Tuesday, November 19, 2013

HALMASHAURI ya Busokelo Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya imeanza kutekeleza kwa vitendo miradi iliyozinduliwa na mbio za mwenge wa uhuru uliomaliza mbio zake Oktoba 14, Mwaka huu nchi nzima.

 
Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Crispin Meela alisema ni vema vikundi vilivyopewa mafunzo vikasimamiwa ili matunda yaonekane na iwe fundisho kwa wengine ambao hawataki kujiunga na vikundi.
Abubakari  Getee afisa nyuki mkufunzi toka dodoma



HALMASHAURI ya Busokelo Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya imeanza kutekeleza kwa vitendo miradi iliyozinduliwa na mbio za mwenge wa uhuru uliomaliza mbio zake Oktoba 14, Mwaka huu nchi nzima.
Katika mbio za mwenge katika Halmashauri ya Busokelo ilitolewa mizinga ya nyuki 60 kwa vikundi 6 yenye thamani ya shilingi Milinoni 2.7 ambapo kila kikundi kilipatiwa mizinga 10 tayari kwa ufugaji wa nyuki.
Kutokana na vikundi hivyo kukabidhiwa mradi huo wa ufugaji nyuki Halmashauri iliandaa mafunzo ya siku tatu kwa wenye viti na makatibu wa vikundi 8 pamoja na mafundi seremala kwa ajili ya kupatiwa mafunzo namna ya ufugaji nyuki kwa njia ya kisasa inayochangia uhifadhi wa mazingira.
Msimamizi wa mafunzo hayo, Anamary Joseph ambaye ni afisa mazingira wa Halmashauri ya Busokelo alisema kupitia mafunzo hayo yatasaidia kuhamasisha wananchi kuacha kufuga nyuki kienyeji jambo ambalo huchangia kuharibu mazingira kutokana na njia wanayotumia wakati wa kuvuna.
Alisema ufugaji wa nyuki kwa njia za kienyeji huharibu mazingira kwa sababu wanapovuna hulazimika kuchoma moto ili nyuki waweze kukimbia na wao kuvuna kirahisi lakini hali hiyo huchangia kuchoma moto misitu na pia mazao yanayovunwa kuhosa ubora na kiwango ambacho kitamkomboa mkulima.
Awali akimkaribisha Mkuu wa Wilaya katika ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika Kijiji cha Lufilyo Busokelo Wilayani Rungwe, Mwenyekiti wa Halmashauri Meshack Mwakipunga alisema wameamua kuwajumuisha mafundi seremala katika mafunzo hayo ili mizinga iwe inatengenezwa jirani na wananchi na kwa gharama nafuu.
Alisema mazingira ya busokelo yanaruhusu ufugaji wa nyuki hivyo wananchi wakihamasishwa pia itasaidia kuongeza vipato vyao kupitia mazao ya kilimo ambayo yatasaidiwa na nyuki kufanya uchavushaji wakati wakijitafutia chakula.
Akizungumza wakati akifunga mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Crispin Meela alisema ni vema vikundi vilivyopewa mafunzo vikasimamiwa ili matunda yaonekane na iwe fundisho kwa wengine ambao hgawataki kujiunga na vikundi.
Alisema uchumi wa mtanzania unatokana na juhudi za mtu binafsi kupitia vikundi ambapo kupitia vikundi ni rahisi Serikali kuvisaidia kama ilivyofanya kwa kuwapa mizinga ya nyiki ambapo mradi huo hauna gharama yoyote ambayo kikundi kitapaswa kugharamia wakati wa kuendesha miradi hiyo.
Alisema Nyuki hawana gharama yoyote ambapo wakishawekewa mizinga huingia wenyewe na kuanza kutoa asali jambo ambalo mfugaji atatakiwa kuanza kuvuna na kuuza asali ambayo itakuwa imevunwa kwa kufuata taratibu za kitalaamu.
“ mnajua hawa nyuki hawana gharama zozote ambazo kikundi kitapaswa kugharamia kwa sababu nyuki hawaugui kwamba watatakiwa kupatiwa chanjo, hawali pumba, hawahitaji kuletewa maji bali huyafuata popote yalipo na wala hawataki pembejeo kutoka serikalini hivyo changamkieni fursa hiii.” Alisema Mkuu wa Wilaya.
Aliongeza kuwa ili kudhibiti uharibifu wa mazingira na kujenga mazingira rafiki kwa ufugaji wa nyuki ni vema wanaofuga nyuki kienyeji wakadhibitiwa kwa kuwa ndiyo wanaochoma mazingira hivyo Halmashauri iwadhibiti kupitia kanuni za vijiji na vitongoji kwa kuwaondoa kabisa misituni.
Mafunzo hayo yatolewa na wataalamu wawili kutoka kampuni ya National Beekeeping Supplies kutoka Mkoani Dodoma mafunzo ambayo yaliyofanyika kwa siku tatu ambapo wamefundishwa namna ya uvunaji na ufungaji kwa kuzingatia mahitaji ya soko la kimataifa.

Na Mbeya yetu

No comments: