Friday, December 19, 2014

SIMBA YAVUNJA UONGOZI WA YANGA,NI KIPIGO CHA MTANI JEMBE,MANJI ATANGAZA UONGOZI MPYA

muro 

MWENYEKITI wa klabu ya Yanga Yusuph Manji ameitangaza Sekretarieti mpya ya Uongozi katika Klabu hiyo yenye Maskani Mtaa wa Jangwani Jijini Dar Es Salaam.
Sektretarieti hiyo ambayo itaongozwa na  Katibu Mkuu Dk Jonas B Tiboroha ambae atafanya kazi na Mkuu wa Idara ya habari na Mawasialiano bwana Jerry Cornel Muro,Bwana Omar Kaya yeye anakuwa Mkuu wa Idara ya masoko 

Wengineo ni Bwana Frank Chacha anakuwa Mkuu wa Idara ya Sheria pamoja na bwana Charles Boniface ambae atakuwa Kocha Msaidizi
Akithibitisha Kuteuliwa kwa Viongozi hao wajuu Klabuni hapo mda  huu Jijini Dar Es Salaam wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari na  Mkuu wa Idara ya habari na Mawasialiano bwana jerry Cornel Muro pamoja na kutangaza Viongozi hao wapya alisema 
Wanachama,Mashabiki,Wapen  pamoja na wapenzi wa Klabu hiyo washirikiane na Viongozi hao wapya kuiletea maendeleo Klabu hiyo kubwa nchini.

Aidha,jery Murro alisema Mwenyekiti wa yanga anamshukuru sana Bwana aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo mbrazili MARCIO MAXIMO pamoja na msaidizi wake kwa ushirikiano wo waliouonyesha katika timu hiyo na kuwatakia heri katika maisha yao huko waendako.
Katika hatua nyingine amesema kuwa yanga imeamua kuongeza vijana katika uongozi  wake ili muda wa kustaafu ukifika yanga iyakuwa na waridhi bora watakaoendeleza mazuri waliyoyakuta..

No comments: