Tuesday, May 20, 2014

SAFARI YA MWISHO YA MUIGIZAJI WA FILAMU,MAREHEMU ADAM KUAMBIANA



Shughuli ya kuaga mwili wa aliekuwa muigizaji na muongozaji wa filamu hapa nchini, Marehemu Adam Kuambiana inaendelea hivi sasa kwenye viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam.














Mashada yakiwa tayari juu ya kaburi la Marehemu Adam Philipo Kuambiana,muda mfupi baada ya shughuli za mazishi kukamilika.Jacob Steven 'JB',akiweka shada kwenye kaburi hilo.
Msanii wa fialmu Bongo,Mariam akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Kuambiana.
Mwili wa marehemu Kuambiana ukiwasili makuburini tayari kwa shughuli za kuusitili.
Jeneza lenye mwili wa marehemu Kuambiana likishushwa kaburini hapo.
Mwili huo uliyondani ya jeneza ukizamishwa shimoni tayari kwa kutoa heshima za mwisho.
Msanii wa filamu Richie Richie akiweka udongo kwenye kabuli la Marehemu Kuambiana.
Baadhi ya mafundi wakichanganya zege tayari kwa kumthitiri marehemu Kuambiana.
Mwafundi hao wakikamilisha shughuli za kujengea kabuli hilo.
Mchungaji akiweka msalaba kwenye kaburi hilo.
Mke wa marehemu Janeth Rithe,akiweka shada la maua kwenye kabuli la mmewe.
Mkurugenzi Mkuu wa Global Publishers LTD,Eric James Shigongo akitoa salamu za mwisho kwenye mwili wa marehemu Adamu Kuambiana.
Baadhi ya waombolezaji wakiaga mwili wa marehemu.
Msanii wa Filamu Flora Mvungi akiaga mwili wa marehe Kuambiana.
Mtangazaji wa Kipindi cha Jahazi kinachorusho na Clouds FM,Ephraim Kibonde akipita kuaga mwili wa marehemu Kuambiana.
JB,akiwa chini baada ya kuzidiwa na kudondoka wakati akitoa wasaa wa marehemu Adam Kuambiana.
Baadhi ya mabaunsa na wasanii wenzake wakimnyanyua JB,baada ya kuzidiwa na kudondoka chini.
Msanii wa filamu Jini Kabula akiaga mwili kwa machungu.
Msanii wa filamu Davina akibebwa baada ya kuzidiwa wakati wa kuuaga mwili wa marehemu Adam Kuambiana kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam leo.
Jack Wolper akipita kutoa heshima za mwisho.

No comments: