Wednesday, April 2, 2014

matukio katika picha kamati za Bunge maalum la Katiba

1 (8) 
Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Pius Msekwa (kulia) akitoa ufafanuzi leo mjini Dodoma  kuhusu hati ya Muungano kwa wajumbe wa Kamati namba mbili(2) ya Bunge Maalum la Katiba  baada ya wajumbe hao kumuomba aende kuwaelimisha juu ya hati hiyo. Wengine ni Mwenyekiti wa Kamati namba mbili Shamsi Vuai Nahodha(katikati) na Mwanasheri Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Othaman Masoud Othaman(kulia)
3 (5) Wajumbe wa Kamati namba mbili wakimsikiliza Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Pius Msekwa (hayupo pichani) wakati anatoa ufafanuzi leo mjini Dodoma  kuhusu hati ya Muungano baada ya wajumbe hao kumuomba aende kuwaelimisha juu ya hati hiyo.6Mwenyekiti wa Bunge  Maalum la Katiba Samuel Sitta(kulia) akizungumza na wajumbe wa Kamati namba Sita (6) ya Bunge hilo leo mjini Dodoma wakati akitembelea Kamati mbalimbali kujionea maendeleo ya uchambuzi wa vifungu mbalimbali vya rasimu ya Katiba mpya kwa sura ya Kwanza na Sita. Wengine ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo Stephen Massato Wassira(katikati) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Maua Abeid Daftari (kushoto)
Picha na Bunge la Maalum la Katiba

No comments: