Friday, January 24, 2014

Ugunduzi wa gesi na mafuta wavuta mataifa ya mbali kutafuta fursa za kuwekeza nchini Tanzania.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya madini Mhe. Stephen Massele akifuatilia maelezo toka kwa wajumbe toka Jamhuri ya Czech walipofika ili kuanzisha ushirikiano wa kibiashara katika sekta za nishati na madini  kati ya Tanzania na  Czech. Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Jamhuri ya Czech Mhe. Tomas Dub na kushoto kwake ni Kamishna msaidizi wa madini anayeshughulikia leseni Injinia John Nayopa.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya madini Mhe. Stephen Masele katika picha ya pamoja na ujumbe toka jamhuri ya Czech mara baada ya kumaliza mazungumzo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Nishati na madini.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya madini Mhe. Stephen Masele akiagana na Naibu waziri wa Mambo ya nje wa Jamhuri ya Czech Bw. Tomas Dub mara baada ya kumaliza kikao kifupi kilichofanyika ofisini kwake.

Ugunduzi huu umepelekea Wizara ya Nishati na Madini kupokea wageni wanaowakilisha nchi na watu binafsi wanaofika ili kutafuta fursa za kuwekeza nchini ikiwa ni pamoja na kujenga mahusiano ya kibiashara baina ya nchi husika.

Hivi karibuni wizara ya  Nishati na Madini imetembelewa na ujumbe toka Jamuri ya Czech nchi ndogo miongoni mwa nchi zinazounga umoja wa ulaya waliofika kwa lengo la kutafuta fursa za kuwekeza nchini ikiwa ni pamoja na kudumisha uhusiano baina ya nchi hizi mbili.

Ujumbe huu uliongonzwa na  Bw. Tomas Dub Naibu Waziri wa mambo ya Nje ya Nchi ya Czech aliyeelezea uwezo wa nchi yake katika masuala ya nishati na madini na kusema kwamba awali nchi yao ilijikita katika umeme uliozalishwa kwa maji, gesi  pamoja na nishati jadidifu, na kusema kwamba wana wataalamu wa kutosha katika sekta ya nishati.

Dub alieleza kuwa maendeleo si tu kutegemea utafutaji na uzalishaji wa gesi asilia bali inatakiwa nchi ifanye nguvu ya ziada katika kuongeza thamani ya bidhaa hiyo na hilo litawezekana tu kwa kujenga viwanda jambo lililowavuta ili kuja kutafuta fursa hiyo nchini. 

Dub alikamilisha mahojiano hayo kwa kuitaka Wizara  kuelimisha watanzania katika chuo cha madini katika nchi hiyo na kwamba mawasiliano yataendelea kufanyika ili kufikia malengo ya uhusiano huo.

Kwa upande wake Masele amesema kwamba zipo fursa nyingi  za uwekezaji nchini katika sekta ya madini  na zaidi madini ya viwandani lakini pia sekta ya nishati kwa kufuatia ugunduzi wa gesi na mafuta vitalu vimetangazwa hivyo ni fursa kwa Czech kuomba vitalu hivyo ili kuweza kushiriki katika shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi.


Na Nuru Mwasampeta


No comments: