Friday, January 10, 2014

CCM WILAYA YA MBARALI YAMPONGEZA WAZIRI TIBAIJUKA YASEMA HATA BADILI KAULI YAKE.

 Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mbarali, Matayo Mwangomo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi za Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Mbeya(Mbeya press club) zilizopo Soweto Jijini Mbeya.

 Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa (MNEC) kutoka Wilaya ya Mbarali, Geophrey Mwangurumbi, amesema Mgogoro huo ulianza baada ya Mwekezaji kupewa hati ambayo ilikuwa na kijiji cha Kapunga ndani yake kimakosa hivyo mgogoro huo unaweza kuisha kutokana na kauli ya Serikali.
Waandishi wa habari katika mkutano









CHAMA cha Mapinduzi(CCM) Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya kimemwagia sifa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi Profesa Annah Tibaijuka  kwa uamuzi wake wa kumshinikiza Mwekezaji kampuni ya Kapunga Rice Project kurejesha shamba lenye ukubwa wa Hekta 1870 kwa Wananchi.
Pongezi hizo zilitolewa leo na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mbarali, Matayo Mwangomo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi za Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Mbeya(Mbeya press club) zilizopo Soweto Jijini Mbeya.
Mwangomo amesema kitendo kilichofanywa na Serikali kupitia kwa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, cha kumtaka Mwekezaji huyo kurudisha sehemu ya ardhi ya wananchi aliyoichukua kimakosa kitasaidia kumaliza mgogoro uliodumu kati ya Mwekezaji na wananchi wa kijiji cha Kapunga kwa muda mrefu.
Amesema kutokana na kauli ya hiyo ya Waziri Tibaijuka imetoa faraja kubwa kwa wakazi wa kata ya Itamboleo kijiji cha Kapunga ambao walikuwa na mgogoro na mwekezaji huyo tangu mwaka 2006 hivyo kusababisha wananchi kuishi maisha ya wasiwasi wakihofia kupata madhara kutoka kwa Makaburu hao ambao ni raia ya Nchini Afrika kusini.
Mwenyekiti huyo ambaye aliongozana na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa (MNEC) kutoka Wilaya ya Mbarali, Geophrey Mwangurumbi, amesema Mgogoro huo ulianza baada ya Mwekezaji kupewa hati ambayo ilikuwa na kijiji cha Kapunga ndani yake kimakosa hivyo mgogoro huo unaweza kuisha kutokana na kauli ya Serikali.

No comments: