Thursday, December 5, 2013

CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAKABIDHI TREKTA KWA VIJANA WA NJOMBE WANAOJISHUGHULISHA NA KILIMO

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikabidhi funguo za Trekta kwa Mwenyekiti kwa vijana Tumsume Shemgogo lililotolewa na chama cha Mapunduzi CCM  kwa vijana wa mkoa wa Njombe katika makabidhiano yaloyofanyika kwenye Kambi ya vijana iliyopo kwenye kijiji cha Mlengu Kata ya Kiangala Tarafa ya Ikuo mkoani Njombe ambapo kambi hiyo ina eneo lenye ukubwa wa  hekta 300 za mashamba, Kinana aliahidi kutoa  trekta hilo wakati alipofanya ziara ya kikazi mkoani Njombe mwezi Agosti mwaka huu  baada ya kuelezwa jinsi vijana hao walivyojiunga pamoja katika kikundi na kuamua kushughulika na kilimo ili kujkwamua kiuchumi, Leo Abdulrahman Kinana alishiriki kulima kwa trekta kabla ya kukabidhi trekta hilo kama anavyoonekana katika baadhi ya picha akilima shambani  kwa trekta.  Kushoto anayeshuhudia makabidhiano hayo ni Nape Nnauye Katibu wa NEC  Siasa, Itikadi na Uenezi, Katika Ziara hiyo Kinana  pia ameongozana  na Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kamataifa na Mbunge wa kuteuliwa. 2a 
SOMA ZAIDI...
2b 
Wananchi wa kijiji cha Mlengu wakimsikiliza Abdulrahman Kinana hayupo pichani wakati alipokuwa akizungmza nao. 16 
Mkuu wa mkoa wa Njombe Kapten Aseri Msangi akiuliza swali kwa mwanafunzi Tito Fungo uimara wa matofari hayo huku Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Dr. Asha Rose Migiro  wakisikiliza kwa makini. 22 
Nape Nnauye akijenga njia zinazopita chuni hapo kwa matofari madogo huku Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  na viongozi wengine wakiangalia. 23 

No comments: