Saturday, January 4, 2014

SERIKALI imewaagiza Watabibu wa Tiba mbadala na Tiba Asili kutojihusisha na matibabu ya ugonjwa wa Ukimwi kutokana na Madaktari bingwa na wataalamu wa afya kushindwa kugundua dawa za ugonjwa huo ambapo kufanya hivyo kutaongeza vifo kwa wagonjwa wengi kwa kukimbilia tiba mbadala na kuacha kutumia dawa za kuongeza nguvu.

 Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Mbeya, Leonard Magacha. akiongea na watatibu wa tiba asili kabla yakuwakabidhi vyeti
Boniventura Malongo  Mratibu watiba asili kitaifa akimkaribisha mgeni rasmi
Mratibu wa vikundi , Zahra Mansour akisoma risala mbele ya mgeni rasmi
CHET CHA MMOJA WA WASHIRIKI IUTOKA WILAYA YA RUNGWE MKOA WA MBEYA
Picha ya pamoja
SERIKALI imewaagiza Watabibu wa Tiba mbadala na Tiba Asili kutojihusisha na matibabu ya ugonjwa wa Ukimwi kutokana na Madaktari bingwa na wataalamu wa afya kushindwa kugundua dawa za ugonjwa huo ambapo kufanya hivyo kutaongeza vifo kwa wagonjwa wengi kwa kukimbilia tiba mbadala na kuacha kutumia dawa za kuongeza nguvu.

Alisema kama kuna mtu ametafiti dawa na anadhani zinaweza kutibu ugonjwa wa Ukimwi ni bora akazipeleka kwa wataalamu ili zithibitishwe kwa matumizi ya binadamu kuliko kuanza kuwapa watu hali itakayoongeza vifo visivyokuwa na lazima kipindi hiki ambacho bado watafiti wanaendelea kutafuta dawa halisi za kutibu magonjwa hayo.
Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, wakati wa hafla ya kukabidhi vyeti vya usajili wa Muda kwa Watabibu wa tiba asili Mkoa wa Mbeya, iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Hospitali ya Mkoa, ambapo Mkuu wa Mkoa aliwakilishwa na Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Mbeya, Leonard Magacha.

Mbali na hilo Kandoro  imeiagiza pia Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kuhakikisha inatengewa bajeti kwa ajili ya kuratibu na kufuatilia shughuli zinazofanywa na Matabibu wa Tiba Asili na tiba mbadala ili kujiridhisha na kazi zake.

Alisema ni vema Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa kutembelea vituo vya Waganga wa Tiba mbadala ili kujiridhisha na kazi zao kutokana na masharti ya usajili yanayokataza kupiga ramli, uchawi, ushirikina,mazingaombwe na upigaji ramli chonganishi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wote wanaojishughulisha na tiba asili wanakuwa na vibali halali vya Serikali.

Alisema Serikali imetambua kazi za Wahudumu wa tiba asili na tiba mbadala na ndiyo maana ikaunda baraza ambalo lilipewa mamlaka ya kusajili kwa mujibu wa Sehemu ya 4 kifungu cha 14, 16 na 17 cha Sheria ya Tiba asili na mbadala namba 23 ya Mwaka 2002.

Aliongeza kuwa Matabibu wa tiba asili na mbadala wanatakiwa kujitofautisha na waganga wa kienyeji kwa kuweka mazingira masafi ya kufanyia shughuli za kitabibu ili kuwa kivutio kwa wananchi na wateja wao ikiwa ni pamoja na kutoa tiba kwa bei nafuu ili kuwa msaada kwa wagonjwa wanaoshindwa kumudu gharama za Hospitalini.

Magacha ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa katika Hafla hiyo alisema changamoto inayowakabili wahudumu wa tiba asili na tiba mbadala ni kukosa ushirikiano na Madaktari wa Hospitali ambao ndiyo wataalamu zaidi kuliko wao ambapo aliongeza kuwa wakishirikiana na madaktari itawarahisishia wao kuwatibu vizuri wagonjwa kutokana na vipimo vya Hospitali badala ya kutibu kwa kukisia.
Katika Hafla hiyo jumla ya Watabibu 46 walikabidhiwa vyeti vya usajili wa Muda kutoka Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala, ambapo Mkoa wa Mbeya ukiwa na jumla ya matabibu 3261 ambapo kati yao waliosajiriwa ni 46 pekee.

Kwa upande wake Chama cha Watabibu Mkoa wa Mbeya(ATME) katika  risala yao kwa Mgeni rasmi iliyosomwa na Mratibu wa vikundi hivyo, Zahra Mansour walisema miongozo na taratibu zilizopo WAUJ inayohusu Urasimishaji wa Tiba Asili na Tiba mbadala itolewe kwa wakati kwa wadau wa tiba asili na Tiba mbadala.
Walisema hotuba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyotolewa Septemba 24, 2010 ya kuzindua urasimishaji wa tiba asili na tiba mbadala Nchini isambazwe kwawadau wa tiba asili ili itoe mtazamo wa tiba asili kwa kuweka kwenye vitabu vyote vya mwongozo wa tiba asili  na tiba mbadala sehemu ya utangulizi wa mwongozo.
Pia walisema ni vema idara ya Mkemia mkuu wa Serikalikupewa ruzuku ili kupunguza gharama za upimaji wa dawa asili zinazopelekwa na watabibu wa tiba asili kupimwa katika maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kama zinafaa kwa matumizi ya mwanadamu.
.................................................................................

  MOTO MKUBWA WAZUKA JANCO MOTEL JIJINI MBEYA 


Moto mkubwa umezuka katika hotel ya Janco forest mpya jijini Mbeya chanzo cha moto hakijajulikana mpaka tunaondoka katika tukio hilo






















Picha na Mbeya yetu

No comments: