Wednesday, February 4, 2015

MAGAZETI YANAYOMILIKIWA NA MAKAMPUNI BINAFSI YAONGOZA NCHINI.

1111


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete (kulia), akizungumza na waandishi wa habari Ikilu Februari 3,2015 jijini Dar es salaam akiwa na mgeni wake Rais wa Ujerumani Rais wa Ujerumani Joachim Gauck (kushoto). Rais Gauck yupo nchini kwa ziara ya kikazi kwa siku tano.

Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazosimamia uhuru habari na inaongoza kwa kuwa wa vyombo vingi habari yakiwemo magazeti.

Kauli hiyo ilitolewa Februari 4, 2015 jijini Dar es salaam na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete alipokuwa akijibu swali la mwandishi wa habari aliyetaka kujua sababu za kusimamisha uingizaji nchini gazeti la "The East African", wakati wa mkutano wa waandishi wa habari yeye na Rais waUjerumani.

Rais Kikwete alisema kuwa gazeti hilo halikufuata utaratibu wa kusambazwa nchini kulingana na sheria na taratibu za nchi, hata hivyo Serikali imeshawasiliana na wahusika na wameelekezwa utaratibu wa kufuata kulingana na sheria za nchi.

"Tanzania injali na kusimamia uhuru wa habari, kuna magazeti mengi yakiwemo ya kila siku, wiki ambayo yanayomilikiwa na makampuni binafsi ikilinganishwa na magazeti yanayomilikiwa na Serikali" alisema Rais Kikwete
Rais kikwete aliyataja magazeti yanayomilikiwa na Serikali kuwa ni pamoja na Daily News na Habari Leo ikilinganishwa na magazeti yanayomilikiwa na makampuni binafsi ambapo aliyataja magazeti hayo kuwa ni The Guardian, The Citizen, Majira, Mwananchi, Nipashe na mengine mengi.

Rais wa Ujerumani na msafara wake wapo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tano ambayo ni mwaliko walioupata kutoka kwa Dkt. Kikwete alipotembelea Ujerumani hivi karibuni na kutunukiwa tuzo ya kufanya vizuri katika suala la chanjo kwa watoto.

Ugeni huo wa Rais Gauck watapata fursa ya kujionea maeneo mengi yenye vivutio vya watalii nchini yakiwemo Visiwa vya Zanzibar na Arusha ambayo yanajulikana kwa utajiri wa vivutio hivyo barani Afrika na duniani.

Ujio wa Rais Gauck nchini na msafara wake unafuatia mahusiano mazuri yaliyopo kati ya nchi hizo mbili wa muda mrefu kwa manufaa ya maendeleo ya wananchi wao kiuchumi, kisiasa na kijamii.

.................................................................

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI CHARLES KITWANGA AKUTANA NA UJUMBE WA WAFANYABIASHARA KUTOKA UJERUMANI

unnamed1q 
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Kitwanga (Kulia) akizungumza na ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini   Ujerumani uliomtembelea ofisini kwake kwa ajili ya kujifunza fursa   za uwekezaji katika sekta za nishati na madini.
unnamed2q 
Katibu wa Nchi kutoka Wizara inayohusika na Masuala ya Uchumi na Nishati ya Ujerumani Mattias Machnig (kulia) akisisitiza jambo katika kikao kilichokutanisha ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Kitwanga kwa ajili ya kujifunza fursa za uwekezaji katika sekta za nishati na madini nchini.
unnamed3q 
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Kitwanga (Kulia) akisisitiza jambo wakati alipokutana na ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini   Ujerumani uliomtembelea ofisini kwake kwa ajili ya kujifunza fursa   za uwekezaji katika sekta za nishati na madini.
Katibu wa Nchi kutoka Wizara inayohusika na Masuala ya Uchumi na Nishati ya Ujerumani (wa tatu kutoka kushoto waliokaa mbele) akielezea maeneo katika sekta ya nishati ambayo nchi ya Ujerumani ingependa kuwa unnamed5q 
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Kitwanga na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava pamoja na ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani wakifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia masuala ya umeme, Mhandisi Innocent Luoga ( aliyekaa mbele wa kwanza kushoto) juu ya fursa za uwekezaji katika sekta ndogo ya umeme.

No comments: