Saturday, January 25, 2014

PATO LA TAIFA LIMEONGEZEKA KWA KASI YA ASILIMIA 6.5 KWA KIPINDI CHA JULAI – SEPTEMBA, 2013 IKILINGANISHWA NA ASILIMIA 7.2 KWA KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012

PICTURE NO 01Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi Bw. Morice Oyuke kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (katikati) akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu ukuaji wa Pato la Taifa kwa robo mwaka ya tatu ya mwaka 2013 ambapo katika kipindi cha Julai – Septemba, 2013 Pato la Taifa kwa bei za soko liliongezeka kwa kasi ya asilimia 6.5 ikilinganishwa na asilimia 7.2 kwa kipindi kama hicho mwaka 2012. Kulia kwake ni Bw. Juma Omary, Mchumi Mkuu kutoka Ofisi ya Rais Tume ya Mipango na kushoto ni Bw. Daniel Masolwa Meneja Takwimu za Pato la Taifa kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu.

PICHA NAMBA 02 
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi Bw. Morice Oyuke kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (katikati) akizungumza kuhusu ukuaji wa Pato la Taifa kwa robo mwaka ya tatu ya mwaka 2013 katika ukumbi uliopo Ofisi ya Rais Tume ya Mipango, Dar es Salaam.

No comments: