Sunday, April 27, 2014

RAIS JAKAYA KIKWETE AONGOZA WATANZANIA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA

Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akiingia kwenye uwanja wa Uhuru kuwaongoza watanzania katika maadhinimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania yanayofanyika kila mwaka Aprili 26 kusherehekea muungano wa Tanganyika na Zanzibar  yaliyoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu J.K.Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume Aprili 26 mwaka 1964, Watanzania wengi wamejitokeza katika maadhimisho hayo wakiwemo marais wa nchi mbalimbali za Afrika, Viongozi mbalimbali na wawakilishi wa nchi  katika mataifa mbalimbali ya Afrika, Nchi za kiarabuni, Asia  na  Ulaya, Fullshangwe ilikuwepo kwenye   eneo la tukio na kukuletea moja kwa moja matukio mbalimbali yaliyojitokeza katika maadhimisho hayo ambayo yamefana kwa kiwango kikubwa. 2 
Rais Jakaya Kikwete akiingia kwenye uwanja wa Uhuru. 3 
Rais Jakaya Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya ulinzi na usalama  5 
Viksoi vya ulinzi na usalama vikiwa katika gwaride maalum 7 
Rais Jakaya Kikwete akirejea jukwaa kuu mara baada ya kukagua gwaride.  
 10 
Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Rais Uhuru Kenyata mara baada ya kuwasili  11 
Viongozi mbalimbali wakiwa wamesimama jukwaa kuu wakati wimbo wa taifa  14 
Marais mbalimbali wakiwa wamekaa jukwaani  
  
   19 
Rais wa Malawi Mh. Mama Joyce Banda akiwasili kwenye uwanja wa Uhuru kuhudhuria maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania. 20 
Mpiganaji  Nicholas Mbaga wa TBC akiwa Live kuripoti matukio mbalimbali ya maadhimisho hayo.
Kikosi cha Makomandoo kikionyesha ukakamavu na kutoa heshima mbele ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Kikwete. 4 
Makomandoo hawa wakionyesha uwezo mkubwa wa mapambano na adui. 6 
 9 
Kifaru cha kivita kikipita mbele ya wanahabari na wananchi waliohudhuria katika maadhimisho hayo. 10 
Askari wa miamvuli ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wakishuka kwenye uwanja wa Uhuru baada ya  kuruka kwenye ndege umbali wa mita zaidi ya elfu 4000 angani. 15 
Wakienda kutoa heshima kwa Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Jakaya Kikwete. 17 
Rais Jakaya Kikwete akiwapongeza askari hao wa miamvuli   18 
Vijana wa pikipiki wakipita mbele ya Rais Jakaya kikwete 19 
Vjana wa halaiki wakionyesha maumbo mbalimbali yenye kuuuelezea muungano 20 
Ni maumbo mbalimbali yaliyoonyeshwa na watoto wa halaiki wakati wa maadhimisho hayo.

No comments: