Tanzania Bi Ingunnpamojanaujumbeulioambatananaenawatendajiwa Statoil Norway
WANAFUNZI WA KITANZANIA WANAOSOMEA UHANDISI WA MAFUTA NA GESI NORWAY WATAKIWA KUWEKA MBELE UTAIFA.

Akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kukagua mitambo ya kusindika gesi katika kisiwa hicho Profesa  Muhongo amesema, uwekezaji uliofanywa na serikali ya NORWAY ni wa kihistoria na kwamba umeipa changamoto serikali ya Tanzania ambayo iko mbioni kuanza uzalishaji mkubwa wa gesi na Mafuta katika mikoa ya Kusini.
Akijibu swali la mwandishi wa habari kutoka gazeti la serikali la NORWAY Profesa MUHONGO amesema kutokana na matumizi ya teknolojia ya kisasa ya kusindika gesi katika nchi zilizoendelea, serikali ya Tanzania imeamua kuzitembelea baadhi ya nchi zenye teknolojia hiyo ili kuhakikisha sera ya gesi inayotarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni inatekelezwa kulingana na matakwa ya wadau pamoja na mazingira ya eneo husika.
Muhongo amesema kupitia ziara hiyo amejifunza mambo muhimu kupitia  miundombinu ya kuzindika gesi nchini Norway ilivyojegwa na kwamba uwekezaji wa gesi unahitaji technolojia ya hali ya juu pamoja na rasilimali fedha mambo ambayo yamesaidia kubadili historia ya Norway kupitiamitambo ya usindikaji wa gesi ambapo NORWAY Imetumia kiasi cha dola za kimarekani bilioni 10 Kufanikisha mradi huo.
Halikadhalika Profesa Muhongo amesema dhana ya ushirikishwaji wa wananchi katika utekelezaji wa miradi ya umma halipaswi kupuuzwa na kwamba mradi wa gesi utakaoanza nchini Tanzania  kwanza utatatua matatizo ya wazawa ikiwa ni pamoja na kutumika katika kuzalisha nishati ambayo inahitajika kwa kiasi kikubwa na baadaye kuuzwa nchi jirani.
Muhongo amesisitiza kuwa  watanzania watanufauka na uwekezaji huu kwani serikali inajipanga kuwasaidia wananchi ili waweze kunufaika na mradi mkubwa wa gesi katika masuala ya elimu, afya, barabara, maji na  kama jinsi jamii zilizopo karibu na makampuni ya gesi na mafuta nchini Norway zinavyonufaika.
Kwa upande wake balozi wa Norway nchini Tanzania  Bibi Ingunn Klepsvik alisema nchi yake iko tayari kubadilishana uzoefu na Tanzania na kuahidi kuwabega kwa bega na Tanzania katika kuboresha miradi ya gesi ambayo ndiyo kwanza inaanza nchini.
Ingunn amesema Norway ilianza kuwekeza katika sekta ya gesi kwa kutegemea wataalamu toka Marekani ambapo waliwawezesha kupata utaalamu katika masuala ya gesi mpaka pale walivyoweza kuendesha mitambo  wao  wenyewe na kuwezesha kuinua kipato cha watu wa Norway.
Kwa upande wake Meneja rasilimali watu na mafunzo toka TPDC Flora Salakana amesesema uzoefu alioupata toka hammerfest utasaidia katika kuboresha mipango ya serikali katika kuwaendeleza wataalamu wa tanzania kushiriki kikamilifu katika miradi ya utafutaji, uzalishaji na uendelezaji wa gesi asilia Tanzania.
Pia amesema Serikali ya Norway kupitia kampuni ya Statoil itabadilishana uzoefu na wataalamu wa kitanzania toka (TPDC) hivyo kuwawezesha kufanya mafunzo ya vitendo kwenye mitambo ya kusafisha gesi asilia na kuwawezesha watanzania kujinoa kiutaalamu kwa njia hiyo kupitia Norway.
Salakana amesema uhusiano huu ni mwendelezo wa ushirikiano uliodumu kwa muda mrefu  baina ya nchi hizi mbili na kwamba  wataalamu wengi wa TPDC wamepata mafunzo yao nchini Norway.
Mwishoni mwa miaka ya 1960 na 1970 Ugunduzi wa gesi asilia nchini Norway lakini iliwachukua miaka kadhaa mpaka pale walipoanza kunufaika na uwekezaji huo miaka ya 2004 na mnamo mwaka 2007 Norway ilianza kujishughulisha na usindikaji wa gesi asilia iliyosaidia katika  kuingiza  pesa nyingi za kigeni nchini Norway na kuboresha maisha ya watu wake.

No comments: