Sunday, October 19, 2014

Rais Kikwete na Rais Kabila waongoza sherehe za Kuhitimu Maafisa Wapya wa Jeshi

Rais Kikwete akutana na Rais Kabila Arusha

k1 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikiwete akizungumza na Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya kidemorasia ya Kongo DRC muda mfupi kabla ya marais hao wawili kuongoza sherehe za kutunuku kamisheni na kuhitimu mafunzo kwa maafisa wapya wa jeshi kutoka katika nchi hizi mbili jirani.Sherehe hizo zilifanyika katika chuo cha kijeshi Monduli mjini Arusha leo


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo DRC wakiwa katika sherehe ya kuhitimu mafunzo ya maafisa wanafunzi kundi la 54/13 kutoka Tanzania na DRC. DRC katika chuo cha Mafunzo ya kijeshi kilichopo Monduli Mkoani Arusha leo. D92A3866 
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Rais Joseph Kabila wa DRC na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange wakijadili jambo wakati wa hafla ya kuhitimu mafunzo na kutunuku kamisheni kwa maafisa wa kundi la 54/13 DRC yaliyofanyika chuo cha kijeshi Monduli Mkoani Arusha jana.(picha na Freddy Maro) D92A4025 
Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) akimpa zawadi ofisa kadeti Yusup kutoka DRC baada ya kuibuka mwanafunzi bora katika kundi la 54/13 wakati wa hafla ya kumaliza mafunzo iliyofanyika huko Monduli jana. D92A4033 
Rais Joseph Kabila wa DRC akimpa zawadi Ofisa Kadeti Ibrahim Mwamtemi baada ya kuibuka mwanafunzi bora katika mafunzo ya porini wakati wa hafla ya kutunuku kmaisheni baada kumaliza mafunzo ya kundi la 54/13 DRC yaliyofanyika Chuo cha kijeshi monduli jana. D92A4050 
Amiri Jeshi Mkuu, Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitunuku kamisheni kwa maofisa wa Jeshi wanafunzi kundi la 54/13 DRC katika chuo cha Mafunzo ya kijeshi kilichopo Monduli Mkoani Arusha jana. D92A4097 
Maafisa wapya wa jeshi la Wananchi wa Tanzania wakila kiapo cha utii kwa Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla ya kutunuku kamisheni kwa maafisa wapya wa jeshi la wananchi wa Tanzania iliyofanyika katika chuo cha mafunzo ya kijeshi kilichopo Monduli Mkoani Arusha jana.

No comments: