Thursday, October 2, 2014

DStv Bomba yazinduliwa Tanzania

index
MultiChoice Africa ina furaha kuwatangazia kuwa imezindua kifurushi kipya maalumu kwa watanzania. Kifurushi hiki kimetengenezwa mahususi kwa watanzania kikiwa na chaneli zaidi 65 za kitaifa na kimataifa zitakazotoa burudani pekee kwa familia za kitanzania.
Kifurushi hiki kipya cha Bomba kina chaneli nyingi nzuri ikiwemo chaneli iliyozinduliwa hivi karibuni ya Maisha Magic Swahili inayoonyesha filamu za kitanzania; chaneli ya Telemundo inayojulikana kwa michezo ya kuigiza ya kimapenzi ya Amerika ya Kusini pamoja na Nickelodeon na Disney Junior zinazoonyesha vipindi vya watoto.
Meneja Mkuu wa MultiChoice Tanzania, Peter Fauel, alisema kuwa kifurushi kipya cha Bomba kitagharimu kiasi cha TSh 17,000 tu kwa mwezi: ” Uzinduzi wa kifurushi hiki cha Bomba ni jambo la furaha na msisimko sana kwetu, kuona kuwa sasa watanzania wanaweza kupata kifurushi kinachokidhi mahitaji yao. Kila wakati, MultiChoice inafanya jitahada za kubuni namna ya kuwapa wateja wetu uwanja mpana wa burudani. Sasa, watanzania wameongezewa uwanja wa uchaguzi kwa bei iliyo chini na kiwango cha juu cha burudani ikiwemo filamu, makala, habari, vipindi vya watoto, muziki, vipindi vya dini na michezo.”
Usikose ofa yetu ya uzinduzi huu – watakaojiunga watapata DStv ikiwemo gharama ya ufundi kwa TSh 99,000 tu kwa kipindi maalum. DStv Bomba pia itakuwa na chaneli za Africa Magic Epic Movies, Discovery World, CBS Action, CBS Reality na CBS Drama pamoja na Select Sport 1 na 2 kwa vipindi vizuri vya michezo.
SuperSport Select na SuperSport Select 2 zitaonyesha ligi kuu ya Uingereza, Kombe la klabu bingwa Ulaya, Ligi Kuu ya Hispania, Ligi kuu ya Ujerumani pamoja na riadha na ngumi. SuperSport Blitz itawaletea habari zote za michezo.
Kwa habari zaidi kuhusu burudani kwa ajili ya familia, tembelea tovuti:
www.dstv.com

No comments: