Wednesday, March 19, 2014

CHELSEA HIYOO.... ROBO FAINALI LIGI YA MABINGWA ULAYA


Samuel Eto'o akishangilia baada ya kuifungia Chelsea bao la kwanza dakika ya nne Uwanja wa Stamford Bridge

Prolific: The goal was the African forward's 30th strike in the Champions League
Hilo lilikuwa bao la 30 la Mwafrika huyo tishio kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya
Cushion: Cahill's strike extended Chelsea's aggregate lead to 3-1 and sent them towards the last eight
Cahill akiifungia Chelsea na kukamilisha ushindi wa jumla wa 3-1 kwa michezo yote miwili ilichezwa
Jumping for joy: Chelsea players celebrate Cahill's goal on the stroke of half-time
Wachezaji wa Chelsea wakisherehekea ushindiReturn: Former Chelsea striker Didier Drogba emerges from the tunnel for Galatasaray
Mshambuliaji wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba akiingia Uwanja wa Stamford Bridge na timu yake ya Galatasaray
Reunited: Drogba hugs Chelsea manager Jose Mourinho before the game
 Drogba akikumbatiana na kocha wa Chelsea, Jose Mourinho kabla ya mechi
Hero: A banner saluting former striker Drogba on show at Stamford Bridge during the game
Bango la kumpa heshima yake Drogba likiwa limetungikwa Stamford Bridge wakati wa mechi
CHELSEA itaendelea kupeperusha bendera ya England kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya usiku huu kuitoa Galatasaray ya Uturuki kwa jumla ya mabao 3-1 Uwanja wa Stamford Bridge, London.

Baada ya kutolewa kwa Manchester City na Arsenal katikati ya wiki iliyopita, Chelsea imejikatia tiketi ya kuingia Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa kuifunga mabao 2-0 timu hiyo ya mchezaji wao wa zamani nyota, Didier Drogba.

Mabao ya Chelsea yamefungwa Samuel Eto'o 'Kikongwe' dakika ya nne na Gary Cahil dakika ya 43. Katika mchezo mwingine usiku huu, Real Madrid imeifunga Schalke mabao 3-1 Uwanja wa Santiago Bernabeu na kuwatoa Wajerumani hao kwa jumla ya mabao 9-2 baada ya awali kushinda 6-1 ugenini. Leo mabao ya Real yalifungwa na Cristiano Ronaldo dakika ya 21 na 74 na lingine Alvaro Morata dakika ya 75, wakati la Schalke limefungwa na Tim Hoogland dakika ya 31

No comments: